Ukweli unaoogopwa kusemwa kuhusu bwawa la umeme la Nyerere

Ukweli unaoogopwa kusemwa kuhusu bwawa la umeme la Nyerere

mike2k

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2016
Posts
1,571
Reaction score
3,448
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme.

JNHPP itakuwa na uwezo wa kufua umeme megawati 2,100 na kuuingiza gridi ya taifa kila siku. Hatua kubwa kuelekea nchi kujitosheleza katika nishati ya umeme.

Kukamilika kwa JNHPP bila shaka utakuwa mwanzo wa kupotea kwa hisia na maneno kuwa mradi huo ulikuwa unahujumiwa usifike mwisho. Muda ni tiba thabiti.

Pamoja na kipengele hicho chanya, upo ukweli ambao si Rais Samia Suluhu Hassan wala Waziri wa Nishati, January Makamba, wanaweza kuusema.

Kwamba JNHPP ni mradi ambao hawakuwa na namna zaidi ya kuukamilisha kwa sababu waliukuta umeshakaribia nusu na tayari ulishateketeza fedha nyingi za Watanzania.

Ukweli ni kuwa mradi wa JNHPP ulikuwa uamuzi wa hovyo kuwahi kutokea. Kwanza unakuja na athari kubwa ya kimazingira. Ushauri wa wataalamu ulipuuzwa. Mradi ukajengwa kwa kulazimisha.

Karibu miti milioni tatu imekatwa. Eneo la msitu la kilometa za mraba 1,500 limeharibiwa (deforestation).

Yaani, Serikali iliamua kujenga mradi wa umeme wa maji kwa kuharibu vyanzo vya maji.

Hivi sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi. Mvua hazinyeshi. Mto Rufiji umekuwa mkavu. Je, sio athari za kuharibu msitu wa Selous.

Mtangulizi wa Rais Samia, Dk John Magufuli, alipoingia madarakani, alikuta mradi mkubwa wa gesi Mtwara. Nchi ilikuwa ina tabasamu kuelekea uchumi wa gesi.

Fedha zaidi ya Sh11 trilioni zilizotumika kujenga JNHPP, nusu yake tu ungewekezwa kwenye gesi Mtwara, sasa hivi nchi ingekuwa na umeme wa gesi, nishati ya kupikia ya gesi na kufanya mauzo ya gesi nje ya nchi. Tungeepuka janga la vita ya Ukraine na Urusi.

Umeme wa gesi ndio wa kisasa. Umeme wa maji sio wa uhakika. Ndio maana mara kwa mara nchi ikitetereka kidogo kupata mvua, umeme unakuwa shida.

Changamoto ya umeme wa maji na kukauka kwa mabwawa ya kuzalishia umeme ndio matokeo ya nchi kuingia mikataba ya hovyo ya IPTL na Richmond kwa sababu ya uhitaji wa umeme wa dharura.

Pamoja na kutambua hayo, bado Serikali ya Magufuli ikafanya uamuzi wa kujenga mradi wa umeme wa maji.

Maswali ni mengi mno, unawezaje kujenga mradi wa umeme wa maji katika nchi ambayo tayari ina gesi ya kutosha?

Kuutelekeza mradi wa gesi Mtwara, ilikuwa kumkomoa nani? Hii hulka ya Rais akiingia madarakani anatelekeza miradi ya mtangulizi wake inaumiza mno wananchi.

Ingekuwaje Rais Samia angeamua kutoendelea na JNHPP? Fedha za Watanzania zingetolewa maelezo gani? Yatolewe maelezo ya kutelekezwa gesi Mtwara na miradi mingine yote ambayo ipo njiani miaka saba sasa.

Mwisho tuhoji; miti milioni tatu iliyokatwa Msitu wa Selous kupisha mradi wa JNHPP, ilipelekwa wapi? Iliuzwa? Fedha ilikwenda wapi? Uchunguzi maalum unahitajika katika hili.

Kuna harufu kubwa ya ufisadi wa miti milioni tatu iliyokatwa Selous.

Ndimi Luqman MALOTO
1671686508562.jpg
1671686505503.jpg
 
Jifunze ku attach hizo picha vizuri.

Anyway watakuja na blaa blaa za kusema gas imeuzwa na umeme wa gas Ni ghali Sana 😂😂.

Ila Hilo bwawa ni expensive Sana kuliko uhalisia wake.Til.11 Ni Pesa nyingi Sana aisee..
WEKENI ANALYSISI ZA KITAALAMU TUONE HAPA..KAMA MAJI YAKIKOSA HATA BINADAMU WATAKUFA
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme...
Misri lile bwawa lao la kufua umeme katika mto Nile walijenga juu ya miti?. Ghana na Zimbabwe yale mabwawa makubwa walijenga kwenye hewa bila kukata miti?

Ulaya miradi mikubwa ya nyuklia wanajenga hewani? Acha kushikiwa akili we dogo
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme...
Mradi wa JNHPP upo ktk POINT OF NO RETURN BACK! Acheni maneno mengi yasiyojenga nchi. Serikali za CCM tangu Uhuru viongozi wanaongozwa na Dira ya nchi.

Marais wetu wote waliongoza kwa Dira ya nchi. Mhe. Rais Samia alishasema hakuna mradi wa kimkakati ulioanzishwa na mtangulizi wake utakwama.

Tuwe na hoja za kujenga nchi siyo porojo za uchonganishi kila siku zinakera sana. Jiandae kushuhudia Mhe. Rais akibonyeza kitufe.🙏🙏🙏
 
Jifunze ku attach hizo picha vizuri.

Anyway watakuja na blaa blaa za kusema gas imeuzwa na umeme wa gas Ni ghali Sana 😂😂.

Ila Hilo bwawa ni expensive Sana kuliko uhalisia wake.Til.11 Ni Pesa nyingi Sana aisee..
Hiyo ni kazi ya admin na mods wa JF mkuu. Wamesoma comment yako na wamerekebisha tayari
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme....
Sidhani Kama ni vibaya kuwa na sources za kutosha za kuzalisha umeme. Tatizo la gesi ya Mtwara nadhani ni zito. Zipo taarifa kwamba gesi ya Mtwara ilishauzwa for the next 25 years na ndio maana Magufuli alikuwa anainyanyapaa. Kama hii ni kweli, huu ni ufisadi wa kutisha sana. Ni kweli hata hivyo kwamba gesi ingesaidia nchi sana kupata umeme.

Kuhusu swala la Bwawa la Nyerere, sidhani kama ni mradi worthwhile, eventually it will just be a White Elephant hasa ukizingatia Climate Change. Water resources are drying up everywhere around the World and Tanzania will not be an exception. Believe me, there won't be enough water for the dam considering the Climate Change Geo-engineering terrorism going on unabated around the World. The best option would have been Geothermal power.

 
Mradi wa JNHPP upo ktk POINT OF NO RETURN BACK! Acheni maneno mengi yasiyojenga nchi. Serikali za CCM tangu Uhuru viongozi wanaongozwa na Dira ya nchi. Marais wetu wote waliongoza kwa Dira ya nchi. Mhe. Rais Samia alishasema hakuna mradi wa kimkakati ulioanzishwa na mtangulizi wake utakwama. #Tuwe na hoja za kujenga nchi siyo porojo za uchonganishi kila siku zinakera sana. Jiandae kushuhudia Mhe. Rais akibonyeza kitufe.🙏🙏🙏
Sasa hapa Kuna hoja gani ya kujenga umeiweka wewe?

Ni kweli mradi huwezi kuacha kwa Sasa lakini haiondoi ukweli kwamba Mwendazake alikosea Sana na kaisababishia Nchi hasara..

Unatumia Til.11 kuzalisha megwt 2115 na kuharibu Mamilioni ya hekta za misitu na vyanzo vya maji.

Ni akili hiyo?
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme...
Kwani umeme wa Gas Principle ni ipi? Si kuchemsha maji? Sasa kama hamna maji ya kuchemsha si sawa tu kukosa maji kwa ukame? Ile mitungi mirefu inawekwa nini?

Hydro haihitaji mitungi na kuchemsha maji, inahitaji "gravity" tu kuziendesha Turbines na umeme unawake, kipi gharama rahisi kati ya hivi viwili?

Mto au bwawa la Maji => Gravity = Turbines au
Gasi = mitungi ya maji kuchemsha mvuke halafu ukapige turbines na coolers vile vile!

Shule nzuri
 
Hii nchi bna! Now nasikia 'kuna mabadiliko ya tabia ya nchi ndio maana ememe unasumbua coz vyanzo vya maji vimekauka' sasa najiuliza hili bwawa la Nyerere wanalijengea na mvua yake au coz kama sivyo after muongo mmoja or so tutajikuta nalo maji halina tunarudi tena kwenye mgao.
 
Yaani shida ya mtoa hoja ni miti mil.3 iliyokatwa ndio isababishe mabadiliko ya tabia ya nchi duh. Hivi unajua ni kiasi gani cha misitu kinapotea kwa mwaka pasipo na manufaa yoyote ya kitaifa sembuse hiyo miti iliyokatwa kwa kujenga bwawa.

Halafu kujenga bwawa sio maji yatakauka maji yataendelea kuwepo kitakachofanyika ni control ya maji iki kuzalisha umeme si sawa na maji yanayotumika kwenye umwagiliaji yanapotea ardhini na sio kwenye kuzalisha umeme. Mtoa hoja hebu njoo na hoja za kitaalam sio siasa.
 
Kuna program za upandaji miti zaidi ya milioni 20 kila mwaka. So inaweza kureplace haraka.

Kinachofanya mvua isinyeshe ni jambo jingine ambalo wazungu hawawezi kukwambia.

Mungu asaidie Mradi huo ukamilike, lakini isiwe excuse ya kutotumia gas yetu kuketa unafuu kwa watanzania.
 
Kwani umeme wa Gas Principle ni ipi? Si kuchemsha maji? Sasa kama hamna maji ya kuchemsha si sawa tu kukosa maji kwa ukame? Ile mitungi mirefu inawekwa nini...
Bro amount ya maji yanayotumika kuzungusha turbines ni kidogo sana af inshu nyingine ni construction time in short plant ya power kwa gas ingeshakuwa imeisha af tungekuwa na uhakika wa long time coz mi cjawahi sikia eti gas powered plant imesimama coz ya ukame ila nowadays nasikia mara china wamesimamisha hydro plant yao coz ya ukame na hapa hapa kwetu nadhani unasikia kuwa now hydro plant hazitengenezi power ya kutosha coz ya ukame in short tunahitaji mabadiliko kwenye uzalishaji wa umeme either we should go solar on day and gas by night
 
Back
Top Bottom