Uliwahi kuzingua kwenye mapishi, iwe ni mara ya kwanza unapika ama ukiwa mzoefu tayari?

Uliwahi kuzingua kwenye mapishi, iwe ni mara ya kwanza unapika ama ukiwa mzoefu tayari?

Mimi hakuna pishi linalonichenga kupika, sema tu nashukuru maisha niliyopitia yalinifanya kujua kupika pika vitu vingi nikiwa teenager, so hata geto nikiwaga staki kula migahawani huwa naingia mzigoni chap tu shida ni kua chakula cha kupika mwenyewe afu ule hakina mzuka unajikuta umeshiba tu naamuaga kutafuta msela alie free aje tufinye!
 
Tukio La kwanza Nilipika wali ukaiva kabisa sasa wakati nahesabu dakika niutoe jikoni nikakumbuka sijaweka chumvi yaani hata punje moja....Maza alisafiri nilibaki mzee.nikaenda kumuita shangazi akauweka sawa baada ya hapo nilipigwa BAN na mzee kupika chakula.

Tukio la pili Mimi na dada yangu tulipika ugali kujaribu kama umeivaa tulikuwa tunatupia ugali ukutani ukinasa hujaiva Sasa kila tukitupa unanasa(yani hujaiva ),sister akaniambia kamwangalie Kaka kama anakuja(ili tupike mwengine) nilivyoenda kumuangalia nikamkuta anakuja ,nakaenda kumpa taarifa sister akesema tukajifiche chini ya uvungu wa kitanda.

bro alivyorudi ana njaa katuka jikoni kumepikwa kufunua msosi hakuna na kumbe aliniona wakati na mchungulia alivyo ingia ndani akatuona tumejificha chini ya uvungu sister aliniweka mbele(chambo) bro akaniambia toka chini huko na sister akatoka katuonyesha jikoni na ukutani mmefanya Nini hapa ,tujitetea kwamba tumepika Sasa tukawa tunajaribu kama umeivaa kauliza na ugali uko wapi (tuliutupa ) sister akachezea kofi mm nimejikunyata pembeni bro alimwambia Yani na ukbwa wako huu hujui kupika unaharibu unga si ungeenda kumuomba shangazi akusaidie......
Nilipigwa fimbo tatu yeye ndio alichezea nyingi zaidi

Tukio LA tatu nilivyokuwa chuo ,geto na washkaji nakumbuka ilikuwa mwaka mpya tukasema oya tusipite hivi hivi tukanunua nyama kilo mbili mchele kilo 4 Mimi ndio stelingi jikoni...loooh mboga iliiva Lkn wali he he he ulikuwa hujaiva ,umeungua na umetoka boko boko yaani wahuni walikuwa wananung'unika huku wanakula yaani mwanangu utanulisha wali na mchele..uzuri sisi geto tuliwekeana Sheria kwamba hakuna aliyemuoa mwezie humu ukiona chakula kibaya kale hotelini so kilo nne zote ziliisha
 
Pole Sana kwenye tembele sipati picha aibu yake,,mi sikumbuki kuwahi kuzingua ila kuna siku napika kienyeji(kuloweka)
Nilijiskia aibu na mbwembwe nilizokuwa nazo zikaisha,
hiyo ya kuamua kuloweka huwa haina shida, mbaya ni ile kuaibika...
 
Hakuna kitu kimenisumbua kupika kama ugali, nakumbuka katika harakati za maisha nilichomoka home nikaenda sehemu nyingine kupambana na maisha, nikatafuta room, kuoa muda bado, kumiliki mtoto wa kike wa kukupikia chenga mazingira mageni pia mambo hayaruhusu.. Nakumbuka nilikua napika ugali unakua ma uji uji hivi naumwaga, narudia mara ya pili, ya tatu bado unatoka vile vile kazi yangu ikawa n kuweka tu sukari naula kama uji na mboga ambazo nakua nimeshazipika tayari. But nipo good..
 
Mimi hakuna pishi linalonichenga kupika, sema tu nashukuru maisha niliyopitia yalinifanya kujua kupika pika vitu vingi nikiwa teenager, so hata geto nikiwaga staki kula migahawani huwa naingia mzigoni chap tu shida ni kua chakula cha kupika mwenyewe afu ule hakina mzuka unajikuta umeshiba tu naamuaga kutafuta msela alie free aje tufinye!
hakika,
Na utamu wa chakula ni kampani, mnajikuta mmeshusha mlima.!
 
Tukio La kwanza Nilipika wali ukaiva kabisa sasa wakati nahesabu dakika niutoe jikoni nikakumbuka sijaweka chumvi yaani hata punje moja....Maza alisafiri nilibaki mzee.nikaenda kumuita shangazi akauweka sawa baada ya hapo nilipigwa BAN na mzee kupika chakula.

Tukio la pili Mimi na dada yangu tulipika ugali kujaribu kama umeivaa tulikuwa tunatupia ugali ukutani ukinasa hujaiva Sasa kila tukitupa unanasa(yani hujaiva ),sister akaniambia kamwangalie Kaka kama anakuja(ili tupike mwengine) nilivyoenda kumuangalia nikamkuta anakuja ,nakaenda kumpa taarifa sister akesema tukajifiche chini ya uvungu wa kitanda.

bro alivyorudi ana njaa katuka jikoni kumepikwa kufunua msosi hakuna na kumbe aliniona wakati na mchungulia alivyo ingia ndani akatuona tumejificha chini ya uvungu sister aliniweka mbele(chambo) bro akaniambia toka chini huko na sister akatoka katuonyesha jikoni na ukutani mmefanya Nini hapa ,tujitetea kwamba tumepika Sasa tukawa tunajaribu kama umeivaa kauliza na ugali uko wapi (tuliutupa ) sister akachezea kofi mm nimejikunyata pembeni bro alimwambia Yani na ukbwa wako huu hujui kupika unaharibu unga si ungeenda kumuomba shangazi akusaidie......
Nilipigwa fimbo tatu yeye ndio alichezea nyingi zaidi

Tukio LA tatu nilivyokuwa chuo ,geto na washkaji nakumbuka ilikuwa mwaka mpya tukasema oya tusipite hivi hivi tukanunua nyama kilo mbili mchele kilo 4 Mimi ndio stelingi jikoni...loooh mboga iliiva Lkn wali he he he ulikuwa hujaiva ,umeungua na umetoka boko boko yaani wahuni walikuwa wananung'unika huku wanakula yaani mwanangu utanulisha wali na mchele..uzuri sisi geto tuliwekeana Sheria kwamba hakuna aliyemuoa mwezie humu ukiona chakula kibaya kale hotelini so kilo nne zote ziliisha
Hahahahaha..!
Eti hakuna aliyemuoa mwenzie humu..! Nimecheka sana jamani.!
 
Wakati niko mdogo, wazazi walitoka nyumbani na kuniachia samaki waliokuwa kwenye chungu kwenye mafiga wakichemshwa. Mi katika kumbukumbu zangu, huwa naona baada ya muda fulani huwa wanachukuwa mwiko na kugeuza geuza chakula wakati kinapikwa. Basi nikachukuwa mwiko nikawachanganya changanya kama mboga za majani wale samaki wakawa uji! Waliporudi, walishangaa sana na kusikitika.
 
Mimi ugali mpaka leo inatokea bahati utoke mzuri kama hujatoka na mabuje basi hauivi
Mabuje/ mabuja, yaondoe kwa kuanza kukologea uji then uache uchemke kama ni dona lichemke haswaa. Then songa

Ila wakati wa kukologa uji usitoke jikoni mpk uji utengemae.
 
Hakuna kitu kimenisumbua kupika kama ugali, nakumbuka katika harakati za maisha nilichomoka home nikaenda sehemu nyingine kupambana na maisha, nikatafuta room, kuoa muda bado, kumiliki mtoto wa kike wa kukupikia chenga mazingira mageni pia mambo hayaruhusu.. Nakumbuka nilikua napika ugali unakua ma uji uji hivi naumwaga, narudia mara ya pili, ya tatu bado unatoka vile vile kazi yangu ikawa n kuweka tu sukari naula kama uji na mboga ambazo nakua nimeshazipika tayari. But nipo good..
Jamani, umeteseka, ila sahii si umeshaweza sasa..?
 
Me kwenye kupika nashukuru Mungu najua na naenjoy kupika yaani hata kula chakula alichopika mwingine naona kama hajapika vzr[emoji849][emoji849][emoji849][emoji849]
Hongera dear..!
Na toka unajifunza hukuwahi zingua kabisa.?
 
Ubwabwa umenisumbua sana enzi hizo.. I mean ule ubwabwa standard kabisa.

Nilikuwa natoa boko' kila nikipika lazima maji yazidi. mpaka nilipoelekezwa kuwa kabla ubwabwa haujakaukia maji usiugeuze geuze sana.

Now natoa vitu fresh.

Heeeey. Hebu nifundishe vyakula vya bsness... Ndio vipi?
 
Back
Top Bottom