Umri unapokuwa umeenda na hujaoa au kuolewa unakabiliana vipi na maneno ya jamii inayokuzunguka?

😂😂 ndiyo hivo sasa utajuta
 
Swali la utaoa au kuolewa lini ni swali la unyanyapaa linaloingilia uhuru wa mtu.

Mtu asiyekuhusu akikuuliza hivyo, muulize, kwani tulikubaliana kuhusu hilo?

Pengine unaukizwa na watu wa karibu kwa maoenzi mazuri tu, pengine wanatafuta wajukuu.

Kuna siku mtu ambaye kifamilia ninamuheshimu kabisa aliwahi kuniuliza hilo.

Nilimjibu kitu kimoja tu.

"I don't want to talk about that".

Habari nzima ikafikia tamati hapohapo, na yeye akajua sipendi mjadala juu ya jambo hilo, kama kuna habari nitamueleza.

Sasa inategemea na familia yenu ikoje, inawezekana jibu hilo likakubalika, au likaonekana la dharau.

Kwetu lilikubalika nikaachiwa uhuru wangu.
 
Huwa nawajibu nikipata mda mzuri tutazungumzia Hilo swala[emoji57][emoji57]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…