Umoja wa Mataifa: Afrika itakumbwa na uhaba wa ngano kutokana na vita vya Urusi na Ukraine

Umoja wa Mataifa: Afrika itakumbwa na uhaba wa ngano kutokana na vita vya Urusi na Ukraine

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
1647336283983.png

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameonya kwamba vita vya Urusi dhidi ya Ukraine vinaweza kusababisha kile alichokiita "kimbunga cha njaa" na uhaba wa chakula kote duniani.

Alisema nchi nyingi za Afrika na maskini zinategemea zaidi uzalishaji wa ngano wa Urusi na Ukraine, ambayo sasa iko hatarini kutokana na mzozo huo.

Hii ni pamoja na Burkina Faso, Somalia na Yemen ambazo tayari zinahangaika kulisha watu wao.

Bw. Guterres ametoa wito wa kusitishwa kwa vita hivyo mara moja ili kuepuka kuharibika kwa mifumo ya chakula duniani.

Pia alitangaza kifurushi cha $40m (£31m) kusaidia mamilioni ya Waukraine wanaokabiliwa na njaa na kupungua kwa usambazaji wa maji na dawa.

BBC Swahili
 
Afrika sisi tunavyo vyakula vyetu mahindi, muhogo, maharage, mchele, viazi ndio vyakula vikuu. Wa,ungu ndio wala mkate, pizza,n.k iweje waafrika wapate njaa kwa chakula wasichokula kwa wingi?

Pili afrika hakuna ukame kwani mazao hayo pia huzalishwa kwa baadhi ya nchi hiyo bado wanaweza kununua huko. Poor wazungu always using Africans as scape goat.
 
Hawa jamaaa ni wajinga sana

Any way ni wakati sasa wa sisi African kulima ngano kwa wingi sana kwasabu
1. Tunalo soko la ndani ambalo washindani wetu wapo vtani acha waendeleee tujipgie hela
2. Tutapata na soko la nje pia maana muuzaji wa kimataifa yupo kukpiga chabumbu

Tulimen tuwaoneshe kwamba hawatujui vzur kama waliopta kenge hawa
 
Huwa mabalaa yatokea huko dunia africa ndio ka forecast yao.[emoji2] Pumbavu sana

Walisema kwenye UVIKO 19 kwamba waafrika wataokota maiti barabarani matokeo yake wameokota wao waafrika wanadunda.

Mwafrika hata mizizi atakula na ataishi waache ujinga wapambane na matatizo yao wenyewe waliyoyatengeneza kwa tamaa za miili yao
 
Eti katoa wito kusitisha vita sababu ya mifumo ya chakula itaharibika na Africa itapata njaa hiyo sio sababu ya msingi ya kusitisha vita atafute sababu zenye mashiko na sio kusingizia Afrika sababu tu ni masikini.

Africa tuna mifumo yetu imara ya chakula tunayotumia tangu enzi ndio maana hata vita ya pili ya dunia walioteseka ni wenyewe huko huko na ikawafanya waje Africa ili wajiimarishe sàsa sahivi angalau afrika tuna uelewa kwahiyo wanavopigana na sisi tunaweza pata upenyo wa kupiga ela.
 
Hiyo haisababisha njaa huku mashambani! Sisi hofu Ka bei za manumbu, mihogo na magimbi zitapanda, tutaathirika kiukweli!
Njaa itakuwa huko Zenji Kwa wala mikate na maandazi!

Ingekuwa sembe bei itapanda Sana, ningesema tunakufaaah!
 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameonya kwamba vita vya Urusi dhidi ya Ukraine vinaweza kusababisha kile alichokiita "kimbunga cha njaa" na uhaba wa chakula kote duniani.

Alisema nchi nyingi za Afrika na maskini zinategemea zaidi uzalishaji wa ngano wa Urusi na Ukraine, ambayo sasa iko hatarini kutokana na mzozo huo.

Hii ni pamoja na Burkina Faso, Somalia na Yemen ambazo tayari zinahangaika kulisha watu wao.

Bw. Guterres ametoa wito wa kusitishwa kwa vita hivyo mara moja ili kuepuka kuharibika kwa mifumo ya chakula duniani.

Pia alitangaza kifurushi cha $40m (£31m) kusaidia mamilioni ya Waukraine wanaokabiliwa na njaa na kupungua kwa usambazaji wa maji na dawa.

BBC Swahili
Imbombo ngafu !!! Viazi vitamu na mihigo ipo kibao,tusumbukie ngano marvelous !!
 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameonya kwamba vita vya Urusi dhidi ya Ukraine vinaweza kusababisha kile alichokiita "kimbunga cha njaa" na uhaba wa chakula kote duniani.

Alisema nchi nyingi za Afrika na maskini zinategemea zaidi uzalishaji wa ngano wa Urusi na Ukraine, ambayo sasa iko hatarini kutokana na mzozo huo.

Hii ni pamoja na Burkina Faso, Somalia na Yemen ambazo tayari zinahangaika kulisha watu wao.

Bw. Guterres ametoa wito wa kusitishwa kwa vita hivyo mara moja ili kuepuka kuharibika kwa mifumo ya chakula duniani.

Pia alitangaza kifurushi cha $40m (£31m) kusaidia mamilioni ya Waukraine wanaokabiliwa na njaa na kupungua kwa usambazaji wa maji na dawa.

BBC Swahili
Europa pia wanategemea ngano ya urusi. Sio ngano tuu mafuta, gas na mbao.
 
Back
Top Bottom