Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Ulifikishaje Milioni 10 ya kwanza?

Needs vs wants. Ukifanya tathmini hio 3m au 4m uliyofikisha kutunza halafu ukatumia, utaona kwamba wala matumizi yake leo hii hayaonekani. Watu kinachowamaliza ni matumizi. Nilitoka Tz maskini hata buku ikawa inanipiga chenga, nikaenda USA nikaanza shika usd 5000 kwa mwezi... ambayo kwa exchange rate ya sasa hio ni zaidi ya tshs 10m. Nikawa nanunua suti za $1000 (Sean John), viatu ni jordans, nike, etc. Bling bling kibao. Magari nikawa nabadilisha kila mwaka (USA gari unalipia kwa mwezi kwa hio ni kama mkopo tu). Matanuzi kibao. USD5000 ikawa hata haitoshi kwa matumizi yangu kwa mwezi.
Kwa sasa nimemudu kuwa saver mzuri. Matumizi yasio na msingi sifanyi tena. Nguo sijanunua sijui miaka mingapi. Nanunua viatu tu mara moja moja. Nimeweza ku-save millions and millions and millions. Na nimejenga sana na nina rasilimamali kibao tena kwa hela binafsi na SIO YA MKOPO. PIA NDUGU SIKU HIZI NIMEWAFYEKELEA MBALI. Hakuna mnyonya damu mkubwa na mbaya kama ndugu ambaye hajapambana kama ww kimaisha ila anataka ale tu kwa mrija kupitia jasho lako.

Mkuu naomba niku inbox unipe namna hapa
 
Haya mambo mara nyingine inawezekana kabisa mkuu.
Mie ni suppliers wa raw materials kiwanda fulani(japo siko peke yangu). Ila mzigo wa kujaza gari 1(pulling) unanigharim 1.2M. Mwenye kiwanda anatuma gari kwa gharama zake.
Ukifika kiwandani mie napata net profit sio chini ya 2M kwa gari 1. Na ni kazi ya siku 2 au 3 tu gari imejaa.
Duuuh hongera sana mkuu
 
Habari jf

Katka kupambana na maisha kuna malengo tunajiwekea Shida n changamoto ya kuyafikia. Mwanzo mwa mwaka 2016 nilijiwekea target kufikisha milion 3.

Kwangu ilikua hela nyingi coz nilikua nasoma na hela ambazo nilikua nashika ni laki laki mwisho laki 5 balance ya akiba laki moja!!...lakini baadae nilipataga kazi kwaiyo kushika milion 3 ikawa cyo kazi but siyo akiba!! Unakuta hiyo milion tatu ndo ufanye kila kitu akiba au saving ndo laki 3 au 5.

Najaribu kupambana nifike milioni 10 wap!!

Kila ikifika milioni 3 au 4 napata shida natumia. Sasa nilitaka tubadilishane experience na wanajf wenzangu ambao mmeshavuka huko au mna idea

Nb:hapa naongelea saving ,hela unayoisave baada ya kufanya mambo mengine

Je, wewe ulifikishaje milioni 10 yako ya mwanzo?
Mwaka 2016 baada ya kumaliza chuo,Maisha yalikuwa magumu Sana,nilikuwa siwezi hata kupata vocha na Kula kulikuwa ni kwa manati.nikaanza kufanya kazi za saidia fundi kujenga nyumba,,KWA KWELI NILIDHARAULIKA SANA PALE MTAANI!!,niki-apply kazi siitwi hata kwenye interview,nikipeleka CV door to door,wanaishia tu kusema CV ni nzuri lakini kazi sipewi!!home hali ni Mbaya,nikimuangalia mama nasikitika sana, mana Kipindi niko shule ilikuwa inafika kipindi anauza ardhi na vitu muhimu ili nisome, lakini ajira hakuna!!Mwaka 2017 nikaweka vyeti pembeni nikaanza kuokota vyuma chakavu(screper)kwenye Madampo na Mahali popote pale nitakapo pata ilimradi tu isiwe ya kuiba,ilikuwa ni fedheha lakini nilikuwa sina namna nyingine,mwezi wa Saba nikawa nimefikisha tani1½ nikauza nikapata laki5,baada ya hapo nikanunua piglets8 wa kienyeji@30000,nikatumia kama Laki2½ hiv,2wakafa maana nilikuwa nawafuga kibabe, wakabaki6 nikawakuza hadi mwezi3,2018,nikaja kuuza kila mmoja lak1.75 nikapata million 1na elf50..nilikaa mwezi mzima nikitafakari ni biashara gani naweza kufanya..baada ya hapo niliamua kufanya biashara za kujumua mpunga mwezi 5,,nikawa naenda Mbalari na Kamsamba-ya ziwa Rukwa.nilikuwa nachukua shambani kwa Bei rahisi nakuja mjini Mbeya nakoboresha nauza. Mwezi wa 9 pesa ikawa imeshakua million 2.8.msimu wa mpunga ukawa umeisha.nikarudi home kutafakari tena nifanye nini..siku moja napitia baadhi ya timu barani ulaya na africa nikaona Kama Kuna fursa flani,.(maana wakati niko kwenye msoto,ilibidi nijifunze kubeti) ,nikasema potelea mbali wacha nirisk elf 30 leo,nikaingia parimatch wakati ule walikuwa hawakati Kodi nikaweka Odd 35.6,KWELI NIKAAMINI MWENYE NACHO HUONGEZEWA,,tiketi ika-WIN nikapata mili1.10 hiv.,wakati nafanya kazi za saidia fundi hakuna tiketi niliyo bet na ika-WIN..na hakuna pesa niliyopata kiurahisi Kama hii..baada ya hapo nikawa nafanya scalping natafuta odd ndogo nastake pesa kubwa nikakuta pesa inakuwa kiutani utani hadi najishangaa..sikumoja nikajiRISK tena nikaweka STAKE ya mill.2 kwa ODDS.3 nikapata milioni 6,sikuamini Kama ni pesa yangu,,NIKAJIULIZA MBONA KIPINDI KILE KWENYE MSOTO MAMBO HAYAKUWA HIVI,?!maana niliitumia takriban karibu miezi7 kupata Tani moja ya vyuma chakavu!!BAADAE ukafika msimu wa kilimo Nikaenda Mbeya vijijini kulima viazi mviringo nikatumia Kama milio1.8,nikavuna nikapata millioni3.4.mpaka Sasa naendelea kujishughulisha na kilimo ufugaji na NA PESA YANGU TAYARI ILISHAVUKA MILION10,naelekea 20mill.
 
Maisha haya! Input yako ya ntaji mbona haiendani na output ya faida?

Mimi niliwekeza milion 1.9 na kila siku nikawa natengeneza net profit ya 300k kwa miezi kadhaa!
Biashara Gan mzee
 
Mwaka 2016 baada ya kumaliza chuo,Maisha yalikuwa magumu Sana,nilikuwa siwezi hata kupata vocha na Kula kulikuwa ni kwa manati.nikaanza kufanya kazi za saidia fundi,,KWA KWELI NILIDHARAULIKA SANA PALE MTAANI!!,niki-apply kazi siitwi hata kwenye interview,nikipeleka CV door to door,wanaishia tu kusema CV ni nzuri lakini kazi sipewi!!home hali ni Mbaya,nikimuangalia mama nasikitika sana, mana Kipindi niko shule ilikuwa inafika kipindi anauza ardhi na vitu muhimu ili nisome, lakini ajira hakuna!!Mwaka 2017 nikaweka vyeti pembeni nikaanza kuokota vyuma chakavu(screper)kwenye Madampo na Mahali popote pale nitakapo pata ilimradi tu isiwe ya kuiba,ilikuwa ni fedheha lakini nilikuwa sina namna nyingine,mwezi wa Saba nikawa nimefikisha tani1½ nikauza nikapata laki5,baada ya hapo nikanunua piglets8 wa kienyeji@30000,nikatumia kama Laki2½ hiv,2wakafa maana nilikuwa nawafuga kibabe, wakabaki6 nikawakuza hadi mwezi3,2018,nikaja kuuza kila mmoja lak1.75 nikapata million 1na elf50..nilikaa mwezi mzima nikitafakari ni biashara gani naweza kufanya..baada ya hapo niliamua kufanya biashara za kujumua mpunga mwezi 5,,nikawa naenda Mbalari na Kamsamba-ya ziwa Rukwa.nilikuwa nachukua shambani kwa Bei rahisi nakuja mjini Mbeya nakoboresha nauza. Mwezi wa 9 pesa ikawa imeshakua million 2.8.msimu wa mpunga ukawa umeisha.nikarudi home kutafakari tena nifanye nini..siku moja napitia baadhi ya timu barani ulaya na africa nikaona Kama Kuna fursa flani,.(maana wakati niko kwenye msoto,ilibidi nijifunze kubeti) ,nikasema potelea mbali wacha nirisk elf 30 leo,nikaingia parimatch wakati ule walikuwa hawakati Kodi nikaweka Odd 35.6,KWELI NIKAAMINI MWENYE NACHO HUONGEZEWA,,tiketi ika-WIN nikapata mili1.10 hiv.,wakati nafanya kazi za saidia fundi hakuna tiketi niliyo bet na ika-WIN..na hakuna pesa niliyopata kiurahisi Kama hii..baada ya hapo nikawa nafanya scalping natafuta odd ndogo nastake pesa kubwa nikakuta pesa inakuwa kiutani utani hadi najishangaa..sikumoja nikajiRISK tena nikaweka STAKE ya mill.2 kwa ODDS.3 nikapata milioni 6,sikuamini Kama ni pesa yangu,,NIKAJIULIZA MBONA KIPINDI KILE KWENYE MSOTO MAMBO HAYAKUWA HIVI,?!maana niliitumia takriban karibu miezi7 kupata Tani moja ya vyuma chakavu!!BAADAE ukafika msimu wa kilimo Nikaenda Mbeya vijijini kulima viazi mviringo nikatumia Kama milio1.8,nikavuna nikapa millioni3.4.mpaka Sasa naendelea kujishughulisha na kilimo ufugaji na NA PESA YANGU TAYARI ILISHAVUKA MILION10,naelekea 20mill.
Ukifikisha mil 20 unataka uzifanyie nini
 
Nilipata kazi kwenye mradi ambayo monthly plan ya kila mwezi ni lazima nibakie na 3.5m -4m kila mwezi..

Km nimeomba million sita ya kazi basi 3.5m ni yangu kwahiyo mwendo ulikuwa huo kwa kama miaka 3,baada ya hapo wabongo walivyo wangese wakaanza kuleta uswahili kwenye pesa za wezi wa madini yetu ikawa inashuka tu mara 2m mara million moja kufika mwaka wa tano wa kazi hela ya kupiga ilikuwa 500k tu kwa mwezi...


Kwahiyo million 10 niliipataga ndani km ya miezi mitatu ya kaZi.Nashukuru sikuwa na mambo mengi hivyo ile pesa ilinifikisha mbali.Mradi umeisha nimepata kazi kwenye kampuni eti deal kwa mwezi unapata km 200k tu [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] yaani maisha haya .

Nikikumbuka nilipotoka basi nacheka tu
 
Kwanza hongera sana kwa kazi uliyopata ni jambo la kumshukuru Mungu walau una sehemu ya kupata ujira wako!

Kuhusu suala lako, pia naomba nikupongeze kwa kuwa na malengo chanya. Tukirudi kwenye suala lako la msingi ningependa kukwambia yafuatayo:

1) Jitengenezee utaratibu wa kuweka akiba na uwe na nidhamu.
Hapa nataka kusema nini? Kwamba chagua bank ya aina yoyote enenda kafungue saving account [zipo aina mbali mbali za saving account - utachagua itakayo kufaa].

Then after, chagua kiasi chochote ambacho kila mwezi utakuwa unakipeleka kwenye account akiba yako. Mfano kama unapokea 1.5m, hakika kila mwezi ni lazima 500,000 uipeleke kwenye account. [Hii iwe mandatory]

Mfano unaweza kwenda pale KCB Bank ukafungua ile saving inayotoa 7% interest per annum.

Sambamba na kufungua lazima nidhamu ya pesa ishike mkondo wake, bila nidhamu itakuwa ni ngumu sana kufikisha malengo yako [Hakikisha kila mwezi unapeleka hiyo pesa na isipungue hata sent labda uzidishe!

2) Tafuta biashara ndogo ndogo ufanye ili zikuongezee kipato, ujue kutegemea only one source of income ni tatizo! Hii biashara utakayoanzisha ndo itakupa pesa ya kula na itakusaudia usipate tamaa yq kwenda kuchokinoa kwenye saving account yako!

3) Punguza matumizi yasiyokuwa ya lazima, hili kitakusaidia sana kufanikisha point no. 01

Mungu akubariki katika utekelezaji wako, Amina[emoji1317]
Ushauri mzuri, sema changamoto ipo hapa "Tafuta biashara ndogo ndogo ufanye ili zikuongezee kipato", kupata hiyo "biashara ndogo ndogo" ndio changamoto kwa walio wengi wetu
 
Ndiyo hivyo. Shida kubwa watu wengi wakienda shule kidogo anaona biashara za mtaani ni kama kushika uchafu. Kuna kijana mmoja mwalimu s/msingi wa kichaga alipanga chumba kwetu akaona fursa akafungua genge la mbogamboga hapo nje kalitengeneza kwa mabanzi tu ya kawaida. Saizi anauza laki 8 kwa siku. Tunataka kuanza kumtoza kodi lakini tunajishtukia kwa aibu, coz ni kasehemu ambacho wala hatukujua kuwa ni potential. Sasa mwambie graduate wa Mzumbe au Udsm afungue genge.
Hapo kwenye kuuza laki nane kwa siku hapo mmmh kweli magenge yanalipa.
 
Back
Top Bottom