Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Paskali,
Kitabu toleo la Kiingereza tunakwenda toleo la tatu na cha Kiswahili
tunakwenda toleo la nne.

Kitabu kithaminiwe vipi?

Je. unajua kitabu cha Kivukoni kimechapwa mara ngapi baada ya 1981
kilipochapwa kwa mara ya kwanza?
Kiukweli sifahamu kwa sababu mimi nimekijibia mtihani wa CSEE mwaka 1985 baada ya hapo sijujua chochote. Wakati nikuwa skuli sikuwahi kusoma kitabu chochote cha mwandishi Muhammed Said kwa sababu maabdishi yake hayakupitishwa kwenye ithbati ya kufundisha shule yoyote ya Tanzania!. Muhammed Said tuliyemsoma sisi ni Mzee MSA, Mohemed Said Abdullah
1.Duniani kuna watu
2.Kisima cha Giningi
3.Mke Mmoja Watume Watatu
4.Siri ya sifuri
5.Mzimu wa watu wa kale
6.Kosa la bwana msa

Paskali
 
Shimba...
Hakika mimi naipigania historia ya Waislam.

Kitabu changu kinaitwa: ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika.''

Hapo kamata ''Untold,'' ilikuwa bado haijaelezwa.
Kisha kamata ''Muslim.''

Unaweza ukakejeli kwa maneno ya ''Maimuna,'' nk. lakini hiki ni kitabu kimeeleza mengi ambayo hayakuwa yakijulikana.

Mimi siandiki nikatokwa ''povu,'' sina sababu ya kufanya hivyo.
hapa anaetokwa na povu ni wewe si mie.

Soma hizo kejeli zako za ''vihela,'' nk.
Huu si uungwana.
[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Paskali,
Mimi sina nguvu ya kulazimisha chochote kwako au kwa mtu yeyote awae yule.

Nilichonacho mimi ni mantiki na ukweli katika historia ya Tanganyika ambayo
nimetafiti na kuandika kitabu, na ''paper,'' kadhaa ambazo watu wamesoma
bila ya kulazimishwa.

Wala mimi sijakataa kuwa Mwalimu Nyerere ni muasisi wa TANU.

Ila ninachosema mimi ni kuwa ikiwa utaifunga akili yako ibakie hapo bila ya
kutaka kuisoma historia nzima atakaepunjika ni wewe.

Ukweli ni kuwa Nyerere haiwezekani mgeni mno afike Dar es Salaam, awe na
ofisi, awe na wanachama na aanzishe TANU huu ni sawa na muujiza.

Haiingii akilini kuwa wewe uione kadi ya TANU ya Nyerere no. 1 lakini usitake
kujua nani ana kadi no. 2, 3, 4 na kuendelea hasa kwa mtu mwenye ''A'' ya
historia.

Hili haliwezekani lakini ukipenda kuamini hivyo hakuna wa kukulazimisha vinginevyo
hasa kwa kuwa una ''A'' ya historia ya Kivukoni.

Hii maana yake ni kuwa wewe ni mjuzi.

Kuna kitu kipya umekileta kuwa African Association ni ya kina Sykes na wao hapa
si kwao kwa hiyo ni sawa kwa historia hiyo kufutwa.

Mantiki ya hoja yako inakuwa kwa kuwa hawa ni Wazulu ''watu wa kuja,'' na
wameanzisha African Association basi historia hii haitakiwi.

Hoja hii itatambaa hivyo hivyo hadi kufikia wao kuunda TANU 1954.

Katika historia ya uhuru wa Tanganyika na mwamko wa Waafrika wa Tanganyika
kupambana na ukoloni utakutana na Waafrika wengi ambao Tanganyika si kwao.

Katika hiyo African Association utakutana na Kleist Mzulu aliyezaliwa Pangani na akina
Plantan waliokuja kutoka Mozambique lakini ni Wazulu pia.

Utakutana na Ibrahim Hamisi Mnubi wa wazee wake wametokea Dafur, Sudan.

Utakutana na Erica Fiah Mganda kutoka Uganda, utakutana na Mzee bin Sudi
Mmanyema wazee wake wametokea Belgian Congo.

Hawa nimekutajia wachache tu katika historia ya kupambana na wakoloni katika
miaka ya 1920 hadi kufikia mwisho wa Vita Vya Pili 1945.

Katika hiyo TANU halikadhalika wako pia ''wakuja,'' wengi tu.

Tuanze na Patwa Muhindi, Saadan Abdul Kandoro, Mmanyema, Sheikh
Mohamed Ramiya
Mmanyema,

Dome Okochi Budohi
Mluya kutoka Kenya, Patrick Aoko Mjaluo Mkenya, Denis
Phombeah
Mnyasa kutoka Nyasaland, Iddi Faiz Mafungo Mmanyema kwa
kukutajia majina machache.

Kulikuwa na Earle Seaton kutoka Bermuda, haonekani lakini yuko aliyetiwa katika
siasa za Tanganyika na Abdul Sykes kizazi cha pili Mzulu kuzaliwa Tanganyika.

Hawa wote wana historia zao ukizisoma mwili lazima ukusisimke.

Namaliza na babu yangu Salum Abdallah, Mmanyema aliyezaliwa Shirati Musoma
aliyekuwa mmoja wa wa wapigania uhuru wa Tanganyika kuanzia 1947 na 1955
akawa Mwenyekiti muasisi wa Tanganyika Railway African Union (TRAU).

Najua haya huyajui labda kwa kuwa waandishi wa historia kutoka Kivukoni kama
wewe hawakuwa wanayajua.

Inawezekama kwa kuwa una ''A'' ya historia ya Kivukoni ukaona Dictionary of
African Biography iliyochapwa na Oxford Univeristy Press, 2011 si chochote lakini
hii ni katika rejea muhimu sana katika historia ya Afrika.
Povuuuuuu !!!
56cae118f4bd2bd81fcbf9cacb9d824c.jpg
 
Mkuu Maalim Mohamed Said
mtaka nyingi nasaba hupata mwingi msiba, kama lengo ni kuzungumzia historia ya TANU, ilianzishwa mwaka 1954 na Mwalimu Nyerere. Hatutafuti nyingi nasaba za historia ya TAA kwa sababu hatutaki mwingi msiba!. Kama lengo ni historia ya TANU kwa ajili ya Watanzania, then ni historia ya TANU ya Kivukoni ya kupatia A kwenye macheti, halafu hiyo ya Oxford na Cambridge yenye TAA, iwafae wasomi wa Oxford na Cambridge na sio Watanzania wa UDSM. Siku ukiitwa kutoa mhadhara pale Nkrumah Hall nijulishe nije nikisikize, lakini ukiitwa Oxford na Cambridge wala usihangaike kunijulisha, bali ukirejea ndipo unihadithie!.

Nabii wa kweli ni yule anayethaminiwa nyumbani na sii ugenini!. Historia ya kweli ya TANU ni ile ya Kivukoni na sio hiyo ya DAB!.

Paskali
Pascal Mayalla

Kwanini unaikwepa "TAA" ?
 
Nina mashaka na hiyo Alama "A" yako.. Ulikua unajibu maswali ya historia bila kui trace back history!?

Historian yeyote lazima tujue chimbuko lake, historia inaleta mvuto pale unapoi trace sio kuja juu juu tu.
Usiwe na mashaka nayo, ni ile historia ya kujibia mitihani, TANU ilianzishwa mwaka 1954 na musisi wake ni Mwallimu Julius Kambarage Nyerere pekee!. Uhuru wa Tanganyika ulipatikana December 9 mwaka 1961na shujaa wa Uhuru ni Mwallimu Julius Kambarage Nyerere pekee!. Jamhuri ilipatikana December 9 mwaka 1962 na shujaa wa Jamhuri ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pekee. Muungano ni 1964 mashujaa ni Nyerere na Karume, etc etc.

Hao wengine sio mashujaa wanaotambulika rasmi ila kwa heshima yao wote wamepewa majina na mitaa na kwa bahati nzuri sasa, mimi naishi huku Cleist Sykes Close!.

Paskali
 
Usiwe na mashaka nayo, ni ile historia ya kujibia mitihani, TANU ilianzishwa mwaka 1954 na musisi wake ni Mwallimu Julius Kambarage Nyerere pekee!. Uhuru wa Tanganyika ulipatikana December 9 mwaka 1961na shujaa wa Uhuru ni Mwallimu Julius Kambarage Nyerere pekee!. Jamhuri ilipatikana December 9 mwaka 1962 na shujaa wa Jamhuri ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pekee. Muungano ni 1964 mashujaa ni Nyerere na Karume, etc etc.

Hao wengine sio mashujaa wanaotambulika rasmi ila kwa heshima yao wote wamepewa majina na mitaa na kwa bahati nzuri sasa, mimi naishi huku Cleist Sykes Close!.

Paskali
Nakubalian na wewe, sote tuanajua Hayati Mwaliimu Nyerere ndio shujaa Wa Taifa. Lakini kwa afya ya Taifa na vijana wetu, kwanini wasiwatambue na hawa waasisi Wa harakati za Uhuru akina Sykes nk?

Unadhani wataathiri heshima ya Baba Wa Taifa?
 
Pascal Mayalla
Kwanini unaikwepa "TAA" ?
Siikwepi TAA, tunapozungumzia historia ya kitu inaanzia kilipozaliwa!. Hata wewe historia yako huanzia ulipozaliwa na sio ulipotungwa!.

TANU ilizaliwa 1954 na historia hiyo safi imeandikwa kwa umahiri kabisa na Chuo cha Chama Kivukoni. Tusilazimishe historia ya wale walowezi wa Kizulu wa TAA kuwa ndio historia ya TANU, TANU ni TANU, TAA ni TAA na CCM ni CCM, kama somo ni chimbuko then ndipo tufukue makaburi ya TAA!.

Paskali
 
Nakubalian na wewe, sote tuanajua Hayati Mwaliimu Nyerere ndio shujaa Wa Taifa. Lakini kwa afya ya Taifa na vijana wetu, kwanini wasiwatambue na hawa waasisi Wa harakati za Uhuru akina Sykes nk?

Unadhani wataathiri heshima ya Baba Wa Taifa?
Wanaotambulika sana ndio maana wote wamepewa mitaa!.

Paskali
 
Siikwepi TAA, tunapozungumzia historia ya kitu inaanzia kilipozaliwa!. Hata wewe historia yako huanzia ulipozaliwa na sio ulipotungwa!.

TANU ilizaliwa 1954 na historia hiyo safi imeandikwa kwa umahiri kabisa na Chuo cha Chama Kivukoni. Tusilazimishe historia ya wale walowezi wa Kizulu wa TAA kuwa ndio historia ya TANU, TANU ni TANU, TAA ni TAA na CCM ni CCM, kama somo ni chimbuko then ndipo tufukue makaburi ya TAA!.

Paskali
Paskali,
Mohamed Said: MEDALI YA ABDULWAHID SYKES: MWENGE WA UHURU 1961 - 2011
 
Marehemu Oscar Kambona alizaliwa mwaka 1925 katika kijiji cha Kwambe kilichopo mwambao mwa ziwa Nyasa, karibu na Mbamba-bay, wilaya ya Mbinga, Mkoa wa Ruvuma. Alikuwa mtoto wa marehemu Rev. David Kambona na Bibi Miriam Kambona.

Rev. Kambona alikuwa ni miongoni mwa waafrika wa kwanza kupata upadre katika kanisa la Anglikana la Tanganyika. Wakati Oscar Kambona akiwa mdogo, baba yake alikuwa akimweleza kuhusu ndoto zake juu ya uhuru wa nchi yake, hivyo Oscar alikuwa akiwa na hamu sana ya kuitumikia nchi yake.

Oscar alipata elimu ya msingi nyumbani kwao, chini ya mwembe (ambao bado upo), katika kijiji chao kwa kuwatumia wazazi wake wote wawili na mjomba wake, ambao wote walikuwa walimu. Baada ya hapo alipelekwa shule ya kati ya Mt. Barnabas, Liuli, na baadaye shule ya Sekondari ya Alliance, ambako alilipiwa ada na Askofu mzungu wa Anglikana kwa vile baba yake hakuweza kumudu kulipa ada ya paundi 30 kwa mwaka.

Oscar alikuwa akisimulia jinsi alivyoweza kumshawishi Askofu huyo amlipie ada kwa kusema sala ya Baba yetu kwa kizungu. Oscar alichaguliwa kwenda ‘Tabora Boy’s Senior Government School’, ambako alionana na Julius Nyerere kwa mara ya kwanza; wakati huo Nyerere alikuwa anafundisha katika shule ya kikatoliki.

Baada ya kumaliza masomo ya sekondari alienda katika shule yake iliyopita ya Alliance kama mwalimu na baadae alichaguliwa kuwa ‘Schoolmaster’. Ilikuwa katika mkutano wa kitaifa wa walimu, mnamo mwaka 1954, ambapo Kambona na Nyerere walikutana tena.

Kambona alikuwa tayari kukitumikia chama cha TANU ambacho kilikuwa kimeanzishwa muda si mrefu, lakini Nyerere akasema wasingeweza kumwajiri kwa vile chama kilikuwa hakina fedha.

Kambona akasema chama hakikuwa na fedha kwa vile hakikuwa na ‘organising secretary, na ndipo alipoamua kufanya kazi hiyo ili kujenga chama, bila ya malipo’. Aliishi kwa kutegemea akiba aliyojitunzia kwa kufanya kazi miezi 6.

Katika kipindi hiki Kambona alisafiri sehemu mbalimbali za nchi na kuonana na machifu na wazee wa vijiji ili kusajili wanachama. Katika miezi 6 alifanikiwa kusajili wanachama 10,000, na hadi kufikia mwaka mmoja alikuwa amepata wanachama hai 100,000. Kambona alitumia michango aliyopata kufungua akaunti ya kwanza ya TANU.

alienda Butiama kumshawishi Nyerere achukuwe uongozi wa chama moja kwa moja. Baada ya miaka mitatu Kambona aliamua kwenda kusomea sheria katika Chuo cha Middle Temple, nchini Uingereza mwaka 1957 kwa ufadhili wa Gavana.

Akiwa London Kambona alikuwa kiongozi wa chama cha wanafunzi wa Tanganyika na Mwenyekiti wa tawi la TANU la London. Ni wakati huo ambapo Kambona alipata fursa ya kukutana kwa mara ya kwanza na watu mashuhuri kama George Padmore, mwanaharakati wa umoja wa Afrika, ambaye alimshawishi ahudhurie mkutano wa mwaka 1958 wa waafrika wote(All Africa’s Peoples Conference), uliofanyika nchini Ghana muda mfupi baada ya kupata Uhuru.

Akiwa Ghana Kambona alipata nafasi ya kukutana na mwanaharakati mwingine maarufu wa siasa za Afrikla, Kwame Nkurumah. Akiwa uingereza Kambona alikuwa mwaafrika wa kwanza kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili katika idhaa ya kiswahili ya BBC.

Aliporudi nchini Tanganyika, mwaka 1959, TANU ilikuwa imeshaweka bayana madai yake ya kupewa serikali ya madaraka, vinginevyo TANU ilikuwa tayari kuanzisha mapambano kama ilivyokuwa kwa Mau Mau ya Kenya. Wakiwa London wakisubiri kupewa madaraka ya ndani, Nyerere na Kambona walijadili hatua mbalimbali ambazo zingechukuliwa ili kuepuka kutoweka kwa amani.

Wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Londoni 1991, Kambona alikumbuka matukio kama hivi, ‘’Bwana Nyerere alikuwa akiishi nami katika chumba kidogo nilichopewa chuoni.

Tulijadiliana ni namna gani angeweza kurudi nyumani na kuonana na wafuasi wake bila kupewa serikali ya madaraka. Baadae nilifanikiwa kumshauri kuwa wakati atapozungumza na vyombo vya habari katika the East African Arch aseme kuwa walowezi wa kizungu ambao wapo Tanganyika wana hekima zaidi katika kanda ya Afrika Mashariki.

Alikubali kusema hivyo endapo na yeye Kambona angekubali kukatisha masomo yake ya sheria huko London na kurudi Tanganyika ili ampe nguvu na kumuunga mkono katika kikao cha kamati kuu ya TANU wakati akitetea tamko lake la wenye hekima zaidi.

Katika uchaguzi wa kwanza TANU ilishinda viti vyote isipokuwa kimoja. TANU iliunda serikali ya mambo ya ndani chini ya Nyerere ambaye alikuwa Waziri kiongozi wa kwanza.

Na katika harakati hizo za matayarisho ya serikali ya ndani, Kambona alimwoa Flora Moriyo wakati wakiwa kwenye msafara wa harakati za kukamilisha matayarisho ya uhuru na serikali ya Uingereza. Harusi ilifungwa katika kanisa la Mt. Paul, London, na Nyerere ndiye alikuwa msimamizi. Kambona aliteuliwa kuwa waziri wa Elimu.

Baadaye alishika nyadhifa za waziri wa Mambo ya Ndani, Mambo ya nchi za nje na Ulinzi na Tawala za Mikoa. Pia alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa Kamati ya Ukombozi ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika na mwenyekiti wa utayarishaji wa AOU charter.

Mwaka 1964, Kambona alifanya kazi kubwa katika kuunganisha Zanzibar na Tanganyika, akiwa pamoja na Raisi Nyerere, Raisi Karume na Waziri Kiongizi Hanga. Hii ilikuwa ni baada ya mapinduzi ya Zanzibar.

Wakati wa wanajeshi wa kikosi cha Calito walipoasi mwaka 1964 Kambona alikuwa msuluhishi mkuu kati ya serikali na wanajeshi hao. Nyerere na Kawawa walienda mafichoni Kigamboni. Baada ya siku tatu za majadiliano Kambona aliafiki kuongeza kasi ya kuwawezesha waafrika kushika hatamu jeshini.

Katika mahojiano na gazeti la Daily Telegraph la London Kambona alisema, ‘baada ya kuwatuliza wanajeshi nilikwenda kuwatafuta viongozi wengine na kuwarudisha mjini kwa kutumia Land Rover yangu’. Hatimaye maasi hayo yalidhibitiwa kabisa na majeshi ya Uingereza na Nyerere alimsifu Kambona bushara na uaminifu wake.

Tofauti kati ya Nyerere na Kambona zilianza kujitokeza baada ya maasi ya wanajeshi. Nyerere alitaka kuanzisha mfumo wa chama kimoja nchini ili kuimarisha usalama. Kambona alipinga hoja hiyo kwa maelezo kwamba mfumo huo ungezorotesha uhuru wa watu na maendeleo ya demokrasia.

Hata hivyo, Kambona alishindwa bungeni; alikataa kusaini muswada (bill). Mwaka 1967, baada ya safari ya China ya mwaka 1965, Nyerere akiwa amependezwa na mfumo wa kikomonist wa Mao, alitaka kuanzisha mfumo kama huo kwa jina la ujamaa.

Dhana ya msingi ya mfumo wa ujamaa ilikuwa ni kuwahamishia watu katika vijiji vya ujamaa na kutaifisha viwanda ana mali. Kambona hakukubaliana na utaratibu huo kwa maelezo kwamba ungeongeza umaskini na udhibiti wa serikali kwa watu.

Alijiuzulu kutoka katika serikali na Chama na hatimaye yeye na familia yake walikimbilia Kenya na kisha Uingereza ambako walipatiwa uhifadhi wa kisiasa. Mara baada ya kuondoka mali za Kambona zilichukuliwa.

Ndugu zake wawili, waliwekwa kizuizini bila ya kufikishwa mahakamani na kufungwa kwa zaidi ya miaka kumi. Wanafamilia wengine walinyanyaswa na kuwekwa kizuizini. Wengine kati yao walibambikiziwa kesi za uhaini, wakafikishwa mahakamani na kisha kufungwa na serikali.

Kati yao walikuwa Bibi Titi ambaye alipigania uhuru pamoja ana Nyerere na alikuwa kiongozi wa jumuia ya kina mama. Alikuwepo pia Michael Kamaliza ambaye alikuwa mwanaharakati wa chama cha wafanyakazi, mwanachama wa TANU na waziri.

Wengine ni pamoja na Gray Mattaka, John ana Eliya Chipaka na Prisca Chiombola. Kambona alituhumiwa kuwa kiongozi wa wahaini wakati akiwa London na alihukumiwa bila kuwapo. Watuhumiwa hatimaye walikata rufaa katika mahakama kuu ya Afrika Mashariki na wakaachiwa huru.

Hata hivyo, baadae walikamatwa na serikali na kufungwa tena. Kambona alituhumiwa kuwa aliiba pesa nyingi sana zikiwa ni mali ya umma, kitu ambacho Kambona alikataa katika taarifa yake na waandishi wa habari Septemba 6 huko London 1967.

Tuhuma hizo zilisema kuwa ‘’ Kambona amekutwa na pesa nyingi sana kama karanga alipopekuliwa katika Uwanja wa ndege Embakasi Nairobi’’ Hata hivyo Kambona katika taarifa yake kwa waandishi wa habari alikanusha kuhusika na tuhuma hizi na badala yake akaipa serikali ya Tanzania kuiomba serikali ya Kenya kutoa ukweli juu ya jambo hilo- jambo halikufanyika.

Akiwa Londoni Kambona aliishi maisha ya shida na dhiki. Katika mwaka 1982 ndugu zake Kambona na Otini Kambona walifunguliwa kutoka kizuizini baada ya juhudi za waziri mkuu wa New Zealand Robert Muldoon. Katika mwaka 1990 Kambona akiwa na matumaini makubwa ya mabadiliko ya kisiasa katika Tanzania hususani mabadiliko ya demokrasia, aliunda chama kiitwacho Tanzania Democratic Alliance.

Wakati vyama vingi vilipoanzishwa Tanzania 1992 Kambona aliomba kurudi Tanzania. Serikali ya Tanzania ilimkatalia katakata na kudai kuwa Kambona hakuwa Mtanzania. Kambona badala yake aliomba Serikali ya Uingereza kumpa pasi ya kusafiria kurudi Tanzania. Hata hivyo Serikali ya Tanzania ilitamka kwamba pamoja na kupata pasi hiyo itamweka ndani pindi atakapoingia Tanzania.

Pamoja na msimamo huo wa Serikali, Kambona alitua kwenye ardhi ya Tanzania tarehe 5 september 1992. Hakuna mamlaka iliyomkamata bwana Kambona bali alipewa miezi mitatu awe amekamilisha utata wa uraia wake. Baada ya kurudi, Tanzania aliona kuwa harakati za kuelekea kwenye demokrasia ya kweli zilikuwa zikienda kwa mwendo wa kinyonga.

Hata hivyo Kambona hakuweza kujihusisha kwa kiasi kikubwa na siasa kutokana na matatizo ya kiafya hususani shinikizo la damu. Hatimaye Oscar Kambona alifariki akiwa katika matibabu mjini London mwezi Juni 1997.

Mdogo wake Otini Kambona naye alifariki katika kipindi hichohicho kutokana na magonjwa ya moyo. Wote wawili walizikwa Tanzania, na serikali ya Tanzania iligharimia gharama zote za usafirishaji miili ya marehemu ndugu hawa.

Oscar Kambona ameacha mke na watoto wawili. Mtoto wao wa kwanza Mosi Kambona aliuawa mjini London katika mazingira ya kutatanisha. Roho ya Oscar Kambona na ndugu na jamaa wote waliotangulia MWENYEZI MUNGU aziweke pema peponi, Amin.
Duh!
 
Hata muda ungerudi nyuma msidhani ingekua tofauti. The code of conduct doesnt change
 
Asante sana....historia nzuri kuhusu Kambona...kumbe nyuma ya mafanikio ya Nyerere kulikua na watu majembe sana kama wakina Kambona na wengine..R.I.P
 
Kiukweli sifahamu kwa sababu mimi nimekijibia mtihani wa CSEE mwaka 1985 baada ya hapo sijujua chochote. Wakati nikuwa skuli sikuwahi kusoma kitabu chochote cha mwandishi Muhammed Said kwa sababu maabdishi yake hayakupitishwa kwenye ithbati ya kufundisha shule yoyote ya Tanzania!. Muhammed Said tuliyemsoma sisi ni Mzee MSA, Mohemed Said Abdullah
1.Duniani kuna watu
2.Kisima cha Giningi
3.Mke Mmoja Watume Watatu
4.Siri ya sifuri
5.Mzimu wa watu wa kale
6.Kosa la bwana msa

Paskali
Ongezea na Mwana wa Yungi Hulewa
 
Pascal,
Mimi naomba tuweke mipaka katika majadiliano yetu ili yapendeze.

Tumalize hili la historia ya TANU kisha tuje katika historia hii ya Maji
Maji na mashujaa wengine kama Sultan Abdul Rauf Songea Mbano
wa Wangoni.

Nadhani wewe unamjua kwa jina la Songea Mbano tu kama unavyomjua
Mtwa Mkwawa pia bila ya jina lake la Abdallah.
Mzee Mohamed Said
Unaona ufahari gani hao machief kuwa waislam?

Hakuna ajabu yeyote,wangeanza kuja wahindi Pwani yetu Mkwawa asingeitwa Abdallah angeitwa Vishal au Gunpreet.

Hakuna Mwafrika yeyote aliyekua Muislam/Mkristo by default, wote wamerithi tu dini za kuletewa.Waafrika tulikua na dini zetu wenyewe na kiuhalisia Misri(Kemet) ndio asili ya Ukristo hivyo basi ndio asili ya uislam pia.
 
Huenda Mwl Nyerere atakuwa ni Mwenye heri Mwenye Roho Mbaya zaid kuwahi kutokea kwny Historia ya Kanisa Afrika Mashariki Kama utatumia Maisha ya Oscar Kambona na mateso na Manyanyaso waliopewa na Mwl Nyerere katika Miaka yote ya Utawala wake !
 
Siikwepi TAA, tunapozungumzia historia ya kitu inaanzia kilipozaliwa!. Hata wewe historia yako huanzia ulipozaliwa na sio ulipotungwa!.

TANU ilizaliwa 1954 na historia hiyo safi imeandikwa kwa umahiri kabisa na Chuo cha Chama Kivukoni. Tusilazimishe historia ya wale walowezi wa Kizulu wa TAA kuwa ndio historia ya TANU, TANU ni TANU, TAA ni TAA na CCM ni CCM, kama somo ni chimbuko then ndipo tufukue makaburi ya TAA!.

Paskali
Cynical and satirical
 
kifimbo cheza aisee wakati mwingine hakuwa na shukran. mambo mengine inaweza kuwa aliadhibiwa na Mungu tu ndio maana alikufa hakuwa na furaha maishani kwasababu ya yale aliyowafanyia watz wenzake. kambona hakuwa mtu wa kumgeuka namna hiyo. na kile kweli kilikuwa kichwa cha mwanasheria, alikuwa na akili sana aisee hata katika speech zake huwezi kabisa kulinganisha na za kifimbo. kifimbo aisee alipitwa mbali na huyu jamaa.
 
Back
Top Bottom