Uliwahi kuzingua kwenye mapishi, iwe ni mara ya kwanza unapika ama ukiwa mzoefu tayari?

Uliwahi kuzingua kwenye mapishi, iwe ni mara ya kwanza unapika ama ukiwa mzoefu tayari?

Kwanza kabisa mie napenda kupika . yano raha ya maidha yangu naipata jikoni😂😂😂😂😂
Nilipozingua sasa, siku ya kwanza kujifunza vileja nikaandaa vizuri mpka kuweka kweny oven kuchoma, baada ya muda nkachungulia nakaona vinabonyea nikaona nipunguze moto niswali magharibi nije nitoe, vitu nilivyokuta hapo vimekua kama mkaa vyote vimeungua sasa zile mbwembwe za kuwaambia watu leo nawaandalia vileja zikakata zote.
Mara ya pili kuzingua ilikua kweny chapati. Kiufupi mie fundi wa chapato sasa ktk kuzidisha manjonjo nikawa nimekata yale madonge tayari kwa kuyatia mafuta kishaa baadae nichome chapati, pembeni kukawa na peanut butter, sa siunajua mafuta yake hupenda kujichuja juu nikaona niyatumie ktk kusukumia zile chapati ili nifunge yale madonge, bwana bwan chapat zikawa tayari.mezani sasa chapat mchambuko ila ile harufu ya karanga ikabaki.kweny chapati zikawa haziliki pona yangu nilikua na mtoto mdgo ndo nikasingizia nilikuta amemiminia mafuta ya peanut kwny chapati
Haha,
Maskiini, ukamsingizia malaika wa watu jamani.!
 
Siku moja niko home maza akanipa kazi nipike ubwabwa. Ilibidi nimuite mdogo wangu wa kike ana 9yrs akawa ananielekeza jinsi ya kufanya. Siku hiyo nilikoma maana kalikua kananielekeza kananisema na kunicheka
Haha..!
9 years ndiyo akaendesha mtambo.! Hapo ukute ulikuwa unamuoneaga lazima ujute.!!
 
mkuu hii mambo ni ngumu kidogo, nakumbuka
1. nilitaka kula ndizi zilizochanganywa na nyama. ktk mapishi nikachanganya vyote vikiwa vibichi baada ya muda kilichotokea sikuona ndizi hata moja na nyama bado zikiwa mbichi, nikahisi hapa kuna sinema na chezewa na wazee wa kaz. baadae nilipo kuja kugundua nikajiona bonge la fala.
2. kuna siku nikataka kutengeneza supu ya ng'ombe nika katakata kila kitu nikaweka kwa jiko including nyanya, kilichotokea ni kama mboga ya kulia ugali. Dogo akaniuliza kwani umefanyaje? nilivyomuelekeza akaniambia malizia kupika ugali tule.
3. mwaka huu mwezi wa 9, mtoto wangu wa kiume kapika kitu kinachofanana na pilau, nikamuuliza hii nn? with confidence akajibu pilau!! nikapiga picha nikamtumia mama ake nikamwambia mwanao kasema kapika pilau, nikamuuliza wewe unadhan nn hii? akajibu sijui labda ningekuwepo.
Enjoy your life.
bonus
juz mwanangu mdogo wa kike kanivalisha wigi la mama ake alaf kaniambia baba umependeza.
Naseama enjoy your life as it is tooooo short
Hahahahahaaaa..
Nimecheeeeka, eti nikahisi kuna sinema nachezewa na wazee wa kazii.!!
 
😆😆 Kweli ulizingua mwenyewe bi mkubwa aliniachiaga samaki wa kubanika watoka kutanda (kuvua kwa kutumia chandalua ) wengine akaenda kuwauza , na wengine akaniachia maagizo niwabanike Sasa badala ya kuweka mkaa tu juu ya mfuniko Mimi nikajaza majivu kabao na mkaa...wakati nafunua ningalie wamefikia wapi mfuniko ulikuwa wa moto nikaurusha jivu lote kwenye samaki...Maza alivyorudi akataka kujua imekuaje nikawa Nampa taarifa huku nimekaa mita 100
Haha..
Muujiza ungekufuata huko uliko.!!
 
Ya mbele ya watu mbona kawaida saana[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Nishawahi kimbia nikawaachia ugali sijui mchele jikoni maana ulikuwa unatawanyika tu[emoji2297]
Hahahaa...
Ukaja kujiteteaje sasa..???
 
Mimi pamoja na kua ME lakini nilifunzwa na nimejua kupika ugali ulioiva kabisa bila mabonge nikiwa darasa la 4 tu. Tena nilikua napikia familia yetu ya watu 6 sema sometimes kukadilia ndiyo ilikua shughuli siku nyingine ugali unakua mdogo [emoji16] hivyo italazimika ambao hawajashiba wasonge wa kukazia.

Sababu iliyopelekea kujua kupika nikiwa bado mdogo ni malezi niliyoyapata kwa bibi na babu kijijini walikua wazee so walikua anaishi na sisi wajukuu tu make mshua aliniondoaga mjini akihofia kidume ntaharibika na makundi niwe mla dagsativa akaona bora nikasomee primary kijiji, mwanzo nilipata shida sana kuzoea mazingira ila mwishoe nikazoea tu, ila maisha ya kijijini yana raha yake na yanafunza vitu vingi sana ambavyo ni faida ya baadae katika mzunguko wa maisha kwa ujumla.
Una bahati sana, shukuru mno mzee wako walaqhi'...!!
 
Wakati niko mdogo, wazazi walitoka nyumbani na kuniachia samaki waliokuwa kwenye chungu kwenye mafiga wakichemshwa. Mi katika kumbukumbu zangu, huwa naona baada ya muda fulani huwa wanachukuwa mwiko na kugeuza geuza chakula wakati kinapikwa. Basi nikachukuwa mwiko nikawachanganya changanya kama mboga za majani wale samaki wakawa uji! Waliporudi, walishangaa sana na kusikitika.
Eti katika kumbukumbu zangu[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Wakati niko mdogo, wazazi walitoka nyumbani na kuniachia samaki waliokuwa kwenye chungu kwenye mafiga wakichemshwa. Mi katika kumbukumbu zangu, huwa naona baada ya muda fulani huwa wanachukuwa mwiko na kugeuza geuza chakula wakati kinapikwa. Basi nikachukuwa mwiko nikawachanganya changanya kama mboga za majani wale samaki wakawa uji! Waliporudi, walishangaa sana na kusikitika.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Hakuna kitu kilinisumbua kupika kama egg chop sijui, daah!! Zilikuwa nikiziweka kwenye mafuta zinatawanyika zinakuwa kama chura.
 
Una bahati sana, shukuru mno mzee wako walaqhi'...!!
Mkuu umenikumbusha mbali Sana enzi izo 2010 naenda kureport advanve kusini uko nikafikia kwa bro wangu mwanajeshi nitumie angalau week mbili tatu kabla sijaingia shule, sasa siku nimefika nikakuta kapika fresh Sasa kesho yake akanielekeza mazaga ya kupika yalipo nirekebishe ugali(yeye alikua stand bay) kwenye Sasa sita wakaja wanajeshi kibao pamoja na bro waje wale then waendelee na Mambo yao uko, nikawa nmepika mboga fresh tuu baada ya kuwaona nikawa naweka maji nisonge ugali nikapata kama panic flan, maji hayakuchemka vzuri pia sikuacha uji uchemke, bhana bhna ugali ukatoka mbichi aufai wazee uko wanapiga kelele dogo tunachelewa leta ugali huo. Ili kuuwa so nikafunikua ugali kwenye sinia moja na mboga nikawatengea nikawa pembeni nasikiliza. Daah kama mnavyojua wanajeshi walivyo baada ya kuanza kula tuu kuona ugali mbichi walianza kushusha matusi pale bro akawa anacheka tuu npo apo nataka hadi kulia, waliula wote Ila kwa matusi, bro badae akanambia dogo usipanic ndo kawaida yetu Ila ujifunze kupika. Toka ile siku nilijifunza kupika ugali ulionyooka wakawa kila siku wananisifia balaa hadi Sasa wengine ni washkaji zangu Sana.
 
Mkuu umenikumbusha mbali Sana enzi izo 2010 naenda kureport advanve kusini uko nikafikia kwa bro wangu mwanajeshi nitumie angalau week mbili tatu kabla sijaingia shule, sasa siku nimefika nikakuta kapika fresh Sasa kesho yake akanielekeza mazaga ya kupika yalipo nirekebishe ugali(yeye alikua stand bay) kwenye Sasa sita wakaja wanajeshi kibao pamoja na bro waje wale then waendelee na Mambo yao uko, nikawa nmepika mboga fresh tuu baada ya kuwaona nikawa naweka maji nisonge ugali nikapata kama panic flan, maji hayakuchemka vzuri pia sikuacha uji uchemke, bhana bhna ugali ukatoka mbichi aufai wazee uko wanapiga kelele dogo tunachelewa leta ugali huo. Ili kuuwa so nikafunikua ugali kwenye sinia moja na mboga nikawatengea nikawa pembeni nasikiliza. Daah kama mnavyojua wanajeshi walivyo baada ya kuanza kula tuu kuona ugali mbichi walianza kushusha matusi pale bro akawa anacheka tuu npo apo nataka hadi kulia, waliula wote Ila kwa matusi, bro badae akanambia dogo usipanic ndo kawaida yetu Ila ujifunze kupika. Toka ile siku nilijifunza kupika ugali ulionyooka wakawa kila siku wananisifia balaa hadi Sasa wengine ni washkaji zangu Sana.
[emoji38][emoji38][emoji1] Kwamba wajeda walikua wanatukana mmae huyu dogo msnge tu hajui kupika anatupikia ugali mbichi sie wacha tule na hii njaa hakuna namna, ila dogo uache ufaler siku ingine usitulishe ugali mbichi.

Nmecheka sana hii
 
Huu uzi umekuja muda muafaka, iko hivi kuna mboga ile wanaita brocol nadhani basi kiukweli sikuwahi kuiona udogoni mwangu na mkoa niliopo haipo ama sikuwahi kuiona na itoshe kusema niliionea ukubwani kabisa tena youtube kipindi cha mapishi basi siku moja hamaaadii mtaani nikaziona zinauzwa nikanunua na kwenda kuzipika kwa muongozo wa youtube acha niishie hapa mana nachoka kabisaaa kiufupi haikulika nilikua kama nakula mironge yani
 
Naendelea kufatilia najua tu kuna mwanaume wa daslam hachelewi kuja kutoa ushuhuda jins alivyo fundi wa kupika wali nazi
 
Mi nilikua nakamwanamke kangu kupika 0 ila masifa Sasa .Siku moja kalinipikia kisamvu Cha chukuchuku ugali na maziwa mgando.Mchanganuo ulikua hivi ; Kisamvu kilikua Kama upalato wa mtoto .Maziwa Kama maji ya kwenye beseni walioshea watu wenye mikono michafu na yananuka hata ukoroge vipi yanajitenga.Nilivyo mnafiki nikakaambia leo umeniweza mapishi Kama ya mama yangu.Nikaenda kutapikia mbele huko.
 
Back
Top Bottom