Ulaji wa Panya mikoa ya Kusini: Safari yangu ya siku 37 ilivyonifungua mambo mengi

Ulaji wa Panya mikoa ya Kusini: Safari yangu ya siku 37 ilivyonifungua mambo mengi

Safari yenye takribani kilomita 600+ hadi Mkoani Mtwara wilaya ya Masasi kijiji cha Nangoo napata fursa ya kuifahamu jamii ya watu wa mikoa hii japo kwa uchache.

Nikiwa eneo hilo nilipata fursa ya kufahamu baadhi ya tamaduni za kule, baadhi tu kama vile Unyago na aina ya vyakula ambavyo vipo tofauti na vingine.

Achana na kufanya Upupu kama ni chakula ila hili la ulaji panya lilinivutia zaidi, Panya!! Ukuaji wangu umenikuza nikiamini Panya ni sehemu ya wadudu waharibifu wa kwenye nyumba za watu au mashambani.

Biashara ya kitoweo hiki kule Kusini siyo ya kificho, ni biashara ya wazi inayotembezwa kama bidhaa nyingine tu ya kawaida. Panya wanawekwa kwenye mtungo wa mti au kupangwa fungu kwa idadi fulani na kufungwa na kamba.

UPATIKANAJI NA UANDAAJI WA PANYA
Mwanzo nilidhani ni rahisi tu kupata Panya kwasababu ni kawaida kuwakuta kwenye nyumba zetu za kawaida kumbe la hasha! Siyo kila panya ni kitoweo.

Panya wa Porini Vs Panya wa Nyumbani.

Ikae akilini mwako kuwa kule wametofautisha Panya kwa aina hizo mbili, sasa taarifa ikufikie wale Panya wa Porini ambao kwa kawaida wanapatikana mashambani huko hasa ndio maalumu kwajili ya Kitoweo. Muda wangu wote kule sijashuhudia Panya wa nyumbani wakifanywa kitoweo bali uuliwa na kutupwa kama ilivyo sehemu nyingine.

Panya wa Porini wanapatikana kwenye mashimo huko shamba na kuna utaalamu katika uwindaji wake. Sasa tutazame namna wanaandaliwa Panya hadi kuwa Kitoweo.

Wakishapatikana wanaondolewa uhai wao kwa kupigwapigwa chini, hatua inayofuata ni kuwasafisha/ kuwaandaa kwa kuweka viungo kama chumvi na pilipili kiasi halafu unawabanika jikoni kwa moto wa wastani.

Ni kama tu unavyobanika Kuku au vile wamasai wanavyoweka Nyama kwenye Mtungo na kubanika. Baada ya zoezi hilo hatua inayofuata ni kuwafunga mafungu au kuuza mmoja mmoja tayari kwa kitoweo.

JE, INASHANGAZA?
Hapana bali inavutia, hata mimi mwanzo kila nilipojaribu kuonesha kuwashangaa nao walinishangaa kwanini nina washangaa basi tukawa tunashangaana.

Hoja yao wanasema huo ni utamaduni wao na uheshimiwe ni kitu kilichobadili mtazamo wangu juu yao, wanasema mbona ipo jamii inakula Mbwa kitu ambacho kule kusini siyo utamaduni wao kabisa. Mwingine aliniambia wapo watu wa Mkoa fulani wanakula panzi, bahati nzuri kwao waliamua kukipa thamani kitoweo chao.

FAHAMU
Siyo watu wote wa Kusini wanakula Panya HAPANA, wapo wengine ni tofauti kabisa na hawajawahi kula hata mara moja. Nafikiri hii ni kawaida tu kwenye mambo mengi.

Siku zangu 37 za kuishi kusini nilijifunza mengi sana, watu wake ni wema na wakarimu wanaojali zaidi wageni kuliko wenyewe kwa wenyewe. Huu ni udhaifu toka kwao.

Mwisho.
Mleta Mada Wale Sio Panya bali wanaitwa Fuko Fuko na huwa hawali nyama au dagaa au unga, ila wanakula mizizi ya mimea kama karanga, mihogo na vinginevyo.

Blaza ungeuliza wanaitwaje hao viumbe kuliko kuja na jina la Panya tena wakati umeshatambua ni kiumbe gani. Umehswahi kuona panya hali nyama au samaki au dagaa?
 
Kuna kisa kimoja cha mwalimu wangu juu ya ulaji wa panya..
nimesoma kusini mkoa wa Lindi shule moja inaitwa mahiwa high school

Mwalimu wangu wa geography aliitwa Mr mwazembe jitu la miraba minne kutoka mbeya alibahatika kupata binti wa pale kijijini,.Ruti za shuleni kwenda kijijini Kwa mchumba wake zilikuwa nyingi sn.

Km unavyojua mikoa ya Lindi na Mtwara ulaji wa panya ni kitu cha kawaida sn,Kwa hiyo mke wa ticha alikuwa mlaji mzuri sn wa panya.Km ilivyo kawaida ya wabongo,ticha alidharau sn watu wanokula panya,lkn Yule dada (demu wake) alikuwa mlaji wa panya..siku moja ticha akaamua kujaribu kuonja..asee Radha aliyokutana nayo,kuanzia siku hiyo akageuka kuwa ndiyo kimara wa walahi panya

Ticha akaenda mbali zaidi,akawa na mtu wake maalumu anachukua panya kwa bili,kisha analipia mwisho wa mwezi mshahara ukitoka..

Mleta Mada Wale Sio Panya bali wanaitwa Fuko Fuko na huwa hawali nyama au dagaa au unga, ila wanakula mizizi ya mimea kama karanga, mihogo na vinginevyo.

Blaza ungeuliza wanaitwaje hao viumbe kuliko kuja na jina la Panya tena wakati umeshatambua ni kiumbe gani. Umehswahi kuona panya hali nyama au samaki au dagaa?
Ni Panya, jamii yenyewe wanaita Panya how comes niite jina tofauti?? Inawezekana unachosema ni kweli lakini siyo kwa jamii ya watu wa Kusini.
 
Safari yenye takribani kilomita 600+ hadi Mkoani Mtwara wilaya ya Masasi kijiji cha Nangoo napata fursa ya kuifahamu jamii ya watu wa mikoa hii japo kwa uchache.

Nikiwa eneo hilo nilipata fursa ya kufahamu baadhi ya tamaduni za kule, baadhi tu kama vile Unyago na aina ya vyakula ambavyo vipo tofauti na vingine.

Achana na kufanya Upupu kama ni chakula ila hili la ulaji panya lilinivutia zaidi, Panya!! Ukuaji wangu umenikuza nikiamini Panya ni sehemu ya wadudu waharibifu wa kwenye nyumba za watu au mashambani.

Biashara ya kitoweo hiki kule Kusini siyo ya kificho, ni biashara ya wazi inayotembezwa kama bidhaa nyingine tu ya kawaida. Panya wanawekwa kwenye mtungo wa mti au kupangwa fungu kwa idadi fulani na kufungwa na kamba.

UPATIKANAJI NA UANDAAJI WA PANYA
Mwanzo nilidhani ni rahisi tu kupata Panya kwasababu ni kawaida kuwakuta kwenye nyumba zetu za kawaida kumbe la hasha! Siyo kila panya ni kitoweo.

Panya wa Porini Vs Panya wa Nyumbani.

Ikae akilini mwako kuwa kule wametofautisha Panya kwa aina hizo mbili, sasa taarifa ikufikie wale Panya wa Porini ambao kwa kawaida wanapatikana mashambani huko hasa ndio maalumu kwajili ya Kitoweo. Muda wangu wote kule sijashuhudia Panya wa nyumbani wakifanywa kitoweo bali uuliwa na kutupwa kama ilivyo sehemu nyingine.

Panya wa Porini wanapatikana kwenye mashimo huko shamba na kuna utaalamu katika uwindaji wake. Sasa tutazame namna wanaandaliwa Panya hadi kuwa Kitoweo.

Wakishapatikana wanaondolewa uhai wao kwa kupigwapigwa chini, hatua inayofuata ni kuwasafisha/ kuwaandaa kwa kuweka viungo kama chumvi na pilipili kiasi halafu unawabanika jikoni kwa moto wa wastani.

Ni kama tu unavyobanika Kuku au vile wamasai wanavyoweka Nyama kwenye Mtungo na kubanika. Baada ya zoezi hilo hatua inayofuata ni kuwafunga mafungu au kuuza mmoja mmoja tayari kwa kitoweo.

JE, INASHANGAZA?
Hapana bali inavutia, hata mimi mwanzo kila nilipojaribu kuonesha kuwashangaa nao walinishangaa kwanini nina washangaa basi tukawa tunashangaana.

Hoja yao wanasema huo ni utamaduni wao na uheshimiwe ni kitu kilichobadili mtazamo wangu juu yao, wanasema mbona ipo jamii inakula Mbwa kitu ambacho kule kusini siyo utamaduni wao kabisa. Mwingine aliniambia wapo watu wa Mkoa fulani wanakula panzi, bahati nzuri kwao waliamua kukipa thamani kitoweo chao.

FAHAMU
Siyo watu wote wa Kusini wanakula Panya HAPANA, wapo wengine ni tofauti kabisa na hawajawahi kula hata mara moja. Nafikiri hii ni kawaida tu kwenye mambo mengi.

Siku zangu 37 za kuishi kusini nilijifunza mengi sana, watu wake ni wema na wakarimu wanaojali zaidi wageni kuliko wenyewe kwa wenyewe. Huu ni udhaifu toka kwao.

Mwisho.
Ugeweka na kapicha ingependeza zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mleta Mada Wale Sio Panya bali wanaitwa Fuko Fuko na huwa hawali nyama au dagaa au unga, ila wanakula mizizi ya mimea kama karanga, mihogo na vinginevyo.

Blaza ungeuliza wanaitwaje hao viumbe kuliko kuja na jina la Panya tena wakati umeshatambua ni kiumbe gani. Umehswahi kuona panya hali nyama au samaki au dagaa?
Acha uongo..panya ni panya na fuko ni fuko..wanyama wawili tofauti
 
Acha uongo..panya ni panya na fuko ni fuko..wanyama wawili tofauti
Umemwelewa mto mada wewe kweli? Umewahi kuona panya anakula mizizi na anatengeneza shimo lenye urefu hata wa mita 100? Watoto mmekua wengi sana Jamii forum siku hizi
 
Panya walioungwa kwa Nazi au karanga wanapatikana?!
 
Ni Panya, jamii yenyewe wanaita Panya how comes niite jina tofauti?? Inawezekana unachosema ni kweli lakini siyo kwa jamii ya watu wa Kusini.
Mie naishi Masasi na ninalima Tunduru kwahiyo naelewa zaidi ya unavyofikiria. Ukanda wote wa kusini kuanzia Namtumbo, Lusewa, Tunduru, Mtambaswala, Mangaka, Masasi, Ndanda, Mtama, Newala, Lindi hadi Kilwa wanakula hao viumbe. Pia na chatu analiwa vizuri sana
 
Umemwelewa mto mada wewe kweli? Umewahi kuona panya anakula mizizi na anatengeneza shimo lenye urefu hata wa mita 100? Watoto mmekua wengi sana Jamii forum siku hizi
Kula mizizi? Kwani mihogo na viaz vitamu siyo mizizi?au mizizi kwako unaelewaje..
Kutengeneza shimo la urefu wa Mita Mia hapana..panya wa porini ana uwezo wa kuchimba shimo refu lkn siyo Mita Mia[emoji16]
 
Kula mizizi? Kwani mihogo na viaz vitamu siyo mizizi?au mizizi kwako unaelewaje..
Kutengeneza shimo la urefu wa Mita Mia hapana..panya wa porini ana uwezo wa kuchimba shimo refu lkn siyo Mita Mia[emoji16]
Hakuna viumbe wanaosumbua kama hao shambani ndo maana kuna mitego hiyo na watu wanawafukizia moshi. Ila ukitaka kuchimba shimo ulifatilie unaweza jikuta umefikisa kilometa moja na usimpate. Kinachosaidia kumpata ni pale utakapokuta udongo aliotufua kwa juu ambao ni mbichi, hapo ndo utajua hayupo mbali na hapo. Maana akishaingia ndani huwa anafukia shimo lake kwa ajili ya usalama.
 
Siyo watu wa mtwara tu ndio wanaokula panya! Hata jule iringa hasa wilaya ya kilolo hao wanyama wanaliwa sana
 
Nami pia nimebahatika kukaa na watu wa sumbawanga nao ni walaji wazuri wa panya
 
Back
Top Bottom