Ukweli unaoogopwa kusemwa kuhusu bwawa la umeme la Nyerere

Ukweli unaoogopwa kusemwa kuhusu bwawa la umeme la Nyerere

Panda miti sehemu nyingine mbona tuna mapori kibao, yaani unataka wananchi tuishi maisha mafupi sababu ya miti au haujui faida za umeme??
 
Nilimpinga JPM mambo mengi ila kuna jambo moja ambalo nilikubaliana naye 100%! Ni ujenzi wa hilo Bwawa, alifanya maamuzi sahihi 100%

Hizo km za mraba 1500 ni sehemu ndogo sana kulinganisha na misitu tuliyo nayo. Ukiona watu wanapinga ujenzi wa hilo Bwawa ni kwa maslahi yao wenyewe. Wanajua kabisa umeme wao wa magenerator hawatauza tena sasa watapigia wapi hela?

Pili hiyo gas yenyewe ilishapigwa mikataba ambayo wewe mtanzania huwezi faidi chochote hapo!! Sana sana utaishia kuwafaidisha ambao wamepewa mkataba kuchimba na atakupangia bei anavyotaka yeye!! At the end umeme utauziwa juuu, gharama za uzalishaji nchini zitanenda juu, uharibifu wa uchumi utakuwa mkubwa sana

Chanzo sahihi kilikuwa ni hilo Bwawa!! Apokee kongole 👏👏huko alipo kwa hili hata kama mengi aliharibu
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme.

JNHPP itakuwa na uwezo wa kufua umeme megawati 2,100 na kuuingiza gridi ya taifa kila siku. Hatua kubwa kuelekea nchi kujitosheleza katika nishati ya umeme.

Kukamilika kwa JNHPP bila shaka utakuwa mwanzo wa kupotea kwa hisia na maneno kuwa mradi huo ulikuwa unahujumiwa usifike mwisho. Muda ni tiba thabiti.

Pamoja na kipengele hicho chanya, upo ukweli ambao si Rais Samia Suluhu Hassan wala Waziri wa Nishati, January Makamba, wanaweza kuusema.

Kwamba JNHPP ni mradi ambao hawakuwa na namna zaidi ya kuukamilisha kwa sababu waliukuta umeshakaribia nusu na tayari ulishateketeza fedha nyingi za Watanzania.

Ukweli ni kuwa mradi wa JNHPP ulikuwa uamuzi wa hovyo kuwahi kutokea. Kwanza unakuja na athari kubwa ya kimazingira. Ushauri wa wataalamu ulipuuzwa. Mradi ukajengwa kwa kulazimisha.

Karibu miti milioni tatu imekatwa. Eneo la msitu la kilometa za mraba 1,500 limeharibiwa (deforestation).

Yaani, Serikali iliamua kujenga mradi wa umeme wa maji kwa kuharibu vyanzo vya maji.

Hivi sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi. Mvua hazinyeshi. Mto Rufiji umekuwa mkavu. Je, sio athari za kuharibu msitu wa Selous.

Mtangulizi wa Rais Samia, Dk John Magufuli, alipoingia madarakani, alikuta mradi mkubwa wa gesi Mtwara. Nchi ilikuwa ina tabasamu kuelekea uchumi wa gesi.

Fedha zaidi ya Sh11 trilioni zilizotumika kujenga JNHPP, nusu yake tu ungewekezwa kwenye gesi Mtwara, sasa hivi nchi ingekuwa na umeme wa gesi, nishati ya kupikia ya gesi na kufanya mauzo ya gesi nje ya nchi. Tungeepuka janga la vita ya Ukraine na Urusi.

Umeme wa gesi ndio wa kisasa. Umeme wa maji sio wa uhakika. Ndio maana mara kwa mara nchi ikitetereka kidogo kupata mvua, umeme unakuwa shida.

Changamoto ya umeme wa maji na kukauka kwa mabwawa ya kuzalishia umeme ndio matokeo ya nchi kuingia mikataba ya hovyo ya IPTL na Richmond kwa sababu ya uhitaji wa umeme wa dharura.

Pamoja na kutambua hayo, bado Serikali ya Magufuli ikafanya uamuzi wa kujenga mradi wa umeme wa maji.

Maswali ni mengi mno, unawezaje kujenga mradi wa umeme wa maji katika nchi ambayo tayari ina gesi ya kutosha?

Kuutelekeza mradi wa gesi Mtwara, ilikuwa kumkomoa nani? Hii hulka ya Rais akiingia madarakani anatelekeza miradi ya mtangulizi wake inaumiza mno wananchi.

Ingekuwaje Rais Samia angeamua kutoendelea na JNHPP? Fedha za Watanzania zingetolewa maelezo gani? Yatolewe maelezo ya kutelekezwa gesi Mtwara na miradi mingine yote ambayo ipo njiani miaka saba sasa.

Mwisho tuhoji; miti milioni tatu iliyokatwa Msitu wa Selous kupisha mradi wa JNHPP, ilipelekwa wapi? Iliuzwa? Fedha ilikwenda wapi? Uchunguzi maalum unahitajika katika hili.

Kuna harufu kubwa ya ufisadi wa miti milioni tatu iliyokatwa Selous.

Ndimi Luqman MALOTO
View attachment 2454151View attachment 2454152
Mtoa Post wewe unaelimu Gani? Nawasiwasi naelimu yako ukianza kuhoji pesa zamiti zilienda wapi hujui kuwa nchi inaserikali? Hujui nchi inaviongozi? Hujui kuwa nchi ina hazina? Hujui kuna watoto wanasoma bure? Hujui kuna watumishi wanalipwa? Mbona hujahoji kuhusu pesa za faini za barabarani zinakoenda? Hitimisho by educationally unapaswa kuangalia hata mataifa yalio tutangulia mwaka juzi tu Ethiopia wamejenga bwawa kubwa zaidi yahili lakwetu kwani wao hawakukata miti? Au lengo lako tu umchafue magufuli? Use properly your medulla oblongata
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme.

JNHPP itakuwa na uwezo wa kufua umeme megawati 2,100 na kuuingiza gridi ya taifa kila siku. Hatua kubwa kuelekea nchi kujitosheleza katika nishati ya umeme.

Kukamilika kwa JNHPP bila shaka utakuwa mwanzo wa kupotea kwa hisia na maneno kuwa mradi huo ulikuwa unahujumiwa usifike mwisho. Muda ni tiba thabiti.

Pamoja na kipengele hicho chanya, upo ukweli ambao si Rais Samia Suluhu Hassan wala Waziri wa Nishati, January Makamba, wanaweza kuusema.

Kwamba JNHPP ni mradi ambao hawakuwa na namna zaidi ya kuukamilisha kwa sababu waliukuta umeshakaribia nusu na tayari ulishateketeza fedha nyingi za Watanzania.

Ukweli ni kuwa mradi wa JNHPP ulikuwa uamuzi wa hovyo kuwahi kutokea. Kwanza unakuja na athari kubwa ya kimazingira. Ushauri wa wataalamu ulipuuzwa. Mradi ukajengwa kwa kulazimisha.

Karibu miti milioni tatu imekatwa. Eneo la msitu la kilometa za mraba 1,500 limeharibiwa (deforestation).

Yaani, Serikali iliamua kujenga mradi wa umeme wa maji kwa kuharibu vyanzo vya maji.

Hivi sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi. Mvua hazinyeshi. Mto Rufiji umekuwa mkavu. Je, sio athari za kuharibu msitu wa Selous.

Mtangulizi wa Rais Samia, Dk John Magufuli, alipoingia madarakani, alikuta mradi mkubwa wa gesi Mtwara. Nchi ilikuwa ina tabasamu kuelekea uchumi wa gesi.

Fedha zaidi ya Sh11 trilioni zilizotumika kujenga JNHPP, nusu yake tu ungewekezwa kwenye gesi Mtwara, sasa hivi nchi ingekuwa na umeme wa gesi, nishati ya kupikia ya gesi na kufanya mauzo ya gesi nje ya nchi. Tungeepuka janga la vita ya Ukraine na Urusi.

Umeme wa gesi ndio wa kisasa. Umeme wa maji sio wa uhakika. Ndio maana mara kwa mara nchi ikitetereka kidogo kupata mvua, umeme unakuwa shida.

Changamoto ya umeme wa maji na kukauka kwa mabwawa ya kuzalishia umeme ndio matokeo ya nchi kuingia mikataba ya hovyo ya IPTL na Richmond kwa sababu ya uhitaji wa umeme wa dharura.

Pamoja na kutambua hayo, bado Serikali ya Magufuli ikafanya uamuzi wa kujenga mradi wa umeme wa maji.

Maswali ni mengi mno, unawezaje kujenga mradi wa umeme wa maji katika nchi ambayo tayari ina gesi ya kutosha?

Kuutelekeza mradi wa gesi Mtwara, ilikuwa kumkomoa nani? Hii hulka ya Rais akiingia madarakani anatelekeza miradi ya mtangulizi wake inaumiza mno wananchi.

Ingekuwaje Rais Samia angeamua kutoendelea na JNHPP? Fedha za Watanzania zingetolewa maelezo gani? Yatolewe maelezo ya kutelekezwa gesi Mtwara na miradi mingine yote ambayo ipo njiani miaka saba sasa.

Mwisho tuhoji; miti milioni tatu iliyokatwa Msitu wa Selous kupisha mradi wa JNHPP, ilipelekwa wapi? Iliuzwa? Fedha ilikwenda wapi? Uchunguzi maalum unahitajika katika hili.

Kuna harufu kubwa ya ufisadi wa miti milioni tatu iliyokatwa Selous.

Ndimi Luqman MALOTO
View attachment 2454151View attachment 2454152
Wewe ni mpuuzi na akili huna.Unadhani nchi itakaaa hivyohivyo tu miaka yote blia kuchukua maamuzi magumu.Unadhani maendeleo yanakuja kuongeaongea ?Vilaza wa mawazo halafu mnajifanya eti ni wachambuzi.Nonsense.
 
Yaani bawa lisijengwe eti kisa miti milioni tatu. Hivi unajua ni miti mingapi inakatwa kila siku kwa ajili ya matumizi ya mkaa na kuni?

Hiyo miti milioni tatu mbona inaweza kupandwa na watanzania milioni tatu kati ya watanzania milion 60 ndani ya dakika 10 tu.

Uamuzi wa kujenga bwawa uliambatana na uanzishwaji wa hifadhi ya Taifa ya Nyerere huko sio kuhifadhi mazingira?.

Bwawa likikamilika litakuwa ni makazi ya viumbe kama samaki, kiboko na mamba huku kilimo cha umwagiliaji kikuendelea huku nako sio kuhifadhi mazingira. Ukifanya assessment utagundua ujenzi wa bwawa unafaida mara 100 kuliko hasara na ndio maana JPM aliamua kujenga.
 
Mtangulizi wa Rais Samia, Dk John Magufuli, alipoingia madarakani, alikuta mradi mkubwa wa gesi Mtwara. Nchi ilikuwa ina tabasamu kuelekea uchumi wa gesi.

Fedha zaidi ya Sh11 trilioni zilizotumika kujenga JNHPP, nusu yake tu ungewekezwa kwenye gesi Mtwara, sasa hivi nchi ingekuwa na umeme wa gesi, nishati ya kupikia ya gesi na kufanya mauzo ya gesi nje ya nchi. Tungeepuka janga la vita ya Ukraine na Urusi.

Umeme wa gesi ndio wa kisasa. Umeme wa maji sio wa uhakika. Ndio maana mara kwa mara nchi ikitetereka kidogo kupata mvua, umeme unakuwa shida.
Alichokifanya Mkwere kwenye gas nacho ni uharibifu tu, hiyo gas wananufaika nayo wageni
 
Karibu miti milioni tatu imekatwa. Eneo la msitu la kilometa za mraba 1,500 limeharibiwa (deforestation).

Yaani, Serikali iliamua kujenga mradi wa umeme wa maji kwa kuharibu vyanzo vya maji.

Hivi sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi. Mvua hazinyeshi. Mto Rufiji umekuwa mkavu. Je, sio athari za kuharibu msitu wa Selous.
Toa takwimu za miti inayokatwa huko Morogoro, Pwani kwaajili ya mkaa
Athari hizi zisemwe kote
 
Yaani shida ya mtoa hoja ni miti mil.3 iliyokatwa ndio isababishe mabadiliko ya tabia ya nchi duh. Hivi unajua ni kiasi gani cha misitu kinapotea kwa mwaka pasipo na manufaa yoyote ya kitaifa sembuse hiyo miti iliyokatwa kwa kujenga bwawa.

Halafu kujenga bwawa sio maji yatakauka maji yataendelea kuwepo kitakachofanyika ni control ya maji iki kuzalisha umeme si sawa na maji yanayotumika kwenye umwagiliaji yanapotea ardhini na sio kwenye kuzalisha umeme. Mtoa hoja hebu njoo na hoja za kitaalam sio siasa.
Kwa hiyo Kwa wingi Wa watu mil.60 unategemea watapata wapi chakula bila kilimo cha umwagiliaji?

WENGI WANALAUMU BWAWA LA Mwalimu Nyerere kutokana na Chuki zao Kwa JPM na Wengine wanalisifia kutokana na mapenzi Yao Kwa CCM na Sasa Kwa Dr. Samia.
Watanzania tunaweka utaalam pembeni tunaweka mbele maslahi na Mahaba Kwa vyama na watu. Hapo ndipo kwenye tatizo kubwa. Nia ya Nyerere na JPM ilikua NZURI lakini alipaswa kuzingatia ushauri Wa Kitaalamu zaidi.Hasa Wa watu wasio na maslahi.
Baadhi ya wakuu Wa Tanesco na wizara ya Nishati kwao Tatizo la umeme ni mtaji Mkubwa sana unaowatajirisha vya kutosha. HIVYO Suala la MGAO Wa umeme ni connection ya wapigaji walioshauri na Kuunga mkono wazo hilo BILA kujali madhara mengine ya ukame ambayo hayakwepeki kutokana na MGAO Wa Mvua Kila basada ya kipindi Fulani.


Hiví hatuoni kuwa ni Binadamu wapumbavu na wasio na akili kwenye nchi yenye mito na Ardhi wanapozuia watu kutumia Maji kumwagilia mazao Yao Ili tu Maji yazalishe umeme Wa MAJI YA MGAO WA MVUA kwenye nchi yenye gesi ,joto la kutosha kuzalisha umeme Kila mkoa nchi nzima. Wakiambiwa wabinafsishe baadhi ya shughuli za Tanesco Ili waruhusu watu Binafsi wazalishe umeme kwenye shughuli Zao wanaleta kiswahili kirefu. Kuna Upepo Wa kutosha Maeneo Mengi wangewekeza hizo tril. 10 tungepata umeme Wa uhakika Kwa karne Mbele .
Umeme Wa Kale kamfereji ka Maji ka Rufiji wanataka walinganishe na mto Nile inayokusanya mito ya nchi karibu Sita KUBWA kabisa. Kale kamfereji ka Rufiji hakawezi kuwa na Maji Miaka 40 ijayo Kwa wingi Wa Watanzania wasikuwa na mpangilio Wa kimaisha unaoratibiwa na serikali. Watu wanakatazwa wasimwagilie Maji wakati huo huo idadi Yao inaongezeka Kwa Kasi ya kutisha. Mifugo inaongezeka. Ukame unaongezeka, Misitu inakatwa kuanzia Rufiji kwenyewe . Mlima Kilimanjaro unaungua moto karibu Mwezi Sasa haujazimika .

Bwawa lenye angalau Maji ya uhakika kidogo ni Nyumba ya Mungu na Hale mana Maji yake yanaanzia mlima Kilimanjaro na Ziwa Jipe. Lakini ni vibwawa vidogo sana.

Umeme Wa Maji unategemea sana mvua Sasa ,Je, Maji yatapatikana wapi kama hakuna mvua ?
Au CCM italeta mvua kwenye Ahadi zake?
Hakuna MTU anayepanda miti ya muda mrefu isiyo na faida Kila MTU analenga faida kwenye Maisha yake Binafsi.
Waliozalowa Miaka ya Sabini kuruni Nyuma wanalelewa kuwa miaka hiyo palikua na misitu mingi sana mvua zilikua ni nyingi sana Lakini watu walikua chini ya mil. 30. Kilimo kilikua sio cha Biashara. Palikua na wakulima wakubwa Wa maharage ya mpunga, Ngano na mahindi. Kwa Sasa hakuna wakulima wakubwa Bali ni wale wadogo wadogo wananyanganyana Maji ili kupata mazao ya Biashara.

Watu watavumilia njaa na ukosefu Wa Ajira Kwa muda mfupi tu Lakini HUKO mbeleni Kama serikali haitabadili mfumo wake Wa kimaisha Kwa WANANCHI Tanzania itakua kama Ethiopia ,uchumi Utakua kwenye makaratasi lakini umaskini na ukosefu Wa Ajira Utakua Mkubwa sana na uhalifu utaongezeka sana na Chuki itakua kubwa sana mana kwenye njaa hakuna AMANI . Kitakachofanyika ni Kila mmoja kuwekeza kwenye kilimo mana ndipo penye Ajira ya kumwezesha Binadamu kuishi . Hapo ni lazima miti iendelee kukatwa ,matumizi ya madawa ya kubust mazao na madawa lazima yatatumika Kwa wingi. Ongezeko la ujenzi na Miundo Mbinu Utakua ni Mkubwa sana hivyo mazingira yataharibiwa sana . Ujenzi Wa viwanda hauwezi kuyaacha mazingira Salamá HIVYO ukame hautakwepekea Miaka 20 ijayo mbele.

Kwa vyovyote Tanzania uharibifu Wa MAZINGIRA haukwepeki Kwa Sasa mana ,tunajenga miundo mbinu mingi, na makazi ya watu yanaongezeka Kiholela kutokana na Tamaa ya Kila MTU kutaka kumiliki nyumba na gari Binafsi au pikipiki. Mabetri na vifaa vingine vya kichina vingi ni Feki na vya muda mfupi vinatupwa kuharibu mazingira .

Mvua hazitanyesha za kutosha na ujenzi Wa Bwawa haukuzingatia ushauri Wa Kina Wa Kitaalamu Bali ulizingatia Moyo tu Wa Kizalendo Wa Hayati John Joseph Pombe Magufuli ( Mungu amlaze Mahali pema Peponi Kwa uzalendo wake uliokosa washauri mahiri na Wa kweli wasiojali maslahi Yao Binafsi . Wameuza miti million Tatu na kuchikichia FEDHA mifukoni mwao .

Miaka 20 ijayo Mbele patakua na ukame Kila Mahali Duniani hasa nchi zenye ongezeko kubwa la watu na wafugaji kuhamishwa kutoka Porini kwenda mijini. Wanyama wanaongezeka Porini ,watu wanaongezeka na mifugo inaongezeka,ujenzi unaongezeka,joto linaongezeka na Mafisadi wanaongezeka.

Waliosababisha Hali hiyo watakua wamezikwa ardhini na Wengine watakua hai lakini wakiwa wamezeeka.
Familia zao watafungia Tuzo zao Kwenye makabati mana zitakua ni Tuzo za janga kuu.
Tril. 10 zitakuwa zimeteketea Kwa muda mfupi BILA faida iliyokusudiwa Kwa muda mrefu kwenye mipango ya iliyoko kwenye makaratasi.
Tuzo zitageuka kuwa mjukuu Wa Tozo. Watakaoshindwa kuhamia Burundi wategeuka kuwa Bundi.

ACHENI CHAWA WAONGEZEKE KULINGANA NA UCHAFU WA MWILI.
 
Kuna program za upandaji miti zaidi ya milioni 20 kila mwaka. So inaweza kureplace haraka.

Kinachofanya mvua isinyeshe ni jambo jingine ambalo wazungu hawawezi kukwambia.

Mungu asaidie Mradi huo ukamilike, lakini isiwe excuse ya kutotumia gas yetu kuketa unafuu kwa watanzania.
Ujenzi Wa miundo mbinu na makazi yasiyo na utaratibu ni Mkubwa sana mkuu.

Kilimo cha umwagiliaji unakikwepa vipi kwenye mahitaji makubwa ya chakula Duniani na ongezeko kubwa la Watanzania Kwa Sasa mil. 61.
Miaka 20 ijayo watu watafikia mil. 80.
Miaka 80 tulikua mil. 24. Sasa mil. 60 . Unaepuka vipi uharibifu Wa MAZINGIRA kwenye nchi isiyo na ujenzi Wa makazi rasmi Kwa WANANCHI wake . Jiji la Dodoma tulitegemea lizibiti kabisa ujenzi Wa MTU Mmoja mmoja Badala yake wakaacha ujenzi holela uendelee na wakawa wanahamasisha watu Kununua viwanja. Jiji Kwa muda mfupi linakaribia Kibaigwa na Kondoa. Huo ni uharibifu Mkubwa sana Wa MAZINGIRA . Dar es Salaam inakaribia Rufiji na kuungana na Morogoro bila sababu za Msingi . Wasomi Wa Mipango miji wanajinufaisha na kuuza viwanja mara mbili mbili Wala HAWANA haja ya kuishauri serikali Namna Bora ya kulitumia Shirika la nyumba kujenga makazi Bora ya WANANCHI na kupangisha Kwa Bei nafuu. Wao nao WANALENGA kujinufaisha na ujenzi holela Ili tu waweze kumiliki nyumba nyingi za kupangisha watakapostaafu.
Hii mentality itaondokaje vichwani mwa watu bila Shirika la nyumba kujenga nyumba Bora Kwa watu Wa chini na kudhibiti ujenzi holela unaoharibu mazingira Kwa Kasi. Watu wanajenga Kila Mahali. Wanaanza kulima na ghafla panageuka makazi na ujenzi Wa vitu kama mashule ,Hospitali ,Barabara n.k unaendelea. Hiyo miti itapandwa wapi. ?
 
Nilimpinga JPM mambo mengi ila kuna jambo moja ambalo nilikubaliana naye 100%! Ni ujenzi wa hilo Bwawa, alifanya maamuzi sahihi 100%

Hizo km za mraba 1500 ni sehemu ndogo sana kulinganisha na misitu tuliyo nayo. Ukiona watu wanapinga ujenzi wa hilo Bwawa ni kwa maslahi yao wenyewe. Wanajua kabisa umeme wao wa magenerator hawatauza tena sasa watapigia wapi hela?

Pili hiyo gas yenyewe ilishapigwa mikataba ambayo wewe mtanzania huwezi faidi chochote hapo!! Sana sana utaishia kuwafaidisha ambao wamepewa mkataba kuchimba na atakupangia bei anavyotaka yeye!! At the end umeme utauziwa juuu, gharama za uzalishaji nchini zitanenda juu, uharibifu wa uchumi utakuwa mkubwa sana

Chanzo sahihi kilikuwa ni hilo Bwawa!! Apokee kongole [emoji122][emoji122]huko alipo kwa hili hata kama mengi aliharibu
Ni wale wale ndio wanaotaka umeme Wa Maji? Kumbuka kuwa Jenereta zinauzwa kutokana na MGAO Wa umeme Wa Maji Wa Mgao Wa Mvua ?
Kwa hiyo wanaoshabikia umeme Wa Maji ni wale wale wanaouza majenereta na wengi wao wako ndani ya mifumo. JK na Mtaalam Profesor Muhongo walikuja na Suluhisho la kutumia umeme Wa Gesi ,Upepo na Joto la ardhini lakini walipowaachia Wengine mfumo ulioingia ukaona utajiri walionao wenzao unakana na nini wakagundua kuwa unatokana na miradi mikubwa na Suala la mikataba ya Madini ambayo JPM alidhibiti ndio wakakumbushia wazo la Umeme Wa Maji uendelee ili Kila baada ya Miaka miwili mitatu Wanajua Mgao Wa Mvua utakuwepo na watauza majenereta na umeme wa mkataba na IPTL pesa zitaendelea kupigwa Kwa mabilioni.


Mfumo usio na Katiba ya kudhibiti Siku zote unaendeshwa Kwa Kupiga madili kwenye Kila Sekta . Wale ni watu na wanajuaa Kila anayekuja anakuja na watu wake HIVYO wasipopiga pesa nyingi watapotea kwenye Siasa na kimaslahi watakua hohehahe HIVYO wanawaza kujitafutia pesa nyingi Kwa muda mrefu. Ukiwasikiliza juu juu unaweza usielewe
 
Khs gesi ya mtwara jiwe ata hajafa alishafafanya kua ile gesi ya mtwara tuashaingia Cha kike, sio Mali yetu Tena.

Msoga na timu yake walishaingia mkataba wa kimangungo, gesi ile inchimbwa inapelekwa nje ya nchi.

Mradi wa stigler ndo lilibaki tegemeo pekee la watanzania.

JIWE ANA MABAYA YAKE, ILA KWNY GESI MNAMUONEA. ALISHALIFAFANUA Tayar
 
Acha kuongea utafikiri ulizaliwa na Magufuli by cloning. Wewe huelewi haya mambo ya long term impacts, unachoona hapa ni suluhisho la load shedding basi unasema project has long merits.

Na kama umeelewa mada, katika case kama hii huwa tunaconsider alternative sources of power generation - natural gas was the obvious option. Na kumbuka kwamba tuna miradi ya HEP ambayo iko well below generation capacity kwa sababu za diminishing of river flow rates, ambapo hata hii Nyerere HEP itakuja kuwa impacted. The fact kwamba kuna concern kuwa hata season mbili zinaweza zisijaze Nyerere dam ni kwa kuwa kuna athari katika river flow rates nchini, kutokana na climate change, uharibifu wa catchment areas na wetlands na siltation kutokana na mashamba upstream

With gas turbines unakuwa na uwezo wa kuongeza generation capacity any time you want. Kwenye Nyerere tupo capped kweye 2100MW, na sijui kama tutafikisha hiyo generation level. Tungechukua option ya gas turbines tungeanza na units za 100MW tukiongeza taratibu hata kufika 5000MW kutokana na national power demand hata na exports kupitia grid ya Southern Africa (SAPP) na hata ya East Africa.

Choosing Nyerere dam over Mtwara gas turbines was one of the many dumb things done by Magufuli. In fact leadtime ya gas turbines is way shorter than HEP ya size ya Nyerere dam. Sasa tuna gas Mtwara lakini haitatusaidia kwa kuwa yote itauzwa nje kama LNG kwa bei ambayo wala sio sisi tutakaopanga. Then people kama Magufuli walijiona wana akili sana kuliko Watanzania wengine? Incompetent fools.
Unachanya vingereza ili tujue unaongea point,kumbe mashudu matupu.

Acheni uhuni nyie,
Mradi wa gesi ya mtwara tushapigwa kitu kizito, ile gesi sio Mali yetu Tena.

Msivyo na aibu mnataka kuturudisha kulekule ili mtupige tena, hovyo kabisa[emoji3525]
 
Sehemu ilipokatwa miti kutakuwa ziwa lenye urefu wa kilomita 100. Ziwa victoria lina ukubwa wa kilomita za mraba 68,000 na eneo lote ni maji na hakuna miti lakini maeneo yanayozunguka ziwa Victoria mvua huwa inanyesha ya kutosha.

Kwahiyo hapo lilipo ziwa Victoria kulikuwa na miti wakaikata ama? Unajua nature inavyofanya kazi?
 
Lema ni seti tupu kichwani.anadhani kukusanya umume wa Solar wa kutosha na kuutia kwenye Gid ya taifa ni rahisi kama kupanda ndege kwenda Canada.Maneno ya wanasiasa yanachefua,wanajifanya wanajuaaaaaaaa ! kuliko hata wenye fani zao.
 
Huu ndiyo ikweli mchungu mike2k . Nina unerline maneno yako haya;
Ukweli ni kuwa mradi wa JNHPP ulikuwa uamuzi wa hovyo kuwahi kutokea. Kwanza unakuja na athari kubwa ya kimazingira. Ushauri wa wataalamu ulipuuzwa. Mradi ukajengwa kwa kulazimisha.

Sera ya ya magufuli katika kupumbaza watanzania ilikuwa ni "Give Dog a bad name and kill It". Magufuli aliponda kila alichofanya Kikwette kuwa kina harufu ya rushwa na kisha akapandikiza UHAYAWANI wake wa kukata miti zaidi ya Milioni 4 ya pori la akiba la Selous.
Hivi nyie wapuuzi mnajisikiaje sasa

Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom