Ulishawahi kukosea muamala wa kiasi gani kwenye simu yako?

We ndio maana voda walikupa onyo uwe makini..🀣
 
wakati nna tigopesa alikuja mteja kutuma 10k nyie nikakosea nikatuma 100k πŸ˜€πŸ˜€aaah

mwingine kaja kununua umeme wa 20k nikanunua wa 200k
 
wakati nna tigopesa alikuja mteja kutuma 10k nyie nikakosea nikatuma 100k πŸ˜€πŸ˜€aaah

mwingine kaja kununua umeme wa 20k nikanunua wa 200k
Uwiiii,, wa umeme ulifanyaje? Maana wa 100k unaweza rudisha muamala, ila kama ndo alikimbilia kutoa
 
wakati nna tigopesa alikuja mteja kutuma 10k nyie nikakosea nikatuma 100k πŸ˜€πŸ˜€aaah

mwingine kaja kununua umeme wa 20k nikanunua wa 200k
Hiyo kazi ukiwa na mawazo kidogo tu lazima upuyange.
 
Kishingo upande πŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Mm nilikuwa nanunua vocha ya tigo kutokea CRDB application

Badala ya 1500...nikanunua vocha ya laki nanusu ..nilihaha


Ila nilimpata mshika wa tigo anaitoa kujirushia alivomaliza akanipa pesa yangu ila alikata arobain nikapoa tu bora nusu shari kuliko shari kamili
 
Usicheze na crdb simbaking nimetuma ikaniambia network problem hapo 1.5mil nikatuma tena baada ya dk 2 ikaanza kuniambia nimetuma 1. 5 kqenda airtelmoney ikaleta tena nikawa nimetuma 3mil. Msala kurudisha yile jamaa. Sitaki nimalizie..
 
Mimi hata sio muda sana ni tarehe 15 au 16 mwezi uliopita nilikosea namba ya malipo pesa ya thamani ya laki 2 na vocha ya elfu 50 iliingia kwa mtu asiemuaminifu hakupokea simu wala kupatikana tenaaaa nafikiri yule mshenzi Christmas yake ilikuwa nzuri sanaaa tokea azaliwe
 
Milioni moja na laki 2, siku hiyo Jamaa alinipa Hela nimuwekee Rafiki yake ila kwa kule nilipo ilinibidi nikusanye kidogo kidogo kwa Mawakala.... pale laki 2 kule laki 1, hapa Elfu 50 hadi ikatimia Milioni 1 na laki 2 ila nilikua naweka katika Line yangu....

Bwana Bwana kumbe zile namba kakosea na mbaya zaidi hakunipa Jina.... kesho yake ananipigia ILE HELA MBONA HAJAIPATA kumutumia ile meseji ya Muamala akasema AYAAAAA... HII NAMBA NILIIKOSEA nikapiga Tigo kama kujaribu tu, Tigo wakaniambia HII HELA ILIKUA TU HEWANI SABABU HII NAMBA ULIYOTUMA PESA BADO HAIJASAJILIWA ndo pona yangu
 
Duh! Bahati ilikuwa upande wenu sikuhiyo.
 
Binafsi sijawahi kukosea ila binafsi nimewahi kupokea hela kutoka sehemu mbili.

Kwanza niliwahi kupokea shilingi elfu kumi na mbili, baada ya muda akapiga mwanamke akilalamika amekosea na alikuwa anatuma hela ya mchezo ila akakosea namba. Akaniambia nimsaidie kuirudisha kwake au anipe namba ya alipokuwa anatuma niirushe kule. Kweli baada ya kunitumia namba zilifanana kabisa na yangu isipokuwa namba mwisho ndio zilibadilishana nafasi tu. Kweli nilituma na alishukuru.

Mara ya pili, niliibiwa simu. Siku iliyofuata nikaenda kurenew line na kununua kiswaswadu cha kuanzia maisha tena. Baada ya kurenew nilipata sms ya MPesa nimepokea shilingi elfu 25. Sikuwa na appointments zozote na watu, ikabidi nipigie kila mtu wa karibu ila hakuna aliyetuma. Sikuitoa, nikasubiri simu ya aliyekosea au kama itarudishwa ila hakuna. Ikanidi niishi nayo kwa uchungu mkubwa, nikawaza labda aliyenipiga smartphone yangu kanitumia kiinua mgongoπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Sijawahi kukosea ktk kutuma, ila mtu alikosea kutuma ikaingia kwangu. Ilikua 170k.
Wakati huo niko Likizo, aseeh nikakaa kmya tyuuh, ile hela sikuitoa, na ilitumwa kutoka bank, niliiacha humo humo,

Hadi likizo inakaribia kuisha ckupokea text ya kuuliziwa kuhusu pesa wala muamala kurudishwa bank, ilipobaki siku 1 ili nirudi shule, nkajiandaa zangu sku ya 2 nkasepaa.

Nimefika shule nkakaa week, sku ya weekend nkaenda town nkatoa ile hela na nkanunua ukumbusho had leo upoo. Cjui ile 170k ilitumwa na nani, had leo sijui hata .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…