Umewahi kuchapwa/kupigwa na mzazi/mlezi?

Umewahi kuchapwa/kupigwa na mzazi/mlezi?

[emoji23][emoji23][emoji23] mama alikua anapenda kunifinya mapajani aisee!!! Anakukamata mnakaa wote chini na kukutandaza miguu kufinya mapaja [emoji23][emoji23][emoji23]
Wamama wengi wanautaalamu huo tena unaweza shtuka tu mtoto analia kumbe kaishafinywa kimyakimya
 
Mimi nilikuwa Mtundu sana. Hii ilisababisha mpaka nikapelekwa shule ya boarding nikiwa na miaka minne pekee.

Siku moja ambayo mama na baba walinichangia ni siku ambapo nilienda kumtega mzee kipofu na kumwangusha. Nilitengeneza kamba alafu nikaitegesha njiani, mzee kipofu alipokuja anatembea na mkongojo wake nikainyanyua na kumuangusha. Nikabaki hapo pembeni nacheka kwa nguvu.

Asee, hiyo kipigo nilichopata sitakaa nisahau asee. Nilichapwa fimbo za kutosha maana nilishakuwa sugu kwenye mkanda.

Mungu anisamehe kwa niliyomtendea yule Mzee. Naamini hata huyo mzee kanisamehe pia, nilikwenda jumuomba msamaha kabla hajafariki, RIP.
Duh!!!
 
Nilikula bakora za hatari na adhabu ya kubeba mawe mikono juu kwa kosa la uzurulaji baada ya kutoroka wakati tuliingia makubaliano nibaki home maana wote waliondoka. Niliamua kutoroka ili nikaangalie Sinema ambayo nilikuwa tayari kwa lolote ila lazima niiangalie. Nilimchukia mother ila nilimuelewa baada ya kufaulu peke yangu Drs la Saba katikati ya watoto watukutu mtaani kwetu. Mkono wa chuma wa mama ni zawadi tosha maishani mwangu.
 
Nilikuwa mtundu sana nilipokuwa primary, kuna siku mzee alirudi na radio mpya, nikaifungua yote, nikashindwa kuifunga, na hii ilikuwa radio ya tatu kuiharibu. Sasa mzee aliporudi toka job alipa bakora nne za maana, na adhabu ikaendelea kwa wiki nzima kila akitoka job ni salam na fimbo moja then tunaendelea na mambo mengine.
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hivyo vifinyo marehemu Bibi yangu alikua mtaalam Sana. Anakufinya tumbo then anazungusha kama anawasha gari halafu anainua juu,
Hapo nimetoka kumchapa ka Mia moja kake nimeenda kuwa mfalme shule,kurudi ndio nakutana na hiko kibano.
Tumbo liliniuma mwezi mzima na sikurudia tena kumchapa visenti vyake[emoji23][emoji23] Mungu amhifadhi vyema Bibi wa-Abraham
 
Mimi mama alikua ananitikisa tikisa tu na kuniambia sasa Wenawe nichape wapi make sioni hata pa kupiga mwishowe nikuue tu ananiambia hebu toka hapa
 
Nikilia si utanibembeleza super Dear wako jamani?? Hautanionea hata ka Huruma jamani jamani??
Na ulivyo na kasuti kazuri... Unalia kama utani vile... Ati unalia huku unazidi kunikumbatia tight.. Nikikuachia unanivuta nisikuachie...

Sasa hapo nitakuoneaje huruma supee dear...
 
Na ulivyo na kasuti kazuri... Unalia kama utani vile... Ati unalia huku unazidi kunikumbatia tight.. Nikikuachia unanivuta nisikuachie...

Sasa hapo nitakuoneaje huruma supee dear...
Lol my lovely super Dear .
A man of action achapa mahondaw kisawasawa
 
Mmh... mi nimechapwa hadi niliwachukia. Tena saingine kosa la mmoja tunapigwa wote watatu. Mdogoetu alikua mdogo.
Nilichokuja kugundua baadae ni kua wazazi walikua na stress mno.
Watu na ndugu walitamani maisha yetu ila hawakujua tu yanayoendelea. Migogoro yao ya ndoa ilitutesa sana sana.. SANA!
Mkisikia ukatili kwa watoto ndio ule. Kila siku Nilitamani kuihama ile nyumba. Nilivyomaliza six tu nikabahatisha kibarua cha hela nzuri halafu mkoa wa mbali. Nilishukuru

Mdogoangu anaenifatia ni wa kiume. Yeye alifaulu mkoani kuanza kidato cha kwanza ikawa sababu. Hakurudi tena hata likizo.

Nimepigwa hadi form 6 nachapwa vikosa vyenyewe sasa. Saingine kutoa Radio Tumaini kuweka radio One.
 
Back
Top Bottom