Umebaini tofauti gani Uwanja wa Mkapa na Uwanja wa Samia unaotarajiwa kujengwa Arusha?

Umebaini tofauti gani Uwanja wa Mkapa na Uwanja wa Samia unaotarajiwa kujengwa Arusha?

Dah! Wanachuo wa Mwaka wa kwanza 2023/2024 wanalia kwa kupewa mkopo kiasi kidogo sana almost 70% wamepewa kiasi kidogo na wengine 20% kukosa kabisa ila bajeti ya uwanja wanaiweka juu sana au ndo michezo kwanza elimu baadae🤔
 
Uwanja wa Mkapa ulijengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya #Tanzania na #China, mpango uliopo mezani ni mchakato wa ujenzi wa uwanja mwingine wa kisasa ambao Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu Utamaduni na Michezo imesema itawasilisha mapendekezo uitwe Uwanja wa Samia Suluhu Hassan.

Pia, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo nayo ilieleza mipango iliyopo ni kuwa Uwanja wa Samia ukamilike kabla ya Mwaka 2027 ili utumike kwenye Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).


Uwanja wa Mkapa
Mkoa: Dar es Salaam
Idadi ya siti: 60,000
Ulizinduliwa: Mwaka 2007
Gharama za Ujenzi: Dola Milioni 56 (Tsh. Bilioni 64 wakati huo)
Umiliki: Serikali ya Tanzania
Mkandarasi: Beijing Construction Engineering Group (BCEG)


Uwanja wa Samia
Mkoa: Arusha
Idadi ya Siti: 30,000
Kuzinduliwa: Kati ya Mwaka 2025 hadi 2027
Gharama za Ujenzi: Dola Milioni 112 (Tsh Bilioni 286) kabla ya kodi
Umiliki: Serikali ya Tanzania
Mkandarasi: China Railway Construction Engineering Group (CRCEG)

View attachment 2940937
View attachment 2940938
Muonekano wa Uwanja wa Samia unavyotarajiwa

View attachment 2940941
Uwanja wa Mkapa​
Mimi nimebaini kitu kimoja tu hapa!! Wahuni siyo watu wazuri hata kidogo.

Kama kwenye ununuzi wa ndege ya mizigo, Mama mwenyewe alikiri hadharani wahuni waliongeza cha juu! Ndiyo washindwe kwenye huo uwanja!! Narudia tena kusema Wahuni siyo watu poa hata kidogo.
 
Hivi kwann jina la uwanja usingeitwa MANGI MELI STADIUM jina la chief wa eneo hilo tukabak tunawaenz machifu katika eneo husika la uwanja kupunguza miradi mingi kuitwa majina ya raisi wakat machifu wa maeneo husika wakienda kusahaulika kabisa
 
Hii nchi wajinga ni wengi sana. Yani kabisa mtu unalinganisha gharama za miaka 17 iliyopita na leo hii?
Mfano mdogo, mfuko mmoja wa cement mwaka 2007 ulikuwa bei gani na leo hii ni bei gani? Kibarua atakayepewa kazi pale atalipwa sawa na 2007? Hapo hatujaongelea skilled labor.

Wakati mwingine ni vyema kutumia akili kabla ya kupinga kila kitu.
Ndio tofauti iwe bilioni 200?
 
Wakati mnajadili juu ya Gharama ,angalieni hivi vipengele.
1.Thamani ya shilingi ahidi ya Dola imepungua.
2.Mfumuko wa bei
3.Aina ya Sanifu
4.Eneo la Nje ya uwanja litakalofanyiwa matengenezo ni kubwa kuliko awali.
5.Matilio yatakayotumika kwenye uwanja mpya ni bora zaidi.
6.Teknolojia itakayowekwa kwenye uwanja mpya ni bora zaidi
7.Riba ya Mkopo kwa miaka hii ni kubwa kutokana na kupanda kwa Interest ya Federal Bank.

Tusiwe wepesi wa kukurupuka na kulaumu...Tafiti muhimu
 
Uwanja wa Mkapa ulijengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya #Tanzania na #China, mpango uliopo mezani ni mchakato wa ujenzi wa uwanja mwingine wa kisasa ambao Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu Utamaduni na Michezo imesema itawasilisha mapendekezo uitwe Uwanja wa Samia Suluhu Hassan.

Pia, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo nayo ilieleza mipango iliyopo ni kuwa Uwanja wa Samia ukamilike kabla ya Mwaka 2027 ili utumike kwenye Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).


Uwanja wa Mkapa
Mkoa: Dar es Salaam
Idadi ya siti: 60,000
Ulizinduliwa: Mwaka 2007
Gharama za Ujenzi: Dola Milioni 56 (Tsh. Bilioni 64 wakati huo)
Umiliki: Serikali ya Tanzania
Mkandarasi: Beijing Construction Engineering Group (BCEG)


Uwanja wa Samia
Mkoa: Arusha
Idadi ya Siti: 30,000
Kuzinduliwa: Kati ya Mwaka 2025 hadi 2027
Gharama za Ujenzi: Dola Milioni 112 (Tsh Bilioni 286) kabla ya kodi
Umiliki: Serikali ya Tanzania
Mkandarasi: China Railway Construction Engineering Group (CRCEG)

View attachment 2940937
View attachment 2940938
Muonekano wa Uwanja wa Samia unavyotarajiwa

View attachment 2940941
Uwanja wa Mkapa​
Nilidhani utakuwa na idadi kubwa kuliko wa mkapa ,your projects do not think about future generations
 
ni kweli gharama zimepanda, ila kiuhalisi thamani halisi ya uwanja wenye capacity ya 30k kwa standard zetu ni $60m, haizidi hapo!

kikawaida kiti kimoja kinagharimu $1000 (ndio simple calculation ya viwanja ilivyo), so at maximum uwanja wa 30k unaojengwa tanzania (nchi ambayo maeneo wazi ni mengi wala hulipi fidia) haikutakiwa kyzidi $60m
Hata mimi kwa tathmini ninaona hio ndio thamani halisi ya 30k capacity Arena. Ingekuwa 60K ndio ingefika kwenye 100B kihaki tu.
 
Ndio tofauti iwe bilioni 200?
Inashangaza mno, hebu waza nyumba tu ya room 3 ya ukubwa wa 9×12 kama mwaka 2007 ilikuwa inakamilika kwa 40M hadi finishing, mtu akikwambia kwamba leo atakujengea nyumba nyingine mpya ya vyumba viwili ya 8×10 lakini gharama zitakuwa 160M utakubali?

Kigezo akwambie dollar imepanda sijui material na cement bei iko juu. Hivi inaingia akilini kweli hio?
 
Inashangaza mno, hebu waza nyumba tu ya room 3 ya ukubwa wa 9×12 kama mwaka 2007 ilikuwa inakamilika kwa 40M hadi finishing, mtu akikwambia kwamba leo atakujengea nyumba nyingine mpya ya vyumba viwili ya 8×10 lakini gharama zitakuwa 160M utakubali?

Kigezo akwambie dollar imepanda sijui material na cement bei iko juu. Hivi inaingia akilini kweli hio?
Hivi sasa ndio watu wanapiga pesa balaa yaani inafikilisha sana imagine
Tena mfano uliotoa wewe una nafuu kumbuka uwanja wa mkapa ni mkubwa kuliko wa Arusha then Gharama zinaongezeka bilion 200😳 duuh ni pesa nyingi hata kama ni 2007 na 2024 daah watu hawana huruma na kodi zetu
 
Hii nchi wajinga ni wengi sana. Yani kabisa mtu unalinganisha gharama za miaka 17 iliyopita na leo hii?
Mfano mdogo, mfuko mmoja wa cement mwaka 2007 ulikuwa bei gani na leo hii ni bei gani? Kibarua atakayepewa kazi pale atalipwa sawa na 2007? Hapo hatujaongelea skilled labor.

Wakati mwingine ni vyema kutumia akili kabla ya kupinga kila kitu.
Duuuh,na hapa umetumia akili???
Aisee
 
Si bora wale hiyo hela na uwanja ukajengwa kuliko kula hela bila mradi wowote. Kwani mnadhani hozo bilioni 200 hawawezi kuchukua bila kupitia kwenye mradi wowote? Hata wangekula bila kujenga uwanja mngewafanya nini?
 
Duh! Yani uwanja wa Benjamin Mkapa wenye capacity ya 60,000 thamani yake inaingia mara 4 na upuuzi kwenye huu uwanja wa capacity ya watu 30,000!

Haya maajabu, ngojea tuuone huo uwanja mpya!
Value ya hela miaka20 iliyopota ni ile ile ya leo? Billions 60 miaka 20.iliyopita unajua leo itakuwa kiasi gani?
 
Back
Top Bottom