1. BJP sio mtu ni chama ( tena kikubwa cha siasa )pia hili ulielewe kwanza kwahiyo ni mtazamo wa kichama vilevile ni mawazo ya wawakilishi wa vyama vya siasa , ndio maana SONIA akaamua kukaa pembeni , halafu waliomchagua sio wananchi kwa ujumla wao , bali ni wawakilishi kutoka vyama vya siasa wanaita LOKSABHA, sio suala la Raia , ndio maana mama yule kwa maslahi mapana ya nchi akaamua kukaa pembeni , wewe unaona dogo wakati limemfanya mtu asiwe PM ndipo ninapokushangaa sana , siasa za kidini na itikadi zina nguvu sana INDIA, halafu mawazo yake kukubalika na kupewa TOP JOB ni vitu viwili tofauti , huwezi kumpa top job mtu aliezaliwa huko ata kama ni muhindi ndio maana hii propaganda alishindwa kuipangua , akaamua kukaa pembeni maana ni kweli hakuwa mzaliwa wa INDIA, sasa wewe unalalamika kipi , ata Lowasa Propaganda ya ufisadi imemtesa sana japo hakuna aliethibitisha jambo hilo mahakamani, ujui wewe nguvu ya propaganda kwenye siasa kaa pembeni
2.kubembeleza ndio nini !! ndio maana nikakwambia huyu alikuwa kiongozi wa kiroho , lakini siasa ilikuwa na wenyewe wakina NEHRU , hawa katu wasingekubali kumwachia nchi Jinhah , na hili liko wazi , Gandi alitishia kuto kula lakini nani alijali , hivyo Gandi akuwa na ubavu wa kumuweka madarakani Jinnah
3.suala la kujitenga ni la kawaida sana , ata Pakistan kuna eneo linaitwa Boluchustan mpaka leo wanataka kujitenga japo nao ni waislamu , ni suala la maslahi hapa tu , mnapokaa pamoja nikawaida kufarakana , lakini hii haina maana hamuwezi ishi pamoja ndio maana mpaka leo bado WASIKH wamebaki INDIA, lakini WApakistani hawawezi kurudi INDIA maisha yao yote
4.umekubali kuwa PM muislamu hayupo , labda uniambie katika cabinet ya INDIA waislamu ni wangap ? tuanzie hapo
5. Umeona sasa unavyo payuka kijana , Hoja hapa ni dini za asili bado wahindi wamezikumbatia na zimewapa matokeo chanya , awe MUHINDU au MSIKH bado hizi zote ni asili yao , wewe ulioacha chako na kufata cha wenzako hiko ni kiherehere chako na kujipendekeza bureee