Ukweli usiosemwa juu ya dini za Kiafrika

Ukweli usiosemwa juu ya dini za Kiafrika

Mkuu
Tutakaokuelewa ni wachache sana humu, watu wengi walishafanyiwa kitu ninachookiita " kuuwawa kwa tabia zao halisi" Yaani karibu kila kitu hapa Afrika kimeharibiwa. Angalia maisha yetu, mathalani lugha zetu, mavazi yetu, sayansi yetu, dini zetu, usomaji wetu, majina yetu n.k hadi unajiuliza hivi sisi watu weusi tutaacha alama gani hapa duniani!!!???

Kuna jamaa mmoja nilimponda tukiwa wengi kwa kumwita mtoto wake mchanga jina la kiingereza la ajabu ajabu kisa tu eti ni zuri (si ni la kizungu bwana) nilipomwambia kuwa asiendekeze utumwa wa fikra aliniita mimi mshamba yaani akasema sijaelemika! Nikamtazamaaaa, nikamwambia waziwazi mimi naitwa TATA MKURIA na najisikia fahari kuwaita watoto wangu majina yao kama Bhoke, Ghati,Marwa, Mwita n.k.

Mkuu Frustration hakuna bara linadharauliwa kidini kama Afrika! Yaani ni aibu, halafu waafrika hawa wa sasa tena wasomi wanaendelea kuwatumikia wale jamaa wakidhani wapo sahihi yaani waafrika tumeenda hatua zaidi ya wao kujiona hizi dini zao ni bora sana hadi zinatugombanisha! Zinafanya tuuwane! Ni aibu.

Ukienda mabara mengine, huwaambii kitu kuhusu dini zao! Kama hujui nenda nchi za Ulaya, nenda nchi za Uarabuni, nenda Uhindini, nk. Ila sasa njoo Afrika! Yaani akili zetu ni nyepesi nyepesi mno. Kila kitu kinaaminika kirahisi tu, tumesoma sasa lakini bado tunaendekeza yale yale yaliyotuletea madhila siku za nyuma. Tumelala fofofo tunadhani kila kitu kipo sawa. Yaani hadi nimewakumbuka Prof Ngugi wa Thiong'o na maelekezo yake katika kitabu cha "Decolonizing the Mind" pamoja na Okoth p'Bitek na vile vitabu vyake pendwa (najua wengi mlisoma kile maarufu Song of Lawino na Song of Ocol) hawa waafrika wenzetu wametuandikia tushtuke kidogo lakini bado tupo ziii!

Wale wenzangu wanaopenda dini zetu, tuendelee nazo ingawa tunaitwa washirikina mi nasema ni sawa tu nitaendelea kutambika ila siyo kwa kafara za watu kama hawa washenzi wa baadhi ya dini hizi za kisasa wanavyofanya!

Najua tupo wengi tu ingawa makanisani na misikitini pia tunaingia mara kwa mara ila mioyoni mwetu tunaujua ukweli na pia tumeisha enda wapi na wapi kupata tiba zetu za kujikinga na mabalaa. Ukituona kwa nje tuna heshima lukuki katika jamii ila kiundani tunaamini dini za Kiafrika kimya kimya.

Tata mkuria.
kuna sababu kwanini imani za kiafrika hazikuwa na nguvu, nazo ni;

1) hazikuwa zikijitambua kama dini, kila kabila liliamini mizimu ya mababu zao kuwa iliwaunganisha na mungu (ni kama saints ktk ukatoliki), hivyo kila kabila na kila mtu alitegemea mababu zake, hakuna aliyeamini mababu wa wezake wangeweza kumsaidia

hiyo ikapelekea kujengeka kwa utamaduni wa kutotafuta wafuasi na waumini, (wakati uislamu na ukristo ni imani zinazotamani dunia nzima wafuate imani hizo)

hiyo ilipelekea kutokuwa na umoja miongoni mwa waafrika maana ilikuwa mtu akiacha kuamini mababu zake ama jamii nzima ikiacha kuamini mizimu ya mababu haikuwa ikionekana kama tatizo kwa wengine ambao wao hawakuona kitisho katika idadi yao, maana wao wakijiona hawahusiki na kuamuni mababu wa wezao , lilikuwa jambo lisilowahusu, hivyo hawakupinga ushawishi wa wamishionari katika kuwabadili waafrika wezao kufuata imani zisizo za kiafrika ( tofauti na ilivyo kusambaza dini mpya huko asia ama ulaya, ni kazi ngumu kila muumini hapendi kusikia wezie wa imani moja wana imani mpya, wao wana hamu dunia nzima waamini chao wao)

pia sie hatuna scriptures, wezenu wana bibbles, qurani, wahindu wana veda, pia wana makanisa, misikitu, temples nk

sisi hatuna

wezetu wana sikukuu zao sie hatuna

wezetu wana siku za ibada sie hatuna

wana miezi ya mfungo, japokuwa unaweza kudharau funga za waja kipindi cha mifungo ila huo huwa ni muda wa kuwakumbusha imani yao, mavazi nk, hivyo kuzidi kuwasimika na identity ya umani yao, kitu hicho afrika pia hatuna

halafu dini zetu zilikuwa ni za sababu maalum, huna mtoto, kuna magonjwa na vifo ndio unaenda kuabudu sio kwenda kuabudu kila jpili ama kila ijumaa

zilikuwa ni imani zisizoeleweka na viongizi wa dini hawakuwa na elimu hiyo ilipelekea kutumia vitisho na kutishatisha kuimarisha taswira zao. plus mambo ya kafara na uchawi, imani hazikueleweka zikaachwa
 
ila sidhani kama ni tatizo, imani za kiafrika ni historia na zitabaki kwenye historia , sasa hivi tuna imani mpya za kigeni ila haimaanishi na uafrika umefia hapo
 
Kama wezee walipinga hizi dini na wajukuu zao kwa kupewa mashati wakazikubali,basi na ss vitukuu tunaweza kuzikataa pia. Kama vipi waende huko Asia wakafanye dini hizi na kama kweli wapo sahihi. 4% Christian, 3% Muslims na hawa sio wote ambao kwa mafundisho yao wataenda sijui peponi mara mbinguni. Jamani kwa hyo 97% to go in hell, how crazy it's? Basi nitamlaumu huyo mungu kwa nn aliniumba akijua naenda kuzaliwa sehemu ya Buddha,Hindu,Masai, etc.
Fact
 
ila sidhani kama ni tatizo, imani za kiafrika ni historia na zitabaki kwenye historia , sasa hivi tuna imani mpya za kigeni ila haimaanishi na uafrika umefia hapo
Kabisa na kuna haja ya dhati kufanya kitu ili kurudisha asili yetu.
 
kuna sababu kwanini imani za kiafrika hazikuwa na nguvu, nazo ni;
1) hazikuwa zikijitambua kama dini, kila kabila liliamini mizimu ya mababu zao kuwa iliwaunganisha na mungu (ni kama saints ktk ukatoliki), hivyo kila kabila na kila mtu alitegemea mababu zake, hakuna aliyeamini mababu wa wezake wangeweza kumsaidia
hiyo ikapelekea kujengeka kwa utamaduni wa kutotafuta wafuasi na waumini, (wakati uislamu na ukristo ni imani zinazotamani dunia nzima wafuate imani hizo)
hiyo ilipelekea kutokuwa na umoja miongoni mwa waafrika maana ilikuwa mtu akiacha kuamini mababu zake ama jamii nzima ikiacha kuamini mizimu ya mababu haikuwa ikionekana kama tatizo kwa wengine ambao wao hawakuona kitisho katika idadi yao, maana wao wakijiona hawahusiki na kuamuni mababu wa wezao , lilikuwa jambo lisilowahusu, hivyo hawakupinga ushawishi wa wamishionari katika kuwabadili waafrika wezao kufuata imani zisizo za kiafrika ( tofauti na ilivyo kusambaza dini mpya huko asia ama ulaya, ni kazi ngumu kila muumini hapendi kusikia wezie wa imani moja wana imani mpya, wao wana hamu dunia nzima waamini chao wao)
pia sie hatuna scriptures, wezenu wana bibbles, qurani, wahindu wana veda, pia wana makanisa, misikitu, temples nk
sisi hatuna
wezetu wana sikukuu zao sie hatuna
wezetu wana siku za ibada sie hatuna
wana miezi ya mfungo, japokuwa unaweza kudharau funga za waja kipindi cha mifungo ila huo huwa ni muda wa kuwakumbusha imani yao, mavazi nk, hivyo kuzidi kuwasimika na identity ya umani yao, kitu hicho afrika pia hatuna
halafu dini zetu zilikuwa ni za sababu maalum, huna mtoto, kuna magonjwa na vifo ndio unaenda kuabudu sio kwenda kuabudu kila jpili ama kila ijumaa
zilikuwa ni imani zisizoeleweka na viongizi wa dini hawakuwa na elimu hiyo ilipelekea kutumia vitisho na kutishatisha kuimarisha taswira zao. plus mambo ya kafara na uchawi, imani hazikueleweka zikaachwa
Imani ya kiafrika ilikuwa haimtegemei sana mtu fulani ili kuwaongoza mfano wa shehe au askofu. Na hii ilisaidia hakuna upigaji katika dini zetu na wala ubabaishaji kama ilivyo Sasa kwa dini za wazungu. Suala la kuunganisha kuwa kitu kimoja labda kwa kipindi hicho haikuwa na sababu sababu kila mtu alikuwa anaamini na hakukuwa na ushawishi ili watu wafuate dini. K
 
Mkuu Frustration hata mzungu alikuwa na dini yake ya asili lakini alipopelekewa ukristo aliupokea na akazipiga chini dini zake za asili za kipuuzi kabisa.
Sio kweli ndg, America na Ulaya ni influence ya dola la Roma ndio maana kuna makanisa mengi. Kama tawala ilibariki na kulazimisha watu kwa nguvu kuingia,hii ni sawa na tulivyofanyiwa Afrika kwa wakati huo. Utofauti ni kwamba Africa tulilazimishwa na wageni ila wenzetu walilazimishwa na viongozi wao wenye mamlaka.
 
Watu wanapokutana wanakutanisha pia na tamaduni zao.
Tamaduni zinapo kutana zinaanza kujishindanisha zenyewe.
Zinapojishindanisha, kama ilivyo katika Nadharia ya Evolution of Nature, mkubwa anamla mdogo.
Mwenye nguvu anasimama na Dhaifu anakufa.
Dini za Makabila ya Kiafrika zilikuwa Dhaifu.
Zilishindwa Kuhimili ushindani, zikafa.

Yako wapi Maandiko ya hizo dini za Kiafrika ?

Yako wapi maandiko ya Manabii wa Kafrika kama Nabii Ng'wanamalundi ?

Yako wapi Mafundisho ya Miungu yao ?

Kama miungu inashindwa kuyalinda mafundisho yake, na Manabii wake basi hakika miungu hiyo ni dhaifu Sana.
 
Watu wanapokutana wanakutanisha pia na tamaduni zao.
Tamaduni zinapo kutana zinaanza kujishindanisha zenyewe.
Zinapojishindanisha, kama ilivyo katika Nadharia ya Evolution of Nature, mkubwa anamla mdogo.
Mwenye nguvu anasimama na Dhaifu anakufa.
Dini za Makabila ya Kiafrika zilikuwa Dhaifu.
Zilishindwa Kuhimili ushindani, zikafa.
Yako wapi Maandiko ya hizo dini za Kiafrika ?
Yako wapi maandiko ya Manabii wa Kafrika kama Nabii Ng'wanamalundi ?
Yako wapi Mafundisho ya Miungu yao ?
Kama miungu inashindwa kuyalinda mafundisho yake, na Manabii wake basi hakika miungu hiyo ni dhaifu Sana.
Kwanza Afrika technology ya kuandika na kusoma ilichelewa sana ila uwezo wa kuhifadhi kwa kumbukumbu mambo yao walifanikisha sana. Wao hawakushindinisha bali walipiga ban dini zote za Afrika na wao ndio watawala na viongozi wa wakati huo.

Kizazi cha kwanza ambacho wazungu walikikuta hakikukubali na kilikataa dini za wazungu na katika hili walikuwa tayari kuteswa. Na waliteseka sana,i.e kutengwa,kunyanyaswa,kutokubalika,kudharauliwa na hata waafrika wenzao waliojipendekeza na kujiona nao wazungu pia.

Baada ya mda fulani hali ya kuona chochote anachofanya mzungu kipo sahihi na kuwafanya kama semi-gods. Walitamani na hao wajue na wafanye kama wazungu walivyo na ukizingatia uduni wa mwafrika ilipelekea kuiga kila kitu.

Dini zetu hazikupendwa kwa kuwa waafrika walipenda zaidi tamaduni za mzungu kwakuwa tu kwa wakati huo alikuwa mtawala na superstar.
 
Mkuu Frustration hata mzungu alikuwa na dini yake ya asili lakini alipopelekewa ukristo aliupokea na akazipiga chini dini zake za asili za kipuuzi kabisa.
Kunaukweli unaongea ila amini mzungu alichukua vingine vya kipagani alivyokua navyo akavichanganya na huo ukristo kwa manufaa yake. Na ndio maana sasa hivi anatumia haki za binaadamu kuhalalisha upuuzi wake na kuuchanganya na huo huo ukristo. Kwanza mazungu yameanza kuuacha ukristo umebaki umotivational speaker na sio michongo ya kiroho ya vipofu wanaona na viwete wanaenda. Wahindu ni wapuuzi, Mabudha je?
 
Kule Afrika Kusini wameanzisha 'movement' ya kuenzi dini na utamaduni za kale za kiafrika, inaitwa UBUNTU. Lengo ni kuishi kwenye mila, desturi na utamaduni za kiafrika. Ubuntu ni sawa na Utu kwenye kiswahili, kwa hiyo wanazingatia sana heshima ya binadamu na fundisho kuu ni kuishi kwa upendo. Watu wengi wanashangilia Ubuntu yao, na huku bado wamebaki wakristo. Desturi zote za kuiga mila na utamaduni za wazungu wanakataa na wanapenda kuishi kwa desturi za mababu zao. Pengine huu Ubuntu tukifanyia kazi inaweza kua dina la kiafrika???
 
Kule Afrika Kusini wameanzisha 'movement' ya kuenzi dini na utamaduni za kale za kiafrika, inaitwa UBUNTU. Lengo ni kuishi kwenye mila, desturi na utamaduni za kiafrika. Ubuntu ni sawa na Utu kwenye kiswahili, kwa hiyo wanazingatia sana heshima ya binadamu na fundisho kuu ni kuishi kwa upendo. Watu wengi wanashangilia Ubuntu yao, na huko bado wamebaki wakristo. Desturi zote za kuiga mila na utamaduni za wazungu wanakataa na wanapenda kuishi kwa desturi za mababu zao. Pengine huu Ubuntu tukifanyia kazi inaweza kua dina la kiafrika???
Nilikuwa sijui kama SA wameanza harakati hizi,soon nashuka Madiba
 
Sema mm namjua mola wa Asia kwa masimulizi ya vitabu vyao. Yaani ww umjue Mungu na nikikuuliza yupo vipi na anataka nn huwezi nijibu. Unajifariji tu kusema unamjua hapo ndugu umejificha kwenye kichaka cha karanga kuzani huonikani.
Mkuu huyo jama labda humjui..
Kwake lugha bora ni kiarabu.
Watu bora waarabu.
Dini bora, islam.

Yaani humu jamvini watu wanamjua sana, kila uzi anataka amtangaze allah.
Anapinga dini za asili za kiafriaka lakni ukigusa upande wa allah na Islam atakushushua knoma.

Binafsi nilishaga achana na mambo za dini lakni ni bora nikasapot vya kwetu, na sio vya kigenj.
 
huu ni uchochezi wa kidini..nasubiri wiki ianze nikufungulie mashitaka
 
Mkuu huyo jama labda humjui..
Kwake lugha bora ni kiarabu.
Watu bora waarabu.
Dini bora, islam.
Yaani humu jamvini watu wanamjua sana, kila uzi anataka amtangaze allah.
Anapinga dini za asili za kiafriaka lakni ukigusa upande wa allah na Islam atakushushua knoma.
Binafsi nilishaga achana na mambo za dini lakni ni bora nikasapot vya kwetu, na sio vya kigenj.
Upo sahihi Sana, watu wanatupa utu 4 granted.
 
huu ni uchochezi wa kidini..nasubiri wiki ianze nikufungulie mashitaka
Mashtaka Gani Tena? Mje na Dini ya wenzako na mm nafika na Dini ya kwetu Kwa hoja na tushindanishe na tuone Nani AMEJISALITI MWENYEWE.
 
Back
Top Bottom