Ulitumia njia gani kuishi kwa mtu bila kukuchoka?

Ulitumia njia gani kuishi kwa mtu bila kukuchoka?

Me nilikuwa naamka mapema mtoto wa kiume nawapikia chapat za maji watoto na wazazi walikuwa wanazipenda balaa plus naziweza kupika na viungo vyote.... Nikimaliza napika tena sup wakiamka wanakuta supu tayari wanakunywa na chapat juu...
 
Maisha yako unaishi kama unajimudu sasa unaishije maisha yako wakati umejipeleka kuomba msaada kwenye maisha ya watu wengine. Uwepo wako pale ushawabadilishia mfumo wao wa maisha so na wa kwako lazima uadjust mwende sawa.
Ni kwel kma yupo kwa mtu inabdi awe mbwa tu
 
Ndugu zangu humu hamjambo wote?

Humu ndani kuna wakati tunakuwa au tumewahi kuishi kwa watu au ndugu, lakini huwa baada ya kuishi kwa kipindi fulani mkiwa pamoja linakuja suala la kuchokana au kuchokwa. Hii inatokana na wewe kuhitaji msaada wao zaidi hasa wa hifadhi na chakula.

Sasa mimi nakumbuka nilipoacha kazi kwa Wahindi nikaenda kuishi kwenye familia moja huko Gongo la mboto, kutokana na maisha ya hiyo familia kuwa ni ya hali ya chini hivyo ilibidi nitumie akili sana ili wasinichoke.

Kwanza kabisa ilikuwa nikienda baharini kuvua samaki, nikirudi nabeba samaki kama wa 20,000 hivi maana nilikuwa nikienda Msasani au Feri nilikuwa namaliza hata mwezi ndio nashuka Gongo la mboto.

Baada ya kucha kazi ya uvuvi nikawa tu pale nyumbani, sasa ilikuwa maji ni ya shida kidogo ila uyapate ni umbali kama wa Km 1 hivi, kwahiyo nilihijitahidi sana maji yasiishe ndani, na kunawakati nikipiga saidia fundi narudi nyumbani na mazaga ya kula pale nyumbani. Kuna wakati nilimsaidia mama kufua, kufanya usafi wa ndani, kupika hasa ugali.

Nilifanya mambo mengi tu, ila zaidi ni baada pia ya kuonyeshwa upendo na ile familia.

Mpaka leo hii huwa wanatamani nirudi japo nilishajitegemea. Ila nikienda kuwasalimia mwendo ni ule ule, japo zingine mama ananiambia niache maana nimeshakuwa na familia na mimi.

Pia Mungu aibariki ile familia, nilijuana nao toka 2014 mpaka leo hii tumekuwa kama ndugu.
Hiyo uliyofanya wewe ni mgeni njoo mwenyeji apone.

Sehemu yeyote kinachofanya mtu achokwe ni kujipweteka na kuongezea wenyeji mzigo.

Huna uwezo pesa basi jitoe hata kusaidia shughuli za nyumbani. Unakuta jitu lipo ugenini linaweka miguu juu kuangalia tv asubuhi mpaka jioni. Likila hata kutoa vyombo haliwezi. Sasa jitu kama hilo usilichoke kwanini.
 
Kuishi kwa mtu au kwa watu sio poa nishalala pale mbagala bus terminal mara kibao nilikuwa nafanya kazi za shift sasa ikifika ile shift ya kutoka usiku nikifika nimefungiwa mlango nyumba ina geti huwezi kuruka narudi mbagala rangi tatu mpaka asubuh ndio naenda nilikuja kuhama nikatafuta chumba changu baada ya mda maana nilikuwa ndio nimeanza kazi sikuwa na hela za kulipia siwezi sahau nilivyopata hela kitu cha kwanza nikanunua kiwanja.
 
Hiyo uliyofanya wewe ni mgeni njoo mwenyeji apone.

Sehemu yeyote kinachofanya mtu achokwe ni kujipweteka na kuongezea wenyeji mzigo.

Huna uwezo pesa basi jitoe hata kusaidia shughuli za nyumbani. Unakuta jitu lipo ugenini linaweka miguu juu kuangalia tv asubuhi mpaka jioni. Likila hata kutoa vyombo haliwezi. Sasa jitu kama hilo usilichoke kwanini.
Anataka ahudumiwe sawa na mume wa nyumba,binafsi nimewazoesha watoto kuondoa sahani wanapomaliza kula,hata baba yao hukuti kala kaachwa sahani mezani..nkapata mgeni kiazi hatoi sahani wala kikombe alicholia hata kama kala peke yake mezani,baada ya kuona hata fadha Hausi anabeba chombo alicholia kupeleka jikoni alikuwa akimaliza Kula anshkilia kikombe mkononi hadi umpokelee.. hawa ndo wageni mizigo wanapewa chumba banda la uani still anataka afanyiwe usafi chumbani kwake mpaka choo chake peke yake..uzwazwa kabisa huu
 
Jichanganye Sasa vile umetoka ukirudi tu unawakuta wanaongea Ile umefika tu wewe wakikuona tu wote wanakaa kimya... Hata kuanza kuondoka eneo lile au sebuleni mmoja mmoja...
Hapo Ndugu yangu ondoka.
 
Back
Top Bottom