Umeona nini kwenye maziko ya yule tajiri wa Kibaniani, Patel tokea mwanzo hadi mwisho?

Umeona nini kwenye maziko ya yule tajiri wa Kibaniani, Patel tokea mwanzo hadi mwisho?

Asilimia 99 ya waliohudhuria wamevaa barakoa, hili mliliona? Na kujiuliza kulikoni, jamii ya mabaniani ndio karibia wote wamevaa hizo barakoa na sisi tuliokoza rangi ya kiza baadhi walikuwa hawakuvaa kitu, kwenye wafanyakazi wote wamevaa?

Bado unaamini yule kimelea hayupo Tanzania? Na hivi karibuni kumeongezeka vifo vya wazee wazee na tunaopata matangazo tu ni hawa matajiri au vingunge na walio kwenye jamii maarufu kama wasanii, tulio wengi pangu pakavu hutusikiki.

Sasa rudia kuangalia kideo ya mazishi ya Patel, Je, alikumbana na vimelea huko South Africa? Sababu gani jiulize iliyofanya wahudhuriaji kuibuka na barakoa ghafla bin vu?

Anza leo kuvaa barakoa usisikilize redio v
Covid 19 umepamba moto, kama una daktari rafiki yako mhimili muulize, tutakoma kukubali kuongozwa na washamba wapenda sifa za kijinga
 
CORONA haiitaji promo mzee.
Inajionesha yenyewe.
Covid 19 umepamba moto, kama una daktari rafiki yako mhimili muulize, tutakoma kukubali kuongozwa na washamba wapenda sifa za kijinga
 
Kwani waliokufa kidogo ? Tunakaribia milioni 60 kasi ya kuzalishana ikizidi bilioni haipo mbali.
Hebu jiulize siku ya mwisho kuacha kudadavuliwa wagonjwa wa huyu mdudu ni lini ? tulikuwa na wagonjwa wangapi kule rugodzinla.

Ni lini ulisikia na wapi kutangazwa idadi ile ilipoishia ,kama haipo ndivyo tunavyoomba tusijikaze kisabuni halafu tunaendelea kufa kijeshi aka kiofisa.

Ndugu fuatilia mitaani tu mbona habari za vifo vimeongezeka sana ukitofautisha na kabla ya kuzuka huyu mdudu,watu wanaondoka ,sema sio matajiri au mabilionea na hawana hata undugu wa mbali ndio ukaona kimya.Ndio ilivyo huwezi kujua.
Habari za vifo zimeongezeka ila wewe hufi?mashuleni watoto wangekua wameisha

Ifike wakati tusilazimishane kuishi kwa mapendekezo binafsi, mzee jipige lockdown wewe na family yako wala hakukuna wa kukuuliza ila usitake kutulazimisha kitu kisichopo

Kila mtanzania anakiri kwamba Corona ilikuepo ila sasa haipo sababu hawaioni mitaani na hivyo kuibuka maswali kama kweli hiyo ya zamani ilikua Corona kweli au ni tension tu!
 
Dah....waswahili tunapenda drama sie 😏😏

Kwani wewe kama wewe unawajua watu wangapi (na hapa naongelea personally sio hao maarufu ama wakuambiwa) waliokufa kwa corona??? Ndugu yzako wangapi??? Majirani je???
Mie binafsi sina nnaemjua hata mmoja.

Ila walioipata nawajua wakutosha...nikiwamo mimi binafsi, mwanangu, marafiki zangu etc. Etc....ila wote tumepona.

Kwahiyo ndio...CORONA IPO ila tuache kuikuza sana na kujazana hofu. Ukipata wahi kachukue NimrCuff. ..kama huwezi fuata ushauri wa muheshimiwa upige nyungu pamoja na madawa ya asili yanayojulikana siku zote kuwa yanasaidia unapopata mafua na kikohozi.
 
Wamarekani,waingereza wamewekeza billions of money kununua dawa ya corona. Ivi kwanini wasingetumia njia hii yakwako kutibu corona alaf hizo hela wafanyie mambo mengine ?

Kila jambo lina siri zake, hayawekwagi yote hadharani.

Wazungu wana mambo yao.

Sisi ya kwetu waafrika au waswahili ni kuwa siri utaipata shambani.
 
1. Tafuna tangawizi kila siku asubuhi na jioni.

2. Kunywa maji ya uvuguvugu yaliyotiwa binzari mbichi (turmeric) ama ukikosa tumia ya unga pamoja na mdalasini wa magome wa India, kila asubuhi na jioni.

3. Kula matunda ya kutosha kutwa nzima, ikiwezekana mlo mmoja kati ya milo yako 3 ya siku uwe matunda tu.

4. Kunywa maji ya kutosha walau lita 2 hadi 3 kwa siku, vyema yakawa ya vuguvugu.

5. Fanya shughuli ambayo itakutoa majasho kila siku walau kwa dakika 20 hadi 30.

Afya njema ni maamuzi ya mtu binafsi.

Kasinde Matata.
Hapo namba nne utawaua watu kwa ugonjwa wa moyo! Lita 3 - 4 kwa siku? Tiba asilia wanatudanganya sana! Ongeza na Dr. Mohamed Janabi akueleze matatizo ya maji mengi mwilini!
 
Hapo namba nne utawaua watu kwa ugonjwa wa moyo! Lita 3 - 4 kwa siku? Tiba asilia wanatudanganya sana! Ongeza na Dr. Mohamed Janabi akueleze matatizo ya maji mengi mwilini!

Ukinywa lita tatu hadi nne kwa siku halafu hukojoi na umekaa tuu hapo hufanyi zoezi lolote litalokutoa jasho, wala hujitaji maelezo ya Dr Janabi.... mwili utakuletea matokeo hasi tuu.

Uzuri inatakiwa wqtu wapate maarifa nini cha kufanya na kwanini unafanya hivyo. Asilimia kubwa ya kina sisi ni kusoma kukopi na kunakili bila kujiuliza matokeo yake ni yepi, hasi ama chanya...!

Na ili ujue sasa hivi mwili wako una maji mengi au umekaukiwa, utajuaje? Maarifa ndo yatakufikirisha cha kufanya kabla ya kubugia lita 2 au 3 au 1 au glasi 8.

Ukinakili ile ya kwamba mtu anywe glasi 8 kwa siku, je huyo mtu ana kilo ngapi? Mrefu ama mfupi? Wa miraba minne ama kimbaumbau, mtoto wa miaka 12 ama miaka 45 amani mzee wa miaka 78...!!!?
Hiyo ni moja tuu ya vipengele vingi vya kufanyia kazi kabla ya kuchukua hatua.

Alamsiki.
 
1. Tafuna tangawizi kila siku asubuhi na jioni.

2. Kunywa maji ya uvuguvugu yaliyotiwa binzari mbichi (turmeric) ama ukikosa tumia ya unga pamoja na mdalasini wa magome wa India, kila asubuhi na jioni.

3. Kula matunda ya kutosha kutwa nzima, ikiwezekana mlo mmoja kati ya milo yako 3 ya siku uwe matunda tu.

4. Kunywa maji ya kutosha walau lita 2 hadi 3 kwa siku, vyema yakawa ya vuguvugu.

5. Fanya shughuli ambayo itakutoa majasho kila siku walau kwa dakika 20 hadi 30.

Afya njema ni maamuzi ya mtu binafsi.

Kasinde Matata.
K.Matata kwenye ubora wake 😆😆
 
Acha umbea mungu katuepusha na korona wakala wa shetan unamiemko ya kisiasa wew
Kwani waliokufa kidogo ? Tunakaribia milioni 60 kasi ya kuzalishana ikizidi bilioni haipo mbali.
Hebu jiulize siku ya mwisho kuacha kudadavuliwa wagonjwa wa huyu mdudu ni lini ? tulikuwa na wagonjwa wangapi kule rugodzinla.

Ni lini ulisikia na wapi kutangazwa idadi ile ilipoishia ,kama haipo ndivyo tunavyoomba tusijikaze kisabuni halafu tunaendelea kufa kijeshi aka kiofisa.

Ndugu fuatilia mitaani tu mbona habari za vifo vimeongezeka sana ukitofautisha na kabla ya kuzuka huyu mdudu,watu wanaondoka ,sema sio matajiri au mabilionea na hawana hata undugu wa mbali ndio ukaona kimya.Ndio ilivyo huwezi kujua.
 
Back
Top Bottom