SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kumekuwepo na madai kuwa ulaji wa ugali hudumaza akili. Madai haya yana ukweli kiasi gani?

02692B18-05FE-4851-857F-7A5DA6E174CD.jpeg
 
Tunachokijua
Ugali ni chakula kinachotumika sana Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kwa mujibu wa utafiti wa Onu Okpa et al (2019), “Sub-Saharan African Maize-Based Foods - Processing Practices, Challenges and Opportunities” mahindi huchangia 30% ya nishati za vyakula wanavyotumia watu wa ukanda huu kila siku.

Kwa mujibu wa utafiti huu, kila mtu anayepatikana Kusini mwa Jangwa la Sahara hutumia wastani wa kati ya gramu 52-450 za mahindi kwa siku. Ni chanzo kikuu cha ugali unaotumika kila siku kwenye nchi hizi. Kwa Tanzania, 64% ya wananchi wake hula chakula hiki walau mara 5-7 kwa wiki.

Takwimu hizi zinaonesha kuwa ugali ni chakula kinachotumika sana, pengine kuliko aina nyingine za vyakula. Baadhi ya watu huutengeneza kwa kutumia unga wa mhogo, mtama, ulezi pamoja na aina zingine za nafaka.

Bila kujali tofauti ndogo za mgawanyiko wa virutubisho, nafaka zote husifika kwa kuwa na kiasi kikubwa cha nishati na wanga, pia kiasi kidogo cha madini na vitamini muhimu kwa afya.

Kuhusishwa na udumavu wa akili
Kitaalamu, udumavu wa akili husababishwa mambo mengi ikiwemo baadhi ya changamoto za kijenetiki mfano Down’s syndrome, kukosa hewa ya kutosha wakati wa kuzaliwa, maambukizi makali ya homa ya uti wa mgongo, utapiamlo, matumizi ya baadhi ya madawa na pombe wakati wa ujauzito pamoja na sababu zingine siziso wazi sana.

Kwa kurejea mgawanyiko wa virutubusho vinavyopatikana kwenye nafaka zinazotumika kutengenezea ugali, hakuna uhusiano wa moja kwa moja unaoweza kutajwa, au pia kuhusishwa na kusababisha udumavu wa akili kwa watu. Virutubisho na madini yake havina athari hasi kwenye afya ya ubongo.

Pia, JamiiForums imezungumza na wataalamu wa lishe ambao wamethibitisha kuwa chakula hiki ni salama, hakiwezi kusababisha madhara tajwa.

Hivyo, JamiiForums imebaini kuwa madai haya hayana ukweli uliojengwa kwa hoja za kisayansi. Ni uzushi usio na uthibitisho wa tafiti au takwimu.
View attachment 3114645

Ni Chakula cha ajabu huwezi kula bila mboga wala kunywea chai.

Ni chakula maarufu zaidi kwenye sehemu za mateso kama jela, watoto wasiojitambua wanalishwa kinguvu.

vyakula vilivyojitosheleza unaweza kula bila mboga mfano wali, ndizi, mkate, maandazi, chips, chapari, viazi, n.k,

hapo zamani watumwa walilishwa ugali kwa maksudi ili kuwakandamiza uwezo wa kufikiri, ni dawa iliyotumika kupunguza uwezo wa kufikiria (Thinking capacity), Mtu anaweza kuwa genius anaekula ugali lakini ilibidi awe mara 3 zaidi bila ugali.

kwa hapa nchini ukifuatilia sehem zinazotoa vichwa utagundua hawali sana ugali, lakini bado sio uwezo wao kamili kwasababu siku mbili au tatu za wiki wanakula ugali.

Mboga za majani na samaki wanaweza kuongeza akili lakini kosa linalofanywaa huwa ni kutumia ugali, nguvu ya ugali inaenda kuyeyusha / ku dilute virutubisho vya ubongo.

Ushauri wa bure kabisa, ukitaka kumuongezea mtoto uwezo wa akili usimzoeshe ugali, kiwe ni chakula cha kufanyia mazoezi ajifunze kufinya matonge ili ugenini asitie aibu.
Sukar
 
View attachment 3114645

Ni Chakula cha ajabu huwezi kula bila mboga wala kunywea chai.

Ni chakula maarufu zaidi kwenye sehemu za mateso kama jela, watoto wasiojitambua wanalishwa kinguvu.

vyakula vilivyojitosheleza unaweza kula bila mboga mfano wali, ndizi, mkate, maandazi, chips, chapari, viazi, n.k,

hapo zamani watumwa walilishwa ugali kwa maksudi ili kuwakandamiza uwezo wa kufikiri, ni dawa iliyotumika kupunguza uwezo wa kufikiria (Thinking capacity), Mtu anaweza kuwa genius anaekula ugali lakini ilibidi awe mara 3 zaidi bila ugali.

kwa hapa nchini ukifuatilia sehem zinazotoa vichwa utagundua hawali sana ugali, lakini bado sio uwezo wao kamili kwasababu siku mbili au tatu za wiki wanakula ugali.

Mboga za majani na samaki wanaweza kuongeza akili lakini kosa linalofanywaa huwa ni kutumia ugali, nguvu ya ugali inaenda kuyeyusha / ku dilute virutubisho vya ubongo.

Ushauri wa bure kabisa, ukitaka kumuongezea mtoto uwezo wa akili usimzoeshe ugali, kiwe ni chakula cha kufanyia mazoezi ajifunze kufinya matonge ili ugenini asitie aibu.
Hakikisha unachanganya mahindi na ngano au unga wa ngano na unga wa mahindi...kupunguza udumavu wa akili
 
Tatizo la kusomea ungwini badala ya Masomo ya sayansi ....
....
Nchi imezalisha vilaza na wapiga domo wengi.

Ugali ni Carbohydrate kama ilivyo keki kinachotakiwa ni kupamba pishi la ugali(kama mchuzi wa samaki unavyoitwa makange halafu unauziwa 20,000 au mihogo ya kukaanga inayouzwa 20,000) ....
inabidi hoteli za Tanzania ziweke special menu ya Ugali mfano:
-Brown Ugali
-Squared Ugali
-Air dried ugali
-Soft Ugali(kwante) n.k
 
Kweli ugali una punguza uwezo wa kufikiri ndo maana hata ww mleta mada uliyekula ugali umeleta mada ambayo hujaifanyia Tafiti. Wamarekani kutumia mahindi kuzalisha chakula cha wanyama haifanyi mahindi yanapoliwa na binadamu kushusha uwezo wa kufikiri. Labda uje na data za kukusapoti.

Lakini pia hata ukienda supermarket za wazungu mbona mahindi mabichi yako packed na yanaliwa vizuri Sana kwenye salads na matumizi mengine??
Ni kweli mleta mada hajaweka takwimu za kitaalamu hivyo basi hii inabaki kama mtazamo wake binafsi, kimsingi mahindi kama mahindi yana nutrition muhimu kwa kiwango kikubwa kabisa. Mfano food composition ya unga wa mahindi kwa 100g unapata; energy 363kcal, 8.4g of protein na 1.2g of fat. Ukilinganisha na unga wa ngano; energy 364kcal, 10.9g of protein, 1.1g of fat. Hapo tunaona utofauti ni mdogo sana.

Shida ni maandalizi yake, mahindi ni tofauti na ugali. Mara nyingi mahindi yanaliwa yakiwa freshy kabisa tofauti na ugali. Kwa mtazamo wangu na experience yangu binafsi, ugali unaharakisha mchakato wa kuleta usingizi. Sasa basi kama unaleta usingizi hapo tayari ni kisababishi cha kupunguza uwezo wa ufanisi kwa muda. Kama tunavyojua katika hali ya usingizi kunaambatana na uchovu na hali ya uchovu unaathiri utendaji wa ubongo.
 
Ugali waliouharibu ni wale wa kuukoboa ni ugali mbaya sana , Sema mm ugali wangu nauwekea mahindi yasiyokobolewa , Ngano isiyokobolewa, kitu kimoja kitamu sana mboga za majani na samaki weuweeeeee angalau ni chakula ninayokula kila mara nne Kwa wiki.

Ugali mweupe kama yangeyange uwa sili kabisa
 
Ugali ni msosi poa tu. Huwezi kula bila mboga sababu hauna chumvi, mafuta wala sukari kama hivyo vingine. Ugali ni chakula chenye calories nyingi sana. Ekari moja ya mahindi inaweza kulisha watu wengi kuliko ngano, mpunga na nafaka nyingine yoyote ile.
 
Ugali uheshimiwe.. Tulioenda JKT miaka ile... mtakuwa mnanielewa.. Siku za mwanzo, kuna vislay vilikuja na biscuit, na vikawa havichukui ugali..Vinachukua maharage na kula na biscuit..Combania ilivyochanganya wote walinyooka kwenda kukimbilia mkombozi ugali, na makuruta waliokuwa na chati, ni wale walioweza kupata ugali wa ziada, au muda wote kuaccess source ya kupata ugali..
Inadhihirisha ugali ni muokozi halisi, ndio maana unaweza ukatumika maeneo yote , hayo mashuleni, jela, kwenye makambi nk..

Tuheshimu ugali
 
View attachment 3114645

Ni Chakula cha ajabu huwezi kula bila mboga wala kunywea chai.

Ni chakula maarufu zaidi kwenye sehemu za mateso kama jela, watoto wasiojitambua wanalishwa kinguvu.

vyakula vilivyojitosheleza unaweza kula bila mboga mfano wali, ndizi, mkate, maandazi, chips, chapari, viazi, n.k,

hapo zamani watumwa walilishwa ugali kwa maksudi ili kuwakandamiza uwezo wa kufikiri, ni dawa iliyotumika kupunguza uwezo wa kufikiria (Thinking capacity), Mtu anaweza kuwa genius anaekula ugali lakini ilibidi awe mara 3 zaidi bila ugali.

kwa hapa nchini ukifuatilia sehem zinazotoa vichwa utagundua hawali sana ugali, lakini bado sio uwezo wao kamili kwasababu siku mbili au tatu za wiki wanakula ugali.

Mboga za majani na samaki wanaweza kuongeza akili lakini kosa linalofanywaa huwa ni kutumia ugali, nguvu ya ugali inaenda kuyeyusha / ku dilute virutubisho vya ubongo.

Ushauri wa bure kabisa, ukitaka kumuongezea mtoto uwezo wa akili usimzoeshe ugali, kiwe ni chakula cha kufanyia mazoezi ajifunze kufinya matonge ili ugenini asitie aibu.
Ugali umekukosea wapi boss
 
View attachment 3114645

Ni Chakula cha ajabu huwezi kula bila mboga wala kunywea chai.

Ni chakula maarufu zaidi kwenye sehemu za mateso kama jela, watoto wasiojitambua wanalishwa kinguvu.

vyakula vilivyojitosheleza unaweza kula bila mboga mfano wali, ndizi, mkate, maandazi, chips, chapari, viazi, n.k,

hapo zamani watumwa walilishwa ugali kwa maksudi ili kuwakandamiza uwezo wa kufikiri, ni dawa iliyotumika kupunguza uwezo wa kufikiria (Thinking capacity), Mtu anaweza kuwa genius anaekula ugali lakini ilibidi awe mara 3 zaidi bila ugali.

kwa hapa nchini ukifuatilia sehem zinazotoa vichwa utagundua hawali sana ugali, lakini bado sio uwezo wao kamili kwasababu siku mbili au tatu za wiki wanakula ugali.

Mboga za majani na samaki wanaweza kuongeza akili lakini kosa linalofanywaa huwa ni kutumia ugali, nguvu ya ugali inaenda kuyeyusha / ku dilute virutubisho vya ubongo.

Ushauri wa bure kabisa, ukitaka kumuongezea mtoto uwezo wa akili usimzoeshe ugali, kiwe ni chakula cha kufanyia mazoezi ajifunze kufinya matonge ili ugenini asitie aibu.
Mbona ugali uko poa tu kunywea chai, ila lazima uubanike kwenye moto. Pia ukoko wa ugali ni mtamu kuliko pilau au chapati, ukiunyunyuzia mchuzi basi siku hiyo utakukurushana na sufuria mpaka majirani wasikie. Wenzako ugali unaliwa asubuhi badala ya chai, unaliwa mchana na pia unaliwa usiku, wali unaliwa wakati unasubiri ugali uive, familia hizi zina watoto si chini ya kumi.
 
Back
Top Bottom