SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Tatizo wengi tunakariri. Ugali umeliwa enzi na enzi katika nchi nyingi tu za kiafrika, kabla hata hayo mahindi hayajaingia katika bara hili.
Nafikiri ni sahihi kuwaita hawa kama wanavyotakiwa kuitwa. Ni magaidi ya mitandaoni. Yani wanajisahaulisha kwa makusudi(Wanajizima data) . Ulaya wanakula Polente. Ni Ugali tu.😂😂😂 Wao ni kukandia kila kitu chenye Utamaduni na Asili ya Mwafrika.
Yaani kama ni Mahindi, basi Wazungu ndi waliodumazwa, kwani
Wakiamka, Cornflakes🤔 Itoshe, ukiwasikia Wanazuoni wa Ulaya huko na Marekani, utawasikia wakisema "I lived on Cornflakes and Noodles while at College"

Hapooo sasa.


Hakika.
 
wali, ndizi, Pilau, mkate, maandazi, chips, chapari, viazi,
Pamoja na kwamba sipendi wala kuushabikia ugali, lakini hakuna tofau kubwa kati ya ugali na vyakula hivyo ulivyovitaja hapo, hususani kwenye maendeleo na ukuaji wa binadamu (prenatal & postnatal growth).

Sababu ni kuwa hivyo vyakula vyote nina carbohydrates nyingi ambazo hazina kazi ya maana katika brain development.

Ningekusifu zaidi kama ungepigia chapuo watu kutumia zaidi vyakula vyenye asili ya protini kwa wingi huku vile vyenye asili ya wanga vikipewa kipaumbele cha mwisho kabisa
 
Binafsi napenda sana ugali lakini upikwe vizuri na moto mkali na usongeke, usiwe na nabija wala unga unga ninapokula.
Na mboga yoyote ile mlenda, majani au mchuzi, dagaa n.k

Lakini kuupenda kwangu hajui ndio ukweli kuwa huenda ni Chakula kinachodumaza akili.
Afrika yote common food no ugali , it is very unfortunate.
 
Inategemea unakula ugali wa aina gani
Mimi nasaga mwenyewe
Mahindi, mahindi ya njano lishe, muhogo, mchele na mbegu za maboga vyote nachanganya..

Huo ugali ni noma wazee
UGALI NI UGALI JEMBE UNAUREMBA SANA AISEE
 
Ugali ni msamisti wa nafaka iliosagwa. Hata mchele, ngano, mtama nk hutoa ugali.
Vilevile mihogo, ndizi nk nao hutoa ugali
Kama lengo lako ni kukataa ugali wa mahindi weka wazi. Ugali ni ubumifu wa waafrika warabu nk hawana ugali kwa sababu hawana ardhi ya kulima nafaka. Ukishindwa kula ugali kula viazi, ndizi, magimbi nk. Kula vyakula vya kunde kama bagia tambi nk.
Je usipo kula ugali wa aina yoyote mwili wako utaimarika kwa kazi ngumu za maisha yetu? Waafrika kazi zetu nyingi ni manual.
 
Hapa Kuna ulakini flani, nchi karibu zote hawali ugali, ila huku ukila ugali unaonekana wa asili,


Kwa tuliosoma shule za kibishi, mkishakunywa uji saa 4 vipindi vinavyofata ilikua kama kukamilisha ratiba tu, watu wamechoka kama wamekula visungura

Nimekumbuka wakati nipo A level.. baada ya break ya asubuhi, asilimia 90 ya wanafunzi walikuwa wanasinziq kwa sababu ya kunywa uji


Ole uwe umepuliza yaani kunywa uji mkavu😃
Utajikuta umelala hadi unaota ndoto
 
Sio kweli TZ au Aftica yote. Kigoma tumekulia ugali wa mihogo na magimbi na ndizi kwa mboga za xuwani, maharage, kunde na mboga mbiga. Mahindi hayaliwii sana. Usukumani vyakula ni vingi sena. Mtama, uwele, viazi vitamu. Mbeya wanakula sana ndizi, ndofani, wali na ugali wa mahindi ie watu wa mbeya hawapendi mtama japo unastawi .Wapogoro kwa wali huwaambii kitu.
Mikoa ya kati ndio wala ugali wakuu, hawana mbadala. Pwani wanakula sana wali, mihogo, viazi vitamu na vyakula vya kusindika kama mikate. Wakinga hula ngano nyeusi, viazi mviringo na ugali.
Watu wa kipato cha kati ugali wanakula zaidi mchana, usiku ni wali au take away kama maandazi, chapati.
Wanaoongoza kula ugali wa mahindi ni wanafunzi wa shule za boarding, hawa hamna mjadala. Wanasindikizia na maharage. 80% ni ugali maharage. Matunda hio ratiba haipo. Mwanafinxi wa boarding inaweza kuwa anaongoza kwa lishe duni.
 
Kwa hiyo makande ni bora kuliko Ugali?
 
Chakula huendana na utamaduni, mila na desturi pia na mazingira ikiwemo upatikanaji...

Basi Wanaokula vyura na kono kono tungewaiga maana Wana akili sana kuliko sisi.
Wazungu wanalima sana mahindi ila wanaishiabkulisha nguruwe na ngombe,mahindi sio utamaduni wa mwafrika yaliletwa afrika kutokea bara la amerika ya kusini.

Chakula chetu cha asili ni mtama,ulezi,uwele mihogo.


Narudia tena ukiona chakula hakiliwi ulimwengu wa kwanza japo wanakilima jiulize vzri,wazungu sio wajinga,pay attention to small things.
 
Kims
KImsingi nmeacha kabisa kula ugali na shauri watu waendelee kuachana na matumizi ya ugali wa mahindi.
 
Aki
Akili ndogo sana wewe,kwahiyo nchi nyingine ambazo hawali ugali wa mahindi hao mafundi ujenzi hula piza?
 
Hili limesha jadiliwa humu several times..

Kwa kuongezea nafaka ya ugali ni chakula Cha kuwaulia wanyama walio shindikana ie. Marekani

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…