Uliondoka kwenu na kuhamia kwako ukiwa na umri gani?

Uliondoka kwenu na kuhamia kwako ukiwa na umri gani?

taget zangu nimiliki nyumba yangu nikiwa na miaka 27 lakini ilipita hata kiwanja Sina mpaka miaka 29 nikapata kiwanja kwa bei nzuri chapu nikanunua kumbe kilikua na migogoro ya kifamilia aisee nilizunguka mahakamani Kama mweu nikipambanaia haki yangu zaidi ya mwaka nikafanikisha .

Then nikajikusanya Sana kwa kujinyima punguza baadhi ya mambo ya siyokua ya maana hadi ndg na najamaa wa vizinga wakanisema Sana me bahili.

Nimefaniki hamia kwangu mwezi wa sita mwaka huu ambapo na miaka 31
nashukuru kwa hili kikubwa tupambane kidg kdg unaweka kitu.View attachment 2675315
Nyumba kali sana
 
Hongera
Sema neno lolote kwa U30 wasio na nyumba
Wazidi kupambana tu, kuiheshimu pesa na kuweka nadhili kwamba naweza basi, mfano wakati naanza kujenga nyumba kaka yangu aliniambia nile maisha kwanza kujenga baadae, nikasema ninachopata ntakusanya mdogomdogo mambo yaende na kweli nilihamia kwangu kwa kipindi cha miaka na nyumba ya ukweli ila watu wanajua kuwa nimepanga nawachora tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mtu amejenga chanika kajumba hakaeleweki alafu anafanya kazi Mjini haoni kabisa adha na gharama yeye kwake muhimu kumiliki nyumba any way ni mtazamo tu.
Ni mtazamo wako pia
Kwako ni kwako hata uwe nje ya mji na unafanyia kazi mjini.

Unaweza kufuga na mifugo ikakulipia nauli za kazini town na ikakulisha.

Mshahara ufanye mengine.

Pili...watu wanaoona mbali hununua nje ya mji kwasababu bei ni ndogo ili anunue eneo kubwa zaidi.

Eneo likiwa kubwa, mji ukikufikia na ukakakata kipande cha ardhi...utapata ndefu inayoweza kukupa mtaji.

Ishi kwa malengo mkuu sio ubanane Manzese na haikusaidii kitu ...zaidi ya kujifariji ni karibu na kazini
 
Back
Top Bottom