Uliwahi kuzingua kwenye mapishi, iwe ni mara ya kwanza unapika ama ukiwa mzoefu tayari?

Uliwahi kuzingua kwenye mapishi, iwe ni mara ya kwanza unapika ama ukiwa mzoefu tayari?

[emoji38][emoji38][emoji1] Kwamba wajeda walikua wanatukana mmae huyu dogo msnge tu hajui kupika anatupikia ugali mbichi sie wacha tule na hii njaa hakuna namna, ila dogo uache ufaler siku ingine usitulishe ugali mbichi.

Nmecheka sana hii
🤣🤣🤣🤣Kama vile ulikuwepo mkuu
 
Nlilud kazin saa4 usiku,nmechokaaa toop!!!
Nakaingia kuoga,nkakaanga chips
Nkagongea mayai
Sasa ile nigeuze upande wa pili sahani ikateleza
Yakalia pwalaaaaatu chini ,mayai yanalendemka tu
Nkasema pumbav!!! Nkazima jiko nkajitupia kitandan
 
Hi guys,
Natumaini mmekuwa na J'pili njema na yenye baraka..!

Nakumbuka miaka ya nyuma ndiyo najifunza funza kupika maskiini, siku hiyo nikaambiwa nipike uji tena wa ulezi bhaana bhaana, nikatoa una madonge kama vichwa vya ndege, nilivyo 'phaller special' eti nikautia kwenye chupa na kujikausha kama vile hakuna kilichotokea.

Yule Mama kumimina tu, akakutana uso kwa uso na muujiza, dadeki, alinimind jamani mpaka machozi yakanilenga, wala hakujali nikaambiwa nikunywe hiyo chupa yote hakuna kumwaga.

Nikaambiwa 'ile takataka unataka kunywesha watu, hebu wewe ndiyo uikunywe', hapo yeye kawa wa moto hatari, nikaanza kunywa huku machozi yanatoka, kitu ni 'kipaaaya' jamani, usiombe unywe liuji lina madonge..! Na unaambiwa hakuna kumwaga mpaka uishe.

Jamani, nilikunywa mpaka mchana, ilikuwa niupige tena jioni, cousin akanionea huruma (alikuwa mkubwa) akaniambia mwaga, me nitamuambia shangazi umeumaliza ndiyo ikawa pona pona yangu, vile ni mtu mzima Mama akaamini.!

Ya pili, hii nilizingua kwenye ubwabwa, kama kawaida Mama anakuambia tu 'unajua nini cha kufanya', ila hiyo by that time napenda ubwabwa hata sikuona shida nikapiga vitu vyangu ambavyo havieleweki, sahii nisingeweza kukula akii, wenyewe wakarudi jikoni, sheria ni ile ile 'ile takataka unataka lisha wenzio, unakula wewe yooote',

Hiyo sikuteseka, kesho nikarudi kutoka shule na crew yangu, tukapasha zetu kwa akili ile muujiza kikaleta maana kidogo tukakifuta chooote.

Ya tatu, hii sasa ni mkubwa kabisa nipo chuo, nimeenda ugenini kwa Ba mdogo, hapo nimewapigisha story wamecheqa mbavu hawana wakajua wako na mtu wa maana, wakawa wanapika zao ugali, mboga mojawapo ikawa tembele, nikawaambia 'hilo tembele nataka mtoto wa kike nikae jikoni niwapikie', nilivyoisema kwa mbwembwe, nikaenda chukua na kanga nikajifunga kiunoni unaweza dhani mtoto wa kitanga anaingia jikoni.

bwaana bwaaaana, naomba tusimame dakika mbili tuhuzunike tafadhali sana, nikawasha gesi, kumbe lile jiko halipunguzi moto, nikaanza kuhaha viungo sijaandaa, jiko lina moto mkali..! nyiieeeeeh'.

'ile kiere-ere yoote ikaisha sahiyo hiyo', nilitoa upande mmoja umerojeka mwingine haueleweki, niliona aibu na masifa nikapunguza, wakawa tu wananichekea ila am sure kimoyo moyo walinisema walaqhi'..! Nilikaa nao siku chache kabla niondoke ila niaminini Mimi sikuwaangusha tena ninyi wanangu.

anyways, I'm thankful sahii siyo kupika tu cha nyumbani ila ninapika mpaka chakula cha biashara sometimes na kila kitu kinaenda sawa bin sawia and am still learning.

Je, Iliwahi tokea ukazingua kwenye mapishi na Ilikuwaje?
Ndugu, mimi nilizungua mara yangu ya kwanza kupika, na ikawa ndio kama ile ya yesu na wafuasi wake maana siku hiyo nilipozingua nilipika ugali usioiva na mimi pia mdogo wangu tukaula hadi mwisho... baada ya hapo, nikaenda kuchunga ng'ombe, huku nyuma mdogo wangu akakwea mti wa ma maembe, akaanguka, ubongo ukamwagika na kufa pale pale... Siku hiyo siwezi isahau, ilikuwa 24.10.1987. Ugali ule ulikuwa lunch yangu ya mwisho na mdogo wangu- R.i.P
 
Msinikumbushe maana naweza lia.
Kulikuwa na 40 ya marehemu somewhere Ilala. Mie nikajifanya kushika jungu la pilau la mchele wa kilo 15....acha tu, uchawi upo jamani.
Kila nikigeuza pilau, ni kama nimeloweka mchele yaani full bichi, pilau limepiga msamba kila kiungo kipo upande wake.
Kuondoa lawama,nikategua jifya moja...jungu chini, pilau likamwagika hapo ndo ikawa pona pona yangu. Maana nikaaga na kuaga.

Sahv, hata unipe majungu ya kilo 100 napika.
Uchawi kwenye mashughuli upo jamani.
 
Kuna jamaa aliitwaga Dotto wa kanda ya ziwa alisomaga Ulayasi secondary alikuwa anapika msosi mbichi kila siku akawa ana harisha mwaka mzima siku 365 na robo.
 
Mkuu umenikumbusha mbali Sana enzi izo 2010 naenda kureport advanve kusini uko nikafikia kwa bro wangu mwanajeshi nitumie angalau week mbili tatu kabla sijaingia shule, sasa siku nimefika nikakuta kapika fresh Sasa kesho yake akanielekeza mazaga ya kupika yalipo nirekebishe ugali(yeye alikua stand bay) kwenye Sasa sita wakaja wanajeshi kibao pamoja na bro waje wale then waendelee na Mambo yao uko, nikawa nmepika mboga fresh tuu baada ya kuwaona nikawa naweka maji nisonge ugali nikapata kama panic flan, maji hayakuchemka vzuri pia sikuacha uji uchemke, bhana bhna ugali ukatoka mbichi aufai wazee uko wanapiga kelele dogo tunachelewa leta ugali huo. Ili kuuwa so nikafunikua ugali kwenye sinia moja na mboga nikawatengea nikawa pembeni nasikiliza. Daah kama mnavyojua wanajeshi walivyo baada ya kuanza kula tuu kuona ugali mbichi walianza kushusha matusi pale bro akawa anacheka tuu npo apo nataka hadi kulia, waliula wote Ila kwa matusi, bro badae akanambia dogo usipanic ndo kawaida yetu Ila ujifunze kupika. Toka ile siku nilijifunza kupika ugali ulionyooka wakawa kila siku wananisifia balaa hadi Sasa wengine ni washkaji zangu Sana.
Hahaha..
Kama nakuona ulivyojikunyata maskiini wakati wazee wa kazi wanakusimanga.! Pole sana ndiyo kukua!;
 
Huu uzi umekuja muda muafaka, iko hivi kuna mboga ile wanaita brocol nadhani basi kiukweli sikuwahi kuiona udogoni mwangu na mkoa niliopo haipo ama sikuwahi kuiona na itoshe kusema niliionea ukubwani kabisa tena youtube kipindi cha mapishi basi siku moja hamaaadii mtaani nikaziona zinauzwa nikanunua na kwenda kuzipika kwa muongozo wa youtube acha niishie hapa mana nachoka kabisaaa kiufupi haikulika nilikua kama nakula mironge yani
Hahahahaha..!
Eti mironge cheese sana wewe.!
 
Naendelea kufatilia najua tu kuna mwanaume wa daslam hachelewi kuja kutoa ushuhuda jins alivyo fundi wa kupika wali nazi
Haha..!
Siku hizi mpaka wa mikoani tunashindana jikoni..!
 
Mi nilikua nakamwanamke kangu kupika 0 ila masifa Sasa .Siku moja kalinipikia kisamvu Cha chukuchuku ugali na maziwa mgando.Mchanganuo ulikua hivi ; Kisamvu kilikua Kama upalato wa mtoto .Maziwa Kama maji ya kwenye beseni walioshea watu wenye mikono michafu na yananuka hata ukoroge vipi yanajitenga.Nilivyo mnafiki nikakaambia leo umeniweza mapishi Kama ya mama yangu.Nikaenda kutapikia mbele huko.
Hahahahhahahaaa...
We phaller, ni nini lakini..???!
 
  • Kicheko
Reactions: EEX
Kuna jamaa aliitwaga Dotto wa kanda ya ziwa alisomaga Ulayasi secondary alikuwa anapika msosi mbichi kila siku akawa ana harisha mwaka mzima siku 365 na robo.
Hahaa...
Niacheni hebu bhaana..
 
Ndugu, mimi nilizungua mara yangu ya kwanza kupika, na ikawa ndio kama ile ya yesu na wafuasi wake maana siku hiyo nilipozingua nilipika ugali usioiva na mimi pia mdogo wangu tukaula hadi mwisho... baada ya hapo, nikaenda kuchunga ng'ombe, huku nyuma mdogo wangu akakwea mti wa ma maembe, akaanguka, ubongo ukamwagika na kufa pale pale... Siku hiyo siwezi isahau, ilikuwa 24.10.1987. Ugali ule ulikuwa lunch yangu ya mwisho na mdogo wangu- R.i.P
Good Lord,
Pole sana mkuu jamani..!!
 
Mwezi uliopita tu hapo nilifanya kituko kwenye kupika wali na rost maini. Wali ulitoka bokoboko flani kabisa ila una ladha nzuri tu (mchele wa Kilosa tena)vitunguu vilisaidia flani kuongeza harufu kwenye hii nilijitetea sababu ya kupikia kwenye jiko la gesi. Kwenye maini sasa nyanya kadhaa na tomato paste niliweka yote wakati yale maini yalikuwa nusu mwenyewe najua leo naua kwa diko adimu doh! hiyo mboga kilichotokea balaa tupu. Lengo ilikuwa kumsaidia wife kupika lakini tamati ilikuwa vyote kumwagwa kisha akapika ugali dagaa tukala. Mpaka leo mzuka wa kukaa kitchen bado haupo hata chai sitaki kuchemsha
 
Sikuwahi kupata shida kubwa kwa. Mapishi maana nilikuwa nacheki kwa mama kupita kawaida licha ya kuwa ni mtoto wa kiume nikicheki kitu anapika nikija pika napita mulemule

Siku moja tu nilipika wali kama kilo 5 hivi haukuiva vzr, alipokuja kutest unakaubichi ka mbali akaongeza maji ukaiva sie tushakula hivyo hivyo na kusepa mishe

Sent from my Nokia C1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom