SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kumekuwepo na madai kuwa ulaji wa ugali hudumaza akili. Madai haya yana ukweli kiasi gani?

02692B18-05FE-4851-857F-7A5DA6E174CD.jpeg
 
Tunachokijua
Ugali ni chakula kinachotumika sana Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kwa mujibu wa utafiti wa Onu Okpa et al (2019), “Sub-Saharan African Maize-Based Foods - Processing Practices, Challenges and Opportunities” mahindi huchangia 30% ya nishati za vyakula wanavyotumia watu wa ukanda huu kila siku.

Kwa mujibu wa utafiti huu, kila mtu anayepatikana Kusini mwa Jangwa la Sahara hutumia wastani wa kati ya gramu 52-450 za mahindi kwa siku. Ni chanzo kikuu cha ugali unaotumika kila siku kwenye nchi hizi. Kwa Tanzania, 64% ya wananchi wake hula chakula hiki walau mara 5-7 kwa wiki.

Takwimu hizi zinaonesha kuwa ugali ni chakula kinachotumika sana, pengine kuliko aina nyingine za vyakula. Baadhi ya watu huutengeneza kwa kutumia unga wa mhogo, mtama, ulezi pamoja na aina zingine za nafaka.

Bila kujali tofauti ndogo za mgawanyiko wa virutubisho, nafaka zote husifika kwa kuwa na kiasi kikubwa cha nishati na wanga, pia kiasi kidogo cha madini na vitamini muhimu kwa afya.

Kuhusishwa na udumavu wa akili
Kitaalamu, udumavu wa akili husababishwa mambo mengi ikiwemo baadhi ya changamoto za kijenetiki mfano Down’s syndrome, kukosa hewa ya kutosha wakati wa kuzaliwa, maambukizi makali ya homa ya uti wa mgongo, utapiamlo, matumizi ya baadhi ya madawa na pombe wakati wa ujauzito pamoja na sababu zingine siziso wazi sana.

Kwa kurejea mgawanyiko wa virutubusho vinavyopatikana kwenye nafaka zinazotumika kutengenezea ugali, hakuna uhusiano wa moja kwa moja unaoweza kutajwa, au pia kuhusishwa na kusababisha udumavu wa akili kwa watu. Virutubisho na madini yake havina athari hasi kwenye afya ya ubongo.

Pia, JamiiForums imezungumza na wataalamu wa lishe ambao wamethibitisha kuwa chakula hiki ni salama, hakiwezi kusababisha madhara tajwa.

Hivyo, JamiiForums imebaini kuwa madai haya hayana ukweli uliojengwa kwa hoja za kisayansi. Ni uzushi usio na uthibitisho wa tafiti au takwimu.
Wazungu na warabu wako vizuri kiafya wala hawayajui maugali ni nini wao wanajilia ngano, wali, nyama na maziwa, sisi Watanganyika kutwa usiku tunakula maugali na milenda kama tumerogwa
Unajua watanzania tunaona Kwa sababu ugali ni mgumu basi tunaona ndio unatufanya tuwe wagumu na miguvu, lakini hamna chochote. Bora wanaokunywa urojo wanapata virutubisho vya aina mbalimbali lakini ugali ni wanga Tu.
 
Nini kilitangulia kati ya wakoloni na kilimo cha mahindi,.!?,nyie watu mna matatizo kichwani hata kutumia google hamjui. Ila mna justify upumbavu wenu kwasababu nyepesi nyepesi..
Mbona kama unateseka sana?
Hujaambiwa usile ugali, kama unaona ni mchongo we fakamia tu.... ila ukae ukijua unakula chakula cha mufugo.
 
Hivi hizi Pumba munazoshusha hapa JF huwa munazitolea wapi?
 
Na sehemu wakoloni waliyokuja kumaliza mchezo kwa kuwavuruga akili mazima wazee wetu ni pale walipoingia porini kutafuta majani yanayoteleza na kuyapa jina la mlenda na kufanya hiyo ndio combinations bora ya mlo wa ugali.
Usielewe hata ukichanganya bamia na mboga ya maboga unatengeneza mlenda! Poor you.
Muda mwingine punguzeni ujuaji
 
Asili ya mahindi ni Amerika ya kati na Mexico.

Hata ukiangalia katika nchi zenye uzalishaji wa mahindi kidunia utaona katika nchi 15, ni nchi 3 tu ambazo ni za Afrika.

Nazo hizo zimeshika nafasi ya mwishoni.
View attachment 2944737


Mahindi yalikuja Afrika karne ya saba yakianzia Pwani ya Afrika.

Kabla ya karne ya saba, Afrika hakukuwa na kitu kinachoitwa mahindi.
Mihogo na mtama vilikuja karne ipi?
 
Mwenyewe nilishtuka mapema nashukur Mungu nikajiuliza kwann wazungu hawali maindi, binafsi mm kitu kama mzungu hatumii na mm siwez tumia ndio utamadun wangu coz wazungu wapo mbele kifikra miaka elfu tano kuliko sisi ngozi nyeusi!! Hata kama mtakataaa.

Hvo nikapiga marufuku ugal pale home ni mwendo wa wali ndizi,viazi.naona positive changes nyingi sana .

Ugali na maindi kiujumla ni chakula Cha wanyama..wengi hamuwez elewa huyu mtoa mada anamaanisha nn sabb ugali ushawaathiri uwezo wenu wa kufikiri!!

Mwisho ugali ni sumu inayoua taratibu kama sigara na pombekali
Na hivyo vyakula vyao ndo vinawafanya kuwa laini laini na kuwapa hamu ya kufukuliwa nyuma na kuwapa akili za kutambua haki za Mashoga, endelea kuika damiza familia yako kwa kuleta uzungu wa kishamba
 
Na ukisoma historia zinadia kuwa kabla ya wakoloni kuja Afrika, Afrika haikuwa na utamaduni wa kula ugali.

Kwa hiyo ujio wa wakaloni ndio mwanzo wa ugali.

Kabla ya wakoloni Afrika ilikuwa na wazee timamu sana kwenye kichwa ila hayo yote yalikuja ku change ghafla baada ya ugali kuwasili.

Ukifanya tafakuri ya kina utaona wakoloni walitumia ugali kama bio weapon ya kuwadhoofisha wazee wetu kiakili.

Na sehemu wakoloni waliyokuja kumaliza mchezo kwa kuwavuruga akili mazima wazee wetu ni pale walipoingia porini kutafuta majani yanayoteleza na kuyapa jina la mlenda na kufanya hiyo ndio combinations bora ya mlo wa ugali.

Baada ya hapo ndio tumefikia hapa tulipo kila mtu amepoteana, tumekata ringi hatuna dira.

And sometimes if we're being honest, we gotta admit to speak the truth, that the world is better off without us.
Aiii sikuwahi kujua ugali ni mbaya kiasi hiki..
 
Watu wengi wanaamini ugali ndio chakula pekee cha kuupa mwili nguvu na afya njema lakini si kweli

Ugali ni mlo hatari ni kama sumu ndio maana hata wanyama wachoyo kama mbwa, nguruwe, paka, nk. Hawana akili lakini katu huwakuti wakila ugali maana ni chakula kisicho na nutrients zozote mwilini.

Hapa Tanzania jamii na makabila makabila makubwa hatupendelei ugali mfano sisi watu wa mkoa wa Kagera, Moshi(wachaga) na Mbeya hawali ugali lakini Tanzama mikoa duni kama Dodoma, Singida, Lindi, na watu wa Pwani wala ugali

Wenzetu wamataifa mengine wana afya afya na wala hawajui ugali ni nini Tazama wenzetu kutoka west Africa hawali maugali kama Watanganyika wana body zimejengeka.

Waganda, Wakenya, Wanyarwandwa hawali ugali. Mtu ukila ugali kwanza unalewa kama umepiga jibapa la Konyagi masaa mawili, ukila ugali wa Mara digestion ni ngumu mwilini chakula hakushuki hupati choo siku mbili, sasa hicho chakula au uchafu tu.

Wazungu na warabu wako vizuri kiafya wala hawayajui maugali ni nini wao wanajilia ngano, wali, nyama na maziwa, sisi Watanganyika kutwa usiku tunakula maugali na milenda kama tumerogwa

Madhara ya ugali kwa watu wetu, tumekosa washiriki wazuri kwenye michezo yani leo umpeleke Kibwana amkabe Sadio Mane AFCON haiwezekani.

Watoto hawana akili mashuleni wapo tu wamechoka yaani wamelewa chakali shuleni hawaewi kisa kula maugali.

Miili kama midogo kama digidigi unakuta mwanaume Dar anavamiwa na panya road anajificha kisa kula maugali

Sipendi ugali nakushauri usije ukala haya sumu ya akili na mwili ugali ni sumu kali

Nikiwa Rais nitapiga marufuku ugali

#kataa ugali Mtanganyika
Habari Mtoa Mada ngara23
Unaweza kuwa unahoja lakini uwasilishaji wako Ukavuruga hata maana ya amada yako uliyoitoa..

Ni kweli kuna baadhi ya vitu unaweza ukawa ulisema kweli..

Kama uliposema (Ntanukuu)

"Watu wengi wanaamini ugali ndio chakula pekee cha kuupa mwili nguvu na afya njema lakini si kweli"

Hili ni Kweli kabisa watu wengi wanaamini hivyo Ilihali si kweli...Kuna vyakula vingine vya kuupa Mwili nguvu vya kiasili kama magimbi,Viazi aina zote,Mihogo n.k

Hilo ni jambo ambalo kati ya yote Ndilo uliloelezea ukweli mengine ila mengine yanatia mashaka

MisInformation Ulizotoa Kuhusu Ugali

  • KUHUSU SUMU Na KUWA UGALI HAUNA NUTRIENTS ZOZOTE
Ugali Ni Sumu , Jibu "Partially True and Partially false "Ni ukweli na pia ni Uongo"

ni kweli kwamba kuna baadhi ya mahindi, Unga na hata ugali una chembe chembe za Heavy metal ambazo ni mycotoxins zinazoitwa Aflatoxins au kwa jina jingine Aspergillus flavus zipo kiwango kidogo sana yaani (μg g−1)..

Japo kama utakula Wingi sana wa mahindi na ugali wenye chembe za Aflatoxin..Utapata Kitu kinaitwa kitaalam aflatoxicosis..
Ambazo inaweza kukusababishia maradhi mengine kama cancer, Infertility, organ failure hasa Kidney..

Lakini Angalizo ni kuwa Si kila Ugali au kila unga unakuwa na Mycotoxin mpaka uwe umekula Mahindi au Ugali wenye Toxin hiyo ndo utapata hayo maradhi...


Lakini kwa Tanzania Kuna case ambazo.ni chini ya 2% ya wagonjwa wote waliowahi kutibiwa kwa kupata Aflatoxicosis...
Kwahyo Tanzania Tuko safe na ugali tulionao..

  • KUHUSU UGALI KUTOKUWA NA NUTRIENTS YOYOTE
Hili lina Ukweli kwa 0.001% na lina uongo kwa 99.99%
kwanini..?

Katika vyakula vya Asili,Ugali ni miongoni mwa vyakula vyenye Lishe bora sana na hasa chanzo kikubwa cha wanga na Nishati..
Katika kila 100 grams ya Unga wa Ugali kuna viti vifuatavyo (Kumbuka Mtu mzima anakula Walau robo ya Ugali ila hapo kwa kila Tonge au Nusu tonge)
  • Calories 370
  • Total Fat 1.8 g ambayo ni sawa na 2% ya Daily value kama utakula hivyo kila siku
  • Saturated fat 0.2 g daily value ya 1%
  • Trans fat regulation 0 g
  • Cholesterol 0 mg
  • Sodium 7 mg0%
  • Potassium 142 mg4%
  • Total Carbohydrate 79 g26%
  • Dietary fiber 3.9 g15%
  • Sugar 1.6 g
  • Protein 7 g14%
  • Vitamin C0%Calcium0%
  • Iron6%Vitamin D0%
  • Vitamin B610%
  • Cobalamin0%
  • Magnesium8%
Hapo ni kwa kiasi sijataja zote halafu unakuja unasema kuwa Haina Nultrients unajua maana ya Nutrients??

Umezungumzia kuhus Mataifa mengine afrika kwmaba hawali Ugali

Hapa ndo nilipogundua kumbe kuna uwezekano hujatembea hata Afrika yote hata kenya Tu hujafika! Uganda pia Hujafika?

Sasa nisikilize!
Hakuna nchi Afrika ambayo haili ugali..

Uganda na Kenya na Tanzania wote wanakula Ugali..
  • Ukienda kenya watauita Sima/Nsima
  • Ukienda uganda wataita Posho
  • Tanzania wataita Ugali/Nguna/Dona/Bondo
  • Central Africa na zambia,Malawi pamoja na Kongo huko wanaita Nshima
  • Zimbabwe wanaita Sadza
  • South Africa na sehemu na Botswana wanaita Pap kwa ule mlaini ila ule wenyewe wa Kisukuma mgumu wanaita Bogobe au
    Stywe
  • Sierra Leone, Guinea, Liberia, Cote D'Ivoire, Burkina Faso, Benin, Togo,Nigeria, Cameroon, Angola na Gabon huko wao wanaita Fufu
  • Ghana wanaita Banku au Akple
Kama kuna Nchi au sehemu sijataja nikumbushe nitakuambia wanaitaje..

Mwishoni Umeweka sawa kuwa hupendi ugali bhasi kitu ambacho hukipendi usikipakazie Mambo mabaya ili na wngine wakichukie..
Hata mimi sipendi ugali ila siwezi kuufanya wengine wasile
 
Watu wengi wanaamini ugali ndio chakula pekee cha kuupa mwili nguvu na afya njema lakini si kweli

Ugali ni mlo hatari ni kama sumu ndio maana hata wanyama wachoyo kama mbwa, nguruwe, paka, nk. Hawana akili lakini katu huwakuti wakila ugali maana ni chakula kisicho na nutrients zozote mwilini.

Hapa Tanzania jamii na makabila makabila makubwa hatupendelei ugali mfano sisi watu wa mkoa wa Kagera, Moshi(wachaga) na Mbeya hawali ugali lakini Tanzama mikoa duni kama Dodoma, Singida, Lindi, na watu wa Pwani wala ugali

Wenzetu wamataifa mengine wana afya afya na wala hawajui ugali ni nini Tazama wenzetu kutoka west Africa hawali maugali kama Watanganyika wana body zimejengeka.

Waganda, Wakenya, Wanyarwandwa hawali ugali. Mtu ukila ugali kwanza unalewa kama umepiga jibapa la Konyagi masaa mawili, ukila ugali wa Mara digestion ni ngumu mwilini chakula hakushuki hupati choo siku mbili, sasa hicho chakula au uchafu tu.

Wazungu na warabu wako vizuri kiafya wala hawayajui maugali ni nini wao wanajilia ngano, wali, nyama na maziwa, sisi Watanganyika kutwa usiku tunakula maugali na milenda kama tumerogwa

Madhara ya ugali kwa watu wetu, tumekosa washiriki wazuri kwenye michezo yani leo umpeleke Kibwana amkabe Sadio Mane AFCON haiwezekani.

Watoto hawana akili mashuleni wapo tu wamechoka yaani wamelewa chakali shuleni hawaewi kisa kula maugali.

Miili kama midogo kama digidigi unakuta mwanaume Dar anavamiwa na panya road anajificha kisa kula maugali

Sipendi ugali nakushauri usije ukala haya sumu ya akili na mwili ugali ni sumu kali

Nikiwa Rais nitapiga marufuku ugali

#kataa ugali Mtanganyika
Ww hujasafiri africa yote wanakula ugali huko nigeria chakula kikuu ni ugali hakuna mtu mweusi ambae hali ugali huko kwenu kagera ndio mkoa maskini zaidi tz sasa kama hamli ugali huoni umaskini wenu unatokana na kutokula ugali?
 
Back
Top Bottom