Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
- Thread starter
- #41
Sijawahi kufuatilia maisha ya mtu mimi.We jamaa mbona unafuatiliya maisha ya watu sana.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sijawahi kufuatilia maisha ya mtu mimi.We jamaa mbona unafuatiliya maisha ya watu sana.
Bila shaka hujalielewa andiko.hata hivyo utaelewa taratibu kulingana na uwezo wa akili yako.Kama unamwonea wivu Tulia
Njoo na wewe tukupakate ndugu mwashambwa
Kaa kwa kutulia na kujikita katika hoja.Acha bangi mkuu,ya kwako yanakushinda.
Kama ulisoma sayansi ya siasa basi uliforce taaluma.
Hivyo umelala YOO
Amefanikiwa pia kulituliza jiji la Mbeya na wana Mbeya.Tulia ametulia
Huko sijui usiniwekee maneno mdomoni.Amefanikiwa pia kulituliza jiji la Mbeya na wana Mbeya.
Huko nimekuongezea tu kwa faida ya wengine.Huko sijui usiniwekee maneno mdomoni.
Sisi wenye jicho la kiroho hiyo ni tambiko na ibaada za kishetaniNdugu zangu Watanzania,
Hapa chini ni picha ya Mama mzazi wa Mheshimiwa Dkt Tulia Acksoni Mwansasu ,speaker wa Bunge letu pamoja na Rais wa umoja wa mabunge Duniani yaani IPU. Tukio hili la kugusa hisia za watu na ambalo liliteka hisia za watu wengi sana mitandaoni na DUNIA nzima kwa ujumla wake lilitokea mara baada ya Dkt Tulia kurejea Nchini kama Rais mpya wa IPU.
Ambapo ni katika tukio hilo ambapo Dada wa Taifa,fahari ya nyanda za juu kusini,msomi Nguli wa sheria kuwahi kutokea nyanda za juu kusini na chaguo la wana Mbeya alionyeshwa upendo wa kipekee kabisa kutoka kwa Mama yake huyu Mzazi aliyeamua kumpakata Mwanae kwa upendo na hisia kali sana na kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake na kuiheshimisha Mbeya na Tanzania nzima kwa ujumla wake..
Bila shaka Mama huyu na mama yetu aliyemleta DUNIANI speaker wetu kijana kabisa na mwenye akili kubwa ,mfano wa kuigwa kwa watoto wengi wa kike wanaosoma na mwenye moyo wa ukarimu,huruma,upendo, unyenyekevu,utu na ucha Mungu alimkumbusha mama yake na kumrejesha mbali sana kimawazo.
Bila shaka Mama yetu aliwaza mapito na magumu aliyopitia kimaisha katika kumlea mwanae mpaka kufika hapo alipofika ,mahali ambapo Dunia ikakubali uwezo wake na kumpatia Urais wa IPU kwa kishindo.bila shaka alikuwa anajionea kwa macho yake matendo makuu ya Mungu,bila shaka alikuwa anaona maneno yaliyoandikwa katika kitabu cha Samweli kuwa Mungu humuinua mnyonge kutoka mavumbini na kumpandisha mhitaji kutoka jaani ili kumketisha pamoja na wakuu , yakitimia kama ndoto machoni pake.
Bila shaka mama yetu ndani ya moyo wake alikuwa akibubujikwa na machozi ya furaha na shukurani kwa Mungu wake ,kwa kumkumbuka na kumuinulia Mwanae kama Nuru katikati ya giza kama ambavyo Mungu alimkumbuka Hana ambaye alikuwa ni Tasa na ambaye alikuwa akilia kila siku ili Mungu ampatie mtoto na hatimaye Mungu akajibu Maombi ,kwa kumpatia watoto na miongoni mwake ni Samweli aliyekuja kuwa mfalme.
Akina Mama wanapaswa kupewa heshima yao na kuheshimiwa sana.tunapaswa kuwapenda Mama zetu.jiulize ni mangapi amepitia Mama huyu katika kumsomesha mwanae mpaka kumfikisha alipofika? Ikumbukwe ya kuwa mama huyu na familia yake hakuwa tajiri wala kumiliki utajiri.lakini kwa uweza wa Mungu alihakikisha mtoto wake anatimiza ndoto zake za kielimu mpaka mwisho.
Ni kupitia tumbo la Mama huyu mpole na mkarimu leo Dunia inafaidika na akili na kipawa cha uongozi cha Mwanae Dkt Tulia,leo watu wanapata tabasamu na matumaini katika maisha yao baada ya kusaidiwa na kufikiwa na mkono wa huruma wa mwanae Dkt Tulia,leo mabinti wa kike mkoani mbeya wanasoma huku mfano wao ukiwa Dkt Tulia.
leo yatima ,wajane na wazee wasio jiweza mkoani Mbeya wanapata matumaini na kuishi kwa furaha kwasababu ya kusaidiwa kwa hali na mali na Dkt Tulia,leo maelfu ya watu mkoani Mbeya wanaishi bila wasiwasi na kuwa na uhakika wa kupata matibabu wakiumwa baada ya kuwa wamegawiwa bure kabisa Bima za afya, na wengine kujengewa nyumba huku wengine wakipewa na kuwezeshwa mitaji ya kufanyia biashara zao za kuwapatia na kuwaingiza kipato cha kila siku.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Ingekuwa ni hivyo asingekuja na hoja ya kuligawa jimbo.Huko nimekuongezea tu kwa faida ya wengine.
Hata kama mkoa mzima wa Mbeya ukawa ni jimbo moja bado dkt Tulia atashinda na kupita kwa kishindo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima.Ingekuwa ni hivyo asingekuja na hoja ya kuligawa jimbo.
😂 dunia litetemeke kwa jimbo lenye maharage ? We mgonjwa kweli mkuuHata kama mkoa mzima wa Mbeya ukawa ni jimbo moja bado dkt Tulia atashinda na kupita kwa kishindo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima.
Hapa umenena...Hakuna jiwe litakalo bakia pasipo kugeuzwa.
Naona unahangaika sana na mimi mpaka unapata presha.kaa kwa kutulia usije ukapata maradhi ya moyo ya kudumu .Mbona unarukiarukia watu kama ngedere anavyohama matawi hatulii kwenye tawi moja,mara umemrukia samia,mara makonda,mara Tulia Epson firigisi wewe
Kwa sasa Mbeya inafahamika hadi white house Marekani kutokana na Dr Tulia Acksoni Mwansasu kuwa mbunge wake.😂 dunia litetemeke kwa jimbo lenye maharage ? We mgonjwa kweli mkuu
Aisee samahani sikusoma vizuri kichwa cha thread kumbe kiliuliza tumejifunza nini katika hiyo picha,tulichojifunza wewe ni "kijakazi" mwandamizi unaepata ujira wako kwa kupiga zumaliNaona unahangaika sana na mimi mpaka unapata presha.kaa kwa kutulia usije ukapata maradhi ya moyo ya kudumu .
Kweli EPN anakuchanganya mpaka unaanza kuongea visivyoeleweka, ila teuzi utapata tu mkuu kwa mapambio haya usipopewa hata kitongoji baada 2025 achana na siasa.Kwa sasa Mbeya inafahamika hadi white house Marekani kutokana na Dr Tulia Acksoni Mwansasu kuwa mbunge wake.
Acha ukurupukaji .Aisee samahani sikusoma vizuri kichwa cha thread kumbe kiliuliza tumejifunza nini katika hiyo picha,tulichojifunza wewe ni "mshobokaji" mwandamizi
Niachieni ephen 😃😃Kweli EPN anakuchanganya mpaka unaanza kuongea visivyoeleweka, ila teuzi utapata tu mkuu kwa mapambio haya usipopewa hata kitongoji baada 2025 achana na siasa.
Tafuta kuachiwa jimbo kwanza alafu ndio uachiwe huyo ili ububujikwe na machozi vizuri 😂Niachieni ephen 😃😃