Ulianzaje kukaa gheto?

Wakuuu nitaleta uzi niliuahidiissue Ni kua Nilikua site. But nimerudi home usiku huu.
Pia kuna wahuni wamedukua account yangu ya Instagram. Yaan Ni shida Kama Kuna mtu anajua namna ya kurudisha anisaidie.
Aisee pole sana mkuu,vp ukijaribu ku recovery password kuptia email yako na namb yako,au walisha change kila kitu?
 
Chief kumbuka ukinunua hayo mahitaji uliyotaja hapo juu unatumia zaidi ya siku moja,week,mwezi mpaka miezi mfano mafuta na gesi. So kupika kuna save sana pesa pia kunakupa options za kuchagua ule nini na sio kuchaguliwa.

Mfano mimi naweza kupika mboga ya gharama za 2000 mpaka 3000 na nikaila kwa siku tatu. Mboga haifunikwi ili kuzuia isichache kama huna fridge.
 
Nenda kinyerezi utanishukuru mkuu
 
Bro kuna vitu ukiwa ghetto unaweza nunua kwa wingi mfano mafuta ya kupikia,unga,mchele sukar na vya aina hio,unakua unabadili mboga tu...Kujipikia ina save sana pesa
Kwa sisi tunaokaa bachela....kupika sio inshu...inshu ni kuosha vyombo...hapo ndo napataga changamoto naona bora nikale mgahawani...lakini economically, kupika kuna save cost.
 
Kwa sisi tunaokaa bachela....kupika sio inshu...inshu ni kuosha vyombo...hapo ndo napataga changamoto naona bora nikale mgahawani...lakini economically, kupika kuna save cost.
Kuosha vyombo bro,imagine umepika usiku asubuhi unatakiwa uwahi mishe mishe hapo vyombo vinakuangalia
 
chakula cha mtu mmoja mkuu ni ghali. mboga tu kununua hapo hujaiunga haipungui 3000. haya viungo mafuta ya kula labda umenunua vya mwezi mzima. bado moto. Bado muda + kuongeza kazi ya kuosha vyombo.
 
chakula cha mtu mmoja mkuu ni ghali. mboga tu kununua hapo hujaiunga haipungui 3000. haya viungo mafuta ya kula labda umenunua vya mwezi mzima. bado moto. Bado muda + kuongeza kazi ya kuosha vyombo.

Wewe sijui upo nchi gani aisee
Samaki mmoja 1000
Nyama inaanza kupimwa 1000 na robo ni 2000
Njegere 1000 glass (huwa nakula milo miwili )
Mboga majani 500 fungu ( huwezi maliza)
Dagaa ndo tusiseme bei
Sasa hio buku 3 ya mboga gani ya 3000 ?
Ukinunua njegere za buku na nyanya za mia mbili unapata mboga ya siku nzima (Mchana na jion)
 
Bora umenisaidia kujibu.

Nilivokuwa chuo mboga ya buku nakula mara tatu.

Dagaa wa jero.
Karanga 200.
Nyanya 200.
Pilipili naomba ya bure.

Mafuta nilikuwa na dumu la lita 3 natumia miezi 4. Vitunguu nilikuwa nanunua Nata pale mwanza kimfuko jero au buku. Nikinunua vimfuko viwili natumia miezi mitatu nachagua tule tudogodogo nachanganya na tangawizi.

Unga wa ugali.

Nanunua mahindi sado moja 2500. Nasaga kama dona. Nikisaga unga mwngi utaoza that's why. Unadumu kwny kideli mwezi na nusu. Sili ugali daily lakini
 
haya unayoyazungumza me nayaishi singumzii nadharia kupika msosi wa mtu mmoja ni gharama.
huyo samaki yupi wa buku tuma hata picha tuone. Hvyo vikorombwezo vyote ukija ukipiga hesabu 4000-5000+ imwkatika.
 
haya unayoyazungumza me nayaishi singumzii nadharia kupika msosi wa mtu mmoja ni gharama.
huyo samaki yupi wa buku tuma hata picha tuone. Hvyo vikorombwezo vyote ukija ukipiga hesabu 4000-5000+ imwkatika.
Hapana mkuu, kujipikia ni gharama nafuu kuliko kununua hotel. Ila ni kazi kama hupendi kupika.
Hizo gharama za 4,000 unazopiga hapo ni milo kadhaa sio mmoja. Kwa hapa nilipo Kuna visamaki vya mafungu vya 1,000 vinakuwa 4, hapo nikiamua ni milo 4 tayari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…