Mkuu she died from cancer, ila alilala chini miezi miwili lakini mwaka mzima aliugua sana.
Yani nyumba ilikuwa ni full of stress, yani tangu wadogo maisha yaliandamwa na vipigo vikali vikali, imagine nikiwa drs la pili tayari nilikuwa namuogopa mama, mbaya zaidi Tabia ya kunyimwa chakula ikapelekea udokozi Wa hela sasa ohoooo! Fimbo jamani tena ukiwa uchi. Wakati mwingine upupu anauweka kwenye Gunia alafu unavua nguo unaambiwa uingie humo, alikuwa ana pesa ila haya hazionekani( nahis hata mungu alichukia) hakuwahi kukaa na sisi km binti zake au rafiki zake,... Tukiwa tunatoka shuleni jioni nilimuangalia my lovely twin nikawa naona jinsi sura yake inavyojaa hofu wakt wenzetu wanashangilia kwa kelele "kwaheri mwalimuuuuu"... Simanzi asubuhi hakuna chai, shuleni mchana hakuna msosi, na ukikaa vibaya Nyumbani pia mnaweza kuacha kupika..
Alikuwa MTU Wa kutafuta kasoro muda wote MTU Wa kubeza, majirani walipenda kutupa msaada Wa chakula ila waliogopa ukali wake. Heeeeee!!!!!! Nilikuwa nikijiona Mie siyo MTU kabisa, nikawa naogopa hadi watoto wadogo.. Kuna Sikh moja alitufungia nje hadi asubuhi tukajibanabana kwenye magofu na baridi na mbu[emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji24]
Alianza kupunguza ukali na kupiga tulipoenda kidato cha 5 Mie nilienda musoma nikakaa hukohiko hadi nikamaliza, twin akichaguliwa arusha... From there tulijitambua kuwa na die ni mabinti wazuri, tukaanza kuheshimiana na kupendana zaidi,
Tulifaulu chuo kikuu, mwaka Wa kwanza mama aligundulika kuwa ana maradhi ya cancer, nilimuuguza kwa UPENDO MKUBWA SANA, KWA GHARAMA KUBWA KWA KUJITOA BILA KINYONGO!! 2014, Aliaga dunia. Mungu amrehemu na ampumzishe kwa amani.