Unaazaje kumueleza Mkeo kuwa una mtoto nje ya ndoa, Mwanamke unalipokeaje kutoka kwa Mumeo?

Unaazaje kumueleza Mkeo kuwa una mtoto nje ya ndoa, Mwanamke unalipokeaje kutoka kwa Mumeo?

Gazeti elimu ya saikolojia inahusika hapo, kinyume na hapo mtaharibu kila kitu!
 
kwa hyo wanaume ndio wepesi kuelewa?

Kimaubile mwanamke ndie anaekaa na watoto kwa muda mrefu na ndie mlezi kwa asilimia 80 hivyo unaweza kuuona huo ukaribu

Wanawake wanakuwa wagumu sana kwasababu za wivu yaani kila akimuona yule mtoto anakuwa anamuona kama mumewe amemsaliti na inasababisha amuone mtoto nae ni mkosaji sana na kuanza kumsumbua na kumtesa

Kwa upande wa wanaume ni wachache sana wanajali kuhusiana na watoto na mara nyingi baba yeye wala hashindi nyumbani hivyo inakuwa ngumu sana kujali kuhusiana na hilo

Wanaume wengi sana wameoa wanawake wenye watoto lakini wanawake wachache sana wameolewa na wanaume wenye watoto na hao wachache kunakuwa na sababu kama nilizozisema hapo juu

Mimi ni mmojawapo wa wanaume ambao wala sitajali sana kuhusiana na mwanamke kama akiwa na mtoto,tutalizungumza hilo na wala hicho sio kitu ambacho kitanifanya nisimuoe au kuanzisha mahusiano na mwanamke!
 
Baba paroko hapo ni upande zote...

imagine mie nakuletea mtoto sasa tena nilimpata wakati tuko
kwenye ndoa...na nimekuficha muda wote sidhani ka utaelewa kwa urahisi

Hilo ni tatizo lakini mada haizungumzii sula la kupata watoto mkiwa kwenye ndoa!
 
Utachekesha jamiii.........uhame kwa tambo then uanze kuinyemelea nyumba uliyoishi kuingia giza kutoka giza........shaurilo!!!!!!
Sinaga utaratibu wa kurejea matapishi yangu!!!
Niinyemelee kizani nimesahau nini ninachokirudia?
Haikufaa lami litafaa vumbi la mkaa??
 
Sinaga utaratibu wa kurejea matapishi yangu!!!
Niinyemelee kizani nimesahau nini ninachokirudia?
Haikufaa lami litafaa vumbi la mkaa??


Zilongwa mbali zitendwa mbali!!!!!!!!
Na ndio maaana sijakuambia about those twins!!!!!
 
Imetokea kwa baba yangu Mdogo, kwa sasa mtoto wake wa nje ya ndoa yuko mwaka wa pili
Hapo UDSM lakini mkewe hajui..............

Si jambo zuri, hakika si jambo zuri, Lakini imeshatokea unafanyaje, yaani unalifikisha
vipi kwa mkeo? Unaanzaanzaje?
Na wewe Mwanamke unalipokeaje? Uko tayari kumchukulia huyo mtoto kama mwanao?

Mkuu inategemea huyo mtoto alimpata kipindi gani,?kama alimpata kabla hajafunga nae ndoa anaweza kumtambulisha hana shida ila kama amempata akiwa ndani ya ndoa hiyo ni balaa kubwa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Imetokea kwa baba yangu Mdogo, kwa sasa mtoto wake wa nje ya ndoa yuko mwaka wa pili
Hapo UDSM lakini mkewe hajui..............

Si jambo zuri, hakika si jambo zuri, Lakini imeshatokea unafanyaje, yaani unalifikisha
vipi kwa mkeo? Unaanzaanzaje?
Na wewe Mwanamke unalipokeaje? Uko tayari kumchukulia huyo mtoto kama mwanao?

Inategemea huyo mtoto alipatikana lini. Kama umri wa mtoto ni mkubwa kuliko umri wa ndoa yao hapo mke atachukia tu kwa kudanganywa, I mean wakati wakianza uhusiano ilifaa huyo bwana aseme ukweli. Ngoma ni pale ambapo umri wa mtoto wa nje ni mdogo kuliko miaka yao ya ndoa! HAPO BABA MDOGO ASHIKE MOYO NA AITE WACHUNGAJI WAMSAIDIE MAANA LOLOTE LAWEZA KUTOKEA. Ila kama ni waislamu mbona siiiimplee, kama kumuua sisimizi
 
Back
Top Bottom