Ukweli unaoogopwa kusemwa kuhusu bwawa la umeme la Nyerere

Ukweli unaoogopwa kusemwa kuhusu bwawa la umeme la Nyerere

LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme.

JNHPP itakuwa na uwezo wa kufua umeme megawati 2,100 na kuuingiza gridi ya taifa kila siku. Hatua kubwa kuelekea nchi kujitosheleza katika nishati ya umeme.

Kukamilika kwa JNHPP bila shaka utakuwa mwanzo wa kupotea kwa hisia na maneno kuwa mradi huo ulikuwa unahujumiwa usifike mwisho. Muda ni tiba thabiti.

Pamoja na kipengele hicho chanya, upo ukweli ambao si Rais Samia Suluhu Hassan wala Waziri wa Nishati, January Makamba, wanaweza kuusema.

Kwamba JNHPP ni mradi ambao hawakuwa na namna zaidi ya kuukamilisha kwa sababu waliukuta umeshakaribia nusu na tayari ulishateketeza fedha nyingi za Watanzania.

Ukweli ni kuwa mradi wa JNHPP ulikuwa uamuzi wa hovyo kuwahi kutokea. Kwanza unakuja na athari kubwa ya kimazingira. Ushauri wa wataalamu ulipuuzwa. Mradi ukajengwa kwa kulazimisha.

Karibu miti milioni tatu imekatwa. Eneo la msitu la kilometa za mraba 1,500 limeharibiwa (deforestation).

Yaani, Serikali iliamua kujenga mradi wa umeme wa maji kwa kuharibu vyanzo vya maji.

Hivi sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi. Mvua hazinyeshi. Mto Rufiji umekuwa mkavu. Je, sio athari za kuharibu msitu wa Selous.

Mtangulizi wa Rais Samia, Dk John Magufuli, alipoingia madarakani, alikuta mradi mkubwa wa gesi Mtwara. Nchi ilikuwa ina tabasamu kuelekea uchumi wa gesi.

Fedha zaidi ya Sh11 trilioni zilizotumika kujenga JNHPP, nusu yake tu ungewekezwa kwenye gesi Mtwara, sasa hivi nchi ingekuwa na umeme wa gesi, nishati ya kupikia ya gesi na kufanya mauzo ya gesi nje ya nchi. Tungeepuka janga la vita ya Ukraine na Urusi.

Umeme wa gesi ndio wa kisasa. Umeme wa maji sio wa uhakika. Ndio maana mara kwa mara nchi ikitetereka kidogo kupata mvua, umeme unakuwa shida.

Changamoto ya umeme wa maji na kukauka kwa mabwawa ya kuzalishia umeme ndio matokeo ya nchi kuingia mikataba ya hovyo ya IPTL na Richmond kwa sababu ya uhitaji wa umeme wa dharura.

Pamoja na kutambua hayo, bado Serikali ya Magufuli ikafanya uamuzi wa kujenga mradi wa umeme wa maji.

Maswali ni mengi mno, unawezaje kujenga mradi wa umeme wa maji katika nchi ambayo tayari ina gesi ya kutosha?

Kuutelekeza mradi wa gesi Mtwara, ilikuwa kumkomoa nani? Hii hulka ya Rais akiingia madarakani anatelekeza miradi ya mtangulizi wake inaumiza mno wananchi.

Ingekuwaje Rais Samia angeamua kutoendelea na JNHPP? Fedha za Watanzania zingetolewa maelezo gani? Yatolewe maelezo ya kutelekezwa gesi Mtwara na miradi mingine yote ambayo ipo njiani miaka saba sasa.

Mwisho tuhoji; miti milioni tatu iliyokatwa Msitu wa Selous kupisha mradi wa JNHPP, ilipelekwa wapi? Iliuzwa? Fedha ilikwenda wapi? Uchunguzi maalum unahitajika katika hili.

Kuna harufu kubwa ya ufisadi wa miti milioni tatu iliyokatwa Selous.

Ndimi Luqman MALOTO
View attachment 2454151View attachment 2454152
Correction: Ni Megawati 2,115 na sio Megawati 2,100 kama ulivyoandika.
 
Mradi wa JNHPP upo ktk POINT OF NO RETURN BACK! Acheni maneno mengi yasiyojenga nchi. Serikali za CCM tangu Uhuru viongozi wanaongozwa na Dira ya nchi.

Marais wetu wote waliongoza kwa Dira ya nchi. Mhe. Rais Samia alishasema hakuna mradi wa kimkakati ulioanzishwa na mtangulizi wake utakwama.

Tuwe na hoja za kujenga nchi siyo porojo za uchonganishi kila siku zinakera sana. Jiandae kushuhudia Mhe. Rais akibonyeza kitufe.[emoji120][emoji120][emoji120]
[emoji1361][emoji1361][emoji1361][emoji1361]
 
Kikwete alitudanganya na Gesi ya Mtwara Hadi Leo
Gesi iliyopo ni ya kupikia tu
Tusidanganyane kila kitu kina side effects zake
Bora Magufuli alithubutu Hawa wengine wametunyoa tu Wakaondoka zao
 
Mnaosema tungewekeza kwenye gas wala sipingani nanyi, ila kwa sasa busara ni kuanza na huo umeme wa maji. Hilo bwawa ukiacha kutuzalishia umeme pia litasaidia kuokoa lita nyingi za maji yanayomwagika tu baharini na kuyatumia katika shughuli nyingine za kiuchumi kama kilimo na ufugaji wa samaki. Pia, itatoa fursa ya hiyo gas ambayo tungeitumia kuzalishia umeme iende kwenye matumizi mengine ya yatakayochochea ukuaji wa uchumi. Swala la miti ni minor sana kwa hili, tufanye campaign hata tukitumia taasisi za Serikali kama shule miti mil 3 ni michache mno. Kongole kwa JPM na SAMIA kwa kufanikisha hili
Hizo lita zinazopotea ni kwa muda mfupi tu ujao mkuu,we need something sustainable.Kwa hali ya sasa ya Climate Change terrorism by Geo-engineers,Hydropower generation sio sustainable kabisa,so sio busara ku-invest kwenye Hydropower.

Kwa kiasi kikubwa gas power na geo-thermal power generation ndio sources reliable zaidi kwa kuwa zote zinatumiwa maji kidogo kwa kuwa the water is recycled.
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme.

JNHPP itakuwa na uwezo wa kufua umeme megawati 2,100 na kuuingiza gridi ya taifa kila siku. Hatua kubwa kuelekea nchi kujitosheleza katika nishati ya umeme.

Kukamilika kwa JNHPP bila shaka utakuwa mwanzo wa kupotea kwa hisia na maneno kuwa mradi huo ulikuwa unahujumiwa usifike mwisho. Muda ni tiba thabiti.

Pamoja na kipengele hicho chanya, upo ukweli ambao si Rais Samia Suluhu Hassan wala Waziri wa Nishati, January Makamba, wanaweza kuusema.

Kwamba JNHPP ni mradi ambao hawakuwa na namna zaidi ya kuukamilisha kwa sababu waliukuta umeshakaribia nusu na tayari ulishateketeza fedha nyingi za Watanzania.

Ukweli ni kuwa mradi wa JNHPP ulikuwa uamuzi wa hovyo kuwahi kutokea. Kwanza unakuja na athari kubwa ya kimazingira. Ushauri wa wataalamu ulipuuzwa. Mradi ukajengwa kwa kulazimisha.

Karibu miti milioni tatu imekatwa. Eneo la msitu la kilometa za mraba 1,500 limeharibiwa (deforestation).

Yaani, Serikali iliamua kujenga mradi wa umeme wa maji kwa kuharibu vyanzo vya maji.

Hivi sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi. Mvua hazinyeshi. Mto Rufiji umekuwa mkavu. Je, sio athari za kuharibu msitu wa Selous.

Mtangulizi wa Rais Samia, Dk John Magufuli, alipoingia madarakani, alikuta mradi mkubwa wa gesi Mtwara. Nchi ilikuwa ina tabasamu kuelekea uchumi wa gesi.

Fedha zaidi ya Sh11 trilioni zilizotumika kujenga JNHPP, nusu yake tu ungewekezwa kwenye gesi Mtwara, sasa hivi nchi ingekuwa na umeme wa gesi, nishati ya kupikia ya gesi na kufanya mauzo ya gesi nje ya nchi. Tungeepuka janga la vita ya Ukraine na Urusi.

Umeme wa gesi ndio wa kisasa. Umeme wa maji sio wa uhakika. Ndio maana mara kwa mara nchi ikitetereka kidogo kupata mvua, umeme unakuwa shida.

Changamoto ya umeme wa maji na kukauka kwa mabwawa ya kuzalishia umeme ndio matokeo ya nchi kuingia mikataba ya hovyo ya IPTL na Richmond kwa sababu ya uhitaji wa umeme wa dharura.

Pamoja na kutambua hayo, bado Serikali ya Magufuli ikafanya uamuzi wa kujenga mradi wa umeme wa maji.

Maswali ni mengi mno, unawezaje kujenga mradi wa umeme wa maji katika nchi ambayo tayari ina gesi ya kutosha?

Kuutelekeza mradi wa gesi Mtwara, ilikuwa kumkomoa nani? Hii hulka ya Rais akiingia madarakani anatelekeza miradi ya mtangulizi wake inaumiza mno wananchi.

Ingekuwaje Rais Samia angeamua kutoendelea na JNHPP? Fedha za Watanzania zingetolewa maelezo gani? Yatolewe maelezo ya kutelekezwa gesi Mtwara na miradi mingine yote ambayo ipo njiani miaka saba sasa.

Mwisho tuhoji; miti milioni tatu iliyokatwa Msitu wa Selous kupisha mradi wa JNHPP, ilipelekwa wapi? Iliuzwa? Fedha ilikwenda wapi? Uchunguzi maalum unahitajika katika hili.

Kuna harufu kubwa ya ufisadi wa miti milioni tatu iliyokatwa Selous.

Ndimi Luqman MALOTO
View attachment 2454151View attachment 2454152
Akili yako haina maarifa
 
Misri lile bwawa lao la kufua umeme katika mto Nile walijenga juu ya miti?. Ghana na Zimbabwe yale mabwawa makubwa walijenga kwenye hewa bila kukata miti?

Ulaya miradi mikubwa ya nyuklia wanajenga hewani? Acha kushikiwa akili we dogo
Unazungumzia Aswan Dam la Misri? Hiyo miti ya kukata Aswan ingetoka wapi? Unajua kuwa mpaka hivi leo faida ya huu mradi bado watu wanajiuliza? Majengo na makazi mengi ya kihistoria yalipotezwa katika huu ujenzi? Ingawa mradi umeondoa athari za mafuriko lakini vile vile umezuia rutuba zilizokuwa zinaletwa na mto Nile ( hili nalo tutaliona katika Rufiji Delta). Unajua pia kuwa asilimia 85 ya maji yanayojaza mto Nile yanatoka Blue Nile ambao unaanzia Ethiopia ambako nao wamejenga Dam yao?

Akosombo Dam limeongeza matetemeko, limepunguza rutuba down stream na hivyo kulazimisha matumizi ya mbolea ambayo imeathiri udongo, mvua imepungua na joto limeongezeka katika eneo la bwawa na magonjwa kama bilharzia na malaria yameongezeka?

Kariba Dam nayo ina matatizo kama hayo. Na mbaya zaidi kulikuwa na dalili kuwa msingi wake unaathirika na hivyo kuwepo uwezekano wa ku collapse. Na kuhusu ule umeme wa uhakika? Zimbabwe na Zambia Sasa hivi wana shida kubwa ya umeme!

Na ndio bila shaka miti ilikatwa wakati wa ujenzi wa baadhi ya mabwawa haya lakini wakati ule athari za ukataji miti ulikuwa hazijulikani kama huu wakati. Sasa hivi hatuwezi kujitetea kuwa hatukujua kuhusu athari za mabwawa makubwa. Tuliambiwa tukaleta ubishi.

Miradi ipi ya nyuklia Ulaya unayojua yamejengwa porini? Au yaliyolazimu miti mingi ikatwe kwa ajili ya ujenzi wa barabara?

Huu mradi utatuletea matatizo makubwa huko mbeleni. Huu mradi ni albatross yetu. Na hautajaa katika misimu miwili.

Amandla...
 
Ukikumbuka yaliyokuwa yanaahidiwa wakati wa mradi wa gesi, bandari ya bagamoyo, mabasi ya mwendokasi, treni ya Mwakyembe, Sullivan Summit, ugunduzi wa gesi mtwara, na mengine mengi kuhusu miradi ya namna hii inayopigiwa chapuo kuwa ni muarobaini, hutojihangaisha na hili pia. Bahati mbaya si wanasiasa au wataalamu wote lugha zao moja.
 
Mi nashangaa kila siku watu wanalilia gesi ya mtwara, magufuli kaondoka, nchi imerudishwa kwa wenyewe, endelezeni sasa mlipoishia, zalisheni hio gesi tusambaze Africa, Bado Africa ni dark continent, karibu kila nchi ina upungufu wa umeme, muombeni mchina awauzie hio gesi Kama mlivyokubaliana, tunataka umeme wa uhakika na nafuu basi
 
Unazungumzia Aswan Dam la Misri? Hiyo miti ya kukata Aswan ingetoka wapi? Unajua kuwa mpaka hivi leo faida ya huu mradi bado watu wanajiuliza? Majengo na makazi mengi ya kihistoria yalipotezwa katika huu ujenzi? Ingawa mradi umeondoa athari za mafuriko lakini vile vile umezuia rutuba zilizokuwa zinaletwa na mto Nile ( hili nalo tutaliona katika Rufiji Delta). Unajua pia kuwa asilimia 85 ya maji yanayojaza mto Nile yanatoka Blue Nile ambao unaanzia Ethiopia ambako nao wamejenga Dam yao?

Akosombo Dam limeongeza matetemeko, limepunguza rutuba down stream na hivyo kulazimisha matumizi ya mbolea ambayo imeathiri udongo, mvua imepungua na joto limeongezeka katika eneo la bwawa na magonjwa kama bilharzia na malaria yameongezeka?

Kariba Dam nayo ina matatizo kama hayo. Na mbaya zaidi kulikuwa na dalili kuwa msingi wake unaathirika na hivyo kuwepo uwezekano wa ku collapse. Na kuhusu ule umeme wa uhakika? Zimbabwe na Zambia Sasa hivi wana shida kubwa ya umeme!

Na ndio bila shaka miti ilikatwa wakati wa ujenzi wa baadhi ya mabwawa haya lakini wakati ule athari za ukataji miti ulikuwa hazijulikani kama huu wakati. Sasa hivi hatuwezi kujitetea kuwa hatukujua kuhusu athari za mabwawa makubwa. Tuliambiwa tukaleta ubishi.

Miradi ipi ya nyuklia Ulaya unayojua yamejengwa porini? Au yaliyolazimu miti mingi ikatwe kwa ajili ya ujenzi wa barabara?

Huu mradi utatuletea matatizo makubwa huko mbeleni. Huu mradi ni albatross yetu. Na hautajaa katika misimu miwili.

Amandla...
Jinyonge sasa, bwawa limeshajengwa
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme.

JNHPP itakuwa na uwezo wa kufua umeme megawati 2,100 na kuuingiza gridi ya taifa kila siku. Hatua kubwa kuelekea nchi kujitosheleza katika nishati ya umeme.

Kukamilika kwa JNHPP bila shaka utakuwa mwanzo wa kupotea kwa hisia na maneno kuwa mradi huo ulikuwa unahujumiwa usifike mwisho. Muda ni tiba thabiti.

Pamoja na kipengele hicho chanya, upo ukweli ambao si Rais Samia Suluhu Hassan wala Waziri wa Nishati, January Makamba, wanaweza kuusema.

Kwamba JNHPP ni mradi ambao hawakuwa na namna zaidi ya kuukamilisha kwa sababu waliukuta umeshakaribia nusu na tayari ulishateketeza fedha nyingi za Watanzania.

Ukweli ni kuwa mradi wa JNHPP ulikuwa uamuzi wa hovyo kuwahi kutokea. Kwanza unakuja na athari kubwa ya kimazingira. Ushauri wa wataalamu ulipuuzwa. Mradi ukajengwa kwa kulazimisha.

Karibu miti milioni tatu imekatwa. Eneo la msitu la kilometa za mraba 1,500 limeharibiwa (deforestation).

Yaani, Serikali iliamua kujenga mradi wa umeme wa maji kwa kuharibu vyanzo vya maji.

Hivi sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi. Mvua hazinyeshi. Mto Rufiji umekuwa mkavu. Je, sio athari za kuharibu msitu wa Selous.

Mtangulizi wa Rais Samia, Dk John Magufuli, alipoingia madarakani, alikuta mradi mkubwa wa gesi Mtwara. Nchi ilikuwa ina tabasamu kuelekea uchumi wa gesi.

Fedha zaidi ya Sh11 trilioni zilizotumika kujenga JNHPP, nusu yake tu ungewekezwa kwenye gesi Mtwara, sasa hivi nchi ingekuwa na umeme wa gesi, nishati ya kupikia ya gesi na kufanya mauzo ya gesi nje ya nchi. Tungeepuka janga la vita ya Ukraine na Urusi.

Umeme wa gesi ndio wa kisasa. Umeme wa maji sio wa uhakika. Ndio maana mara kwa mara nchi ikitetereka kidogo kupata mvua, umeme unakuwa shida.

Changamoto ya umeme wa maji na kukauka kwa mabwawa ya kuzalishia umeme ndio matokeo ya nchi kuingia mikataba ya hovyo ya IPTL na Richmond kwa sababu ya uhitaji wa umeme wa dharura.

Pamoja na kutambua hayo, bado Serikali ya Magufuli ikafanya uamuzi wa kujenga mradi wa umeme wa maji.

Maswali ni mengi mno, unawezaje kujenga mradi wa umeme wa maji katika nchi ambayo tayari ina gesi ya kutosha?

Kuutelekeza mradi wa gesi Mtwara, ilikuwa kumkomoa nani? Hii hulka ya Rais akiingia madarakani anatelekeza miradi ya mtangulizi wake inaumiza mno wananchi.

Ingekuwaje Rais Samia angeamua kutoendelea na JNHPP? Fedha za Watanzania zingetolewa maelezo gani? Yatolewe maelezo ya kutelekezwa gesi Mtwara na miradi mingine yote ambayo ipo njiani miaka saba sasa.

Mwisho tuhoji; miti milioni tatu iliyokatwa Msitu wa Selous kupisha mradi wa JNHPP, ilipelekwa wapi? Iliuzwa? Fedha ilikwenda wapi? Uchunguzi maalum unahitajika katika hili.

Kuna harufu kubwa ya ufisadi wa miti milioni tatu iliyokatwa Selous.

Ndimi Luqman MALOTO
View attachment 2454151View attachment 2454152
Nachelea kusema unafikiria na matako, Wewe ni aina ya viongozi ambao watapenda kuona Tanzania haipigi hatua milele katika ramani ya dunia
 
Unasubiri uambiwe na wazungu kwa nini mvua hazinyeshi?. Pole sana kizazi hiki. Hata babu zetu ambao hawakua na elimu ya kisasa wasingesubiri wazungu wawaambie.

Walikuwa na njia zao za asili za kujua vyanzo vya maji viliko na kuvihifadhi. Huyo tuliyemzika Chato mwaka jana alipkuwa anakata miti zaidi ya Milioni 4 kupisha ujenzi wa bwawa la JNHEPP mlikuwa mnamshangilia.

Sasa hivi mvua hakuna mnataka wazungu ndiyo wawasemee, poor ypu
Milion 4 tena [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
LEO Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika tukio la kujaza maji kwenye Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP). Hatua muhimu kwenda kuzalisha umeme.

JNHPP itakuwa na uwezo wa kufua umeme megawati 2,100 na kuuingiza gridi ya taifa kila siku. Hatua kubwa kuelekea nchi kujitosheleza katika nishati ya umeme.

Kukamilika kwa JNHPP bila shaka utakuwa mwanzo wa kupotea kwa hisia na maneno kuwa mradi huo ulikuwa unahujumiwa usifike mwisho. Muda ni tiba thabiti.

Pamoja na kipengele hicho chanya, upo ukweli ambao si Rais Samia Suluhu Hassan wala Waziri wa Nishati, January Makamba, wanaweza kuusema.

Kwamba JNHPP ni mradi ambao hawakuwa na namna zaidi ya kuukamilisha kwa sababu waliukuta umeshakaribia nusu na tayari ulishateketeza fedha nyingi za Watanzania.

Ukweli ni kuwa mradi wa JNHPP ulikuwa uamuzi wa hovyo kuwahi kutokea. Kwanza unakuja na athari kubwa ya kimazingira. Ushauri wa wataalamu ulipuuzwa. Mradi ukajengwa kwa kulazimisha.

Karibu miti milioni tatu imekatwa. Eneo la msitu la kilometa za mraba 1,500 limeharibiwa (deforestation).

Yaani, Serikali iliamua kujenga mradi wa umeme wa maji kwa kuharibu vyanzo vya maji.

Hivi sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi. Mvua hazinyeshi. Mto Rufiji umekuwa mkavu. Je, sio athari za kuharibu msitu wa Selous.

Mtangulizi wa Rais Samia, Dk John Magufuli, alipoingia madarakani, alikuta mradi mkubwa wa gesi Mtwara. Nchi ilikuwa ina tabasamu kuelekea uchumi wa gesi.

Fedha zaidi ya Sh11 trilioni zilizotumika kujenga JNHPP, nusu yake tu ungewekezwa kwenye gesi Mtwara, sasa hivi nchi ingekuwa na umeme wa gesi, nishati ya kupikia ya gesi na kufanya mauzo ya gesi nje ya nchi. Tungeepuka janga la vita ya Ukraine na Urusi.

Umeme wa gesi ndio wa kisasa. Umeme wa maji sio wa uhakika. Ndio maana mara kwa mara nchi ikitetereka kidogo kupata mvua, umeme unakuwa shida.

Changamoto ya umeme wa maji na kukauka kwa mabwawa ya kuzalishia umeme ndio matokeo ya nchi kuingia mikataba ya hovyo ya IPTL na Richmond kwa sababu ya uhitaji wa umeme wa dharura.

Pamoja na kutambua hayo, bado Serikali ya Magufuli ikafanya uamuzi wa kujenga mradi wa umeme wa maji.

Maswali ni mengi mno, unawezaje kujenga mradi wa umeme wa maji katika nchi ambayo tayari ina gesi ya kutosha?

Kuutelekeza mradi wa gesi Mtwara, ilikuwa kumkomoa nani? Hii hulka ya Rais akiingia madarakani anatelekeza miradi ya mtangulizi wake inaumiza mno wananchi.

Ingekuwaje Rais Samia angeamua kutoendelea na JNHPP? Fedha za Watanzania zingetolewa maelezo gani? Yatolewe maelezo ya kutelekezwa gesi Mtwara na miradi mingine yote ambayo ipo njiani miaka saba sasa.

Mwisho tuhoji; miti milioni tatu iliyokatwa Msitu wa Selous kupisha mradi wa JNHPP, ilipelekwa wapi? Iliuzwa? Fedha ilikwenda wapi? Uchunguzi maalum unahitajika katika hili.

Kuna harufu kubwa ya ufisadi wa miti milioni tatu iliyokatwa Selous.

Ndimi Luqman MALOTO
View attachment 2454151View attachment 2454152
Hiyo hesabu ya 11 Trilioni umeitolea wapi? Inaonekana aliyekulipa amekulipa mpaka za ziada.
 
Sisi hatukuwa na ulazima wa kukata miti wakati tayari tulikuwa na umeme wa gas, na bomba la gasi tayari lilikuwa hapa Dar. Mpango wa gas ilikuwa ni kuzalisha 5,000mg, kwanini tusingewekeza 3t kwenye gas kufikia hizo 2,115mg, badala yake tukaweka 11t kwenye mg chache kwa uharibifu wa mazingira?
Sehemu ilipokatwa miti kutakuwa ziwa lenye urefu wa kilomita 100. Ziwa victoria lina ukubwa wa kilomita za mraba 68,000 na eneo lote ni maji na hakuna miti lakini maeneo yanayozunguka ziwa Victoria mvua huwa inanyesha ya kutosha.
 
Mafisadi ya gesi yanapinga sana huu mradi.

Mnatudanganya na ishu ya miti wakati hata hiyo gesi haitatunufaisha kwa namna yeyote.
Kama issue ni miti kanda ya ziwa kusingenyesha mvuq kabisa maana ziwa Victoria lenye kilomita za mraba 68,000 hakuna miti ni maji lakini mvua zinanyesha kwa wingi.
 
Maji yanatoka wapi ,na hii changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi ?
Bwawa la kuhifadhi maji lina mrefu wa kilomita 100 ni kama kutokea Dar hadi Chalinze na litakuwa ziwa kubwa kuzidi ziwa Rukwa. Maji yake yakijaa yatazalisha umeme mwaka mzima bila hata mvua kunyesha kwa mwaka mzima.
 
Back
Top Bottom