Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Bila salamu nawapa ujumbe wenu enyi watu.

Mnaweza kusema kuwa najiinua au nawakashifu ila Mimi siko huko. Ni upendo tu.

Waarabu wanasema fikisha ujumbe hata kama ni mchungu.

Miaka 5 inatosha kabisa mtu kupima bahati ya maisha Dar es salaam au mahali popote.

Unaishi Dar miaka zaidi ya 5 huna nyumba, huna kiwanja, kula kwako ndo kule unatafuta leo ili ule leo, kila siku kwenye daladala wewe ukichomoa pesa kubwa basi buku 2.

Unalala store (jiko, meza, sofa, feni, kitanda, pasi, bag la nguo na vitu vingine vyote ukifungua macho tu hivi hapa.

Tanzania hii kuna mahali kama Liwale huko Lindi ukifika kijiji chochote ukiomba ardhi ya kujenga au kulima unapewa bure kabisa. Yet wewe uko dar hata hatua 4 za ardhi Chanika huna . Umerogwa shituka

Kijijini wenzako wenye bidii wanamiliki pikipiki, gari, guta, nyumba, duka nk.

Kijijini ni bidii zako tu. Mjini kuna pesa kuliko kijijini ila kama kila ukihangahika huzipati za kukukwamua ni vyema utafute chimbo kijijini.

Braza alifika kijiji fulani kuuliza ardhi ya kulima huko chobingo akapewa upana wa hekari 5 urefu ajipimie mwenyewe.

Kama akilima hekari 40 na kupanda mikorosho baada ya miaka 5 atakuwa wapi?

Nakuuliza wewe unayelipwa laki 2 na Mwindi.
Ukiondoa kabila la Wakinga hapo mzizima..

Wengine Walio baki ni matajiri wa kutokwa na Jasho kila saa mwili.
 
Kwanini wa mikoani ndo wanalazimisha wenzao waondoke Dsm?

Kama umeondoka si ukae kimya?
Kizuri kula na nduguyo, uoni tunavyoshiliwa bango tusipoenda makanisani, mpaka unasema eeh bhamna nenda peke yako mbinguni.
 
Kaka hapa daslamu ukibahatika kufika kariakoo uka keti zako barazani mwa duka la watu let say pembeni mwa duka la simu wapo hawa mama ntilie wadada wazuri utashangaa tu wanakuliza kaka nikuletee supu na chapati ..... huja kaa sawa utashangaa hii hapa ..... wakiamini wew upo hapo dukani ... ukisha Shiba ndo utamua sasa uendelee kukaa hapo au mchana napo utafte chimbo lingine kwajili ya msosi wa mchana maana...... sasa nikulize wew nikija hko lindi fursa kama hizi zipo au ndo mtaji wa masikini ni nguvu zake
Hahahah! Kwahiyo wewe hiyo supu ndio mafanikio yako
 
Bila salamu nawapa ujumbe wenu enyi watu.

Mnaweza kusema kuwa najiinua au nawakashifu ila Mimi siko huko. Ni upendo tu.

Waarabu wanasema fikisha ujumbe hata kama ni mchungu.

Miaka 5 inatosha kabisa mtu kupima bahati ya maisha Dar es salaam au mahali popote.

Unaishi Dar miaka zaidi ya 5 huna nyumba, huna kiwanja, kula kwako ndo kule unatafuta leo ili ule leo, kila siku kwenye daladala wewe ukichomoa pesa kubwa basi buku 2.

Unalala store (jiko, meza, sofa, feni, kitanda, pasi, bag la nguo na vitu vingine vyote ukifungua macho tu hivi hapa.

Tanzania hii kuna mahali kama Liwale huko Lindi ukifika kijiji chochote ukiomba ardhi ya kujenga au kulima unapewa bure kabisa. Yet wewe uko dar hata hatua 4 za ardhi Chanika huna . Umerogwa shituka

Kijijini wenzako wenye bidii wanamiliki pikipiki, gari, guta, nyumba, duka nk.

Kijijini ni bidii zako tu. Mjini kuna pesa kuliko kijijini ila kama kila ukihangahika huzipati za kukukwamua ni vyema utafute chimbo kijijini.

Braza alifika kijiji fulani kuuliza ardhi ya kulima huko chobingo akapewa upana wa hekari 5 urefu ajipimie mwenyewe.

Kama akilima hekari 40 na kupanda mikorosho baada ya miaka 5 atakuwa wapi?

Nakuuliza wewe unayelipwa laki 2 na Mwindi.
Chunguza watu wengi walioko dar walipelekwa na ndugu zao kutumikishwa wengine waliwaona wenzao wanao ishi dar walipo ludi kijijini kusalimia wakadhani walisha tajirika

Ukweli uko hivi wengi walioko dar wametoka makwao hali yakuwa hawajawahi kufika mikoa mingine tofaoti na wapo zaliwa ndio

Kwamtu alie hamia dar kibiashara ambapo yumbatu mala moja urudi nyuma na kwenda kuanza maisha mikoa mingine
 
Back
Top Bottom