Umri huu ni kete yako ya mwisho, ukikosea ni majuto hadi unaingia kaburini

Umri huu ni kete yako ya mwisho, ukikosea ni majuto hadi unaingia kaburini

" Huyu mwanaume anaboa, hamna matukio kabisa, haya mahusiano yanaboa"

Kama umeshawahi kukutana na mtu wa aina hii utagundua binadamu tunatamani jambo la utofauti kila wakati hivyo siku zote tunaona tulikosea kufanya maamuzi ndo maana usishangae kukutana na tajiri hana furaha.
 
Wakati mwingine wanadamu tunatengeneza scenerio kwenye maisha yetu yanayotupa tabu na mahangaiko yanayopelekea kukosa Raha za maisha na kuyajutia maisha........

Chini ya jua wanadamu tumekosa au hatuna udhibiti wa mambo mengi yanayoendelea au kutokea maishani mwetu kinyume na matakwa ya nafsi zetu......

Kila mwanadamu ni shahidi wa nafsi yake na ni kawaida ya nafsi kupendelea mambo mazuri.......lakini wakati mwingine mambo hutokea maishani ambayo huleta matokeo kinyume na matakwa ya nafsi au matarajio yetu............

Tusipende kuyapima mambo yetu kwa umri wetu au mitazamo ya watu wengine wanaoonekana kama kwamba wametuacha mbali.....

Katika mlango wa kiimani kuna nguvu kubwa juu ya mienendo yetu na sisi nguvu zetu ni ndogo kubadilisha matokeo ya nguvu hizo......

Ishi maisha yako kwa uwezo wako na kwa namna ulivyorudhukiwa na muumba.... nyakati na umri ni mambo ya kiulimwengu ambayo yako nje ya uwezo wako.......

Usipende kupima mafanikio na umri wako ndio chanzo kikuu na kuiondosha furaha maishani mwako......
 
Nina miaka 37, katika umri huu nimekuwa nafanya mambo mengi ya kiuchumi na kijamii hivyo najikuta nakutana na watu wengi sana tunaobadilishana nao mawazo yanayohusu mambo mengi ya uchumi na jamii, nilichokibaini wengi wa watu wanajutia makosa yao na wameshindwa kuyarekebisha makosa yenyewe ni haya -
umeandika vizuri ila suala la kujutia kwasababu ya kuzaa watoto wachache HAPANA kwakweli watoto wengi zama hizi ni mzigo tu uwe na hela usiwe hela watoto wengi ni mzigooo.. naenda zangu
 
Nina miaka 37, katika umri huu nimekuwa nafanya mambo mengi ya kiuchumi na kijamii hivyo najikuta nakutana na watu wengi sana tunaobadilishana nao mawazo yanayohusu mambo mengi ya uchumi na jamii, nilichokibaini wengi wa watu wanajutia makosa yao na wameshindwa kuyarekebisha makosa yenyewe ni haya -

1. Ndoa wanaume wengi na wanawake wengi wanajutia ndoa zao na wanaona walikosea kuzaa ama kuishi na wenza wao , wengi hujiona wenye hatia na kuona hawakufanya chaguo sahihi , hata waliofanikiwa kuvunja ndoa zao hujutia vile wameshindwa kulea watoto wao pamoja na mwisho wa siku inabaki kuwa ni lawama isiyokwisha

2. Makosa ya kukimbia shule, kukosea kuchagua masomo na kazi wanazofanya ,hapa pana majuto sana , wengine hulaumu mamuzi yao ama wazazi wao kutowapatia elimu sahihi na matokeo yake wanajikuta either hawana elimu sahihi , wengine wanajiiona kazi wanazofanya sio sahihi nk na mbaya muda wakubadili kazi ama kusoma tena haupo,

3. Aina ya uwekezaji , kuna uwekezaji mzuri na uwekezaji mbaya , bahati mbaya sana kipindi tunawekeza tunakuwa hatuna clear mind, mtu ananunua kiwanja maeneo hayakuwa sahihi, mwingine anajenga nk unajikuta umetumia pesa nyingi na huwezi kuja kuipata tena hili ni tatizo na linaleta sana majuto, nina mtu huwa anajutia sana kwa nini alipoanza kazi tu akaoa, akajenga na kuingia kwenye majukumu mapema na kujikuta hana uwezo tena wa kujipanga tena labda akifika uzeeni

4. Kutomjua MUNGU ujanani wapo walioharibu afya na wapo walioharibu uchumi kwa sababu hawakumjua MUNGU , wengi hujutia mamuzi na sifa wanazotambulika nazo

6. Mahali pa kuishi , wengi wanajutia mahali wanapoishi na aina ya mazingira wanayoishi , wengi husema ningejua kipindi kile viwanja, mashamba nk vilikuwepo na bei zilikuwa rafiki ila sikufanya, wengine hujutia aina ya nyumba walizojenga na miji yao walivyoipanga nk na mwisho kabisa ni

8. Umri wa kupata watoto, wapo wanaojuta kwa nini hawakupata watoto mapema, wengine husema ningejua mtoto wa kwanza ningempata atleast na miaka 30 ila ndio hivo nilichelewa, wapo wanaoujuta kwa nini walizaa watoto wachache, sijakutan na mtu anayejuta kuzaa watoto wengi watu wanajutia umri na uchache wa watoto
Nyakati hizi vijana wa umri huo wakike na kiume, ni kweli, wachache wanajuta tena sana lakini wengi wao wala hawajali, hawana habari, hawana mipango na wala hawatishiki kabisa na hali hiyo ni Mwendo wa kula Bata tu......
 
At 26yrs nishaaza kujuta,najuta kwanini sikukaza shule asee mzee wangu kafariki akiwa na kinyongo na mimi kwasababu ya hili.
I hate myself
Relax bro. Kuhusu shule wengi tuna majuto. Tumepishana tu viwango. Kuna mtu alienda Advance na One ya 9 halafu six akapiga div. IV, Mwingine aliingia chuo na one kali ila akatoka na G.P.A ya kishenzi.
 
Wakati mwingine wanadamu tunatengeneza scenerio kwenye maisha yetu yanayotupa tabu na mahangaiko yanayopelekea kukosa Raha za maisha na kuyajutia maisha........

Chini ya jua wanadamu tumekosa au hatuna udhibiti wa mambo mengi yanayoendelea au kutokea maishani mwetu kinyume na matakwa ya nafsi zetu......

Kila mwanadamu ni shahidi wa nafsi yake na ni kawaida ya nafsi kupendelea mambo mazuri.......lakini wakati mwingine mambo hutokea maishani ambayo huleta matokeo kinyume na matakwa ya nafsi au matarajio yetu............

Tusipende kuyapima mambo yetu kwa umri wetu au mitazamo ya watu wengine wanaoonekana kama kwamba wametuacha mbali.....

Katika mlango wa kiimani kuna nguvu kubwa juu ya mienendo yetu na sisi nguvu zetu ni ndogo kubadilisha matokeo ya nguvu hizo......

Ishi maisha yako kwa uwezo wako na kwa namna ulivyorudhukiwa na muumba.... nyakati na umri ni mambo ya kiulimwengu ambayo yako nje ya uwezo wako.......

Usipende kupima mafanikio na umri wako ndio chanzo kikuu na kuiondosha furaha maishani mwako......

Kijana,

Umenena vyema
 
Back
Top Bottom