LGE2024 Ulaghai wa bei ya korosho na kiki za kisiasa za CCM kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

LGE2024 Ulaghai wa bei ya korosho na kiki za kisiasa za CCM kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Mnada wa kwanza wa korosho uliofanyika 11/10/2024 ulifunguliwa kwa bei ya TSh 4150/= kwa kilo moja ya korosho. Kwenye mnada huu kulikuwa na tani chache sana za korosho. Ukafuata mnada wa pili ambapo bei ilishuka mpk kufikia TSh 3750/=, napo pia kulikuwa na tani chache sana za korosho. Bei imeendelea kushuka na sasa imefikia TSh 3400/= ndani ya mwezi October. Na kumekuwa na janja ya kihuni ya kukwepa kubeba korosho za wakulima kupeleka kwenye ghala kuu ili kusubiri bei ishuke halafu korosho za wakulima zinunuliwe kwa bei ndogo baadaye.

Mavuno makubwa ya korosho yatafanyika mwezi huu wa November, ambapo ndipo wakulima wengi watauza korosho zao.
Kwa inavyoelekea bei ya korosho itakuwa TSh 2000/= (bei isiyofaa na inayomuumiza mkulima).

Kwahiyo bei ya TSh 4150/= ilikuwa ni danganya toto iliyovalishwa boksa ya kiki za kisiasa iliyolenga kuisaidia ccm kupiga kampeni kwenye chaguzi za serikali za mitaa.
Kwani nyie wakulima wa korosho hamkulijua hilo! Mtajuta kimfahamu Samia!
 
Shida hizi ziko kote,zao ambalo halina kelele ni maharage,kiukweli korosho ni zao poa,kwani wale Wazee wa ufipa hata kutafuta soko hawawezi,wao kazi yao kulialia,kwanini Wazee wa ufipa kazi yao michango na makesi yasiyoisha.
Ona nguruwe 🐖 hili! Watafute soko kwa mamlaka gani ya kisheria?
 
Mnada wa kwanza wa korosho uliofanyika 11/10/2024 ulifunguliwa kwa bei ya TSh 4150/= kwa kilo moja ya korosho. Kwenye mnada huu kulikuwa na tani chache sana za korosho. Ukafuata mnada wa pili ambapo bei ilishuka mpk kufikia TSh 3750/=, napo pia kulikuwa na tani chache sana za korosho. Bei imeendelea kushuka na sasa imefikia TSh 3400/= ndani ya mwezi October. Na kumekuwa na janja ya kihuni ya kukwepa kubeba korosho za wakulima kupeleka kwenye ghala kuu ili kusubiri bei ishuke halafu korosho za wakulima zinunuliwe kwa bei ndogo baadaye.

Mavuno makubwa ya korosho yatafanyika mwezi huu wa November, ambapo ndipo wakulima wengi watauza korosho zao.
Kwa inavyoelekea bei ya korosho itakuwa TSh 2000/= (bei isiyofaa na inayomuumiza mkulima).

Kwahiyo bei ya TSh 4150/= ilikuwa ni danganya toto iliyovalishwa boksa ya kiki za kisiasa iliyolenga kuisaidia ccm kupiga kampeni kwenye chaguzi za serikali za mitaa.
Leteni updates wazee
 
Leteni updates wazee
Bado hali ni tete. Waandishi wa habari wamekuwa machawa wa ccm.

Kilichofanyika ni kununua tani chache sana za korosho zilizosombwa na kupelekwa kwenye ghala kuu, kati ya matani na matani ya korosho yanayoozea kwenye AMCOS za vijijini.

Hali ni mbaya sana, lkn kwa bahati mbaya sana vyombo vya habari vinaripoti uwongo.
 
Ninachojua Maghala makuu wao wanaogopa kuchukua korosho nyingi kutoka Amcos wakihofia mzigo kubaki alafu wawe na madeni wanaenda mdogo mdogo.
Bei kushuka ilo lipo miaka yote wale wanunuzi wakubwa wakishapata Tani wanazotaka wanaondoka wanakuja wengine wenye bei ndogo kwaiyo bei kufika elf 2 itafika tu kwa watakaouza Dec.
 
Ninachojua Maghala makuu wao wanaogopa kuchukua korosho nyingi kutoka Amcos wakihofia mzigo kubaki alafu wawe na madeni wanaenda mdogo mdogo.
Bei kushuka ilo lipo miaka yote wale wanunuzi wakubwa wakishapata Tani wanazotaka wanaondoka wanakuja wengine wenye bei ndogo kwaiyo bei kufika elf 2 itafika tu kwa watakaouza Dec.
Sasa hapo madeni watapataje?
 
Kwa kweli inaniwia vigumu kuyatamka haya lakini kadri siku zinavyokwenda ndio inazidi kudhihirika kuwa CCM wanatawala watu mfano wa maiti zinazotembea.....maana ni maiti pekee ndio unaweza kuifanya vile unataka bila kutoa upinzani wowote........

Watanganyika walio wengi ni watu mfano wa maiti zinazotembea.....ukitaka kuyajua hayo subiria nyakati za uchaguzi.....
hakika mkuu ila sinahakika sana kama kweli watz wajnga kias hich kwenye ulimwengu huu wa sasa. inawezekana mifumo ya utawala huu inahusika san kuwapa ushind.
 
Hili nalo wazo. Ila kuna maeneo ni korofi maghala yake yatakuwa hayafikiki kiurahisi, kwa hiyo wanunuzi watasita kununua maeneo hayo. Sasa mjini walau kunafikika.
Sheria inaruhusu kumpelekea mteja mzigo kama ni mjini au Dar, hivyo maghaala yanaweza jengwa hata vijijinu kikubwa bodi ya stakabadhi gharani uthibitishe ubora
 
Alichoandika jamaa hapo ni ukweli tupu. Mnapeleka korosho katika chama cha ushirika lakin matokeo yake minada inapita korosho zipo kwenye amcos hata hazijaenda huko na ukiuliza unaambiwa gari za kubeba hakuna kwahiyo tukipata gari tutapeleka na matokeo yake korosho zinazidi kushuka tu bei kila uchwao.
 
Back
Top Bottom