Ukweli usiosemwa juu ya dini za Kiafrika

Ukweli usiosemwa juu ya dini za Kiafrika

Wafuasi wa biblia kwa zama tofauti walikuwa wanajikumbusha na kuanza mianzo mipya.
Wayahudi walikuwa wanarejea maandiko ya mababu wa karne huko na kuamua kubadilika kabisa kiasi cha kuwa tayari kuua, kufukuza na kuharibu.
Sisi mpaka sasa hatuna hata hizo rejea. Hatujui kuelezea namna walivyokuwa wanatunza kumbukumbu kama walikuwa wanatunza.
Tumechanganyika sana.
Mfano. Mimi ni kizazi cha tatu cha mchanganyiko wa makabila na nikijaliwa watoto watakuwa kizazi cha nne.
Tunamfukuza nani? Tunafuata dini ya kabila gani maana hakuna hata fununu za dini iliyohusisha makabila kadhaa. Tunafuata utamaduni wa kabila gani.
Halafu hili sio sisi tu. Wazungu nao walikuwa na jamii ndogo ndogo ambazo zinaendelea kumezwa na jamii kubwa. Kuendekeza kwamba ndio chanzo cha matatizo yetu basi kinamna fulani tunakuwa tumepotoka.
Kama tunaacha labda tufanye walosema hakuna Mungu wakakomaa na maisha halafu pole pole wanaanza kulinda dini za kifamilia kama wachina. Pengine baadaye zitajirudi tena.
Tutakuwa na vitabu vingi vingi mfano kusini karibia makabila yote wanafanana mf, ngoni kwa ruvuma kitabu kimoja kaskazini ni wasukuma na pacha wao kitabu kimoja, hivi kidogokidogo hadi tunatengeneza kitabu chetu kimoja mithili ya bible na qur'an
 
Naomba unipe uongo wa kwenye Qur'aan hata mmoja tu.
Mkuu Zurri naomba usitoke kwenye mada husika, mada ipo wazi kabisa yaani tuangazie ukweli usiosemwa kuhusu dini za Afrika! Hapa hatushindanishi vitabu vya kidini ila tunataka tuthibitishe ukweli uliopewa kisogo juu ya dini za Afrika. Pia hatupo kumlazimisha mtu akubaliane na sisi juu ya uzuri wa dini za Afrika ila tunashawishi kwa hoja ili Waafrika waamue wenyewe na pia tunaheshimu mawazo ya wakuu wote.
 
Mkuu Zurri naomba usitoke kwenye mada husika, mada ipo wazi kabisa yaani tuangazie ukweli usiosemwa kuhusu dini za Afrika! Hapa hatushindanishi vitabu vya kidini ila tunataka tuthibitishe ukweli uliopewa kisogo juu ya dini za Afrika. Pia hatupo kumlazimisha mtu akubaliane na sisi juu ya uzuri wa dini za Afrika ila tunashawishi kwa hoja ili Waafrika waamue wenyewe na pia tunaheshimu mawazo ya wakuu wote.

Hii pia iko ndani ya mada sababu huwezi kusema Qur'aan bila kuzungumzia dini. Kadhalika hatuwezi kufumbia macho uovu.
 
Africa tumewahi kuwa na Sayansi gani yenye tija?
Mkuu
Tutakaokuelewa ni wachache sana humu, watu wengi walishafanyiwa kitu ninachookiita " kuuwawa kwa tabia zao halisi" Yaani karibu kila kitu hapa Afrika kimeharibiwa. Angalia maisha yetu, mathalani lugha zetu, mavazi yetu, sayansi yetu, dini zetu, usomaji wetu, majina yetu n.k hadi unajiuliza hivi sisi watu weusi tutaacha alama gani hapa duniani!!!???

Kuna jamaa mmoja nilimponda tukiwa wengi kwa kumwita mtoto wake mchanga jina la kiingereza la ajabu ajabu kisa tu eti ni zuri (si ni la kizungu bwana) nilipomwambia kuwa asiendekeze utumwa wa fikra aliniita mimi mshamba yaani akasema sijaelemika! Nikamtazamaaaa, nikamwambia waziwazi mimi naitwa TATA MKURIA na najisikia fahari kuwaita watoto wangu majina yao kama Bhoke, Ghati,Marwa, Mwita n.k.

Mkuu Frustration hakuna bara linadharauliwa kidini kama Afrika! Yaani ni aibu, halafu waafrika hawa wa sasa tena wasomi wanaendelea kuwatumikia wale jamaa wakidhani wapo sahihi yaani waafrika tumeenda hatua zaidi ya wao kujiona hizi dini zao ni bora sana hadi zinatugombanisha! Zinafanya tuuwane! Ni aibu.

Ukienda mabara mengine, huwaambii kitu kuhusu dini zao! Kama hujui nenda nchi za Ulaya, nenda nchi za Uarabuni, nenda Uhindini, nk. Ila sasa njoo Afrika! Yaani akili zetu ni nyepesi nyepesi mno. Kila kitu kinaaminika kirahisi tu, tumesoma sasa lakini bado tunaendekeza yale yale yaliyotuletea madhila siku za nyuma. Tumelala fofofo tunadhani kila kitu kipo sawa. Yaani hadi nimewakumbuka Prof Ngugi wa Thiong'o na maelekezo yake katika kitabu cha "Decolonizing the Mind" pamoja na Okoth p'Bitek na vile vitabu vyake pendwa (najua wengi mlisoma kile maarufu Song of Lawino na Song of Ocol) hawa waafrika wenzetu wametuandikia tushtuke kidogo lakini bado tupo ziii!

Wale wenzangu wanaopenda dini zetu, tuendelee nazo ingawa tunaitwa washirikina mi nasema ni sawa tu nitaendelea kutambika ila siyo kwa kafara za watu kama hawa washenzi wa baadhi ya dini hizi za kisasa wanavyofanya!

Najua tupo wengi tu ingawa makanisani na misikitini pia tunaingia mara kwa mara ila mioyoni mwetu tunaujua ukweli na pia tumeisha enda wapi na wapi kupata tiba zetu za kujikinga na mabalaa. Ukituona kwa nje tuna heshima lukuki katika jamii ila kiundani tunaamini dini za Kiafrika kimya kimya.

Tata mkuria.
 
Hii pia iko ndani ya mada sababu huwezi kusema Qur'aan bila kuzungumzia dini. Kadhalika hatuwezi kufumbia macho uovu.
Sawa mkuu
Ninachomaanisha hapa ni kuruhusu watu wawe na mawazo huru, sipo kudharau dini ya mtu naheshimu dini zao kwani ni sahihi kwa mazingira yao. Ninachotetea ni dhana ya kuwa na utambulisho rasmi wa dini za kiafrika. Ili ikifika siku na waafrika tuape kwa namna yetu si kwa kutumia vitabu vya kigeni na miungu ya kigeni.
 
Bado hatujachelewa tunaweza kuanzisha dini yetu , Kwanza hawa wanaojiita manabii wanapotosha sana watu kwa kutumia dini za kizungu.Wanatuchanganya sana, majina yenyewe wametupa ya kizungu .Kizazi cha baadae kitatushangaa sana!!! Nafikiria tu kipindi mvua zilipogoma watu huwa wanaenda kuomba mvua kwenye sehemu ya miti mikubwa au milima na mvua zinanyesha . Tuwe na dini yetu, ukombozi wa kweli wa fikra kwa Waafrika.
 
Mkuu Tata, hata hao wazungu unaowalaumu walikua na dini zao kama ambavyo wafrika wanavyodai wana dini yao. Lakini swali la kujiuliza: je, ni dini ipi ya wafrika ambayo wafrika wanadai ni yao, ambayo wazungu hawakuwa nayo?
Kwa hakika hakuna dini kwa maana ya Mungu au miungu ambayo wafrika wanasema ni yao ambayo wazungu hawajakuwa nayo. Hakuna!
Kama ni dini za uongo-miungu, wazungu ndiyo wameanza.
Kilichopo leo Afrika, ambacho wafrika wanadai kuwa ni dini yao na kuitumikia ni uongo. Kama ilivyo kwa wafrika nyakati zetu na hata mababu zetu waliotutangulia walikataa ukristo kwa uongo huo wa kuwa tuna dini yetu. Hata wazungu walikataa ukristo kwa madai, dhana na upotofu kama huu huu tulionao Afrika.
Shida kubwa ya Afrika ni elimu. Wafrika hatujawa na elimu. Hatuelewi dini ni nini, inaundwa na mini na ina sifa gani. Lakini pia wafrika siyo tu kwamba hatujaweza kuandika historia ya maisha ya vizazi vyetu, lakini hatuna elimu ya historia ya ulimwengu na mwanadamu.
Sasa kama hatuna tu elimu na uelewa wa jambo dogo la historia ya ulimwengu na maisha ya mwanadamu yalivyoanza itawezekanaje kwa jambo kama dini?
Tukisema Elimu tunaweza rudi kwenye njia ile ile ya KIMFUMO ambao uasisi wake ni kutoka kwa hao hao Wazungu, LABDA TUSEME TATIZO LIPO KWENYE UFAHAMU UNAOPELEKEA KUJUA (na hasa kuujua UKWELI WENYEWE KUTUHUSU KWA KUHADITHIWA NA MKWELI HALISI NA HATA KIMAANDIKO).
 
Screenshot_2019-04-03-10-25-59.png
nikawaida sana sikuhizi Mtu mweusi kujipeleka utumwani yy na wanae bila hata mijeledi waliokua wanapigwa babu zetu
 
Mkuu umechanganya vitu vingi sana kwanza sayansi sio ya wazungu ni ya watu wote, pili tamaduni zimeenda zikibadiri hatuna haja ya kurudi nyuma tena kwa ajiri ya kuonyesha ubora wetu hata wazungu walikuwa na imani zao kabla ya ukristo hata wao walitupilia mbali. Tatu ligha zina kawaida ya kuzaliwa na kufa kuna lugha ya kiyunani haiongelewi popote kuna lugha nyingi kongwe za kale zilikufa usizionee huruma lugha kuwa inferior.
 
Mkuu Frustration hata mzungu alikuwa na dini yake ya asili lakini alipopelekewa ukristo aliupokea na akazipiga chini dini zake za asili za kipuuzi kabisa.
 
Back
Top Bottom