Uliwahi kuonesha jeuri ya pesa hata kama huna, ili kulinda heshima?

Uliwahi kuonesha jeuri ya pesa hata kama huna, ili kulinda heshima?

Nlinunua mkungu wa ndizi kwenye harambee baada ya kuona madem pale chapo nmenyoosha mkono wananiangalia kwa macho ya wewe shusha huo mkono uwezi panda hapo nikapandishana na wazee wale wa benki nikaishia laki mbili nilijua wangepanda zaidi ili niachie pale
Watu si wakauchuna laki mbili yangu ikanitoka nililia hadi kamasi
Nkaenda kuuza kwa mama ntilie kwa arubaini alfu
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]Aiseee hatari sanaa
 
My bad timeline yangu ndo haikua sawa, 2017 ndo nili purchase iphone 6 plus kwa 500k na kulikua na option ya kuisubiri kutoka china kwa 350k!! Iphone 6 plus haija wahi uzwa 1.6m mwaka 2016!!! Hakuna hiyo kitu. Na by then iphone 7 ilikua available kwa price hiyo it means ilikua ina range kati ya 2-3m haya wewe mjanja wa mjini tuambie kama hili lina ukweli??! Mshajionaga jamii forums ya baba yenu pumbavu.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]Ya baba yako bhasiii...!! Kujikuta wa mjini kumbe kengee mmoja tu
 
Juzi tu nilipanda bajaji eti fala anadai nauli Buku sababu sijui alikuwa na kadada mule ndanii me nkamwambia nilijua 500 ndo nauli ya utaratibu eti ooho kila mtu na utaratibu wake.. Akawasha bajaji akaanza kwenda akasimamisha mbelw kidogo ananiita eti bro njoo upande atakulipia sister nikamjibu nishaita Ubber[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] akawasha kibajaji akasepaaa ikaja bajaji nyingine nikapandaaa kufika mbele kidogo naoma jamaa anapiga debe nauli 500 ile pisii ilikuwa ishashukaaaa falaa sanaaaa mbwa yuleee jusii kengeee yuleee..
 
Jana nimeingia salon moja kali sana, ikabidi niulize bei ya kunyoa nikaambiwa 7,000/-. Nilitaka kukimbia ila nilipoangalia zile pisi mle ndani ikabidi nivimbe Nika nikanyoa nikalipa 7000 nikabakiwa na 3000/- siku ikaisha.
Umenikumbusha aisee mara ya kwanza kuingia hizi mnazoita barbar shop nilikuwa najiandaa kupeleka mahali ukweni, nilikuta vipisi humo ndani asikwambie mtu, sina hili wala lile naiona pisi inanishika shika kichwani inaniuliza unahitaji huduma gani Nilipata mshtuko wa ajabu, halafu wote wakajua na wakaona mshtuko wangu, wakatafsiri kuwa nimevamia mtumbwi wa vibwengo😂😂 wakawa na wasiwasi kama nina hela.
Wakati wa kulipa nilitoa burungutu la wekundu wa msimbazi kama 500k nikatoa 20k nikalipa. Vile vipisi vilitoa ukelele fulani hivi vya kujutia na sikuvipa hata shilingi 1😂😂😂
 
Hii inakubalika kabisa, Mimi nilikua Kasulu, nikawa na mazoea kwenda Bar kuangalia mpira, Kila nikienda pale naagiza maji, basi wahudumu wakawa wananipotezea. Hawana mzuka wa kunihudumia.

Basi, nikarudi Tena nakumbuka ilikua game ya Simba, wakagoma kunipa hata Kiti, akanihudumia Dada mmoja hakua na makuu, kwa hasira nikaagiza Castle Light 20. Nikamwambia Kaa hapa, hizi ni za kwako na yule mwenzio aliyenihudumia Jana.
Hahahahaha 🤪 sometimes you got to fight to prove you're a Man (Kenny G)
Mkuu siyo Kenny G ni Kenny Rogers ( the coward of the county)
 
Baada ya kumaliza chuo miaka hiyo nilienda mkoa x sasa ikatokea tu nimekuwa urafiki na mrembo fulani na amekuja kuwa mtu maarufu kwa sasa hapa tz.
Sasa kipindi hicho ilikuwa lazima kile wikiendi tutoke out na ilikuwa ni zamu wiki hii yangu wiki inafuata yeye, alikuwa na vi-bussiness vyake kwa hivyo ela ya kula sio ishu plus wanaume walikuwa wahonga na wanajigonga hovyo hovyo na alikuwa akiniambia kabisa jinsi watu wanafunguka na mimi pia nilikuwa najishtukia naona kabisa huyu hii sio level tangu..
kipindi hicho nilikuwa namiliki mashamba ya umwagiliaji hivyo j3 mpaka ijumaa kisha narudi mjini weekend .sasa nikija mjini nakuja na kiasi kamili 50000 tu kuspend ili nibalance hesabu sasa uchumi ukajumba mvua hainyeshi hela ya kuspendi naitumia kwenye vibarua..
aisee nilimis zile out mpaka nikajiona mnyonge nikampigia ndugu yangu mmoja anikopeshe laki tano kwamba nimepata matatizo nikatumiwa chapu sababu tu dogo analalamika zamu zangu nazingua...
Nilitumia tu kama 150K kwenye hizo out kisha from no where nika-change laini na nikapotea mazima mjini nikawa siendi tena niliona huyu dogo sio level yangu acha atafute mwanaume mwenye maisha mimi bado nilikuwa napambana tulikuja kukutana arusha ila bado nilimkazia mno mpaka nikaona hatia ila basi niliona ibaki hivyo!
 
Umenikumbusha aisee mara ya kwanza kuingia hizi mnazoita barbar shop nilikuwa najiandaa kupeleka mahali ukweni, nilikuta vipisi humo ndani asikwambie mtu, sina hili wala lile naiona pisi inanishika shika kichwani inaniuliza unahitaji huduma gani Nilipata mshtuko wa ajabu, halafu wote wakajua na wakaona mshtuko wangu, wakatafsiri kuwa nimevamia mtumbwi wa vibwengo[emoji23][emoji23] wakawa na wasiwasi kama nina hela.
Wakati wa kulipa nilitoa burungutu la wekundu wa msimbazi kama 500k nikatoa 20k nikalipa. Vile vipisi vilitoa ukelele fulani hivi vya kujutia na sikuvipa hata shilingi 1[emoji23][emoji23][emoji23]

Una tabia Kama ya jamaa fulani
Huwa nakunywa chai sehemu 1500-2000 kwa Kikombe

Ila wakati wa kulipa lazima atoe bundle la 1m achomoe 10,000 ndo alipe
Sijui huwa anamaanisha nini
 
Huu uzi umenifundisha mambo mengi maana kuna wakati napita kwenye viwanja naona watu wanatumbua pesa mpaka najiuliza hivu hawa wenzangu pesa wanazipataje
Kumbe wakirudi wanaenda kunywa diclopa kupunguza maumivu[emoji23][emoji23]
 
Dah nakumbuku ilikuwa kibondo hiyo nipo na wanangu kama wanne iv na mimi watano tulikuwa tunacheki game ya simba na yanga kwenye bar moja iv ya wanajeshi sasa mimi na crew yangu huwa tukikaa sehem tunapendelea kunywa sana spirits hasa k vant sio kwamba pesa hamna pesa ipo sana tu ila ni pombe ambayo tulitokea kuipenda sana! Sasa wakat tumekaa tunaendelea kucheki game maana crew yetu wote ni yanga na tulikuwa tunakunywa k vant kubwa tuna share wote watano mbele yetu kuna jamaa mmoja alikuwa anakunywa serengeti light yeye alikuwa ni mshabiki wa simba


Sasa kwenye utani na kushangilia jamaa akawa kama anatumind iv mixer dharau nyingi mara jamaa akaropoka “ nyie vipi nyie kwanza mnakujaje sehem kama hizi kundi alafu mnakunywa k vant moja watu 5 mnajaza nafasi tu pisheni watu wenye pesa zao wakae hapo” dah haya maneno tulivyoyasikia tukaangaliana kwanza alafu tukacheka mimi nikasema ngoja nimuoneshe huyu jamaa kwamba sio kila anae kaa sehem nzuri akanywa kitu cha bei ndogo sio kwamba hana hela ni maamuzi tu!


Basi nikamwita mhudumu nikaongea kwa nguvu nikamwambia mpe huyo jamaa shabiki wa simba creti la bia anayo kunywa alafu mwambie shabiki wa yanga anae kunywa k vant amekununulia! Kweli jamaa akapewa creti na akaambiwa kuwa limetoka pale jamaa akawaka hamna pesa ya kuninunulia bia nyie akamwambia mhudumu rudisha nitanunua kwa pesa yangu kweli akatoa pesa nikarudishiwa hela yangu ya creti moja mara jamaa yangu mwingine na yeye akasema mpelekee creti jingine mhudumu akapeleka jamaa wa simba akajifanya kuvimba aka punch tena akasema pesa ninayo na nunua mwenyewe tukarudishiwa tena pesa yetu kwaiyo jamaa wa simba akawa amenunua creti 2 za bia bila kupenda kisa sifa mbele za watu! Mpira ukaisha tukawa tunaanza kusepa tupo tunaelekea parking mara ghafla tunaona jamaa anakuja kwa upole eti tukamuombee kaunta wamrudishie japo pesa ya creti moja sabab creti mbili hawezi kunywa zote tukacheka sana tukamwambia we komaa tu mzee tukamuacha pale jamaa anatia huruma sana sifa zimemponza


Meneja wa bar alikuwa captain alimwambia bia tumeshauza pesa haiwezi kurudi [emoji28][emoji28]
Sifa mbaya[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Haya Maisha bila kujitoa ufahamu na kujikana hayaendi vile unataka, Mmoja katika hao nilidumu Nae katika mahusiano almost miaka miwili, Huyu ilikua Morogoro mjini miaka ya 2013 isivyo bahati Nilipoondoka Morogoro na Mahusiano yakafa. Natamani Nimtaje hata Jina ila Sitaweza. Siku Namuona Kavaa Kininja Full nikasema hapa Lazima nione yaliyomo ndani. Alikua mzuri wa Umbo na Tabia. Sijui alinipendea nini yule dada, ama ujasiri wangu wa kukomaa na nisichokiona [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]muone
 
Tangu useme unavaa Majuba umeshanichanganya, hapa Nataka nikushauri ununue bando ili Niendelee kukuona online wakati Kula ni Muhimu kwa mwanadamu... [emoji3][emoji3][emoji3][emoji41][emoji41][emoji125][emoji125] Ngoja Ni log out. Ninakoelekea kubaya.
Endelea uchapwe viboko mia moja[emoji51][emoji51]
 
Nlinunua mkungu wa ndizi kwenye harambee baada ya kuona madem pale chapo nmenyoosha mkono wananiangalia kwa macho ya wewe shusha huo mkono uwezi panda hapo nikapandishana na wazee wale wa benki nikaishia laki mbili nilijua wangepanda zaidi ili niachie pale
Watu si wakauchuna laki mbili yangu ikanitoka nililia hadi kamasi
Nkaenda kuuza kwa mama ntilie kwa arubaini alfu
Nieleweshe Dr[emoji5]
 
Back
Top Bottom