Umoja wa Ulaya (EU) walaani tukio la kushambuliwa Mbowe jijini Dodoma

KESHO WANAJADILIWA NA WORLD BANK KAMA WAPEWE UNAFUU WA MADENI SABABU YA CORONA AU LA, WAMEANDIKA BARUA NA KULIALIA HADI MAKAMASI YANAWATOKA WAKIRUDI HUKU WANAJIMWAMBAFY NA WORLD BANK WAMEWAAMBIA MAJIBU YATAWEKWA HADHARANI NAAMINI UKATILI HUU NA DHIHAKA ANAYOFANYIWA MBOWE UTAJADILIWA HATA KAMANI KWA DAKIKA 5 ILI WAJUE PESA ZAO ZINAFANYIA KITU GANI HASWA KATIKA MIAKA HII MITANO YA UDIKTETA UTESAJI MAUAJI NA UTEKAJI
 
I heard Mr Mbowe himself is the perpetrator - he is danger to himself, he was drunk and slipped on the stairs!
 
Kumbe wanafatilia ndo picha la uchaguzi lishaanza Hilo.
Yaani mtu ajenge Ikulu mpya aje akalie mwingine kirahisi tu Nani kasema hayo Mambo Africa hayapo
 
Wanyimeni misaada na mikopo vinginevyo huu ushetani utaendelea kwani hatuoni uchunguzi wa maana ukifanyika.
Wanatukanwa wanaitwa eti mabeberu na bado wanatoa misaada huku wanatukanwa na wasio shukrani
 
The government should advice EU and all politicians that if they need the Government protection which will assure them their security, then they should be giving details of their movement to the relevant government organs.
Contrary to that the same politicians will start to complaining that they are being followed and the Government would be deemed to have intervene or have done a social intrusion .
If today an mp is mugged in one of the eu country would it be deemed as an attack on democracy?? Or is it only to Tanzania or Third world countries ??

Labour MP attacked and mugged on way home from Parliament | The Independent
22 Feb 2018 · A Labour MP was attacked and mugged by a group of up to six people on his way home from Parliament.
Imagehttps://www.businessinsider.com › ...
Labour MP Adrian Bailey mugged near Elephant & Castle, South London ...
21 Feb 2018 · A Labour MP was attacked by a gang of hooded thugs in a brutal mugging in south London. Adrian Bailey ...
 
Reactions: mmh
Shambulio la Kiongozi wa upinzani Tanzania mheshimiwa Freeman Mbowe limeshika sura nyingine pamoja na Bunge la JMT kujaribu kuingilia na kupotosha kwa kuwapanga wabunge wa CCM.

Mataifa makubwa na yenye ushawishi na nguvu duniani yameingilia swala hill na kuitaka serikali kufanya uchunguzi wa kina wawalio mshambulia Mbowe na kuwafikisha kwenye sheria.

Agizo la wakubwa hao kiuhalisia no AMRI na isipotekelezwa madhara ni makubwa sana kwa nchi yetu hii masikini.
Jee tutaendelea kukomaa kama awali na kusimamia uongo?

---------

Muungano wa Ulaya, Marekani na Uingereza zimeshutumu shambulio dhidi ya kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Freeman Mbowe siku ya Jumanne.
Katika taarifa tofauti zilizowekwa katika tovuti zao, jamii hiyo ya kimataifa imetoa wito kwa serikali ya Tanzania kuanzisha uchunguzi na hatimaye kukamatwa kwa wale wote waliohusika na shambulio la kiongozi huyo wa upinzani.

Freeman Mbowe alivamiwa na kushambuliwa na watu wasiojulikana wakati akirejea nyumbani kwake jijini Dodoma huku viongozi wa chama chake wakidai kwamba shambulio hilo lilishinikizwa kisiasa.

Katika taarifa yake Muungano wa Ulaya umesema kwamba shambulio lolote dhidi ya mwakilishi wa taasisi ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ni shambulio dhidi ya demokrasia.

Na huku uchaguzi mkuu ukitarajiwa miezi michache ijayo , EU imesema kwamba ni muhimu kuwacha demokrasia kuendelea kushamiri ili kuhakikisha kuwa kuna mazingira ya usawa katika uchaguzi wa haki na ulio wazi.

''Tunaamini kwamba mamlaka itafanya uchunguzi, kuwakamata na kuwashtaki wahusika'', ilisema taarifa hiyo ya EU.

Kwa Upande wake ubalozi wa Marekani umesema kwamba tukio hilo ni la kikatili na lisilo la sababu .

Ubalozi huo umesema kwamba umesjhtushwa na tukio hilo na kutoa pole kwa mbunge huyo na familia yake.

''Ubalozi wa Marekani umeshtushwa na kuhuzunishwa na tukio la kikatili la kushambuliwa kwa mbunge na mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe tarehe 9 Juni, tunatoa pole kwa mbunge huyo na familia yake'',ilisema taarifa hiyo.

Ubalozi huo umelitaja shambulio la kiongozi huyo wa Chadema miongoni mwa mlolongo mrefu wa matukio ya kusikitisha ya utumiaji wa nguvu na unyanyasaji yanayofanywa dhidi ya wanachama wa vyama vya upinzani.

Aidha ubalozi huo umetambua kwamba mojawapo ya mashambulio hayo ya kikatili dhidi ya viongozi wa upinzani ni jaribio la mauaji lililotokea tarehe 7 mwezi Septemba 2017 dhidi ya Tundu Lissu ambalo ufumbuzi wake haujapatikana hadi leo.



Nao ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania umesema kwamba kila mwansiasai nchini Tanzania anapaswa kuwa na uhuru kuwakilisha eneo bunge lake bila ya hofu ama ghasia , hususan wakati ambao kampeni za uchaguzi wa 2020 zinaanza.

Kwa sasa kiongozi huyo wa Chadema anaendelea kupata matibabu katika moja ya hospitali zilizopo jijini Dodoma.

Shambulio dhidi ya Bwana Mbowe linakuja siku moja baada ya mwanasiasa wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu kutangaza rasmi nia ya kuwania urais kupitia chama cha Chadema.

Chanzo: BBC
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…