Umoja Party ni chama chenye mlengo upi, kinaamini katika maendeleo au katika Magufuli?

Umoja Party ni chama chenye mlengo upi, kinaamini katika maendeleo au katika Magufuli?

ngebe

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2020
Posts
1,789
Reaction score
5,117
FB_IMG_16503578496380199.jpg
FB_IMG_16503578553516092.jpg
FB_IMG_16503578597021391.jpg


Naona Nembo mojawapo ya Chama ni picha ya JPM 😀😀😀😀
 
Kama ukiwa asset watu watakutumia tu kufikia ndoto zao na watajaribu kuishi kama wewe, unafikiri ni kwa nini PLO Lumumba alihubiri Magulification of Africa, je alikuwa anamaanisha nini?

Hiki chama kinaweza kuwa chama kizuri kama kitakuwa kinaeneza sera na sio chuki, watu wamemis sana kusikia hoja zenye nguvu.
 
Kama ukiwa asset watu watakutumia tu kufikia ndoto zao na watajaribu kuishi kama wewe, unafikiri ni kwa nini PLO Lumumba alihubiri Magulification of Africa, je alikuwa anamaanisha nini?

Hiki chama kinaweza kuwa chama kizuri kama kitakuwa kinaeneza sera na sio chuki, watu wamemis sana kusikia hoja zenye nguvu.

Unafikiri watafika mbali?
 
NAOMBA KADI KABISA,TUMECHOKA NA HAWA WASHENZI,CCM NA UPINZANI WAMEUNGANA KUIPORA NCHI,

Probably itakuwa kitu vizuri CCM, ACT, Chadema wakaungana pamoja wanakubaliana na kuunganishwa na mambo mengi kikubwa kinachowaunganisha, sera yao kubwa ni Anti- Magufuli, chuki kwa kanda flani, kuangalia nyuma awamu ya tano na kutukana na kubeza kila kitu kilichofanywa wakati huo mazuri na mabaya.

Watanzania wote waliobaki ni vizuri wakaungana pamoja waanzishe chama kipya kitakachosimamia maslahi mapana ya Watanzania wote bila kusahau maslahi ya Tanganyika, kuangalia mbele na kuiunganisha, bila kuendekeza ukabila, udini, ukanda, matabaka, matusi, kejeli, mipasho.

Tanzania tuwe na vyama viwili tu imara.
 
Back
Top Bottom