Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Yaani katika kitu ambacho hutakiwi kuacha basi ni kufile ritani za kampuni pale muda wake unapofika.

Kwa kesi yako utapoenda TRA ukiandika barua watakuambia tu ufanye hayo makadirio ya mwaka huu, na mpaka sasa ushachelewa miezi mitatu tangu tarehe ya mwisho ya kujikadiria ilipofika (31 March)

Penalty kwa kila mwezi unaochelewa ni sh 225,000 kwahiyo mpaka sasa utakutakutana na penalty ya mieizi mitatu ambayo ni 675,000. Na kadiri unavyocheleqa hii Penalty inaongezeka tu, mfano ukienda TRA mwezi ujao Penalty yako itakua 900,000

Fanya kuwahi mapema au tuone Section Twenty tukusaidie kwa hilo
Nilikwenda TRA na kukuta bado hatujakadiriwa kodi, kwa hiyo nikaambiwa natakiwa kufile NIL returns hata kama sifanyi biashara bado ili kuepuka penalty, je nitapata wapi mhasibu wa kuzifile hizo NIL retruns hadi tutakapoanza operations?
 
Usiifunge kampuni kwa sababu hiyo mkuu, kama shida ni kujaza NIL Return za kila mwezi basi karibu ofisini nikueleweshe uwe unafanya mwenyewe kila mwezi.. Itakupunguzia gharama za uendeshaji wa kampuni
Mkuu dondosha mawasiliano hata pm kama hapa ni ngumu
 
Nilikwenda TRA na kukuta bado hatujakadiriwa kodi, kwa hiyo nikaambiwa natakiwa kufile NIL returns hata kama sifanyi biashara bado ili kuepuka penalty, je nitapata wapi mhasibu wa kuzifile hizo NIL retruns hadi tutakapoanza operations?
Hii mbona sio kazi sana,kufile

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Nilisajili kampuni mwaka 2020 nikapata brella certificate tu. Nikaishia hapo sikumalizia upande wa TRA na kampuni haikuwa inafanya tokea nilivyoisajili. Je hatua gani za kufanya ili kampuni ianze kazi na pia upande wa TRA ipoje?
 
Nilikwenda TRA na kukuta bado hatujakadiriwa kodi, kwa hiyo nikaambiwa natakiwa kufile NIL returns hata kama sifanyi biashara bado ili kuepuka penalty, je nitapata wapi mhasibu wa kuzifile hizo NIL retruns hadi tutakapoanza operations?

Mhasibu anapatikana kwetu mkuu, tuwasiliane 0714499248
 
Nilisajili kampuni mwaka 2020 nikapata brella certificate tu. Nikaishia hapo sikumalizia upande wa TRA na kampuni haikuwa inafanya tokea nilivyoisajili. Je hatua gani za kufanya ili kampuni ianze kazi na pia upande wa TRA ipoje?

Kwa hapo unatakiwa kwenda TRA kuomba TIN ya kampuni kwanza, ili kuomba TIN ya kampuni unapaswa kuwa na viambatanisho vifuatvyo

1. Certificate of Incorporation

2. Memorandum and Articles of association

3. Mkataba wa Pango yaani ofisi wenye mhuri wa mwanasheria ambae atakupa receipt ya EFD

4. Barua ya serikali ya mtaa

5. Vitambulisho vya Madirector wote

6. TIN za madirector

7. Fomu za maombi ya TIN ya kampuni (zinapatikana ofisi ya TRA)

8. Pamoja na kufanya makadirio ya kodi ya kampuni kwa njia ya mtandao (Efilling)

Ukimalizana na TRA watakupa TIN na Tax Clearance kwa ajili ya kuomba leseni ya biashara.

Ili kupata leseni ya biashara sasa vifuatavyo vinatakiwa

1. Certificate of Incorporation

2. Memorandum and Articles of association

3. Mkataba wa Pango yaani ofisi wenye mhuri wa TRA kuonyesha kuwa umelipa Stamp duty

4. TIN ya kampuni

5. Tax Clearance Original

6. Vitambulisho vya Madirector wote

Note: Kuna leseni zinaombwa halmashauri na nyengine Brela (inategemea na aina ya biashara) lakini pia kuna aina za biashara ambazo kabla ya kupata leseni unapaswa kuwa na kibali kutoka mamlaka nyengine

Ukimaliza mchakato wa leseni ya biashara hapo kampuni yako inakua ipo tayari kufanya kazi
 
M naomba kuuliza utaratibu wa kufuat ili kupata leseni ya biashara kwa kikundi cha wajasiriamali
(NB: hatutaki kusajili kama kampuni)
pia kupata namba ya utambulisho ya mlipa kodi( TIN NO) Mradi wetu unathaman ya 10M+

Maana kwa sasaivi tunatumia leseni na TIN ya mwenzetu changamoto inakua kwenye utambulisho na kukosa fursa ya mikopo kwenye taasisi mana ukienda bank kitu cha kwanza unaulizwa
1.Mmesajiliwa
2.Mnajihusisha na nn
3.Leseni ya biashara
3.Thamani ya mradi wenu

Kaka hamtaki kusajili kama kampuni then mnaweaza kusajili as Partnership

Partnership ni aina ya usajili wa jina la biashara na ufanyaji wa biashara wa kikundi cha watu kati ya 2-20 ambao wameamua kuungana kwa pamoja na kufanya biashara watazokubaliana.

Hii itakua ni rahisi kwenu endapo kama hamtaki kusajiliwa kama kampuni, maana documents zenu za usajili zitaonyesha majina ya kila Partner aliyekuwepo, muhimu tu kila mmoja wenu awe na namba za NIDA

Mkishajili Partnership BRELA, mtaenda TRA kupata TIN yake na mkimaliza mtaenda manispaa kufuatilia leseni.
 
Kusajili kampuni ya usafii inakuwa na hatua gani za kufuata kukidhii vigezoo
 
Kuna Annual return unatakiwa kuwasilisha kila mwaka Brela. Huwa inagharimu 22,000 tu kwa mwaka.
Nadhani hata kama hufanyi biashara hiki kiwango kwa mwaka huwezi kushindwa kulipia
Mkuu naomba kuuliza, je hii annual return ya brela iko constant??
Je hii return ina husiana na mtaji wa kampuni kama ulioainisha kwny memart?
 
Niko ughaibuni nimemtumia ndugu yangu kusajili kampuni ya ujenzi.
Naye ni director . Kampuni ina wakurugenzi 3
Ila gharama alinambia ni 1,988,500.

Kwa gharama hizo ulizo ainisha maana yake amenipiga na kitu kizito?
Mkuu labda jamaa yako akawa sahihi , chukua hii

mfano, umesema ni kampuni ya ujenzi
Tuassume hizi charges kasajili bila kutumia mtu; E.g
brela 512,000
Tra kupata Tin makadirio mpaka tax clearanc lets say kalipia 200,000
Then kupata leseni ya biashara amelipia ada 500,000
Then tunakuja kwenye bodi la wakandarasi kupata leseni yao CRB
Basically hio kampuni itakuwa ni civil and building kuna ile ada ya 80,000@ nimeisahau inaitwaje, yani hapo 160,000
Afu kuna ile ada yao ya daraja la kampuni mfano kasajili class six[emoji3]ambayo ni jumla 500,000 civil and building (kama ni daraja chini ya hili maanaake hio fee itaongezeka zaidi ya 800k)
Lakini kama kampuni ni ujenzi pekee haihusishi masuala ya civil basi ada zinaweza zipungue ama zisipungue kulingana na daraja ulilosajili , ninachokijua ni hakuna civil bila building

Bado hajaweka facilitation fees kwa wadau wote wanaohusika katika kufanikisha swala zima la mihuri na ukaguzi ili upate vyeti vyote husika kwa kampuni husika tufanye umetumia 200,000 mjini hapa

Hii draft inasoma 2.72mil

Nadhani hizo gharama alikuambia ni maeshakamilisha kila kitu tayari kwa kuanza kazi,,,

Nadhani pia huyo jamaa ako kuna pahala pia amejiongeza ili mambo yaende kama mnavopanga yaende cha muhimu endelea kuaminiana
 
Mkuu mimi nina swali


Kama nimeanza biashara mwaka jana November 2022, na mwaka huu natakiwa ni file Return of income zikiwa na audited financial statements


Lkn niliambiawa siwez fanyiwa audit mpka biashara iwe na miezi sita, sasa pale kwenye kusubmit financial statements ntaweka nini
 
Kampuni ni ndogo haijasajiliwa
Nataka kuanza kutunza hesabu na Sina mhasibu Wala uwezo wa kumlipa.

Ni kampuni ya Technology /IT

Ni vitabu gani vya hesabu natakiwakuwa navyo?

Je ni
Balance sheet
Cash flow statement
Income statement

Au daftari lamapato na matumizi ambalo content Nampa mtaalam.
 
Mkuu mimi nina swali


Kama nimeanza biashara mwaka jana November 2022, na mwaka huu natakiwa ni file Return of income zikiwa na audited financial statements


Lkn niliambiawa siwez fanyiwa audit mpka biashara iwe na miezi sita, sasa pale kwenye kusubmit financial statements ntaweka nini

Andika barua ya kuomba return yako ya mwanzo ufile mwakani na iwe ya miezi 14 badala ya 12, tunatumia Section 20 of Tax Administration Act kuomba hiyo, TRA watakubali na hautosubmit Financial statement kwa mwaka huu bali mpaka mwakani.

Kama nimekuvuruga na maelezo nipigie au WhatsApp nikupe na mfano wa hiyo barua inavyokua
 
Back
Top Bottom