Umuhimu wa mapumziko siku ya Sensa

Umuhimu wa mapumziko siku ya Sensa

Ndugu wana jamvi nmeona Serikali imetoa taarifa kuwa Ile siku inayotangazwa Sana ya Sensa kuwa sio siku ya mapumziko. Kiukweli niseme serikali inakosea Sana na haitapata taarifa sahihi kabisa.

Kuna Baadhi ya nyumba hakuna anaebaki Nyumbani hivyo hata wakienda kesho yake hawatakuta mtu maana wote wanaenda kazini.

Pia wanasema ukiondoka uache taarifa zako Kwa anaebaki. Hilo ni ngumu Kwa vile sio Kila niliepanga nae ninamuamini kiasi cha kueza kumuachia taarifa zangu zote binafsi.

Pia Kwa wale walio na wadada wa kazi haiwezekani kuanza kumuambia mdada wa kazi taarifa zangu na familia Kwa ujumla maana ni kama kuwa wazi sasa kitu ambacho sio wote tupo tayari.

Pia hawajasema ni taarifa zipi ambazo zinatakiwa kuachwa ili wakija waweze jibiwa maana tangazo linasema Tu taarifa ziachwe Nyumbani.

Naishauri serikali hiyo siku waifanye iwe ya mapumziko ili kuondoa hizi dosari lasivyo watapata taarifa potofu kuwa tumefika 67m kumbe tupo pungufu
View attachment 2326622View attachment 2326626
Kwa nini wasingefanya siku ya Jumapili kama ilivyokuwa kwenye uchafuzi?!! Sawa mimi nitaacha taarifa zangu kwenye ghetto langu sasa sijui watazipataje!!!!
 
Mambo ni kujipanga tu hakuna kinachoshindikana.

Kuna watakaokuwa safarini pia bila shaka mipango ipo maana watu wa takwimu ni Wasomi wazuri tu.
 
Yaani kwangu labda waje kuanzia saa3 usiku hata wakisema ni mapumziko,maisha yenyewe ndio haya tukae home na wife tule nini na watoto?life wameliseti wenyewe limekua gumu kama nini!nitawaachia namba ya simu mlangoni wanipigie labda
Hilo neno. Nitaacha namba ya sinu
 
Wapeni taarifa wapate data zakwenda kuombea mikopo nje, lakini pia usawa na ufanisi katika ugawaji wa keki ya Taifa.
 
Wewe nani wa kuishauri serikali....
Watanzania wamepiga kura kuwachagua viongozi ila hawajui lengo la kuwachagua hao viongozi ,kama umepigiwa kura lazima uchukue ushauri WA hao waliokuchagua maneno yako hapo juu inaonesha ni namna gani hujui kazi ya serikali period nendeni darasani
 
Na kuna hii nimeikuta mahali...

Ndugu zangu watendaji huko serikalini naombeni kuconfirm kama siku ya sensa ni siku ya kazi kama kawaida…. And if yes I am worried na quality ya data tutakazozipata …. Few thoughts/concerns

1. Ijumaa nilifanyia kazi nyumbani bahati nzuri kata ya kawe wakawa wanafanya pre-testing na ikaangukia nyumbami kwangu … sikuwa nimejiandaa lakini niliwapokea vizuri and it took two hours kumaliza

2. Kwa maswali yale ya pre- testing wakisema twenda makazini , I have a serious concern na data watakazocollect…. House helpers kamwe hawataweza jibu maswali yote yale …. They are many and detailed in actual fact hata mkuu wa kaya mwenye wakati mwingine atahangaika

3. Mama makinda hapo anasema tuache taarifa nyumbani …. Taarifa zipi na ni nani atajua taarifa gani za kuacha hakuna hata mwongozo… yale maswali yapo kwenye categories nyingi na ni mengi sasa mtu atajua ni taarifa gani za kuacha home? Mfano kama kaya yako inawakazi sita na wote wana NIDA utahitaji kutoa namba zao zote za nida as per the questionnaire, lakini pia kuna taarifa za elimu, vizazi na vifo katika kaya …. Ni house girl gani atakuwa na hizo data zote?

4. Uwezo wa wahojaji wenyewe siyo mkubwa ukilinganisha na maswali halafu ndo aje akutane na house helper …. Itakuwa garbage in garbage out huyu mtoto alokuja hapa kwangu for pre testing it was a disaster mpaka nikaihurumia nchi yangu…. Ilibidi mpaka nimwulize kiwango cha elimu akanambia anasoma VETA lakini ni kadogo na hana confidence kabisa ya kuuliza …. I had to help him maana natamani saana zoezi hili lifanikiwe….

I wish wa reconside hii decision kwakweli…. We need quality data for our next ten years plans.
 
Ndugu wana jamvi nmeona Serikali imetoa taarifa kuwa Ile siku inayotangazwa Sana ya Sensa kuwa sio siku ya mapumziko. Kiukweli niseme serikali inakosea Sana na haitapata taarifa sahihi kabisa.

Kuna Baadhi ya nyumba hakuna anaebaki Nyumbani hivyo hata wakienda kesho yake hawatakuta mtu maana wote wanaenda kazini.

Pia wanasema ukiondoka uache taarifa zako Kwa anaebaki. Hilo ni ngumu Kwa vile sio Kila niliepanga nae ninamuamini kiasi cha kueza kumuachia taarifa zangu zote binafsi.

Pia Kwa wale walio na wadada wa kazi haiwezekani kuanza kumuambia mdada wa kazi taarifa zangu na familia Kwa ujumla maana ni kama kuwa wazi sasa kitu ambacho sio wote tupo tayari.

Pia hawajasema ni taarifa zipi ambazo zinatakiwa kuachwa ili wakija waweze jibiwa maana tangazo linasema Tu taarifa ziachwe Nyumbani.

Naishauri serikali hiyo siku waifanye iwe ya mapumziko ili kuondoa hizi dosari lasivyo watapata taarifa potofu kuwa tumefika 67m kumbe tupo pungufu

View attachment 2326622


View attachment 2326626
Kwa hiyo maofisi yafungwe siku saba? Maana ndani ya siku Saba utakuwa umehesabiwa haijatajwa "kwenu" watafika lini. Acha watu wafanye kazi wewe kaa nyumbani subiri sensa ikishapita nenda kachukue kilicho chako kwenye desk lako ofisini uje usubiri matokeo ya sensa nyumbani.

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Sioni logic, why upumzike siku moja wakati zoezi ni la siku saba, bora ungesema upumzike siku 7.
Imagine mkoa kama Dar es salaam, EA moja tu wanaweza wasimalize plus hata huko vijijini (mf longido kwa wafugaji) maeneo yako very scattered na namna akifikika.

Kuhusu questionnaires sidhani kama ni very secret kiasi hicho kwamba hata dada wa nyumbani asipewe kuepuka UHAINI ndani ya familia [emoji28]
Maswali kama mna choo na mnakitumia, mmeala wangapi usiku wa 23 agost, uchumi wenu unategemea nini, mkuu wa kaya ni jinsia gani nk nk.

Hakuna maajabu sana kwamba questions ni classified kiasi hicho
Moja ya swali ni kipato cha wastani cha kaya. Kwa hiyo umuachie housegirl au jirani hiyo taarifa kwamba bwana wastani wa kipato changu kwa mwezi ni laki 1.
 
Nikiangalia zoezi la postkodi za mitaa lilivyofanyika na lilikuwa zoezi rahisi sana na lilikuwa "straight forward" lakini matokeo yakawa na walakini kwa kiasi kikubwa, napata mashaka sana iwapo hili la sensa litafanikiwa kwa jinsi lilivyo gumu zaidi ya zoezi la postkodi. Vipi hili zoezi la sensa ambalo ni muhimu zaidi aachiwe beki tatu kwa kiasi kikubwa atoe taarifa za familia labda ya watu sita. Na ikumbukwe kuwa hao mabeki tatu wengine hata kusoma hawajui.

Vinginevyo labda ijulikane tu wazi hili zoezi la sensa ni zoezi la kutimiza tu ratiba kwa vile huu ni mwaka wa sensa basi tunafanya tu sensa mpaka mwaka mwingine wa sensa ufike. Muda bado upo kwa serikali kulitafakari hili suala kwani kufeli kujua idadi ya watu kwa usahihi basi ndio mwanzo wa kufeli kwa mipango mengine mingi ya maendeleo. Walau siku yenyewe ya sensa yaani tarehe 23/08/2022 ikiwa siku ya mapumziko serikali itapata kwa asilimia kubwa taarifa sahihi hata kama siku zinazofuata taarifa hazitakuwa sahihi sana.

Kwa heshima na taadhima naiomba serikali iangalie mara mbil mbili kipi bora hasara ya siku moja ya watu kutokwenda kazini au hasara ya muda mrefu ya kutokuwa na takwimu sahihih ambazo zitaisadia nchi kwenye mipango yake mbali mbali.
 
Back
Top Bottom