Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Pascal,
Wala mimi sishangai kwa wewe kusema hayo uliyosema kwani hao waliokuja
kuingia TANU 1954 hapo ndipo ulipo ukomo wao wa kujua mambo mtu hawezi
kuwalaumu kwani hawakuwapo na hawajui kilikuwapo nini kabla yao.

Lakini ukienda kwa waliokuwapo na wa miaka ya 1920 watakuambia kuwa
alikuwa Dr. Aggrey ndiyo aliyempa Kleist Sykes fikra ya kuanzisha African
Association alipokuja Tanganyika 1924.

Hii ni historia na kwa mtu mwenye ubongo uliokaa vyema atataka kumjua huyu
Aggrey ni nani, katoka nchi gani na vipi alikutana na Kleist na kumpa fikra hiyo
na huyi Kleist ni nani katika historia ya uhuru wa Tanganyika?

Ikiwa ubongo wako una maradhi basi utajilazimisha uridhike na TANU bila ya
kuifahamu African Association na waasisi wake wala kujiukiza imekuwaje ndugu
wawili Abdul na Ally Sykes wote wawe waasisi wa TANU na kadi zao za ziwe
zimefuatana na kadi ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere?

Kadi no. 1 Julius Nyerere, no. 2 Ally Sykes na no. 3 Abdul Sykes na kadi
zote hizo tatu ziwe na sahihi ya Ally Sykes?

Hakika haiwezekani kuwa haya yalikuja hivi hivi pasi ya kuwa na sababu.
Waarabu wana msemo: ''Ukiijua sababu huondoka ajabu.''

Sasa ukiwa haya yote huyataki nani mwenye hasara.

Mwenye hasara utakuwa wewe unaebakia na ujinga ilhali elimu ipo wazi na
kwa kuhitimisha nukta hii chembelecho Maalim Faiza, ''Elimu bila khiyana,''
elimu ipo na ukitaka utawezakuipata bure.

Hassan Upeka aliliambia jopo la Chuo Cha Kivukoni la waandishi wa historia
ya TANU kuwa haiwezekani mkamfikia Nyerere katika TANU bila ya kupita kwa
Abdul Sykes, hiyo haitakuwa historia ya TANU.

Lakini wewe unasema historia hii ya Kivukoni ndiyo iliyokupa alama ''A'' katika
mtihani.

Sawa wala mimi sistaajabu.
Leo tuaona nchi inavyohangaika na vyeti vya kughushi.

Haya ndiyo matokeo yake.

Vyuo vyenye kughushi na shule zake na vitabu vya kughushi vitatoa ''A'' kama hiyo
yako na wala mimi sikulaumu wewe.

Itatuchukua muda kukaa vyema.

Lakini Chuo Kikuu Cha Harvard na Oxford University Press baada ya kusoma historia
ya Kleist Sykes wamemtia katika Dictionary of African Biography (DAB).

Ukipenda unaweza kusoma hapo chini ukalinganisha na historia unayoijua wewe:
Mohamed Said: KLEIST SYKES (1894 - 1949) KATIKA DICTIONARY OF AFRICAN BIOGRAPHY (DAB) OXFORD UNIVERSITY PRESS, NEW YORK

DSCN1159.JPG
Naomba unielimishe ndugu Dr. Aggrey ni nani? Maana mie nafahamu yule aliyekuwa mghana sijui kama nipo sahihi.Muelezee kwa kina.
Ile Aggrey street Kariakoo na Mnazi mmoja yamepewa jina la huyu mtu?
Iliuaje hadi amepewa mitaa Tanzania? na anaingiaje kwenye hiyo historia ya Tanganyika?
I'm humbled.
 
Naomba unielimishe ndugu Dr. Aggrey ni nani? Maana mie nafahamu yule aliyekuwa mghana sijui kama nipo sahihi.Muelezee kwa kina.
Ile Aggrey street Kariakoo na Mnazi mmoja yamepewa jina la huyu mtu?
Iliuaje hadi amepewa mitaa Tanzania? na anaingiaje kwenye hiyo historia ya Tanganyika?
I'm humbled.
Herikipaji,
Nakunyambulia habari za Dr. Aggrey kutoka katika kitabu cha Abdul Sykes:

''... alikuwa Dr James Kwegyir Aggrey, Mwafrika kutoka Ghana ndiye mtu aliyemtia Kleist hamu ya kuingia katika siasa. Dr Aggrey alikuja Tanganyika mwaka 1924. Dr Aggrey alikuwa katika Phelps-Stokes Commissions iliyokuwa imeundwa kuchunguza elimu ya Waafrika. Ilikuwa katika kipindi hiki akiwa ndani ya kamisheni hii ndipo alipokuja Tanganyika. Dr Aggrey alikataliwa kupanga New Africa Hotel kwa kuwa alikuwa mtu mweusi. Ikabidi Gavana Donald Cameron amtafutie chumba Government House ajisitiri kwa malazi. Ilikuwa wakati huu alipokuwa Dar es Salaam ndipo Dr Agrrey alipokutana na Kleist. Dr Aggrey alimtunukia Kleist moja ya vitabu vyake na akakitia sahihi yake. Hakuna hata mtoto mmoja wa Kleist ambae anakumbuka jina la kitabu hiki. Kleist alikithamini kitabu hiki na kilipamba shubaka lake la vitabu kwa miaka mingi. Mafanikio ya Dr Aggrey kama Mwafrika yalimtia moyo Kleist.

qTJb620txQRgUfv5ultB68Cno_FC_Ftjyj-cf_nX5hTgFS3cSnksF9JlJjh6KeXCD8p3gQZsVFkXMpBCwcrT1hcWsAYU9IzPoN8wAUDtHwyPm8G8tHbWWY65LZ20GPkZyFIzaQ4UrSZtp5cRTnAAY_9U7o8wAiz7rVUsSqaXLajz_j62Ve3bjbVp3ZPWswd4B77ZWXMfRUuE_dzZ_zBA8ziJwKkaHtuNyxRsX2EKteBhpB1Yequn90mVFKETIXpqXCb2fwQuSW8JUokZZYu7a1xx3wtMROi2eTq5KjXO0EkZ1U3su80J34xJFFARzTAUbK6WtiCQ1MF_6njNqBexWO43fIqqeNkRw_DElGwIlk2TReMyp8q8tIHSfD6t1vIilDTu_t0TpyuXdhAR_7U4ecZpXU6Y5BPd_Di1utftywdUtXjTmpGPy-qqN51E5c7yUMaY2USJE9v1q1Qzo5H-G18PfQa_OWzcgg2dKsHwpOjOAkJq5I3s2huol-HA81vCBZyVYR4GMSoVbEQb3CsRI0kbdOgKydeomxZp-9ebYnKiE9xcaP0nconcSwZfc-QumN09CCqIh3pViAIg0RTdKp4Xa5nGwmJVhbUm9D1xhs3LLPD8qGpzNQ=w955-h692-no


Mwaka wa 1929 Kleist na baadhi ya rafiki zake wa karibu kama Mzee bin Sudi, ambaye wazazi wake walikuwa Wamanyema kutoka Belgian Congo, Ibrahim Hamis - Mnubi ambaye baba yake alitoka Daffur nchini Sudan, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima - Mzaramo, Suleiman Majisu, Raikes Kusi, Rawson Watts na Cecil Matola - Myao kutoka Masasi walianzisha African Association, Kleist akiwa katibu muasisi. Wakati ule Gavana wa Tanganyika alikuwa Sir Donald Cameron ambae alitawala Tanganyika kuanzia mwaka wa 1925 ñ 1929. Cameron alikuwa gavana mliberali na alikuwa akifahamiana na Kleist. Cameron ndiye aliyeanzisha Baraza la Kutunga Sheria la kwanza na mfumo wa Indirect Rule katika Tanganyika. Msimamo wake huu ndiyo hasa uliochangia katika kuwezesha kunzishwa kwa African Association. Lakini juu ya haya yote, chama hiki kiliaswa kisijiingize kabisa katika siasa. Wakati chama hiki kinaanza tayari kulikuwepo na chama cha Wazungu na Waasia. Lakini katika Baraza la Kutunga Sheria Waafrika walikuwa wakiwakilishwa na padri wa Kikatoliki, Father Gibbons, ambae hakuwa hata anaishi na Waafrika bali akikaa Minaki Misheni nje ya Dar es Salaam...''
 
Ibn Hazm Bookshop Msikiti wa Mtoro na Manyema bei shs. 10,000.00 kipo kwa Kiingereza na Kiswahili.
 
Huenda Mwl Nyerere atakuwa ni Mwenye heri Mwenye Roho Mbaya zaid kuwahi kutokea kwny Historia ya Kanisa Afrika Mashariki Kama utatumia Maisha ya Oscar Kambona na mateso na Manyanyaso waliopewa na Mwl Nyerere katika Miaka yote ya Utawala wake !
Najaribu kutafuta uhusiano wa hii post yako na mjadala unaondelea naona kama nafeli.
 
Najaribu kutafuta uhusiano wa hii post yako na mjadala unaondelea naona kama nafeli.

Umeshindwa kujua Mahusiano kwa kuwa Wewe ni Mtoto!

Historia Ya Kambona haikamiliki bila ya kukumbusha Unyama aliofanyiwa na Nyerere ikiwa ni Pamoja na uzushi mwingi na Propaganda chafu alizosambaza dhidi ya Oscar na kumweka Kizuizini Mdogo wake Oscar Kambona kwa zaid ya Muongo mmoja Gerezani kisa ni Ndugu wa Mtu anaemchukia Pamoja na kutaifisha/ ku pora Mali zote ikiwa ni Pamoja na Nyumba za Kambona na za Familia yake!

Wasifu tunaozungumzia hapa Great thinkers tofautisha na vile vi CV vya page mbili vya kuombea Kazi!
 
Kama TANU ilizaliwa 1954, hapa ndipo historia ya TANU ilipoanzia. Kama Tanganyika ilipata uhuru mwaka 1961 historia ya uhuru ndipo ilipoanzia na kama CCM ilizaliwa 1977, hapa ndipo historia ya CCM ilipoanzia, kuitaja historia yoyote nyuma ya hapo ni mapambo tuu au kuremba. Historia ya kitu ni kilipoanzia not necessarily chimbuko lake. Hivyo hiyo historia ya TANU ya Kivukoni ndiyo yenyewe haswa na ndiyo inayofundishwa mashuleni na mimi ndiyo iliyonipatia alama ya A kwenye mtihani wangu wa mwisho pale Tambaza.

P.
Acha uongo,Tunapogusa historia basi iwe historia kweli sio kupapasa juu tu.Lakini nikwambie shule ya msingi inafundisha historia ya TAA isipokuwa kwa uchache
 
Umeshindwa kujua Mahusiano kwa kuwa Wewe ni Mtoto!

Historia Ya Kambona haikamiliki bila ya kukumbusha Unyama aliofanyiwa na Nyerere ikiwa ni Pamoja na uzushi mwingi na Propaganda chafu alizosambaza dhidi ya Oscar na kumweka Kizuizini Mdogo wake Oscar Kambona kwa zaid ya Muongo mmoja Gerezani kisa ni Ndugu wa Mtu anaemchukia!
Duuuuh..!
 
Kama TANU ilizaliwa 1954, hapa ndipo historia ya TANU ilipoanzia. Kama Tanganyika ilipata uhuru mwaka 1961 historia ya uhuru ndipo ilipoanzia na kama CCM ilizaliwa 1977, hapa ndipo historia ya CCM ilipoanzia, kuitaja historia yoyote nyuma ya hapo ni mapambo tuu au kuremba. Historia ya kitu ni kilipoanzia not necessarily chimbuko lake. Hivyo hiyo historia ya TANU ya Kivukoni ndiyo yenyewe haswa na ndiyo inayofundishwa mashuleni na mimi ndiyo iliyonipatia alama ya A kwenye mtihani wangu wa mwisho pale Tambaza.

P.


Kupata Alama A si lazima iwe ni uthibitisho wa Weledi wako inawezekana pia Ikawa Majibu yako yalifanana sana na Marking scheme ya Mitihani uliyofanya, Kama Marking scheme ilikuwa na Makosa lakin bado Majibu yako yakafanana na Marking scheme lazima upate Alama A.


Kusema Historia ya TANU ilianzia 1954 pale ilipozaliwa imenifanya kutafakari Kama baada ya zoezi la uhakiki wa Vyeti feki inawezekana kuanza na uhakiki wa Elimu feki?

Kama Historia ya kitu inaanza pale kilipopatikana Mf TANU ianzie 1954 kwanini Histria ya Uhuru wa Tanganyika isianzie 1961?
 
Siikwepi TAA, tunapozungumzia historia ya kitu inaanzia kilipozaliwa!. Hata wewe historia yako huanzia ulipozaliwa na sio ulipotungwa!.

TANU ilizaliwa 1954 na historia hiyo safi imeandikwa kwa umahiri kabisa na Chuo cha Chama Kivukoni. Tusilazimishe historia ya wale walowezi wa Kizulu wa TAA kuwa ndio historia ya TANU, TANU ni TANU, TAA ni TAA na CCM ni CCM, kama somo ni chimbuko then ndipo tufukue makaburi ya TAA!.

Paskali
TANU ilizaliwa mwaka 1954 Lakini haikuwa mwanzo wa TANU.TAA ndo ilizaaa TANU yaani hii ni sawa na mtoto kuzaliwa alafu hataki kujuwa historia ya wazazi wake
Paskali,
Mimi sina nguvu ya kulazimisha chochote kwako au kwa mtu yeyote awae yule.

Nilichonacho mimi ni mantiki na ukweli katika historia ya Tanganyika ambayo
nimetafiti na kuandika kitabu, na ''paper,'' kadhaa ambazo watu wamesoma
bila ya kulazimishwa.

Wala mimi sijakataa kuwa Mwalimu Nyerere ni muasisi wa TANU.

Ila ninachosema mimi ni kuwa ikiwa utaifunga akili yako ibakie hapo bila ya
kutaka kuisoma historia nzima atakaepunjika ni wewe.

Ukweli ni kuwa Nyerere haiwezekani mgeni mno afike Dar es Salaam, awe na
ofisi, awe na wanachama na aanzishe TANU huu ni sawa na muujiza.

Haiingii akilini kuwa wewe uione kadi ya TANU ya Nyerere no. 1 lakini usitake
kujua nani ana kadi no. 2, 3, 4 na kuendelea hasa kwa mtu mwenye ''A'' ya
historia.

Hili haliwezekani lakini ukipenda kuamini hivyo hakuna wa kukulazimisha vinginevyo
hasa kwa kuwa una ''A'' ya historia ya Kivukoni.

Hii maana yake ni kuwa wewe ni mjuzi.

Kuna kitu kipya umekileta kuwa African Association ni ya kina Sykes na wao hapa
si kwao kwa hiyo ni sawa kwa historia hiyo kufutwa.

Mantiki ya hoja yako inakuwa kwa kuwa hawa ni Wazulu ''watu wa kuja,'' na
wameanzisha African Association basi historia hii haitakiwi.

Hoja hii itatambaa hivyo hivyo hadi kufikia wao kuunda TANU 1954.

Katika historia ya uhuru wa Tanganyika na mwamko wa Waafrika wa Tanganyika
kupambana na ukoloni utakutana na Waafrika wengi ambao Tanganyika si kwao.

Katika hiyo African Association utakutana na Kleist Mzulu aliyezaliwa Pangani na akina
Plantan waliokuja kutoka Mozambique lakini ni Wazulu pia.

Utakutana na Ibrahim Hamisi Mnubi wa wazee wake wametokea Dafur, Sudan.

Utakutana na Erica Fiah Mganda kutoka Uganda, utakutana na Mzee bin Sudi
Mmanyema wazee wake wametokea Belgian Congo.

Hawa nimekutajia wachache tu katika historia ya kupambana na wakoloni katika
miaka ya 1920 hadi kufikia mwisho wa Vita Vya Pili 1945.

Katika hiyo TANU halikadhalika wako pia ''wakuja,'' wengi tu.

Tuanze na Patwa Muhindi, Saadan Abdul Kandoro, Mmanyema, Sheikh
Mohamed Ramiya
Mmanyema,

Dome Okochi Budohi
Mluya kutoka Kenya, Patrick Aoko Mjaluo Mkenya, Denis
Phombeah
Mnyasa kutoka Nyasaland, Iddi Faiz Mafungo Mmanyema kwa
kukutajia majina machache.

Kulikuwa na Earle Seaton kutoka Bermuda, haonekani lakini yuko aliyetiwa katika
siasa za Tanganyika na Abdul Sykes kizazi cha pili Mzulu kuzaliwa Tanganyika na
palikuwa na Mufti Sheikh Hassan bin Amir kutoka Zanzibar.

Hawa wote wana historia zao ukizisoma mwili lazima ukusisimke.

Namaliza na babu yangu Salum Abdallah, Mmanyema aliyezaliwa Shirati Musoma
aliyekuwa mmoja wa wa wapigania uhuru wa Tanganyika kuanzia 1947 na 1955
akawa Mwenyekiti muasisi wa Tanganyika Railway African Union (TRAU).

Najua haya huyajui labda kwa kuwa waandishi wa historia kutoka Kivukoni kama
wewe hawakuwa wanayajua.

Inawezekama kwa kuwa una ''A'' ya historia ya Kivukoni ukaona Dictionary of
African Biography iliyochapwa na Oxford Univeristy Press, 2011 si chochote lakini
hii ni katika rejea muhimu sana katika historia ya Afrika.
 
Nakufuatilia kwa karibu sana wewe na Pascal Mayalla
Mvaa...
Ahsante sana.

Faraja wa mwandishi yeyote yule ni kupata mrejesho kwa wasomaji wake
kuwa wanamsoma kama ulivyofanya wewe hapa.

Kabla ya kuandika kitabu cha Abdul Sykes hakuna mtu aliyenijua katika
duru ambazo unaweza kuziita za ''kisomi,'' ukipenda.

Baada ya kitabu kutoka London na kufanyiwa ''reviews,'' yaani mapitio
ya kitabu na wasomi mbalimbali ghafla nikaona nimekuwa nikitajwa na
kupata mialiko kwingi ndani na nje ya nchi.

Furaha yangu ilizidi siku nilipopekea email kutoka kwa Prof. Ali Mazrui
na siku nilipoona kitabu changu kimeandikiwa, ''review,'' na John Iliffe
katika Cambridge Journal of African History.

Yaliyobakia sasa ni historia.
 
TANU ilizaliwa mwaka 1954 Lakini haikuwa mwanzo wa TANU.TAA ndo ilizaaa TANU yaani hii ni sawa na mtoto kuzaliwa alafu hataki kujuwa historia ya wazazi wake
Forum...
Marehemu Abdul Sykes anasema yeye kumbukumbu yake ya awali kabisa ya TAA
ni kuchukuliwa na baba yake, Mzee Kleist pale New Street wakati inajengwa hiyo
ofisi ambayo ilikuja kuwa ofisi ya African Association kwa mtindo wa kujitolea kwa
wanachama wote kukusanyika pale kila Jumapili kusaidiana na mafundi katika ujenzi.

Wakati ule Abdul Sykes labda alikuwa mtoto wa umri wa miaka 9 hivi au chini ya
hapo.

Hii ilikuwa miaka ya mwanzoni 1930 na ofisi ikafunguliwa rasmi 1933.

Ukimtoa mdogo wake Ally na Tewa Said Tewa katia wale waasisi 17 wa TANU
1954 hakuna mwingine mwenye historia na kumbukumbu kama hii.
 
Mvaa...
Ahsante sana.

Faraja wa mwandishi yeyote yule ni kupata mrejesho kwa wasomaji wake
kuwa wanamsoma kama ulivyofanya wewe hapa.

Kabla ya kuandika kitabu cha Abdul Sykes hakuna mtu aliyenijua katika
duru ambazo unaweza kuziita za ''kisomi,'' ukipenda.

Baada ya kitabu kutoka London na kufanyiwa ''reviews,'' yaani mapitio
ya kitabu na wasomi mbalimbali ghafla nikaona nimekuwa nikitajwa na
kupata mialiko kwingi ndani na nje ya nchi.

Furaha yangu ilizidi siku nilipopekea email kutoka kwa Prof. Ali Mazrui
na siku nilipoona kitabu changu kimeandikiwa, ''review,'' na John Iliffe
katika Cambridge Journal of African History.

Yaliyobakia sasa ni historia.
Ok, ni kweli watu wengi wamekua wakifanya mambo mengi mazuri au mabaya lakini hawafahamiki, anaweza akabahatika jambo moja tu maishani mwake likamfanya jamii imfahamu na aweze kua maarufu, kwa mfano kiongozi wa Alshabab hakuna ambaye angemfaham angeendelea na shughuli zake za awali, lakini alipoanza kumwaga damu kwa jina la Allah hata mimi nikataka kujua chimbuko lake.
 
Ok, ni kweli watu wengi wamekua wakifanya mambo mengi mazuri au mabaya lakini hawafahamiki, anaweza akabahatika jambo moja tu maishani mwake likamfanya jamii imfahamu na aweze kua maarufu, kwa mfano kiongozi wa Alshabab hakuna ambaye angemfaham angeendelea na shughuli zake za awali, lakini alipoanza kumwaga damu kwa jina la Allah hata mimi nikataka kujua chimbuko lake.
Mvaa...
Umetoa mfano ambao mimi sijaupenda hata punje.

Post iliyopita nimeeleza vipi Abdul Sykes alivyokuwa anaijua TAA na TANU kiasi
alishuhudia kwa macho yake wakati ofisi ile ikijengwa katika miaka ya 1933.

Taarifa kama hizi na nyinginezo ambazo hakuna mtafiti yeyote kabla yangu alau
alizigusia kwa mbali ndizo zilizofanya watu wanisikilize.

Ndugu yangu katika historia kama hii unakuja na wauaji AlShabab.
Bahati mbaya iliyoje kwangu.
 
Kusema Historia ya TANU ilianzia 1954
Kama Historia ya kitu inaanza pale kilipopatikana Mf TANU ianzie 1954 kwanini Histria ya Uhuru wa Tanganyika isianzie 1961?
Mkuu Pohamba, historia ya kitu huanzia pale kilivyo anza. Historia ya uhuru inaanzia harakati za kudai uhuru. Historia ya TANU imeanzia 1964. Historia ya CCM imeanzia 1977. Historia ya Muungano imeanzia 1964. Historia ya Pohamba imeanzia siku alipozaliwa na sio alipotungwa.

Lakini kama unazungumzia chimbuko ndipo utarudi nyuma kwa chimbuko la, TANU ni TAA, Chimbuko la CCM ni Muungano wa TANU na ASP. Chimbuko la Pohamba ni Baba Pohamba na Mama Pohamba etc.

Historia ni mwanzo wa kitu not necessarily chanzo.

Paskali
 
Acha uongo,Tunapogusa historia basi iwe historia kweli sio kupapasa juu tu.Lakini nikwambie shule ya msingi inafundisha historia ya TAA isipokuwa kwa uchache
Historia ya TAA ni historia ya TAA. Historia ya TANU ni historia ya TANU na Historia ya CCM ni historia ya CCM. Labda kama unazungumzia Chimbuko, hapo utakuwa sawa kuwa chimbuko la TANU ni TAA, Chimbuko la CCM ni TANU na ASP.

Ukiuliza swali kwenye mtihani TANU ilianza lini, utajibu Tarehe 7/7/1954. Not a word more, not a word less na utapata 100% kama mimi nilivyopata.

Ukianza kuandika kikapanda kikashuka, utapata maksi kama za Bashite.

Paskali
 
Mkuu Pohamba, historia ya kitu huanzia pale kilivyo anza. Historia ya uhuru inaanzia harakati za kudai uhuru. Historia ya TANU imeanzia 1964. Historia ya CCM imeanzia 1977. Historia ya Muungano imeanzia 1964. Historia ya Pohamba imeanzia siku alipozaliwa na sio alipotungwa.

Lakini kama unazungumzia chimbuko ndipo utarudi nyuma kwa chimbuko la, TANU ni TAA, Chimbuko la CCM ni Muungano wa TANU na ASP. Chimbuko la Pohamba ni Baba Pohamba na Mama Pohamba etc.

Historia ni mwanzo wa kitu not necessarily chanzo.

Paskali

Historia ya Kitu ni Pamoja na chimbuko la hicho kitu aliekufundisha kuwa Historia ya kitu na chimbuko lake ni vitu Tofauti kakuhadaa Hata Kama alikupa A kwny Mitihani!

Ukiambiwa Utaje Historia ya Vita ya kwanza ya Dunia ukaanza kueleza kuanzia Siku ya kwanza Risasi kurushwa badala ya kuanza na Matukio yaliyopelekea hiyo vita utakuwa unajiabisha!

akikwambia umueleze History ya CCM usipotaja chimbuko lake la kutokana na ASP na TANU utakuwa umetaja Historia Pungufu!
 
Historia ya TAA ni historia ya TAA. Historia ya TANU ni historia ya TANU na Historia ya CCM ni historia ya CCM. Labda kama unazungumzia Chimbuko, hapo utakuwa sawa kuwa chimbuko la TANU ni TAA, Chimbuko la CCM ni TANU na ASP.

Ukiuliza swali kwenye mtihani TANU ilianza lini, utajibu Tarehe 7/7/1954. Not a word more, not a word less na utapata 100% kama mimi nilivyopata.

Ukianza kuandika kikapanda kikashuka, utapata maksi kama za Bashite.

Paskali
Paskali,
Ukisoma Nyaraka za Sykes kichwaa kitakuuma na utapigwa na bumbuzi kubwa
wakati mwingine kujiuliza hivi haya ninayosoma ni kweli?

Lakini ni kweli kwa kuwa ndiyo hizo nyaraka unazo mkononi unaziona, umezishika
na unazisoma.

Abdul anasema yeye kamuona baba yake na rafiki zake wakijenga ofisi ya African
Association New Street na Kariakoo Street akiwa mtoto mdogo.

Abdul anaongeza anasema baba yake alimwambia kuwa aliyekuwa anawawakilisha
Waafrika katika Legico miaka ya 1920 alikuwa Padri kutoka Misheni ya Minaki akiitwa
Father Gibbons.

Father Gibbons ndiye huyo hapo chini kwenye picha wa kwanza kushoto wa pili kulia
ni Chief Thomas Marealle na huyo mama wa kwanza waliokaa ni mke wa Chief
Marealle
:

Rq1JVX-k0KgXUcw6pMw_fSGJG_pbV64oK5WWgcL9cr3Klf738u8tfzr8W1gzKH8iHd61HnWjB1aVZ3fTcPzET-4kKcztpflVh8bwafawuSRAUPlUh7Q34DfyQlhkP_kLvtM7GYKKbUGbDemjuKR_5dqdwdWrZiQq0Y77YZ-Fqi0UV46v2Mh59eC7zDdBvQpbwHcFduBJ_5iSKgMhnNH8GN6tPwvDwgTeW6dzgngA0kcZnpoRJyrntOiA8d_jsrxsDdcY71X7lm9AHNU_zEyXbnN6SQ9EE_FWo83CS3DFGSTR9Vwg6s3o9UQyjuMa6U0_pCfvO_37XBR3bPNyqZB5a8XBGMTjGkAltDPUFQkEFulLoRo7iIHaNcJ5VbvvSKwFAdlmcxPpjLzT5RQTjbFyNxpf1147UhQZKBtfhhL6mG6nZzSL0gw78A-cCic6IEQs4Ggg-FdqTw7Vz1-V_1p7uPgBTVVbmSdDOl_nv46RxHhioybPkHUCssOvN4QC04uF_8sSoJus-Ww66w77bkvZZ8LcEy4NzWygMVEKcrJWYxf1vAiFjwRNGHvxNVfIRayIIvzqsa2U6tpHtlT2DoFF_Gw4lTT0Mm3lzoWe5E6mjWIounA9Iw=w800-h600-no


Unaendelea kupitia hizi nyaraka unakutana na barua ''handwriiten,'' za Chief Marealle
anaandikiana na Ally Sykes kuhusu harakati na uongozi wa Tanganyika itakapokuwa
huru.

Chief Marealle anaeleza fikra zake kuhusu Mwalimu Nyerere kama kiongozi na TANU
kama chama.

Ikiwa mtu hataki kuisikia historia hii basi lazima atakuwa ana lake jambo.
 
Back
Top Bottom