Umewahi tembea umbali gani mrefu kwa miguu ndani ya jiji la Dar es Salaam?

Umewahi tembea umbali gani mrefu kwa miguu ndani ya jiji la Dar es Salaam?

Hahahah ila life bhana
Niliwahi kupigwa changa na wajanja wakaniacha kwenye waiting lounge ya pantoni pale kigamboni
Sina chochote mfukoni
Nikachapa moyo konde kigamboni hadi hadi vijibweni(nikaomba msaada wa viboti) wakanisaidia kwa masimango sana nikaibukia kurasini..nikachapa mwendo reli kwa reli kurasini,kwa aziz,mtongani nikaungia kilwa road hadi kizuiani pale nikakutana na uncle mudy akanisaidia nauli aisee

Ila nimechapa sana mwendo azania mbagala miaka hiyo
 
Tabata sanene, vingunguti ,via Nyerere road mpaka karume, posta ubungo, mpaka tabata reli via Morogoro road
 
"Nakumbuka 2006 kuna rafiki yangu alikuja Dar, ajira ilikuwa tatizo akakuta tangazo mitaa ya Chang'ombe la vijana.Kufika ofisini wakampatia vitu mbalimbali vya kuuza.
Ndani ya mwezi mmoja jozi tatu za viatu vilikuwa hoi bin taabani.
Umbali alio tembea anajua mwenyewe."
 
Tabata to Manzese, hizi ruti nimefanya sasa nilipokuwa nasoma shule ya msingi zile siku za weekend nikipewa nauli sipandi daladala. Ila kubwa kuliko nilitoka Kiwanda cha Cement cha Wazo kule Tegeta hadi Mwenge nikiwa na miaka 12 tu. Ilikuwaje... Nilikuwa naishi Tabata nasoma Manzese na enzi hizo daladala zinatoka Buguruni zinapitia Tabata zinaishia Ubungo halafu napanda la Ubungo kwenda Kariakoo nashukia Manzese. Hivyo natakiwa kupanda Mabasi mawili, ile usumbufu wa makonda kuwakataa wanafunzi na kubadilisha magari muda unakwenda ikawa nikipata gari la lift napanda kuepuka huo usumbufu. Nikajenga mazoea, siku hiyo likaja basi la kiwanda cha Cement cha wazo nikapanda, kumbe lile gari likichukua wafanyakazi halisimani ni moja kwa moja hadi kiwandani. Nashangaa kufika Ubungo basi limeshika njia ya kwenda Mwenge na kwa utoto wangu sikuwa na ujasiri wa kuuliza gari inakwenda wapi au lisimame wanishushe. Aisee moja kwa moja hadi Kiwandani. Nashangaa watu wanashuka na kutawanyika na mimi sikuwa na jinsi nikashuka. Bahati nzuri basi ilisimama nje ya geti la kuingia kiwandani. Nikafuata barabara ya basi ilipotoka hadi Tegeta, nilikuwa sipajui kabisa Tegeta na nikawa na hofu nisipange gari nyingine nisije kupotea tena. Nikatembea kwa Miguu hadi Mwenge nikasikia wanatangaza magari ya Kariakoo nikapanda hadi Kariakoo kisha nikapanda basi la kwenda ubungo nikarudi nyumbani Tabata. Siku nzima nilimaliza na ilikuwa ni kipindi cha mitihani ya kufunga muhula. Sikusema nyumbani niliogopa ila shuleni nilidanganya nimefiwa wakanipa mitihani ya siku nisiokuja nikafanya peke yangu. SITOSAHAU!!!
Mimi ni mkaziwa Tegeta ungenitafuta ningekusaidia nauli, ******"""


Wakati ninaishi Temeke, safari za miguu Tmk mpaka mbagala nimetembea sana
 
1)Posta to kawe via tanzanite bridge
2)mbezi jogoo to masaki izo one two zilikuwa nyoko sana
 
Ni miaka kama 15 imepita nilikuwa naendesha baiskeli karibu na Kanisa la St Joseph jioni ya 12:30 ghafla trafic akanisimamisha na kuniambia kwanini sitii msafara wa viongozi nikamwambia samahani sikujua kama kuna msafara,akaishika baiskeli na kutoa upepo tairi zote mbili niliikokota hadi mtoni kijichi,nilimuona ni mtu mwenye roho mbaya na sitamsahau.
 
Mara yangu ya kwanza kabisa nilitembea kwa mguu kutoka Azania Sec hadi Kurasis Chuo Cha uhasibu. Mara ya pili nikatembea kutoka Manzese hadi Kariakoo, na mara bya tatu ni kutoka Manzese kwenda chuo kikuu. Hata hivyo niltembea mara nyingi sana kutoka Sinza kwenda Chuomkikuu kila siku
 
Back
Top Bottom