Uliwahi kuzingua kwenye mapishi, iwe ni mara ya kwanza unapika ama ukiwa mzoefu tayari?

Uliwahi kuzingua kwenye mapishi, iwe ni mara ya kwanza unapika ama ukiwa mzoefu tayari?

Carleen

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
7,982
Reaction score
27,272
Hi guys,
Natumaini mmekuwa na J'pili njema na yenye baraka..!

Nakumbuka miaka ya nyuma ndiyo najifunza funza kupika maskiini, siku hiyo nikaambiwa nipike uji tena wa ulezi bhaana bhaana, nikatoa una madonge kama vichwa vya ndege, nilivyo 'phaller special' eti nikautia kwenye chupa na kujikausha kama vile hakuna kilichotokea.

Yule Mama kumimina tu, akakutana uso kwa uso na muujiza, dadeki, alinimind jamani mpaka machozi yakanilenga, wala hakujali nikaambiwa nikunywe hiyo chupa yote hakuna kumwaga.

Nikaambiwa 'ile takataka unataka kunywesha watu, hebu wewe ndiyo uikunywe', hapo yeye kawa wa moto hatari, nikaanza kunywa huku machozi yanatoka, kitu ni 'kipaaaya' jamani, usiombe unywe liuji lina madonge..! Na unaambiwa hakuna kumwaga mpaka uishe.

Jamani, nilikunywa mpaka mchana, ilikuwa niupige tena jioni, cousin akanionea huruma (alikuwa mkubwa) akaniambia mwaga, me nitamuambia shangazi umeumaliza ndiyo ikawa pona pona yangu, vile ni mtu mzima Mama akaamini.!

Ya pili, hii nilizingua kwenye ubwabwa, kama kawaida Mama anakuambia tu 'unajua nini cha kufanya', ila hiyo by that time napenda ubwabwa hata sikuona shida nikapiga vitu vyangu ambavyo havieleweki, sahii nisingeweza kukula akii, wenyewe wakarudi jikoni, sheria ni ile ile 'ile takataka unataka lisha wenzio, unakula wewe yooote',

Hiyo sikuteseka, kesho nikarudi kutoka shule na crew yangu, tukapasha zetu kwa akili ile muujiza kikaleta maana kidogo tukakifuta chooote.

Ya tatu, hii sasa ni mkubwa kabisa nipo chuo, nimeenda ugenini kwa Ba mdogo, hapo nimewapigisha story wamecheqa mbavu hawana wakajua wako na mtu wa maana, wakawa wanapika zao ugali, mboga mojawapo ikawa tembele, nikawaambia 'hilo tembele nataka mtoto wa kike nikae jikoni niwapikie', nilivyoisema kwa mbwembwe, nikaenda chukua na kanga nikajifunga kiunoni unaweza dhani mtoto wa kitanga anaingia jikoni.

bwaana bwaaaana, naomba tusimame dakika mbili tuhuzunike tafadhali sana, nikawasha gesi, kumbe lile jiko halipunguzi moto, nikaanza kuhaha viungo sijaandaa, jiko lina moto mkali..! nyiieeeeeh'.

'ile kiere-ere yoote ikaisha sahiyo hiyo', nilitoa upande mmoja umerojeka mwingine haueleweki, niliona aibu na masifa nikapunguza, wakawa tu wananichekea ila am sure kimoyo moyo walinisema walaqhi'..! Nilikaa nao siku chache kabla niondoke ila niaminini Mimi sikuwaangusha tena ninyi wanangu.

anyways, I'm thankful sahii siyo kupika tu cha nyumbani ila ninapika mpaka chakula cha biashara sometimes na kila kitu kinaenda sawa bin sawia and am still learning.

Je, Iliwahi tokea ukazingua kwenye mapishi na Ilikuwaje?
 
Ndio
Nilikuwa napika wali, nikapika kama uji sijui ndio mnaita bokoboko. Nikautupa halafu nikaenda kununua mchele tena kwa hela yangu maana huo ulioharibika tulitegemea kuutumia hadi Dinner.

Kipindi hicho niliachwa home pekee yangu na kupewa maagizo yakupika Lunch then nibakishe kwa ajili ya Dinner
 
Dah,mie nilizingua kwenye majukumu niliyopewa ya kukata kachumbari buana bhana weee si nikazimenya zile nyanya zote kisha ndio nizikate,sema jamaa yangu yupo very smart sinaga mfano napoelezea wasifa wake zaidi ya yeye mwenyewe, hakunicheka wala kubeza kabisa japo nishamenya nyanya zote,akachukua nyingine akakata ndio nikajua mambo yalivyo...[emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ukorofi tu wa kutaka kujua kama unga wa ngano unaweza kupika ugali..

Nilipika karibu kilo 2 kwa ajili yangu tu, nilikuwa mwenyewe nyumbani..
mama alipokuja hakujua😅😅🤣🤣

part 2.

Nikiwa darasa la 3, enzi hizo majukumu ya jikoni yangu, nikaachiwa mafiga nipike mvua kubwa ilikuwa imenyesha kuni zotw zimeloana.

Nikapika maugali mabichi tupu dadeki.. nilimwaga na kuanza upya
 
Ndio
Nilikuwa napika wali, nikapika kama uji sijui ndio mnaita bokoboko. Nikautupa halafu nikaenda kununua mchele tena kwa hela yangu maana huo ulioharibika tulitegemea kuutumia hadi Dinner.

Kipindi hicho niliachwa home pekee yangu na kupewa maagizo yakupika Lunch then nibakishe kwa ajili ya Dinner
Haha.
Pole sana natumaini ulivyorudia hukutoa muujiza mwingine.!
 
Aaah shazingua mara nyingi tu, haswa nikiwa najifunza pishi jipya.
 
Dah,mie nilizingua kwenye majukumu niliyopewa ya kukata kachumbari buana bhana weee si nikazimenya zile nyanya zote kisha ndio nizikate,sema jamaa yangu yupo very smart sinaga mfano napoelezea wasifa wake zaidi ya yeye mwenyewe, hakunicheka wala kubeza kabisa japo nishamenya nyanya zote,akachukua nyingine akakata ndio nikajua mambo yalivyo...[emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Hahahahahaa..
this made my day, hiyo mtu anaanza kufanya kazi yake mwenyewe huwa inauma, unajua kabisa hapa nimezingua big time..!
 
Ukorofi tu wa kutaka kujua kama unga wa ngano unaweza kupika ugali..

Nilipika karibu kilo 2 kwa ajili yangu tu, nilikuwa mwenyewe nyumbani..
mama alipokuja hakujua😅😅🤣🤣

part 2.

Nikiwa darasa la 3, enzi hizo majukumu ya jikoni yangu, nikaachiwa mafiga nipike mvua kubwa ilikuwa imenyesha kuni zotw zimeloana.

Nikapika maugali mabichi tupu dadeki.. nilimwaga na kuanza upya
Jeeez,
Vile unga wa ngano unanata, huo ugali ulifananaje.? 😂 😂
 
Back
Top Bottom