Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Kampuni ni ndogo haijasajiliwa
Nataka kuanza kutunza hesabu na Sina mhasibu Wala uwezo wa kumlipa.

Ni kampuni ya Technology /IT

Ni vitabu gani vya hesabu natakiwakuwa navyo?

Je ni
Balance sheet
Cash flow statement
Income statement

Au daftari lamapato na matumizi ambalo content Nampa mtaalam.

Sasa mkuu hebu tuanzie hapo kwenye kampuni haijasajiliwa!? Unafanyaje biashara na kuita kampuni pasipo kua una usajili!?

Kama hujasajili kampuni hizo hesabu ukishatunza utazipeleka wapi!? Maana hazitopokelewa TRA, Bank na kokote pale sababu hiyo kampuni unayoiandalia hesabu haipo kisheria

Anyway, nifafanulie hapo kwanza kwenye usajili wa kampuni
 
1. Huwezi kuendesha kampuni bila kulipa kodi, unless hiyo kampuni imesimama kufanya biashara kwa muda huo ndio hutolipa kodi, ila kama inafanya biashara kodi lazima ulipe

2. PAYE (Pay As You Earn) inakatwa katika mshahara wa mfanyakazi, ila ni kwa wafanykazi ambao mshahara wao (baada ya makato y NSSF) ni kuanzia sh 270,001 na kuendelea.. mfanyakazi anaepokea chini ya hapo hutakiwi kumkata PAYE

3. Unapoajiri unaandaa mikataba, mamlaka zitafahamu kuwa umeajiri pale utapoongeza idadi ya wafanyakazi katika sehem tofauti mf. NSSF, WCF, TRA n.k ndio maana inakupasa kuandaa Payroll ya wafanyakazi kila mwezi ili taarifa kama hizo ziwe bayana
Ni utaratibu gani unatumika kuifufua kampuni ambayo imesimama kufanya kazi kwa muda wa miaka inayozidi mitano,kampuni ni ya Construction..Na je kubadilishwa jina inaruhusiwa na utaratibu ukoje!?
 
Sasa mkuu hebu tuanzie hapo kwenye kampuni haijasajiliwa!? Unafanyaje biashara na kuita kampuni pasipo kua una usajili!?

Kama hujasajili kampuni hizo hesabu ukishatunza utazipeleka wapi!? Maana hazitopokelewa TRA, Bank na kokote pale sababu hiyo kampuni unayoiandalia hesabu haipo kisheria

Anyway, nifafanulie hapo kwanza kwenye usajili wa kampuni
Asante kwa fafanuzi.
Niweke swali kwa wepesi.
Nikishafungua kampuni ni hesabu gani za kuhifadhi ili zitumike katika kufanya maamuzi ya kikodi.
 
Hivyo ulivyovitaja hapo juu ni mambo ambayo una utaalamu nayo(umesomea)!? Je una uelewa na uzoefu wa kuvifanya kwa usahihi!?

Ila mchakato kwa ufupi tu unaanza na kujisajili. Usajili unaanzia Brela, TRA then unamalizia kuchukua leseni.
Nimesomea na nina ujuzi..Nina Bachelor Of Commerce in Accounting and Management(Upper Second Class) ya 1998 from University Of Dar es Salaam.Nimeshafanya kazi serikalini na kwenye taasisi binafsi.Naona nijiajiri mwenyewe kwenye anga hizi sababu nina uzoefu huu wa kufill Tax Returns na hata kuandaa Business Plan na Proposal(Hili nimejifunza tu mwenyewe na nimeshawaandikia watu na wakafanikiwa kuchukua mikopo hadi Bank)
Sasa nataka kulifanya serious nifungue ofisi yangu mwenyewe iwe ndiyo full time kazi yangu kwa sasa Mkuu.Asante kwa ushauri.So nianzie Brela then TRA siyo?
Ila sina CPA je hicho kinaweza kuwa kikwazo?
 
Nawezaje kupata tenda, nina kampuni y shughuli za usafi wa maofisini na majumbani
 
Nimesomea na nina ujuzi..Nina Bachelor Of Commerce in Accounting and Management(Upper Second Class) ya 1998 from University Of Dar es Salaam.Nimeshafanya kazi serikalini na kwenye taasisi binafsi.Naona nijiajiri mwenyewe kwenye anga hizi sababu nina uzoefu huu wa kufill Tax Returns na hata kuandaa Business Plan na Proposal(Hili nimejifunza tu mwenyewe na nimeshawaandikia watu na wakafanikiwa kuchukua mikopo hadi Bank)
Sasa nataka kulifanya serious nifungue ofisi yangu mwenyewe iwe ndiyo full time kazi yangu kwa sasa Mkuu.Asante kwa ushauri.So nianzie Brela then TRA siyo?
Ila sina CPA je hicho kinaweza kuwa kikwazo?
Naomba Ajira kabisa kaka hapo nikutaftie Market ya kitu unayofanya.
 
Ni utaratibu gani unatumika kuifufua kampuni ambayo imesimama kufanya kazi kwa muda wa miaka inayozidi mitano,kampuni ni ya Construction..Na je kubadilishwa jina inaruhusiwa na utaratibu ukoje!?

Kwanza kabisa ili kufufua kampuni yako na kama kampuni yuliisajili chini ya Mwaka 2018 (2017 kushuka chini) inabidi ufanye update ya kampuni yako BRELA.

Ukishaupdate sasa zoezi linalofuata ni kwenda TRA kuangalia kama unadaiwa chochote katika kipindi ambacho kampuni haikufanya kazi.

TRA watakuangalizia Tax Account yako na kukuelekeza nini na nini cha kufanya ili kuweza kuendelea.

Ukimalizana na TRA na wakikupa Tax Clearance nenda sasa CRB kuomba usajili wake

Ukimalizana na CRB rudi manispaa kufuatilia leseni ya biashara

NB: zoezi la kubadili jina la kampuni au mabadiliko yoyote yale katika kampuni linaweza kufanyika baada ya kukamilisha update ya kampuni yako
 
Nawezaje kupata tenda, nina kampuni y shughuli za usafi wa maofisini na majumbani

Jisajili kwenye mtandao wa TANEPS, kuna tender nyingi zinatangazwa humo haswa za serikali.

Muhimu tu hakikisha una TIN, Clearance na Leseni ya biashara. (Ukiwa na VAT Certificate ni added advantage)

www.taneps.go.tz
 
Kama una swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa usajili wake, kufanya mabadiliko, kodi za TRA na chochote kile kinachohusu kampuni kwa BRELA na TRA uliza hapa nitakujibu.

Karibu
Process za kupata EFD machine kwa Engineering company ambayo si limited
 
Mtaji wa kakampuni kadogo kadogoka kukopesha "micro credit" regulations zake



Acha nijibu kwa faida ya wengine pia ambao wanataka kujihusisha na biashara za kukopesa, nini na nini wafanye ili kupata kibali cha BOT ambao ndio wasimamizi wakuu wa biashara hii

MAELEZO YA JUMLA

1. Mwombaji anatakiwa awe amesajiliwa kwa mujibu wa sheria ya makampuni

2. Jina la kibiashara la mwombaji linatakiwa liwe na maneno yafuatayo “Microfinance”, “Finance” “Financial Services” “Credit” au “Microcredit”

3. Mwombaji anatakiwa kulipa ada ya maombi ya leseni ya shilingi 500,000 ambayo haitarudishwa

4. Mwombaji anatakiwa kulipa ada ya maombi isiyorudishwa kwa njia ya
uhamisho wa moja kwa moja wa TISS kutoka Benki zao kwenda Benki Kuu ya Tanzania

5. Mwombaji atahakikisha ana mtaji usiopungua shilingi milioni ishirini pale anapoanza biashara na wakati wote.

6. Sera ya Mikopo


Taarifa/Nyaraka zinazohitajika kwa ajili ya Maombi ya Leseni

1 Barua ya maombi

2. Slip ya Bank inayothibitisha malipo ya ada.

3. Uthibitisho wa chanzo na upatikanaji wa mtaji unaopendekezwa na mtoa huduma ndogo za fedha.

4. Nakala zilizothibitishwa za vyeti vya taaluma na utaalam vya wajumbe waBodi na Mtendaji Mkuu.

5. Audited Financial Statement (kama ipo).

6.TIN ya kampuni

7. Sera ya Mikopo.

8. Tamko kwamba fedha itakayotumika kuwekeza haikupatikana kwa njia ya
jinai au haihusiki na shughuli yoyote ya kijinai.

10.Copy za vitambulisho vya Directors na shareholders

11.Dodoso lililojazwa kikamilifu Kwa ajili ya Wakurugenzi, Mmiliki au Mtendaji Mkuu

12.Certificate of Incorporation

13. Memorandum
14.Board Resolution.
 
Asante kwa fafanuzi.
Niweke swali kwa wepesi.
Nikishafungua kampuni ni hesabu gani za kuhifadhi ili zitumike katika kufanya maamuzi ya kikodi.

Hifadhi kila hesabu inayohusiana na kampuni mkuu.. kwanza kuwa na Expenses/Purchases ledger.. Hifadhi risiti zote za manunuzi, kwa manunuzi au matumizi yasiyo na risiti kuwa na angalau petty cash voucher…

na kwa kuongezea Kama uko vizuri kwenye account na kutumia system basi hifadhi kukbukumbu zako pia kwenye accounting software (Tally au Quickbook)
 
Nimesomea na nina ujuzi..Nina Bachelor Of Commerce in Accounting and Management(Upper Second Class) ya 1998 from University Of Dar es Salaam.Nimeshafanya kazi serikalini na kwenye taasisi binafsi.Naona nijiajiri mwenyewe kwenye anga hizi sababu nina uzoefu huu wa kufill Tax Returns na hata kuandaa Business Plan na Proposal(Hili nimejifunza tu mwenyewe na nimeshawaandikia watu na wakafanikiwa kuchukua mikopo hadi Bank)
Sasa nataka kulifanya serious nifungue ofisi yangu mwenyewe iwe ndiyo full time kazi yangu kwa sasa Mkuu.Asante kwa ushauri.So nianzie Brela then TRA siyo?
Ila sina CPA je hicho kinaweza kuwa kikwazo?

Tutafutane mkuu tunaweza kufanya jambo sometimes
 
Hifadhi kila hesabu inayohusiana na kampuni mkuu.. kwanza kuwa na Expenses/Purchases ledger.. Hifadhi risiti zote za manunuzi, kwa manunuzi au matumizi yasiyo na risiti kuwa na angalau petty cash voucher…

na kwa kuongezea Kama uko vizuri kwenye account na kutumia system basi hifadhi kukbukumbu zako pia kwenye accounting software (Tally au Quickbook)
Hivi zile z report,risiti zake natakiwa kuzitunza?
 
Acha nijibu kwa faida ya wengine pia ambao wanataka kujihusisha na biashara za kukopesa, nini na nini wafanye ili kupata kibali cha BOT ambao ndio wasimamizi wakuu wa biashara hii

MAELEZO YA JUMLA

1. Mwombaji anatakiwa awe amesajiliwa kwa mujibu wa sheria ya makampuni

2. Jina la kibiashara la mwombaji linatakiwa liwe na maneno yafuatayo “Microfinance”, “Finance” “Financial Services” “Credit” au “Microcredit”

3. Mwombaji anatakiwa kulipa ada ya maombi ya leseni ya shilingi 500,000 ambayo haitarudishwa

4. Mwombaji anatakiwa kulipa ada ya maombi isiyorudishwa kwa njia ya
uhamisho wa moja kwa moja wa TISS kutoka Benki zao kwenda Benki Kuu ya Tanzania

5. Mwombaji atahakikisha ana mtaji usiopungua shilingi milioni ishirini pale anapoanza biashara na wakati wote.

6. Sera ya Mikopo


Taarifa/Nyaraka zinazohitajika kwa ajili ya Maombi ya Leseni

1 Barua ya maombi

2. Slip ya Bank inayothibitisha malipo ya ada.

3. Uthibitisho wa chanzo na upatikanaji wa mtaji unaopendekezwa na mtoa huduma ndogo za fedha.

4. Nakala zilizothibitishwa za vyeti vya taaluma na utaalam vya wajumbe waBodi na Mtendaji Mkuu.

5. Audited Financial Statement (kama ipo).

6.TIN ya kampuni

7. Sera ya Mikopo.

8. Tamko kwamba fedha itakayotumika kuwekeza haikupatikana kwa njia ya
jinai au haihusiki na shughuli yoyote ya kijinai.

10.Copy za vitambulisho vya Directors na shareholders

11.Dodoso lililojazwa kikamilifu Kwa ajili ya Wakurugenzi, Mmiliki au Mtendaji Mkuu

12.Certificate of Incorporation

13. Memorandum
14.Board Resolution.
Asante sana je mzunguko unaweza unaweza kuchukuwa muda gani endapo nitakupa kazi hii
 
Hivi zile z report,risiti zake natakiwa kuzitunza?

Unaweza kuzitupa kama ukiona zimejaa sana, mana Ukizitunza zote utaishia kujaza maboksi kwa maboksi ya z report, muhimu tu uwe unatoa Z report kila siku
 
Naomba hints nataka kuanzisha kampuni inayofanya kazi kama mtandao wa kupatana.com
 
Back
Top Bottom