Unajua Mungu aliumbwa na nani?

Unajua Mungu aliumbwa na nani?

Kisai naona hatuelewani sasa nikuulize Mungu wenu amewaumba kwa lengo lipi?
 
Yani mtu anang'ang'aniza kwamba hakuna kisicho na mwanzo logically na scientifically halafu hapohapo anasema mungu hana chanzo alikuwepo tu!!
Mtu kama huyu Gasper Mwaluanda hajui hata kuwa maandishi yake yanajipinga.
Inaonyesha hajui hata yeye anaandika nini.
Mkuu Mungu sio kitu wala sio mwanadam wala hafananishwi na chochote ndio maana nkasema Mungu Ni Mungu... wewe Bado hujaelewa concept yangu hapo,, iko hv vitu vyote vina mwanzo lakn Mungu Hana mwanzo,, mkuu huwez kuelewa concept ya Mungu kwa siku1,,

Sawsawa na mtoto mdog huwez mpeleka shule siku1 akarud anaelewa,, ukimpeleka shule mtoto cha kwanza kabsa atafundishwa protocol za shule husika Kama ni English medim atakua akiziishi protocol za English medium au Kama Ni shule za kawaida ataziishi protocol za kawaida,, akienda secondary, high school had chuo atakutana na protocol husika atafundishwa na ataziishi,, hawez kuleta protocol za chuo akiwa primary..

Na suala la kumjua Mungu Lina hitaji elim yake na Lina protocol zake ambazo wew inaonekana huzijui,, huwez kujua aliumbwa na nani wakati humjui yeye,,,
 
Sasa nana aliweka Sukari kwenye maembe..?
Maswali ya kivivu haya...kwahiyo kama hujui sukari imeingiaje kwenye embe kwanini usifuatilie?
unataka kuhitimisha tu kivivu kuwa mungu wenu ndio kaiweka?
Msiwe mazombi hivyo.
 
Mkuu Mungu sio kitu wala sio mwanadam wala hafananishwi na chochote ndio maana nkasema Mungu Ni Mungu.wewe Bado hujaelewa concept yangu hapo,, iko hv vitu vyote vina mwanzo lakn Mungu Hana mwanzo,, mkuu huwez kuelewa concept ya Mungu kwa siku1,
Sawsawa na mtoto mdog huwez mpeleka shule siku1 akarud anaelewa,,ukimpeleka shule mtoto cha kwanza kabsa atafundishwa protocol za shule husika Kama ni English medim atakua akiziishi protocol za English medium au Kama Ni shule za kawaida ataziishi protocol za kawaida,, akienda secondary, high school had chuo atakutana na protocol husika atafundishwa na ataziishi,,hawez kuleta protocol za chuo akiwa primary.
Na suala la kumjua Mungu Lina hitaji elim yake na Lina protocol zake ambazo wew inaonekana huzijui,, huwez kujua aliumbwa na nani wakati humjui yeye,
"Mungu sio mwanadamu"
"Mungu sio kitu"
"Mungu ni Mungu"..!!!

Humjui mungu wako ni nini.
kama mungu sio mwanadamu wala sio kitu, mungu ni nini?
 
Ametuumba ili tumuabudu yeye peke yake pasi na kumshirikisha na chochote.
Mungu wa haki,mwenye upendo anaumba viumbe ili wamuabudu, na wasipomuabudu anawachoma moto!!!

Mantiki ya yeye kutaka kuabudiwa ni ipi?

Mantiki ya kuumba kiumbe ambacho anajua kuwa hakitamuabudu ni ipi?

Mantiki ya kuchoma moto kiumbe ambacho alijua hakitamuabudu hata kabla hajakiumba ni ipi?

Anafurahia kufanya zoezi la kuchoma moto viumbe wake?
 
Mungu wa haki,mwenye upendo anaumba viumbe ili wamuabudu, na wasipomuabudu anawachoma moto!!!
Naam sahihi kabisa, huu ni utaratibu, bali ni uhalisia. Kama ilivyo kwa sisi ambao tuna watoto ukimpa maagizo mwanao akienda kinyume na maagizo au utaratibu unampa adhabu. Ila adhabu ya Allah ni Kali na ni kamili.
Mantiki ya yeye kutaka kuabudiwa ni ipi?
Kutiiwa.
Mantiki ya kuumba kiumbe ambacho anajua kuwa hakitamuabudu ni ipi?
Kujua kwake hakukizuii hicho kiumbe kisitende kinachotaka. Ndiyo maana Allah anajua na uhuru amekupa. Kama ilivyo leo hii ukiwa na mtoto unaye mjua yaani wako, kwamba unaweza kumpa hela na ukajua kabisa hii hela uliyo mpa lazima ataenda kununia pipi tu huyu mtoto na kweli mtoto akaenda kununua pipi. Ila kujua kwa Mola wetu kunalingana na dhati yake ya ukamilifu yaani anajua kwa hakika kabisa. Lakini kujua kwako wewe hakukumzuia huyo mtoto kufanya lile analo litaka.
Mantiki ya kuchoma moto kiumbe ambacho alijua hakitamuabudu hata kabla hajakiumba ni ipi?

Maana ya hilo swali umeshauliza huko juu na nimeshakujibu tayari. Sababu amekipa uhuru kamili wa kuchagua na akakinainishia njia hii nzuri na njia hii mbaya, yaani ni sawa na mtu epewa mtihani na akapewa majibu kwa hiyo kufeli ni kuamua yeye. Kwahiyo lazima aadhibiwe tu kwa uxembe wa makusudi.

Kujua kwake hakumzuii huyo mja kufanya anacho taka.
Anafurahia kufanya zoezi la kuchoma moto viumbe wake?
Mola wetu hafurahii kuwachoma viumbe ila huwa akitaka jambo liwe linakuwa hata kama halipendi. Kuna kitu kinaitwa Mashia na Irada. Huyu ndiyo Mola wetu ndiyo maana hafanani na chochote.
 
Kujua kwake hakukizuii hicho kiumbe kisitende kinachotaka. Ndiyo maana Allah anajua na uhuru amekupa.

Kisai nakuomba kijana acha kudanganya, hakuna uhuru Allah katoa , kila kitu na kila jambo na kila neno kashalipanga utalifanya lini na wapi

Malaika ukiwa tumboni anatuma na Allah kukuandikia kila kitu

Mpaka Mimi nampinga hapa hii msg Alisha panga nitaandika
 
Ndiyo maana Allah anajua na uhuru amekupa.
Kisai naona siku izi umeamua kuwa muongo wa kutisha kabisa

Soma

...Allah sends His angel to it with instructions concerning four things, so the angel writes down his livelihood, his death, his deeds, his fortune and misfortune....Sahih Muslim 2643 a
 
Kuchunguza kama Mungu yupo au hayupo mimi naona ni jambo zuri tu. Ila ni vyema tuendelee kuamini kuwa Mungu yupo, kuliko kutoamini halafu mwisho wa siku tunakuja kugundua alikuwepo kweli.

Maana nchi zilizoendelea ni kama watu wameacha kwenda kusali kwenye nyumba za ibada. Badala yake wamekuwa bize na inshu za kimaendeleo na kupenda soka tu. uwepo wa Mungu imechukuliwa kama ni jambo la kuwajenga watu ili wawe na upendo na amani kwenye maisha yao tu.

Labda kulikuwa na haja pia ya kupata ukweli juu ya wanaofariki hapa Duniani je roho zao zinaenda wapi? Je ni kweli kuna maisha mengine baada ya kufa? Maana hatujapata mtu aliyerudi kutupa ukweli

Je kuna viumbe vingine vinaishi hapa Duniani ambavyo Binadamu hawana uwezo wa kuviona?

Je ni kweli kuna uwepo wa Malaika au uwepo wa Shetani?. au ni mambo ya imani tu ya vitu ambavyo havipo?
 
Mungu ni jinga sana...linashindwa kujiweka wazi linajificha uko machakani linaacha mazombi yake ndio yanalitetea halafu cha ajabu na menyewe hata hayajiongezi hehehehe endeleen kumtetea huyo kima wenu.

Mpaka naogopa hata kusoma
 
Kuchunguza kama Mungu yupo au hayupo mimi naona ni jambo zuri tu. Ila ni vyema tuendelee kuamini kuwa Mungu yupo, kuliko kutoamini halafu mwisho wa siku tunakuja kugundua alikuwepo kweli.

Maana nchi zilizoendelea ni kama watu wameacha kwenda kusali kwenye nyumba za ibada. Badala yake wamekuwa bize na inshu za kimaendeleo na kupenda soka tu. uwepo wa Mungu imechukuliwa kama ni jambo la kuwajenga watu ili wawe na upendo na amani kwenye maisha yao tu.

Labda kulikuwa na haja pia ya kupata ukweli juu ya wanaofariki hapa Duniani je roho zao zinaenda wapi? Je ni kweli kuna maisha mengine baada ya kufa? Maana hatujapata mtu aliyerudi kutupa ukweli

Je kuna viumbe vingine vinaishi hapa Duniani ambavyo Binadamu hawana uwezo wa kuviona?

Je ni kweli kuna uwepo wa Malaika au uwepo wa Shetani?. au ni mambo ya imani tu ya vitu ambavyo havipo?
[emoji817][emoji817][emoji817][emoji817]Hoja kuntu...
 
Usiogope, hakuna mungu wa kukuchoma moto.

Ni matangopori tu mnalishwa halafu mnapewa vitisho mkiyakataa.

Say no to "matangopori"
Wewe unaeamini kwamba hakuna Mungu na unaeamini wanaojiita wanasayansi na sayansi Yao,,je wewe sio zombi wa wanasayansi??

Kingine hudhanii kwamba Mungu humjui kwa sababu ya daraja/class alio nayo,,,,,yaani Kuna watu wenye class na huwezi kuwa nao karibu na Wala huwezi kuwakaribia au kuwafikia?? Basi jueni nyie wafuasi wa sayansi wote kwamba kama Kuna protocol za kuwafikia watu valuable,,,au Kuna protocol za kuvifikia vitu most valuable kama madini ya almasi au any rare earth mineral,,,,,basi mjue kwamba Mungu ni more than valuable things na class yake imesupress class ya Marais,,wafalme na matajiri kwa hio protocol za kumfikia au kumkaribia ni za Hali ya juu mtu kama wewe ambae ukiomba hata appointment ya kumuona mkuu wa mkoa ukakaa mwaka mzima ni Bora ungekuwa humble ujifunze protocol za kumjua na kumkaribia Mungu ambae value na class yake hakuna anaeifikia.
 
Kisai nakuomba kijana acha kudanganya, hakuna uhuru Allah katoa , kila kitu na kila jambo na kila neno kashalipanga utalifanya lini na wapi

Malaika ukiwa tumboni anatuma na Allah kukuandikia kila kitu

Mpaka Mimi nampinga hapa hii msg Alisha panga nitaandika
Poa
 
Kisai naona siku izi umeamua kuwa muongo wa kutisha kabisa

Soma

...Allah sends His angel to it with instructions concerning four things, so the angel writes down his livelihood, his death, his deeds, his fortune and misfortune....Sahih Muslim 2643 a
Poa.
 
Back
Top Bottom