Ulipokeaje na ulikuwa wapi siku ya tarehe 17 Machi, kifo cha Dkt. Magufuli

Ulipokeaje na ulikuwa wapi siku ya tarehe 17 Machi, kifo cha Dkt. Magufuli

Siku 3 kabla ya tangazo la Kifo chake.

Nilipitishwa ktk(ulimwengu wa roho)

Nilimuona JPM akiwa na mpambe wake.

Jpm Alionekana akiwa na huzuni saana,

Kuna briefcase ya flan ya Rais yule mpambe wa Rais alimkabidhi mtu flan(Ambae alikua kivuri sikumtambua sura wala jinsia).

Shortly Nilikuja kuelewa na kukumbuka maono hy usiku ule baada ya tangazo la msiba.



Taarfa za msiba.

Nilikua nimelala wakaja madogo,(walienda kucheki mechi bandani)

Wanaongea kwa sauti ya juu mpk nikashtuka nikaamka.

Ile kufungua mlango nikaskia "Jamani Magufuli kafariki"

Nikamuuliza we umejuaj?

Akaanza kuelezea.



"Si tulikua tunaangalia mpira ghagla akasimama juu muhuni mmoja, akasema kwa sauti kubwa...JAMAAAANI EEEH TAYARI!!!...wakasema kaachini acha ujinga,tyr nini..

Aksema TAYARI MAGU KAVUTA..

KAMA HAMUAMINI WEKENI TBC 1..

Ikawekwa tukamwona Samia Anahutubia kwa huzuni"

Hatujaendelea na mpra wote tumetawanyika"

Aisee tukawasha tv na redio tukakuta nyimbo za misiba zinapigwa .

Nilichoooka nilisikitika niliporudi kitandani ndo nikakumbuka siku 3 nyuma yale maono niliyoyaona kumbee yalikua na maana hyo.

Nilitokwa machooozi.
Sasa machozi yalikutokaje sasa? Hukuona umuhimu wa kunywa bia?
 
Daah kabla ya tarehe 17 tarehe 9 majaliwa anaenda njombe tarehe 12samia ana ziara tanga siku tatu kabla ya hizo tarehe malaika alikua akizungumza na mimi katika roho.

Nilimuota magufuli mara tatu ni baaada ya kuhutubia mbezi pale alinionyesha mungu magufuli amekufa nilipatwa na roho ya kuomba na kujinyenyekeza mbele za bwana kitu ninacho amini magufuli alikufa tarehe 8 mwezi wa tatu.

Nilimpenda huyu mtu kwa mara ya kwanza namuona magufuli nilikua nampelekea demu wangu zawadi katika siku yake ya kuzaliwa alikua anasoma baobab girls bahati mbaya siku ile ilinyesha mvua daraja la ruvu chini lilikatika mawasiliano ya barabara kutoka msata kuja dar kupitia bagamoyo road hayakuwa yanapitika.

ndipo mwamba alipofika na kurekebisha hali nikamuona niliwaza moyoni huyu anafaa kuwa raisi wa nchi na kweli ikawa nilimpenda sana huyu mwamba toka moyoni sijipiga kura tena nilianza kwake utamadun wa kupiga kura na umeishia kwake kibaya na kinachoniuma demu niliyempenda kaniacha na mwamba amelala milele ninamaumivu two side ni hayo
Ulikosea kuwapenda wote,huyo demu na huyu mwamba,
 
Binafsi niliumia sana siku hiyo hakuna wimbo uliokuwa ukiniumiza kila nikiusikia kama ule wa Msechu- UMETUACHA salama. Taarifa za kifo nilizipata mida ya saa sita usiku nikiwa kwenye basi la fikoshi Iringa to Mwanza. Jamaa alikuwa mwamba!!!
Nothing
 
Mimi nikiri sikuwa sawa tangu tetesi za kuumwa kwake nlikuwa naomba Sana kimoyo moyo isiwe kweli yaani.badi bhana siku yenyewe nilikuwa nimetoka kazini ile nalumzika kidogo baada ya kuoga kabla ya Kula nikapitia pitia jf Kwanza ili nilale, ile naenda bafuni kirudi wife ananiambia angalia itv huku analia aisee...kwa mara ya Kwanza nikaonja uchungu wa msiba tangu nizaliwe inauma Kama nini.nilikaa Kama siku mbili sielewi elewi mpaka sasa bado kwa mbali sielewi Mimi.
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
Utakuwa ulifaidi utawala wake
 
SIKU hiyo nilichelewa kulala nikawa busy nacheki movie, baadae nikasema goja niingie online kidg ndipo mfanyakazi mwenzangu Kwenye group ikaingia sms kasema pumzika mwamba kisha kaweka emoji za kulia nikshtuka nikampigia akanambia Magufuli kafa [emoji24][emoji24][emoji24] sikuamini asee.


Nililia siku mzee anaagwa Mwanza baada ya clip moja kuiona anasaidia mama kipofu kule Mara nililia sana.

RIP. mzee
Sawa
 
Taarifa za kifo chake nilizipata trh 9 kutoka kwa mtu ambae hawezi kudanganya ila nikajua uzushi tu.
Tetesi zikaendelea mitandaoni, sasa siku ya trh 17 saa 11 alfajiri nilikosa usingizi nikaingia jf nikakuta mtu kaweka uzi akisema " si watangaze tu raisi wa nchi yupo kwenye fridge wiki nzima si watangaze"

Yesuuuu, moyo ulidunda mbio nikatoka kitanda nikashika biblia sikuifungua nikapiga magoti nikasema Mungu nakuomba hiki nikachokihisi nikilinganisha na tetesi za mitandaoni mungu naomba isiwe ni kweli.
Yaani nilihisi naumivu ila nikajisemea hapana hizi hisia mbaya nikajiandaa nikaenda kazini.

Nikiwa ofisin kuna kijana mmoja kaingia akicheka kweli akasema "jiwe lazima lidondoke" nilimjibu magufuli hafi leo tukaishia hapo.

Nyumbani nilifika saa 3 nikajilaza kwenye sofa nikapitiwa usingizi, sasa nikiona simu ya mama inaita najua ni saa 4 usiku, nikampokea usingizini tukasalimiana mwisho akaniambia eti " dada nimesikia jpm kafa? Nikasema mama hao waongo.
Nilienda chumbani nikalala mida kama ya saa 6 kasoro naona shoga yangu wa moro ananipigia, bila hata salama nikasikia, " wewe unalala hovyo wakati raisi kafa? Yesuuuuuuu, usingizi ukikata nikamjibu, wewe ni uzushi uko mitandaoni, akasema washa tv samia anatangaza.

Fasta nikaingia insta nikakuta samata kapost yesuuuuu nilipiga kelele, na ninavyoishi mwenyewe, nikaanza kupigia watu nikiuliza.

Nikaona haitoshi, kuna ndugu yake jpm namjua nikampigia alivyopokea simu kwa muda ule nilijua tiyari, nilibaki tu napiga ukunga, kila ninaempigia yupo hewani watu wanalia aiseee.

Nakili magufuli nilikuwa namkubali kawaida tu ila sijui baada ya kusikia kifo chake yale maumivu yalitoka wapi yaan utadhani mimi ndugu yake. Nililia sana.

Kuna fala mmoja akanipigia najua hampendaji jpm, nikapokea nikasikia kicheko nikakata simu nikamblock. Siku mbili baadae akanitafuta kwa no nyingine nilimchamba hakuamini. Akinipigia siku hizi lazima awe na adabu sina hasara hata asipokuwa rafiki yangu.

Magufuli ulijua kuniumiza jamani.

RIP JPM.
Sawa
 
Funga domo lako usinisababishie nafungiwa jf, funga bakuli lako hujui watu tumeumia kiasi gani.
Mimi ni mtu wa kawaida kuna watu humu tunajuana face to face. We mjinga ungekuwa karibu yangu ningekudunda mbaya kwa hasira nilizo nazo.
Mamilion wanalia kwa ajili ya jpm wewe unaongea ujinga, hivi unajua jpm alikuwa muhimu kiasi gani?
Unajua nini maana ya uongozi wewe?

Akili kisoda wewe.
Acha kufokea watu sio wote walimpenda
 
Habari za kifo chake nilikua nazisubiria kwa hamu sana,nilikua nashinda Twitter kwenye page ya kigogo kwa ajili ya updates. Niko zangu home usiku mara naona updates za kutoka kwa mama Samia kwamba pombe imemwagika. It bacame the happiest day of the year for me .
 
Nilikuwa zangu kitandani mara my Mr akaja akanambia "magufuli kafa" nilichukua simu yake ghafla kuangalia kama kweli maana wakati ule nilikuwa natumia kitochi na laptop niliona tabu kulogin jf.....
Basi bhana ikawa ni amani tu sikulala mpaka kesho yake saa 10 jioni ndo napata usingizi.
Apumzike tu yule mzee kwa yale mafekeche yake yalokuwa yanaendelea sirini na wateule wake sina budi kusema awekwe mahala alipojiandalia.
 
Mimi nilichukulia poa kwanza nikawa naangalia tv ukapigwa ule wimbo" kaa nami ni usiku sana* nililia mpaka t-shirt na sofa vikalowa mpaka nikabadili nguo
 
M nlikuwa home,.nakumbuka siku hiyo tulikuwa na mechi maeneo ya kazini..tulimaliza mechi mida ya saa 12...ila nlikuja kujua kifo Cha rais muda wa asubuhi..
 
M nlikuwa home,.nakumbuka siku hiyo tulikuwa na mechi maeneo ya kazini..tulimaliza mechi mida ya saa 12...ila nlikuja kujua kifo Cha rais muda wa asubuhi..
 
Nilishtuka Sana [emoji15] nikijua asubuhi wakati najiandaa kwenda job .

Msiba sio mzuri hauzoeleki Ile asubuhi I was like"duuh [emoji15] so sad"

Jioni nikawa "anyway a good riddance,go to hell dear dictator"

Angekuwepo hadi leo.

1.Watu wasingepanda madaraka

2.Mdude angekuwa jela Hadi aozee huko.

3.Masheikh wa uamsho wangekuwa ndani .

4.Watu wangeendelea kuuliwa ,kufunguliwa kesi za kubambikiziwa

5.Wafanyabiashra wangeendelea kuisha Kama mashetani

6.Sabaya angekuwa anatesa Kama kawa mtoto mpendwa

7.Chalamila angekuwa Yuko mbeya anawatandika viboko hadharani wanafunzi

8.Makonda angeendelea kuwa Don wa magenge ya uhalifu.

9.doto James angeendelea kula 10% na kusaini mikataba isiyojulikana Wala kueleweka.

His death was a good riddance ,Yeah a good riddance.

Storm is over , and at least we can see a Sunshine. Somewhere beyond the clouds .
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119] Potelea mbali we elezea tu mambo yasiwe mengi mzee alikuwa katili sana yule.
Kwanza tangu nione Kigogo anaongelea hilo twitter, nilianza kuwa mtazamaji mzuri wa TBC.
Kisha nikadownload ule wimbo wa "hakuna Mungu kama wewe Bwana" nikawa nausikiliza taratibu na ule "Yupo Mungu mbinguni ajibuye maombi yetu".

Siku inatangazwa nilikuwa nimeweka TBC kwa hiyo niliipata pale pale. Nikajikuta naropoka hatimaye[emoji119]. Nikaweka ngoma yangu ya " Hakuna Mungu kama wewe bwana" nilisifu mpaka saa 10 usiku.
 
Back
Top Bottom