Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Ukishindwa kufanikiwa Dar basi hakuna sehemu utayoweza kufanikiwa. Huu mji hauhitaji nguvu nyingi bali ni akili tu uweze kupata pesa za kusurvive. Ukiangalia kwa umakini Dar imejaa wageni wengi kutoka nje ya nchi wapo hapa kutafuta maisha ukienda nchi zingine ukiwaambia habari za Dar wanakuambia Dar kuzuri sana hasa kwenye utafutaji. Huu mji unafursa kwa kijana anayeanza maisha.

Shida inakuja apa, vijana wengi kuendeleza starehe na wanawake kwenye huu mji ndio maana unakuta wengi wao wana maisha magumu hawafikirii kesho yao unakuta siku zinakwenda kijana hata kujenga anashindwa na kipato anapata freshj shida ni kuendeleza starehe na wanawake maana huu mji unavishawishi vingi sana usipokuwa makini lazima ufeli lakini kwa kijana mwenye malengo huu mji utamfaa katika harakati za utafutaji kikubwa akae mbali na starehe na wanawake
 
Pia vijana wengi wa huku Dar ni wavivu sana kwenye kujishughulisha, wengi wao wanakesha kutwa nzima kwenye vibanda vya kubeti mipira na hata kwenye mitandao ya kijamii na wanaridhika na maisha wanayoishi.

Image kijana yuko tayari alale na njaa ili anunue bando au abeti vijana wa Dar wanashindwa kushughulisha ubongo wao ni wavivu haswaa
 
Bila salamu nawapa ujumbe wenu enyi watu.

Mnaweza kusema kuwa najiinua au nawakashifu ila Mimi siko huko. Ni upendo tu.

Waarabu wanasema fikisha ujumbe hata kama ni mchungu.

Miaka 5 inatosha kabisa mtu kupima bahati ya maisha Dar es salaam au mahali popote.

Unaishi Dar miaka zaidi ya 5 huna nyumba, huna kiwanja, kula kwako ndo kule unatafuta leo ili ule leo, kila siku kwenye daladala wewe ukichomoa pesa kubwa basi buku 2.

Unalala store (jiko, meza, sofa, feni, kitanda, pasi, bag la nguo na vitu vingine vyote ukifungua macho tu hivi hapa.

Tanzania hii kuna mahali kama Liwale huko Lindi ukifika kijiji chochote ukiomba ardhi ya kujenga au kulima unapewa bure kabisa. Yet wewe uko dar hata hatua 4 za ardhi Chanika huna . Umerogwa shituka

Kijijini wenzako wenye bidii wanamiliki pikipiki, gari, guta, nyumba, duka nk.

Kijijini ni bidii zako tu. Mjini kuna pesa kuliko kijijini ila kama kila ukihangahika huzipati za kukukwamua ni vyema utafute chimbo kijijini.

Braza alifika kijiji fulani kuuliza ardhi ya kulima huko chobingo akapewa upana wa hekari 5 urefu ajipimie mwenyewe.

Kama akilima hekari 40 na kupanda mikorosho baada ya miaka 5 atakuwa wapi?

Nakuuliza wewe unayelipwa laki 2 na Mwindi.
Hili umwa umwa limemtoka mtu.
 
INASIKITISHA SANA

Vijana wanahangaika na kuomba kazi zisizo na uhakika ajira portal hata buku mfukoni ni changamoto wanasubiria ajira ya 750k per month utakuta wengine huu mwaka wa tatu na zaidi yuko home anasubiri kuitwa kwenye interview nafasi 2 wanaofanyiwa interview 200

Wakati kuna kijana mwenzao sasa hivi anauza gunia moja la vitunguu 350,000 pale soko la Ilala hapo alilima heka 1 akatoa magunia 80

Tanzania ina vijana wa hovyo sana. Sekta ya kilimo na biashara ya mazao kuna fursa sana.

Tatizo vijana hawatembei, hawataki kujifunza kuhusu kilimo, wanachojua ni kwenda Kidimbwi na Kitambaa Cheupe

Kukodi shamba la ekari 1 maeneo yenye ardhi nzuri ya kilimo na baadhi unaweza kufanya hata irrigation hapa Tanzania ni 30,000 mpaka 70,000

Huwa nashangaa kijana anatoka mkoa wenye ardhi nzuri ya kilimo anakuja kuwa boda au machinga Dar
Huruma sana.
Boda kila unayemuhoji ni mgeni kutoka mkoa X,z, n.k
Yaani utafute nauli uje dar kuwa bodaboda
Inasikitisha
 
Huruma sana.
Boda kila unayemuhoji ni mgeni kutoka mkoa X,z, n.k
Yaani utafute nauli uje dar kuwa bodaboda
Inasikitisha
Mimi huwa nashindwa kuelewa halafu utakuta anakuja jijini kuishi maisha magumu kula ya taabu halafu kijijini kwao vyakula vya kutosha na biashara za mazao ni uhakika
 
Maisha ni zaidi ya kula
Soma vizuri nimesema walipotoka kuna biashara ya mazao pia.

Huku mjini wanaishia kuishi maisha ya kupanga kachumba kamoja kama stoo au unakuta geto moja wanashare hata watu 3

Mwisho wa siku kajitahidi sana atajenga kachumba kamoja au kachumba na sebule mabondeni au uswahilini kwao kaacha ardhi nzuri na kubwa ya kutosha kujenga na kuwa na compound hata ya kuweka mifugo na bustani

Kuliko kuwa house boy, boda au machinga huku Dar bora uwe mkulima inalipa kwa mbali sana

Pesa wameicha walipotoka.
 
INASIKITISHA SANA

Vijana wanahangaika na kuomba kazi zisizo na uhakika ajira portal hata buku mfukoni ni changamoto wanasubiria ajira ya 750k per month utakuta wengine huu mwaka wa tatu na zaidi yuko home anasubiri kuitwa kwenye interview nafasi 2 wanaofanyiwa interview 200

Wakati kuna kijana mwenzao sasa hivi anauza gunia moja la vitunguu 350,000 pale soko la Ilala hapo alilima heka 1 akatoa magunia 80

Tanzania ina vijana wa hovyo sana. Sekta ya kilimo na biashara ya mazao kuna fursa sana.

Tatizo vijana hawatembei, hawataki kujifunza kuhusu kilimo, wanachojua ni kwenda Kidimbwi na Kitambaa Cheupe

Kukodi shamba la ekari 1 maeneo yenye ardhi nzuri ya kilimo na baadhi unaweza kufanya hata irrigation hapa Tanzania ni 30,000 mpaka 70,000

Huwa nashangaa kijana anatoka mkoa wenye ardhi nzuri ya kilimo anakuja kuwa boda au machinga Dar
Kalime wewe kama rahisi
 
Kuna MTU alisema DSM pachafu, joto Kali nikamuuliza ulifikia wapi?
Akasema Keko Machungwa alikuja kwenye interview na alikaa siku 4 tu. Alipokuja awamu nyingine nilimtembeza mitaa ya mikocheni ya chini kwa nyerere kupitia mbezi beach ya chini hadi kwa Lipumba kutokea line polisi hadi Ununio kwenda kwenye Nyumba za Lugumi hadi kwa Mh. Rais. Tunapoongea sasa amepata kazi mkoa lakini akipita wiki tatu simu anakuja DSM nimpeleke viwanja
 
Mimi niko Dar mwaka wa 8 sasa ni government employee . Sasa unataka niache kazi ya uhakika nikalime?
Nikitaka kulima huwa nalima mazao ya msimu Njombe viazi mviringo.
Nyie watu mlioajiriwa huwa na kiburi na dharau sana.
Kwa mtu ambaye anatafuta maisha ili atoboe sikushauri uende Lindi, Mtwara,Tabora na Shinyanga mjini. Itakula kwako
 
INASIKITISHA SANA

Vijana wanahangaika na kuomba kazi zisizo na uhakika ajira portal hata buku mfukoni ni changamoto wanasubiria ajira ya 750k per month utakuta wengine huu mwaka wa tatu na zaidi yuko home anasubiri kuitwa kwenye interview nafasi 2 wanaofanyiwa interview 200

Wakati kuna kijana mwenzao sasa hivi anauza gunia moja la vitunguu 350,000 pale soko la Ilala hapo alilima heka 1 akatoa magunia 80

Tanzania ina vijana wa hovyo sana. Sekta ya kilimo na biashara ya mazao kuna fursa sana.

Tatizo vijana hawatembei, hawataki kujifunza kuhusu kilimo, wanachojua ni kwenda Kidimbwi na Kitambaa Cheupe

Kukodi shamba la ekari 1 maeneo yenye ardhi nzuri ya kilimo na baadhi unaweza kufanya hata irrigation hapa Tanzania ni 30,000 mpaka 70,000

Huwa nashangaa kijana anatoka mkoa wenye ardhi nzuri ya kilimo anakuja kuwa boda au machinga Dar
Ushauri mzuri sana ila shida wanaotoa ushauri wengi wameajiriwa.
Mtu ameajiriwa, hata kuacha kazi ajiajiri hataki ila yy anataka watu wakajiajiri kwenye kilimo.
Cha ajabu akifukuzwa kazi, anaomba kazi ila fursa km hiz hazitaki
 
Back
Top Bottom