Ukweli Mchungu kwa Wanasimba: Televisheni ya Yanga kuwa na Thamani kubwa kuliko Klabu ya Simba ni upumbavu

Ujue pia Mo na Azam ni bitter rivals kwenye biashara, ni dhahiri dili nyingi za Azam kwa Mo zitapita kwa Mbinde.
Usije ukasikia Mo nae anaanzisha Media house yake, huyu Mo ni dizaini ya Diamond kimtazamo
 
Wewe ni chizi wanahisa hawagawani mtaji wanagawana faida tu

Umeandika nini.

Chizi ni Mimi au wewe ambaye hukuelewa.

Punguza Mhemko usome tene na uelewe kwanza ndo utukane kabla ya kuwahi kutukana
 
Umemsikia Ghalib? Anakwambia thamani ya yanga ni 60bn to 200bn, simba wabaki na nafasi yao ya 10 Afrika, na yanga ya 80, ila yanga inakuja huko kwenye 10 kwa kishindo, alijibu kijembe cha moo akiweka tu bn 20

Mashabiki wa timu ya Simba wao wanaangalia furaha ya matokeo ya Muda mfupi

Hawaangalii madhara ya huu mkataba .

Mo anapata wap nguvu ya kukataa mikataba mingine just kwa kuwa ni rivals wa Mo Kampuni. ?
 
Yanga wenye elimu wako wapi? Ikiwa kushiriki kimataifa hadi wabebwe.

Wewe unaminyana bure, yaani unajiona upo kwenye banda la mpira. Uzi unakiri kuwa Simba ndo ina Matokeo bora, Simba ni timu bora East Africa.

Uzi unaitambua Simba kuwa na Thamani kubwa sana. Thamani hii haipaswi kuwa kwenye Maneno bali kwenye Makaratasi pia.

Kipi hujaelewa hapo. ?

Timu top 10 kwa Ubora Africa then ina thamani ya B40?
 
Mwanzoni mlisema mbona haweki hizo billioni 20, sasa kaweka Mnaanza mbona ndogo. Hii nchi tabu sana..
 
Eti wao hawataki mtu apate faida. Acha tu apate faida hata mara mbili lakini kikubwa timu ifanye vizuri uwanjani maana hiyo ndiyo furaha yetu mashabiki.
 
Mh. 38bn ni udhamini, 20bn ndio umiliki, tungoje ya hisa za yanga za mara moja
 
Mkuu mbona unaumia sana? toa huo mwiko huko nyuma labda akili zitakukaa sawa, siku zote adui muombee njaa sasa hiyo yanga mnayoisifia ina nini cha maana? hata uwanja wa mazoezi tu upo kwenye makaratasi miaka nenda miaka rudi, kwa wakati tuliopo Mo ni mtu sahihi kwa simba
 
Wewe unavyoona ina thamani ya shillingi ngapi?.
 
Umeandika nini.

Chizi ni Mimi au wewe ambaye hukuelewa.

Punguza Mhemko usome tene na uelewe kwanza ndo utukane kabla ya kuwahi kutukana
Wewe ndio chizi haiwezekani useme kila mpunga utakaoingia kwa simba Mo anachukua 49%, Simba na Mo watakuwa wanagawana faida au hasara itakayopatikana tu, halafu waache simba walingie walichonacho sasa haya ya mbeleni yatajulikana hukohuko
 
Wewe ndio chizi haiwezekani useme kila mpunga utakaoingia kwa simba Mo anachukua 49%, Simba na Mo watakuwa wanagawana faida au hasara itakayopatikana tu, halafu waache simba walingie walichonacho sasa haya ya mbeleni yatajulikana hukohuko
Sasa faida wanagawanaje?..

Faida inayopatikana wanagawana kulingana na kiwango cha uwekezaji wewe.. katika kila 100 inayopatikana Mo anachukua 49.

nenda shule
 
Sasa faida wanagawanaje?..

Faida inayopatikana wanagawana kulingana na kiwango cha uwekezaji wewe.. katika kila 100 inayopatikana Mo anachukua 49.

nenda shule
Ila kumbuka ni kwenye faida, sasa wewe na mazuzu wenzako mnajua simba akipata udhamini wa bilioni moja basi mo ana fungu lake, kumbuka hadi faida ipatikane ndio mo atapata chochote, hii simba kuchukua ubingwa mara4 mfurulizo ndio inakufanya uweweseke
 
Ila kumbuka ni kwenye faida, sasa wewe na mazuzu wenzako mnajua simba akipata udhamini wa bilioni moja basi mo ana fungu lake, kumbuka hadi faida ipatikane ndio mo atapata chochote, hii simba kuchukua ubingwa mara4 mfurulizo ndio inakufanya uweweseke
Tatizo simba wanajiona level moja na alhly ndio shida, hiyo hela mo aliyonunulia timu ndio inasjili mtu kule
 
Zile bill 41 zinazolipwa kila mwezi?..nadhani thaman yake ningekuwa kubwa zaidi ya simba kama wamelipa kwa mkupuo lakini kwa malipo ya kila mwezi sioni la maana nahisi Adam ndio watanufaika zaidi..simba bil 20 zimeshawekwa haya Yanga watuoneshe 41 zao, ndio hapo utaona tofauti ya hizo mbili kaka.
 
Valuation ilifanyika 2016 wakati huo Simba ilikuwa na misimu minne bila ubingwa na haikuwa na Assets zozote zaidi ya jengo la pale Msimbazi centre ungekuwa wewe mwekezaji kipindi hicho ungeweka thamani ya Simba kwa value ya sasa ?
 
Ukiitaka ya Yanga Sc bado haijulikani. Wakitangaza kuwa wanauza Shea kwa 200B basi wao ndo wana Thamani kubwa kama klabu.
Sasa naona umejirekebisha kwa kusema thamani ya Yanga haijulikani, ila pale mwanzo ulitaka watu waamini kuwa hela za udhamini ndio thamani ya timu. Kwa sasa thamani ya Yanga haijulikani, na hiyo 200B ikitokea amepatikana mwekezaji akakubali kuweka 200B (kama yupo atakayekubali), hapo ndipo utakapoanza kusema Yanga ina thamani ya 200B. Kwa sasa inatosha kusema thamani ya Yanga haijulikani.

Tena sio suala la wao kutaka kuuza shea kwa bei hiyo, ni hadi ajitokeze atakayekubali kununua shea kwa bei hiyo. Unaweza ukataka kuuza koti kwa sh. laki tatu, lakini mwenzako mnunuaji anaona kabisa halina tofauti na koti la sh, elfu tatu pale Kariakoo. Thamani ya kitu inaamuliwa na mnunuaji, muuzaji ukikomaa utaendelea kubaki nacho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…