Ukweli wa uwepo wa Mungu na Makazi yake upo hapa

Ukweli wa uwepo wa Mungu na Makazi yake upo hapa

Utafiti wa Sayansi
Kwa upande wangu utafiti wako haukai akilini mwangu...Mungu hakai kwenye nyota yeyote wala sayari na jua letu ni dogo sana kuna mapande ya nyota namaanisha jua ni nyota yani kuna nyota kubwa sana hata jua letu ni dogo sana sizani Mungu akae kwenye nyota ndogo kama hiyo..Mungu yuko popote..Sasa Embu tofautisha hizo nyota mbili hapo Sun na Uy Scuti
View attachment 318974
Utafiti wa Bibilia
Hapa nakubaliana na wewe.Mungu alipokea sadaka kwa njia ya moto..Aliwajia wanaadamu kwa njia ya moto..Kuna story ya Musa umesahau ungeongezea hapo"Musa aliona kichaka kina waka moto bila ya kuteketea na akaambiwa hapo ni mahali patakatifu vua viatu vyako"
Mkuu Rudia kusoma post vizuri , Mungu anaishi katika moja wapo ya Nyota za Majua.
 
Mkuu siwezi kuku laumu mazingira yaliyo wakuza wengi wetu ndio hayo unayo yaonyesha.
pole Mkuu kwa kupoteza muda mwingi kwa kufanya utafiti ambao ingetosha kuwauliza layman wakakupa majibu mazuri zaidi ya hayoo ukaujua ukweli kuhusu Mungu
 
kwa mujibu wa maelezo yako naweza sema kuwa huenda miungu wapo wengi kila mmoja kajenga nyota yake anaishi bila buguza...
ni mawazo tu..
Hapana Mungu ni mmoja kama wangelikuwa tungeona mambo mengi kugongana kwa sayari Vita kati ya huku na kule MUNGU NI MMOJA TU.
 
Huu siwezi kuurefer Kama utafiti was kisayansi Kama ulivyidai mi naona hapa umefanya falsafa tu ambayo haina logic. By the way naomba ni kuulize kwa kuwa umechanganya dini na sayansi kwa mujibu wako hili ndo swali langu. Kwa mujibu wa biblia dunia ndo ilikuwa ya kwanza kuumbwa kabla ya jua nasi tunaamini mungu Hana mwanzo wala mwisho yaani Alfa na omega hivyo kabla ya jua kuumbwa mungu aliishi wapi?
Mkuu hayo ni mawazo yako ya kidini lakini ukweli ndio huu Ukiangalia mfumo wa ulimwengu wetu kuna mambo mengi ambayo ni tata lakini utata unaisha hapa Mungu siku zote alionekana kwaa njia ya moto ina maana anaishi katika moto na moto upo katika nyota za JUA au MAJUA.
 
Asante nmeshaona..

Swali langu kwako ni kwanini unafkiria mungu yupo..?
Mungu yupo hilo sina shaka nalo ndio maana unaona kila kitu katika ulimwengu wetu kipo katika mpangilio sahihi bila kuathiri kingine.
 
Ina maana baada ya kufanya utafiti huo wa miaka 16 ndio kaja na hoja nyepesi kama hizi....???
Mkuu Utafiti unaendelea Lakini sijui uelewa wako maana kwa kazi niliyofanya afu unasema nyepesi sawa lakini zidi kujifunza utayajua mengi.
 
toka zako hapa na utafiti wako uchwaraa.ALLAH anakaa mbingu ya saba juu kabisa.hakuna anayeweza fika iwe malaika au yeyote yule.ni mmoja tu aliyewah kupewa nafas ya kufika nae ni muhammad s.a.w.pekee hata yeye hakumuonaa ila inasemekana aliongea nae.kwa maelezo zaid tafuta kitabu cha safari ya israa na miiraji
Hahah hizi imani hizi sasa mwenzio kaja na nadharia na wewe umekuja na nadharia ,hakuna kati ya haya yameshathibitishwa au kushuhudiwa na mwanadamu yeyote ,credibility ya kuita utafiti wake uchwara unaupata wapi ??
 
H
Tuambie na aliyemleta huyo mwenyezi Mungu, maana hata yeye yupo kwenye mpangilio.
Hakuna aliye mleta, Mungu ni nafsi tukufu iliyo hai Ipo na ilikuwepo na itaaendelea kuwepo milele na milele Nafsi HAIFI wala yeye Ni mwanzo na mwisho
 
Hebu nambie ni kwasababu gani yupo..?
Mungu yupo milele na atakuwepo milele ndio maana yupo kwa kuwa alikuwepo mimi na wewe tumewekwa kama mapambo ya kumtukuza Mungu alituweka katika Dunia kwa sababu yeye alizoona zinafaa kwa Utashi wake Ukijua mfumo wa Ulimwengu na ukaona baadhi ya Sayari na Nyota Jinsi zinavyoonekana hapa Duniani ndiyo Sayari inayo vutia kuangalia kwa maana hiyo sisi ni viumbe alituumba rafiki ili tuwepo kama yeye alivyo baada ya kifo nafsi yako itaishi karibu na MUNGU. Mungu alikuwepo tangu milele yote ndiyo maana yupo.
 
Mungu yupo milele na atakuwepo milele ndio maana yupo kwa kuwa alikuwepo mimi na wewe tumewekwa kama mapambo ya kumtukuza Mungu alituweka katika Dunia kwa sababu yeye alizoona zinafaa kwa Utashi wake Ukijua mfumo wa Ulimwengu na ukaona baadhi ya Sayari na Nyota Jinsi zinavyoonekana hapa Duniani ndiyo Sayari inayo vutia kuangalia kwa maana hiyo sisi ni viumbe alituumba rafiki ili tuwepo kama yeye alivyo baada ya kifo nafsi yako itaishi karibu na MUNGU. Mungu alikuwepo tangu milele yote ndiyo maana yupo.
Sijakuuliza atakuwepo kwa mda gani
nmekuuliza kwanini yupo nachotaka ni sababu za yeye kuwepo..?
 
Back
Top Bottom