Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tatizo liko hapa kuna watu wanaishi na ma housegirl km Wanaishi na mti yaan hawamjali hawamthamini hawajui yy ndo anawapikia chakula na kukaa na watoto wenu ..kwake kuwaua nyie ni rais sana akiweka tu sumu kwenye msosi...Na hasa wanawake mnamidomo sana yaan unakuta unaongea na mfanyakazi kwa dharaaauuu haya ndo malipo pia hata ma houseboy wanaweza hata kulawiti watoto ukaja kushangaa toto lako linakua shoga.Naruduia tena wanawake kaeni na wafanyakazi kwa upendo.Upande wetu sisi wanaume hatuna shida maana sometime tunawapunguzia upwiru na kuwapoza walee watoto shida ni nyie wake zetu.
Daah Mkuu umefanya mpaka nimecheka aisee!wanawake wana upimbi nakubaliana na wewe. kuna mdada wa kazi nilimtafutia mama mzazi. namlipa mwenyewe. dada akawa anasema anaishi vizuri sana nyumbani. kuna mama yangu mdogo matako yake akaja kuhamia hapo. kaleta fitina mpaka dada wa watu akajiondokea zake. moja ya ushenzi alikua analalamika kwanini dada wa kazi J2 tumemuwekea kama siku yake ya off. ningemkula huyu mama mdogo kama adhabu bahati yake.
kwanza hawakai muda mrefuKwanini Mkuu
ulitaka akae muda mrefu umemzaa ww...... alafu ukiona baba na mama hawashindi nyumbani na wadada wa kazi nao hawakai basi ujue kuna changamoto kwa baba na mama hasa kwenye kuishi nae vizuri lazima kuna manyanyaso yanaendeleakwanza hawakai muda mrefu
hata ukiwa unamuacha mwenyewe nyumbani na kazi za kawaida kabisa
still atakuletea za kuleta
Ni kweli Mkuu! Ni ngumu sana kuishi na dada wa kazi ambaye naye ni mtoto tena kama mtoto wako halafu atimize majuumu ambayo wewe mtu mzima umeshindwa.hivi unawekaje dada wa kazi za ndani mwenye umri wa miaka 13 hivi serikali haioni ni utumikishwaji wa watoto?
alafu majumbani mwetu tunawanyanyasa vipigo kuwatenga nao ni binadamu wanafika sehemu wanachoka japo sisemi waue ila wanapitia magumu mengi sana....
ukichunguza kwenye hiyo familia lazima kutakua kuna manyanyaso yaliendelea mtu mwenye akili timamu hawezi tumikisha mtoto wa miaka 13 hapo tu ni ukatili sasa najiuliza humo ndani anakatiliwa na kunyanyaswa kwa mangapi
inaonekana ndugu zako hawana kazi...... huwezi mtegemea ndugu akusafishie nyumba afanye kazi anazofanya dada..... ndugu ataleta maneno hata kama unamlipa bora ujitafutie mtu ujue namlipa afanye kazi niishi nae kuliko ndugu....... hawana jema kabisaaa utasemwa vibaya wwSi tumeacha utamaduni wa kuishi na ndugu majumbani mwetu sababu ya ubinafsi tutegemee mengi zaidi ya haya.
Fungeni camera siku hizi hata elf 40 unafunga chip una connect na simu yako unaona kinachoendelea home
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]wanawake wana upimbi nakubaliana na wewe. kuna mdada wa kazi nilimtafutia mama mzazi. namlipa mwenyewe. dada akawa anasema anaishi vizuri sana nyumbani. kuna mama yangu mdogo matako yake akaja kuhamia hapo. kaleta fitina mpaka dada wa watu akajiondokea zake. moja ya ushenzi alikua analalamika kwanini dada wa kazi J2 tumemuwekea kama siku yake ya off. ningemkula huyu mama mdogo kama adhabu bahati yake.
Mtoto Erickson Kimaro mwenye umri wa miaka nane anadaiwa kunyongwa na dada wa kazi Mei 31, nyumbani kwao Kimara Temboni jijini Dar es Salaam.
Msichana wa Kazi za ndani mwenye umri wa miaka 13 Mkazi wa kata ya Moshono jijini Arusha anadaiwa kumuua kwa kipigo mtoto wa Boss wake mwenye umri wa miaka minne aitwae Natalia Essau.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia mfanyakazi wa ndani, Ashura Suka kwa tuhuma za kumuua mtoto mdogo wa mwajiri wake.
Hizi ni kesi tatu ambazo zimekuwa mfano bora sana wa kinachoendelea ndani ya kaya zetu. Wadada wa kazi ingawa sio wote ila wameonesha namna ya hatari ndani ya makazi haswa wanapoachwa na wanafamilia hususani watoto. Mauaji au majeraha huwa ni matokeo ya baadhi ya vitendo ambavyo hutokea ndani ya nyumba huku wadada wa kazi wakiwa ni wahusika wakuu. Ukiachana na kuhusu kuvunja ndoa za watu wakitumia uchawi na mbinu zingine basi usalama wa familia zetu umekuwa ni dhaifu sana tena pale ambapo tunatoka na kuelekea kwenye harakati za kimaisha.
Leo kupitia mtandao wa Facebook, moyo wangu umeumia sana kusikia taarifa za huyu bi mdada katika picha ambaye anasadikiwa kuwa amemchinja mtoto wa Boss wake huko Goba, mtoto wa miaka minne na kwa sasa anatafutwa na Jeshi la Polisi ili kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Haya ni baadhi ya maoni yangu:
Dada yangu ambaye upo kwenye ndoa na una familia yako, hakuna ambaye anafahamu kumhudimia mume wako vyema zaidi yako, hakuna ambaye anajua taste ya chakula kizuri cha mume wako zaidi ya wewe mwenyewe. Hakuna ambaye anajua glasi pendwa ambayo Mume wako anapenda kutumia kunywa maji. Kama mkiwa faragha unampa mapigo yote basi hakikisha sekta zingine unazicheza vyema kama Xavi au Iniesta. Kukiwa hakuna ulazima wa kuleta dada wa kazi basi usifanye uamuzi huo. Hakuna mlezi bora wa mtoto wako zaidi ya wewe ambaye umembeba miezi tisa na kuingia labour. Usijitoe akili kumkabidhi mwanamke mwingine akulele mtoto wako. Kazi na majukumu zisikufanye upoteze umakini kwa familia yako. Wanaume wenzangu, nyumba zetu zina mambo mengi na Mtume Paulo hakuwa punguwani kiasi hicho mpaka kusema maneno haya "Kwa maana mume ni kichwa cha mke kama vile Kristo alivyo kichwa cha kanisa, ambalo ni mwili wake, naye mwe nyewe ni Mwokozi wa kanisa. 24 Basi, kama vile Kanisa linavyom tii Kristo, vivyo hivyo na wake pia wanapaswa kuwatii waume zao kwa kila jambo. 25 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo alivyolipenda kanisa akajitoa nafsi yake kwa ajili yake ili 26 alitakase (Waefeso 5:23-26) Usije kuruhusu mwanamke mwingine akupe mrejesho wa zao la manii zako eti, amekula tayari na amelala, wala usijali! Yaani nisijali kuhusu mtoto wangu?! Shirikiana na mke wako kufuatilia maendeleo ya mtoto au watoto wenu. Waislamu tunafundishwa “Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi … (Quran 4:34)” Akili kumkichwa wanaume. Kwa jamii, kukiwa na ulazima wa kuishi na dada wa kazi basi hakikisheni mnawapeleka hospitali kupima afya za akili, watu wengi mitaani hupenda wadada waliotoka vijijini tena wenye umri mdogo. Sasa Kitoto kina miaka 16 kimetoka Mufindi ndani ndani huko baada ya kufeli darasa la Saba, kimelelewa na Bibi pekee na hakijawahi kupata upendo wa Baba na Mama, wala kuambiwa na mzazi wake neno Nakupenda sana mwanangu unamchukua unamleta Ubungo Maji na kuishi naye mkiwa na watoto wenu wa miaka 10 hapo nyumbani. Asubuhi wenzake wanaenda shule (English Medium) na yeye anaenda kuosha vyombo vya usiku. Weekend wenzake wanakwenda Kunduchi Wet "N" Wild Water Park kucheza na maji na kula Ice Cream, ila yeye anapewa kazi ya kufua nguo za familia nzima, marundo na marundo ya nguo. Akili yake iaanza kuathirika taratibu na mwishoni atajenga nongwa hatari sana, mdogo mdogo anawaona watoto wenzake kama threat, wapunguzieni kazi na kila baada ya miezi mitatu wapelekeni hospitali wamtazame afya yake ya akili na kuzungumza na wanasaikolojia.NINAWAKUMBUSHA TU, KUMTAFUTA DR. CHRIS MAUKI AZUNGUMZE NA FAMILIA YAKO SIO GHARAMA ZAIDI YA KUMPOTEZA MTOTO WAKO KWA MAKOSA AMBAYO AMBAYO YANAZUILIKA.
Sheikh ponda walimfokea aliposema mabinti kuolewa wakiwa wadogo ila hili la kuajiri vitoto hawalioni.hivi unawekaje dada wa kazi za ndani mwenye umri wa miaka 13 hivi serikali haioni ni utumikishwaji wa watoto?
alafu majumbani mwetu tunawanyanyasa vipigo kuwatenga nao ni binadamu wanafika sehemu wanachoka japo sisemi waue ila wanapitia magumu mengi sana....
ukichunguza kwenye hiyo familia lazima kutakua kuna manyanyaso yaliendelea mtu mwenye akili timamu hawezi tumikisha mtoto wa miaka 13 hapo tu ni ukatili sasa najiuliza humo ndani anakatiliwa na kunyanyaswa kwa mangapi