Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Sasa hizi ndumba kwa nini tusiwaloge wazungu jamani na sie tutawale dunia au wao mganga wao hatari kuliko wetu

Kuna documentary nilikuwa nasikiliza wanasema kuna aina tofauti za uchawi,hata wazungu wanao uchawi ila wengi hutumia for positive outcome,wanasema aina ya uchawi uliopo africa ni wa kuumizana hauna faida na ndio uchawi mbaya sana hata wao hawapendi matumizi ya uchawi huu
So kwa huku africa usitarajie hayo unayo yawaza,wamejifunza uchawi mbaya na ndio wanao ujua huo tu,na huwezi kumroga mzungu maana nae anaujua vizuri tu,anakukalisha chini mapema sana
 
Sisi kwetu Ludewa wapo tena in limited number,sasa mpaka uwapate ni shughuri,kwanza unaelekezwa na mizimu kupitia mtu either live au kwa ndoto na ukifuata kweli unafika ,balaa Lake ni hatari, kwetu ukipigwa tego utajuta,ukoo wetu sisi hauguswi kizembe ukigusa wakagundua wazee umekwisha
 
Dada nimejaribu kukutumia Pm lkn naona haikubali ila kiufupi nina mwanangu ana kama mwezi kapatwa na shida ya akili kachanganyikiwa ana kama wiki tatu tumempeleka hosp mpaka tumetok hali iko vile vile hatulii kabisa

Saizi kila mara anaomba arudi alikokua kila tukimuuliza alikokuwa ni wapi atuambie hawezi anang'anga'ana amechomwa dawa za hosp za kumtuliza na hata vidonge vya kunywa lkn wapi

Naomba msaada kwa huyo babu yako kama itawezekana
 
Pole sana
 
Kuna dawa alinipa ya ku-deneutralize misala job, kila nikiharibu au ikiitishwa vikao naichoma asubuhi nikienda msala unawaangukia wengine tu wanachambwa vilivyo mm kimyaaa hakuna kima yeyote wa kutaja jina langu au wa kuniassociate na chochote hata kama nilishiriki, nikitoka hapo break ya kwanza bar napiga lite tano fasta huku nikitafakari maajabu ya miti aliyoiumba mnyazi Mungu.
 
Aise!!!Dunia ina mapito mengi sana
 
Mganga ndio alikujibu hivyo?
 
Hao ndio marafiki wa faida
 
Bilaa shaka ulipiga mbupu[emoji16]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…