Uliza swali lolote juu ya afya ya ngozi

Uliza swali lolote juu ya afya ya ngozi

Punye ni ugonjwa wa ngozi au n nin!?

Mapunye au Tinea Capitis ni nini?

Aina hii ya maradhi ya fangasi hushambulia eneo la kichwa pekee ukiacha eneo la uso. Kwa maneno mengine, aina hii ya fangasi haishambulii uso bali hushambulia eneo lililobaki la kichwa.
Huwashambulia kina nani?

Haya hushambulia watu wote wa jinsia na umri wote, ingawa huonekana zaidi kwa watoto wadogo. Fangasi hawa hushambulia watoto wadogo ambao hawajafikia umri wa balehe na mara nyingi huacha kushambulia pale mtoto anapofikia umri huo wa balehe.

Mwonekano wake
Mapunye huweza kushambulia eneo lote la kichwa au sehemu tu ya kichwa. Eneo la ngozi ambalo lina mashambulizi ya mapunye huwa na umbo linalofanana na sarafu.

Eneo hili la ngozi lililoathirika kama lina nywele, basi hunyonyoka na hivyo mwonekano wa mfano wa sarafu huonekana vizuri tu hata bila kutumia jicho la kitaalam.

2.jpg


Dalili zake
Ukiachilia mbali mwonekano wa mapunye kama nilivyoeleza hapo juu kuna dalili nyingine za maradhi haya. Hizo ni:

-Eneo la ngozi lililoshambuliwa kuwasha (ingawa si mara zote)
-Kubadilika kwa rangi ya ngozi ya eneo lenye maambukizi
-Ukitazama kwa makini eneo ambalo lina mashambulizi ya maradhi haya utagundua kuna vidoti vyeusi ambavyo vinaonyesha eneo ambalo nywele imeng`oka kutokana na maradhi.
-Ngozi kubanduka kwenye eneo lenye maambukizi
-Ngozi kukauka kwenye eneo lenye maambukizi
-Mara nyingine usaha pia huweza kuonekana kwenye eneo la ngozi lililoshambuliwa na fangasi hawa (hii kwa kitaalam huitwa kerions)
-Kama maradhi haya yakikaa bila kutibiwa kwa muda mrefu husababisha dalili nyingine kuonekana kama kutoka kwa maji maji kwenye eneo la ngozi lililoathirika pamoja na kutoka kwa harufu mbaya kwenye eneo la ngozi lililoathiriwa na vimelea hivi vya fangasi.

Jaribu hizi dawa moja kati ya hizo Dawa tatu hapo chini:

(1) Ndimu au limau: Kabla kwenda kukoga Msuguwe limau ndani ya kichwa na baadae yale maganda ya limau yatie katika maji ya kukoga yaani yawe maji ya Uvuguvugu halafu ukoshe kwa maji yale kwanza na baadae utumie maji yaliyo safi.

(2) (Fenugreek) kwa lugha ya kiswahili inaitwa Uwatu. Uwatu unachukua vijiko 2 vya chai vya Uwatu (fenugreek) unazirowesha katika maji usiku mzima ili zipate kulainika, halafu unazipoda ponda na baadae unapakaa ndani ya kichwa na uwache kwa muda wa saa moja na baadae kuzikosha ikiwa utafanya hivi siku zote mbaa wataondoka Inshallah bila tabu yoyote.

(3) Mshubiri Mwitu au Aloe Vera kwa jina lingine. Ponda paka kichwani kila siku mara mbili asubuhi na usiku.

(4) Pia kuna udongo tuliouvumbua hivi karibuni wa Natural clay.

Tumia Dawa mojawapo sio zote tafadhali kisha utpe feedback.
 
Nina mtoto wa miezi 3 anasumbuliwa na vipele vinakua kama majipu kichwani,atumie dawa gani,je joto linaweza kuwa sababu?
 
Mkuu ninafangasi katikati ya mapaja na sehemu za siri nimetumia dawa mbalimbali lakini zinapungua tu na baada ya muda zinarudi tena,,,,nifanye nini ili ziishe kqbisa na zisirudi tena?
 
Mkuu msaada alama kama hiyo hapo kwenye picha huwa zinatokea mara kwa mara na kapotea zenyewe hasa miguuni na mikononi. Inaweza kuwa ni tatizo gani
20180317_185208.jpg
 
Ningeona picha ingekuwa rahisi. Jaribu kupima kipimo cha mzio pale Muhimbili
Nina mtoto wa miezi 3 anasumbuliwa na vipele vinakua kama majipu kichwani,atumie dawa gani,je joto linaweza kuwa sababu?
 
Mkuu ninafangasi katikati ya mapaja na sehemu za siri nimetumia dawa mbalimbali lakini zinapungua tu na baada ya muda zinarudi tena,,,,nifanye nini ili ziishe kqbisa na zisirudi tena?
Licha ya kutumia dawa, kuna vitu vya kuzingatia ikiwemo kujiepusha kuvaa nguo mbichi hasa za ndani, kutovaa nguo mpya ya ndani kabla hujaifua, badili aina ya maji unayoogea. Tuwasiliane kuna sabuni za udongo uogee kupambana na bacteria eneo hilo
 
Hili tatizo ni miongoni mwa ishara za maambukizi katika damu kapime damu kisha tuwasiliane
 
Mafuta ya nazi yanamfaa mtu mweny ngozi ya mafuta.?
Na nini chanzo cha chunusi kwny eneo nje ya T Zone ya uso.,yani kwenue mashavu.?
 
Mkuu salam ZAGANZA ,nilifanya *hot full leg wax* sasa sehemu husika ni etokwa kama na vipele vidogo vidogo vingi,,like vile kwenye ngozi ya kuku baada ya kumnyonyoa ,,nini shida?kuna kitu nlitakiwa kufanya after waxing?iliku mara yangu ya kwanza,je natibu vipi hivo vipele,,uzuri haviumi japo ngozi imekua rough na kavu sana
 
Mafuta ya nazi yanamfaa mtu mweny ngozi ya mafuta.?
Na nini chanzo cha chunusi kwny eneo nje ya T Zone ya uso.,yani kwenue mashavu.?
Ngozi ya mafuta inahitaji scrub zisizo na mafuta mfano scrub za papaya, lemon . Tuwasiliane kwa 0713-039875 nikuelekeze ntumie picha ya eneo liloathirika nipate mwanga zaidi.

Pia sababu za chunusi zinalingana mwilini kote, hivyo chunusi za mashavu na paji la uso ni sawa
 
Mkuu salam ZAGANZA ,nilifanya *hot full leg wax* sasa sehemu husika ni etokwa kama na vipele vidogo vidogo vingi,,like vile kwenye ngozi ya kuku baada ya kumnyonyoa ,,nini shida?kuna kitu nlitakiwa kufanya after waxing?iliku mara yangu ya kwanza,je natibu vipi hivo vipele,,uzuri haviumi japo ngozi imekua rough na kavu sana
Kama ulitumia multi-blade razors bila umakini, inasababisha tatizo liitwalo shaving bumps, ambalo hupelekea ngozi kujeruhiwa (irritate) na hizo chunusi ndiyo ishara yenyewe
 
Mkuu salam ZAGANZA ,nilifanya *hot full leg wax* sasa sehemu husika ni etokwa kama na vipele vidogo vidogo vingi,,like vile kwenye ngozi ya kuku baada ya kumnyonyoa ,,nini shida?kuna kitu nlitakiwa kufanya after waxing?iliku mara yangu ya kwanza,je natibu vipi hivo vipele,,uzuri haviumi japo ngozi imekua rough na kavu sana
Duh pole ...paka vaseline to soothe roughness and dryness,mi sio mtaalamu wa ngozi bt i wax on the regular vaseline helps anytime anywhere
 
Kama ulitumia multi-blade razors bila umakini, inasababisha tatizo liitwalo shaving bumps, ambalo hupelekea ngozi kujeruhiwa (irritate) na hizo chunusi ndiyo ishara yenyewe
Amesema aliwax mkuu hajashave na kiwembe..u know waxing.?
 
Waxing ni process ya kutoa nywele ukitumia asali ya moto.,ama ni sukari na limao sijui sina hakika
Mimi nimejikita kutibu ngozi kwa njia za Asili tu kuanzia dawa, sabuni,scrub, ukuzaji nywele, kutibu ngozi ilobabuka kwa dawa kama metakelfin au vipodozi. Hivyo tiba kama waxing sina ufahamu nazo
 
Mimi nimetokwa na vipele usoni tu si chunusi bali ni vidogo sana kama mtu anaesisimka mwili kwa barid kali sana....nilishawah kuchomwa sindano ya aleg haikusaidia....je nini tatizo kama x-pen na penadu na sindan ya aleg na dawa juu z kumeza na sabuni nilikua naogea tetmoson had leo pia napaka na enalt bado vipo ......naomba sisaidie kwa ilo Dr.

NB. Si vya kuiva wala haviumi, haviwashi, havikauki havitumbuki na havina msim wa joto wala baridi ni vipo
 
Mimi nimetokwa na vipele usoni tu si chunusi bali ni vidogo sana kama mtu anaesisimka mwili kwa barid kali sana....nilishawah kuchomwa sindano ya aleg haikusaidia....je nini tatizo kama x-pen na penadu na sindan ya aleg na dawa juu z kumeza na sabuni nilikua naogea tetmoson had leo pia napaka na enalt bado vipo ......naomba sisaidie kwa ilo Dr.

NB. Si vya kuiva wala haviumi, haviwashi, havikauki havitumbuki na havina msim wa joto wala baridi ni vipo
Kuna uwezekano mkubwa mwili wako haukubali dawa hizo kutokana na kiasi cha mafuta kwenye ngozi yako. Maadam ushafanya vipimo, nakushauri tuwasiliane nikupatie udongo tiba wa asili na sabuni zake ili kubalance mafuta ya ngozi yako
 
Duh pole ...paka vaseline to soothe roughness and dryness,mi sio mtaalamu wa ngozi bt i wax on the regular vaseline helps anytime anywhere
Aksante mkuu,,naona angalau,,napaka vaseline na parachute yale mafuta ya nazi,,naona vinapotea taratibu,,nahisi sirudii tena waxing
 
Back
Top Bottom