Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Inalogwa ila system ya kibenki iliasisiwa na Illuminati wa kiyahudi na ndio wanamiliki pamoja na zile familia nyingine za uingereza asilimia zaidi ya 90 ya uchumi wa Dunia nzima.

Hiyo familia iliyoanzisha Banking system inaitwa Rothschild. Tukirud kwenye suala lako la Bank hailogwi ni sawa na mchezaji wa timu ya Mkoa wowote Tanzania. Ambayo haijafuzu hata ligi kuu Ya Bara kutaka kucheza na Real madrid, ama Arsenal.

Dunia ina siri nzito sana sana sana.
Hao wayahudi walishaingia contracts na lucifer mwenyewe. Sasa ufanye uchawi WA kumuibia aliyeleta uchawi[emoji23][emoji23]
 
Nakumbuka miaka ya nyuma kidogo wakati nasoma A level kuna mkasa ulinipata, kwanza kuna manzi nilikutana nae katika mazingira ya usafiri kipindi hicho naenda school A level akawa rafiki yangu sana ukafikia kipindi akawa ananiambia mazingira ya kwao namna yalivyo, baba yake alikuwa mwananjeshi na mama yake alikuwa mwalimu bahati mbaya wote walifariki katika vipindi tofauti sasa familia yao ikawa inapitia changamoto kidogo ya kiuchumi... Njia pekee wakaona wamuozeshe binti huyu ambaye alikuwa rafiki yangu kwa tajiri mmoja wa madini kule mikoa ya kusini alikuwa anafanya biashara ya madini Msumbiji na kule Kusini mwa Tz baaadae akanishirikishabas friends kwamba hayuko tayari kuolewa na mtu asiempenda wala kuolewa as mke wa pili na mtu mzima hivyo nimsaidie.. mimi nikiwa form 5 mwishoni nikatafuta namna ya kumpeleka kwetu ili akasikilizie wakati anatafuta hatma ya maisha yake, KOSA KUBWA. nikamfanyia shopping nikampanga maza nikampa nauli(pocket money yangu) akasepa. Ikawa kama nimemtorosha aisee toka siku hiyo nikaanza kuumwa Class nashindwa kusoma n.k nikiwa nje au room niko fresh nikienda tu assembly au sehemu yenye mkusanyiki wa watu nadodondoka sasa hali hiyo ikaendelea siku moja niko uwanjani nikadondoka nikapelekwa hospital wakanicheck kila kitu negative, wakanitundika drip ya gluccose sijui nikarudi shule niko poa. siku hiyo nimetoka hospital nikarudishwa shule hapo mwezi wa 2 huo necta mwezi wa 5 kwa hiyo nikawa mtu wa shule hospital hivyo hivyo.. nakumbuka siku hiyo pepa ya pre necta ya kwanza kabisa tulikuwa tunachokua Geogy tulifanga paper DH kwa hiyo tulikuwa wengi CBG, HGL, HGK n.k.. mzee akasema nirudishwe Dar nifanyinwe uchunguzi hospital... Tukaenda Mnazi mmoja Hospital, Muhimbili, Aghakan na jibu likapatikana pale Ccbrt mwisho wa siku wakasema naumwa macho nikapewa na miwani nikasepa shule, nimetoka Home dsm fresh tu ile nafika stand ya mkoani kushuka tu hapo hapo ngoma ikaaanza nikadondoka hospital.. mwisho wa siku hospital wakasema huyu sio wa hapa fanyeni namna, mzee Rc na maza mshahidi wa yehova wakawa hawahamini hayo mambo wakasema nitapoa tu kwa muujiza, nikarudishwa shule, nakumbuka jumapili yake tulikuwa na mahafali ya dini siku hiyo nimeamka fresh nimeoga vaa suti yangu nyeusi nawahi church, nimetoka na wana tumechelewa sana sasa nimefika church wana fasta wakazama kanisani, mimi nilikuwa tycs sasa siku hiyo kwaya ya shule ndio ilikuwa inahudumu ikabidi nikakae pale nyuma yao maana sikufanya mazoezi, ile nakaa tu naona nguvu zinaisha yaani kama mtu ananisukuma nikaanguka .. kuja kushtuka niko hospital aisee nilimwaga machozi hapa maana nikaona sio bure, sasa kuna maza mmoja alikuwa mpishi pale school wa waalimu, yeye pamoja na Headmaster wakaona wanipeleke kwa mtaaamu.. alikuwa ni mbibi wa kiisilamu, nilikaa siku 4 pale siku ya kwaanza nilipigwa dua pale balaa, kesho yake mkuu akaleta mayai, maji fulani hivi sijui yanaitwaje, mkaa, na chumvi akatengeneza dawa, nikapakwa na kunyweshwa atimaye nikawa niko poa.. wakanipa jaribio next ilikuwa ni mahafali ya shule nikafanya fresh tu nikawa poa, assemly nikienda niko poa na paper nikapiga..

Sasa bwana kumbe yale maujinga yote familia ya yule binti ndio walinifanyia kisa nimemtorosha binti yao( mdogo wao) wamekosa hela ndio maana nao wakaona wanikomeshe, baadae yakaisha na paper ya necta nikapiga ilibaki kidogo nifeli ila mambo yakaenda poa Ustadhati alinisave...

Story ndefu duh
 
Tanzania waganga wakweli wapo wachache na wanafahamiana wengine ni porojo wachawi

fikiria mtu unapigwa dawa, mwamba anapandisha majini anakwambia yule mwamba dawa zake hazionekani ila ni jiwe.

shuhuda za uganga tena wa kweli zipo nyingi sana sema watu hawasemi kwa ajili ya ujuaji wa watu humu.

binafsi nimewahi shuhudia familia iliambiwa mmerejeshewa kipato chenu mzee wa familia hana hili wala lile kapigiwa simu kuulizwa kama ameshalipwa mafao yake ya miaka 5 alipo itumikia serikali kuu (alifanya kazi serikali kuu akaenda kusoma akaja ajiliwa upya afisa wilaya flani)

***** akalamba mafao haamini mpaka kesho, nsha shuhudia mtu anadaiwa akapewa dawa hadi leo mwaka wa 6 deni lisha isha.
 
Kuomba nini sasa? Siendelezi sababu sio jambo la kufurahisha wala kujivunia, hapo kuna sehemu unaona kabisa sikufanya uungwana. Kwa mara yangu ya kwanza naiba, unadhani nilipenda kumuibia mganga Mkuu? Au ni sehemu ya maisha yangu? Hapana nilifanya upuuzi ule ambao umekuja nikost kwa Miaka, nimesema siendelei sababu najutia nilichokifanya na kinaniumiza mpaka leo hii. Sasa ni hivi kama unahisi ilikuwa ni rahisi kiivyo, baada ya boti kuzama kila tulichokuwa nacho kilibaki ndani ya maji. Na hata kuokoka humo ilikuwa ni miujiza tu. Unajua tulikuwa tukienda wapi? Ni safari iliyochukua zaidi ya miaka 3 kufika tulikotaka kufika. Sipendi kuendelea sababu kuna Mengi, ya kufurahisha, kusikitisha, kuchukiza na kuogopesha pia. Destination ilikuwa Canada imagine.
Hiki n kisa kabisa mkuu si ungetoa story kama mpuuzi UMUGHAKA
 
Nilikuwa nasafirisha mkaa mpaka dar bila vibali!

Nikikaa mbele ya gari trafiki na watu wa maliasili hawaioni gari mpaka Dar.

Kwa nin niliacha....with time mganga aliniambia kwa sasa nadaiwa sadaka ya damu ya mbuzi watatu, nikatoa
Baadae akaniambia nipate mimba niitoe nimpelekee.

NIKACHAPA LAPA ILA NILIZULUMIWA HELA, VIWANJA, GARI nikabaki kama mwanafunzi wa secondary

Namshukuru MUNGU nimeanza upya bila ndumba
Nyongeza: Kwa huyo mganga nilikutana na vigogo kadhaa wa mashirika na idara za serikali na NGO ...wakuu wa vyombo vya usalama.

UNAJUA KWA NIN WATU WANANUNUA VX?

UKIONA mtu ana Vx posta anatoka kazini saa 9:30 anakimbia kwa mganga , anajigangua asubuhi saa tisa ,kumi anaanza Safari kurudi kazini.

Nilishangaa kuona VX kibao zikiingia usiku nikawauliza hawa wote ni watoto wa hiki kijiji, mmebarikiwa...jibu hawa ni mabosi na vigogo wa posta.
Uyo kweli ni konki Kwa nnavoijua biashara ya mkaa ilivyo, pamoja na uwingi wa mageti ya ukaguzi njiani[emoji848][emoji848]
 
Niliacha kazi nikawa home tu sina mbele wala nyuma, maisha yameninyoosha kisawasawa. Nikawa mshkaji wa kijiweni tu nimenyonda atari, washkaji wananinyanyapaa usiombe.
Kuna jirani chinga kila akipita ananiona nimejiinamia mande to sande. Ikabidi aje tupige story. We si umesoma sana? Nikamwambia kawaida tu. Basi akawa rafiki yangu alinikubali tu na hali yangu. Ananipeleka sehemu tunamwagilia moyo kiroho safi kifupi akawa best.
Ndio siku akafunguka akanipa kontack na bibi Liwale. Nenda kaweke mambo sawa. Kwakua alishakua mshkaji sikutaka kumdissappoint na nauli alinipa. Nikapanga safari huyoo kwa bibi liwalee.
Bibi kafanya yake hakudai hata sumni ila kanichimba beat tu nikifanikiwa nisiporudi imekula kwangu.
Ndani ya wiki tu napigiwa simu niende sehemu nikafanyiwe intavyuu sikumbuki niliomba lini. Kufika intavyua anajigamba kabisaa kua ananijua ila sometimes anajistukia anasema umeletwa na Boss? Kumbe hata boss mwenyewe simjui.
Nikala shavu kimasikhara nikampigia bibi sikusubiri hata kumaliza mwezi nipate salary, nilikopa nikaenda kwa bibi nikampa asante yake nikarudi zangu.
Salary ilivyoingia nikamtafuta rafiki yangu chinga tulikunywa sanaaa siku ile nikajua itakua ni siku ile tu. Kumbe chinga naye kwa furaha akipata mkwanja lazima anicheki tukagambeke.
Maisha yakawa gambe ile deile, mpaka nilivyohama kazi nyingine mbali na rafiki yangu chinga.
 
Baada ya kuona biashara yangu imekwama nikaongea na wenyeji wa mji, nikapelekwa kwa mganga mwanamke,

Kwanza mganga huyo akikaa anaogea kama anapokea simu au anapokea maelekezo kutoka sehemu,

Nilikutana na watu wa hadhi tofauti wanamiliki mabasi mapya na magari mengine mapya wamepeleka yakafanyiwe uchawi,

Zoezi la kwanza baada ya kujieleza akanituma nikachote maji kwenye kisima chake, hiki kisima ni maalum kwa kazi hiyo ya kiganga, kipo umbali kama wa kilometer moja kutoka mji ulipo,

Hivyo nilipewa mashariti nisigeuke hadi nikifika nyumbani kwa mganga kupeleka maji na endapo nikigeuka napaswa kurudia zoezi upya.... ila nikajikuta nimegeuka nikiwa nakaribia kufika... niling'atwa na nyuki kwelikweli,

Nikaona uvivu kurudi tena kisimani nikaamua kwenda kwa mganga na maji yale yale .. nilipofika tu akaniamba usikae wewe umegeuka (umekosea mashariti) rudia zoezi, ikanibidi nirudie[emoji23]

Tulishindwana alipoanza kuniuliza
Kabila langu, Wazazi wangu kama wapo hai, idadi ya watoto na mke, pia nichague nani nataka afahamu ninachokifanya endapo nakufa ataendeleza mali.

Nikamwambia nimegailisha zoezi kwa leo ngoja nikajitafakari upya, akanigundua namkimbia akanipa adhabu kabla sijaondoka nikanunue jogoo mkubwa zaidi ya wote nitakaemkuta kwenye cage ya wauzaji sokoni nimpelekee,

Kufika sokoni nikakuta bei mbaya nika bargain nikachukua mdogo kati ya yule mkubwa zaidi, ile kurudi kwa mganga akasema sio huyo, kamlete yule mweupe uliyemuacha[emoji23] tulisumbuana zoezi hilo mara 3 ikabidi nikubali kumnunua na kumpelekea.

Nikatoka nduki hata nyuma sikutazama tena.
Wewe habari za waganga acha

Utakuja kufanywa msukule
 
Niliacha kazi nikawa home tu sina mbele wala nyuma, maisha yameninyoosha kisawasawa. Nikawa mshkaji wa kijiweni tu nimenyonda atari, washkaji wananinyanyapaa usiombe.
Kuna jirani chinga kila akipita ananiona nimejiinamia mande to sande. Ikabidi aje tupige story. We si umesoma sana? Nikamwambia kawaida tu. Basi akawa rafiki yangu alinikubali tu na hali yangu. Ananipeleka sehemu tunamwagilia moyo kiroho safi kifupi akawa best.
Ndio siku akafunguka akanipa kontack na bibi Liwale. Nenda kaweke mambo sawa. Kwakua alishakua mshkaji sikutaka kumdissappoint na nauli alinipa. Nikapanga safari huyoo kwa bibi liwalee.
Bibi kafanya yake hakudai hata sumni ila kanichimba beat tu nikifanikiwa nisiporudi imekula kwangu.
Ndani ya wiki tu napigiwa simu niende sehemu nikafanyiwe intavyuu sikumbuki niliomba lini. Kufika intavyua anajigamba kabisaa kua ananijua ila sometimes anajistukia anasema umeletwa na Boss? Kumbe hata boss mwenyewe simjui.
Nikala shavu kimasikhara nikampigia bibi sikusubiri hata kumaliza mwezi nipate salary, nilikopa nikaenda kwa bibi nikampa asante yake nikarudi zangu.
Salary ilivyoingia nikamtafuta rafiki yangu chinga tulikunywa sanaaa siku ile nikajua itakua ni siku ile tu. Kumbe chinga naye kwa furaha akipata mkwanja lazima anicheki tukagambeke.
Maisha yakawa gambe ile deile, mpaka nilivyohama kazi nyingine mbali na rafiki yangu chinga.

angalia inbox yako
 
Niliacha kazi nikawa home tu sina mbele wala nyuma, maisha yameninyoosha kisawasawa. Nikawa mshkaji wa kijiweni tu nimenyonda atari, washkaji wananinyanyapaa usiombe.
Kuna jirani chinga kila akipita ananiona nimejiinamia mande to sande. Ikabidi aje tupige story. We si umesoma sana? Nikamwambia kawaida tu. Basi akawa rafiki yangu alinikubali tu na hali yangu. Ananipeleka sehemu tunamwagilia moyo kiroho safi kifupi akawa best.
Ndio siku akafunguka akanipa kontack na bibi Liwale. Nenda kaweke mambo sawa. Kwakua alishakua mshkaji sikutaka kumdissappoint na nauli alinipa. Nikapanga safari huyoo kwa bibi liwalee.
Bibi kafanya yake hakudai hata sumni ila kanichimba beat tu nikifanikiwa nisiporudi imekula kwangu.
Ndani ya wiki tu napigiwa simu niende sehemu nikafanyiwe intavyuu sikumbuki niliomba lini. Kufika intavyua anajigamba kabisaa kua ananijua ila sometimes anajistukia anasema umeletwa na Boss? Kumbe hata boss mwenyewe simjui.
Nikala shavu kimasikhara nikampigia bibi sikusubiri hata kumaliza mwezi nipate salary, nilikopa nikaenda kwa bibi nikampa asante yake nikarudi zangu.
Salary ilivyoingia nikamtafuta rafiki yangu chinga tulikunywa sanaaa siku ile nikajua itakua ni siku ile tu. Kumbe chinga naye kwa furaha akipata mkwanja lazima anicheki tukagambeke.
Maisha yakawa gambe ile deile, mpaka nilivyohama kazi nyingine mbali na rafiki yangu chinga.
Liwale bwana waganga wakikupenda wanakusaidia ila kama wakikupenda majini Yao wanakusahaulisha kabisaa usiende kusema ahsantee Ili wakutoe kafara ya damu
 
Back
Top Bottom