Na shaka sana na tabia ya baadhi ya wanaojiita "wachambuzi" jinsi wanavyoshindwa kutetea wanachokiamini kwa hoja, orodha ni ndefu sana ya maandiko ya kihistoria ya miaka ya karibuni yanaoonyesha dhahiri kutokuwa na ushahidi(Rejea ndoto ya Mwanakijiji Tanzania Daima na Udhaifu wa Maandiko ya Mohamed Said Kwenye Kitabu Kuhusu Nyakati Za Abdulawaheed Syskes).
Mara nyingi wanahistoria wetu wanapenda kutumia neno "INASEMEKANA"ambalo kimsingi halina uzito wa kimantiki bali limejengwa kiimani na kimasimulizi hivyo linakosa uhalali kwenye jamii iliyoamua kuishi kwa misingi ya kisayansi (iwe sayansi ya jamii, historia n.k)
Hoja yangu leo ni kuhusu aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanganyika na baadaye Tanzania pia katibu mkuu wa Tanu Marehemu Oscar Salathel Kambona.
Nimepitia maandiko mbalimbali, nimejaribu kuonana na watu mbalimbali (wazee) na hata baadhi ya wanataaluma ila nimekosa kupata hoja za msingi kwanini Oscar Kambona anapambwa na baadhi ya waandishi? Katika hilo nimepata simulizi zifuatazo...;
1. Haijawahi kutokea Mtanganyika/Mtanzania anayependwa kama Oscar Kambona(watu walimwiga hadi style ya nywele zake)
2.At least alikuwa Mtanganyika wa kwanza kuthubutu kumpinga Nyerere waziwazi
3.Alimwoa Miss Tanganyika wa mwaka 1960 aliitwa Flora yungalipo mpaka leo(ndoa ilifanyika Anglican catherdral London Nyerere alikwa best man wake)
4.Alikuwa anapenda sana mambo ya kizungu ndiyo maana alipokwenda nje na Nyerere, Nyerere hakupenda kumpa nafasi ya kuongea kwasababu alihofia atasifia wazungu tu mfano ziara ya Marekani kuonana na rais Kennedy 1963 Kambona alikuwa msikilizaji tu.
5.Alipokuwa Uingereza aliendeleza mashambulizi yake dhidi ya Nyerere na aliporejea Tanzania alitangaza azma yake ya kueleza maovu ya Nyerere lakini hakuthubutu(labda alikuwa hana)
6.Siri zilkuja kufichuka kuwa huko Uingereza aliishi mitaa ya hohehohe na aliishi kwa kufanya kazi za kawaida tu
HITIMISHO NA MASWALI YA MSINGI
a. Ni lini Oscar Kambona alikuwa mwandishi wa BBC? na je alikuwa na taaluma gani? na alisoma shule zipi? na vyuo gani? nchi gani?
b.Kwanini Oscar Kambona aligombana na Nyerere? ni tofauti za kiitadi au mitazamo?
c.Kati ya Oscar Kambona na Kawawa nani alikuwa bora kwenye maswala ya uongozi?
d.Je ukweli ni upi? tatizo alikuwa Nyerere au Oscar Kambona? kiini hasa ni nini?
e.Kwanini Oscar Kambona alipokufa , Kikwete akiwa waziri alienda kupokea mwili wake pale Airport? na nini kilimuua Oscar Kambona?
f.Je Oscar Kambona anastahili sifa anayopewa na baadhi ya waandishi? kwa nini? na je kwanini watanzania walikuwa wanampenda sana? na je watoto wake na mkewe (aliwahi kuwa mwenyekiti wa TADEA)wako wapi? na wanafanya nini? waingereza wanamwongeleaje Oscar Kambona?
FINALLY I WANT TO KNOW WHO IS OSACR KAMBONA? NAHISI KAMA BADO SIJAMWELEWA KIUNDANI...........! (NAWASILISHA JF)