Umeumiza watu halafu unataka kuokoka bila kuwaomba msamaha uliowaumiza, hilo haliwezekani!

Mungu angekua katili kama unavyomuelezea hapo, dunia ingekuwa chungu sana kwa wakosefu. Ndo maana tunaambiwa M/Mungu ni mwingi wa Neema na Rehema. Pia M/Mungu ni baba wa wote.
anatudekeza lakini watu tumekuwa wagumum kiama chaja na hukumu itasindikizwa na maumivu makali sana na vilio watu wakisaga meno
 
Ni mwepesi wa ksamehe ukianza kuomba msamaha kwanza kwa uliowakosea kisha mkiweka mambo yenu sawa ndio uende kwake, huwezi mdhurumu mtu alafu uende kwa Mungu mwenye haki akusamehe , NEVER !!!! Huyo uliemdhulumu nae anamuomba Mungu
Kama uliyemkosea kafariki kabla hujamuomba msamaha inakuwaje?
 
Kama uliyemkosea kafariki kabla hujamuomba msamaha inakuwaje?
Jitahidi utafute mabaki yake (watoto wake) uwaeleze kila kilichotokea bila kuruka chochote kisha uwaombe msamaha, ukisaamehewa ndio uombe sasa msamaha kwa Mungu,

Ukikataliwa ama kama hujui alipo wala hujui mabaki yake yalipo hesabia ni deni linalosubiri hukumu
 
Andiko gani limesema haya?
 
Umewahi mpa Mungu sadaka au unawapa wachungaji wako?
Lengo la kutoa sadaka ni iende kwa lengo lililodhamiriwa, kama mchungaji kapiga sadaka hio ni dhambi yake ila kwenye kitabu cha Mungu muumini anaonekana katoa sadaka kwake, mzigo ataubeba huyo mchungaji aliefanya mambo yake gizani
 
Lengo la kutoa sadaka ni iende kwa lengo lililodhamiriwa, kama mchungaji kapiga sadaka hio ni dhambi yake ila kwenye kitabu cha Mungu muumini anaonekana katoa sadaka kwake, mzigo ataubeba huyo mchungaji aliefanya mambo yake gizani
Nimekuuliza ulishawahi mpa Mungu sadaka?
Mungu aliitumia kufangia nini hiyo sadaka?
 
Common sense, sasa hizo dhambi umuombe nani msamaha ??
Mbona unajichanganya. Wewe umeleta injili, tulia ujibu maswali.
Andiko gani linasema Mungu anasamehe dhambi yako binafsi, isiyodhuru wengine???
 
Wanaopotoshaaaa ni hawa manabiiii machoko wa sasa eti nifatishe sala ya toba utasamehewa dhambi nyokoooo kabisa Mungu anafanyiwa pranks
 
Unampangia Mungu namna ya kutenda? Mwanamke Kahaba aliyevunja ndoa za watu wengi na kuwaumiza wengi, alipomuona Yesu alienda kumbusu miguu na kumpaka mafuta, Palepale Akasamehewa dhambi zake zote!
 
Mbona unajichanganya. Wewe umeleta injili, tulia ujibu maswali.
Andiko gani linasema Mungu anasamehe dhambi yako binafsi, isiyodhuru wengine???
Ok ni vema basi tushauriane maana na mimi sijui kila kitu, kwa mtazamo wako unaonaje ?
 
Reactions: 511
Ok ni vema basi tushauriane maana na mimi sijui kila kitu, kwa mtazamo wako unaonaje ?
Dhambi pekee isiyosamehewa ni kumkufuru Roho Mtakatifu. Zingine zote ukitubu na kuacha zinasameheka.

“Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa.

— Mathayo 12:31 (Biblia Takatifu)
 
Nimekuuliza ulishawahi mpa Mungu sadaka?
Mungu aliitumia kufangia nini hiyo sadaka?
Nikitoa sadaka inayoenda kuongeza ukubwa wa jengo la kanisa ni kwamba kuna watu wengi zaidi tutaweza kusali kanisani

Nikitoa sadaka ya kwenda kusaidia wenye shida ni kwamba inaenda kupunguza shida zao, n.k.

Ni mambo yampendezayo Mungu

Tatizo linapokuja ni baadhi ya wachungaji kugeuza sadaka za kufanya yampendezayo Mungu kuigeuza kufanya anasa na kujilimbikizia mali,
 
Sawa .mkuu
 
Nikitoa sadaka inayoenda kuongeza ukubwa wa jengo la kanisa ni kwamba kuna watu wengi zaidi tutaweza kusali kanisani

Nikitoa sadaka ya kwenda kusaidia wenye shida ni kwamba inaenda kupunguza shida zao, n.k.

Ni mambo yampendezayo Mungu
Yanayompendeza Mungu lakini Sadaka yako humpi Mungu.
Maana Mungu hahitaji fedha zako ili kuitwa Mungu. Nchi na vyote viijazavyo ni mali hake, hana uhitaji. Sadaka zinatolewa kwa mchungaji wako, na ndie mtumiaji, Mungu hachukui hizo sadaka.
 
Unampangia Mungu namna ya kutenda? Mwanamke Kahaba aliyevunja ndoa za watu wengi na kuwaumiza wengi, alipomuona Yesu alienda kumbusu miguu na kumpaka mafuta, Palepale Akasamehewa dhambi zake zote!
Hakukuwa na taarifa kwamba alikuwa anaiba waume za watu ila nitalifanyia uchunguzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…